Sunday, May 7, 2023

UMUHIMU WA KUNENA KWA LUGHA KWA MTU ALIYEOKOKA.

UMUHIMU WA KUNENA KWA LUGHA

Sababu Mungu ameweka kunena kwa lugha kwa kusudi, kila kitu Mungu anafanya kina kusudi, na kusudi zuri sana kwa mwanadamu.

Kunena kwa lugha ni namna ambavyo mwanadamu anaweza akawasiliana na Mungu kwa lugha inayowezeshwa na Roho Mtakatifu [inayojaliwa na Roho Mtakatifu].


- Mdo 2:1-4 - Unaona wanafunzi walinena kwa lugha kwa kujaliwa na Roho Mtakatifu.

- Kunena kwa lugha ni Roho Mtakatifu anaweka maneno kwenye roho ya mtu, na kisha mtu ananena hayo maneno kwenye kinywa chake. Aidha kwa mtu kuamua, au Roho kuweka msukumo wa mtu kuyatamka hayo maneno.

- Kunena kwa lugha ni Roho kutuombea kwa lugha ya mbinguni kupitia sisi wenyewe, hasa kupitia roho zetu - Rum 8:26, 27.

- Kunena kwa lugha ni kuruhusu roho zetu kuomba kwa kuwezeshwa na Roho Mtakatifu - 1 Kor 14:14. au kuomba katika roho.

- Mtu anaponena kwa lugha mara nyingi haelewi anachokisema sababu ni maneno ambayo hayaeleweki kwa namna ya nyama [mwili] ni mpaka roho aamue kumjalia kufasiri - 1 Kor 14:2, 14

- Mtu atasema kwanini nisielewe, na naombaje sasa vitu nisivyoelewa - Maombi unaomba kwa Mungu hauombi kwako wewe mwenyewe, hivyo muhimu Mungu kuelewa siyo wewe [sina maana Mungu haelewi kiswahili, ila anapenda unene kwa lugha, sababu ndiyo njia pekee ya kuongea na wewe yaani roho yako kibinafsi bila wengine kuhusika, sababau wanakuwa hawaelewi] 

     - Hivyo lugha ya Mungu ni muhimu kuliko lugha yako. Ila Roho yako inaelewa ndiyo maana kuna wakati mtu ananena anasikia furaha, au kulia, sababu roho yako inakuwa imeelewa [roho yako pekee inaweza elewa mambo ya rohoni, na kukuletea kwenye ufahamu wako Roho Mtakatifu akitaka]


- Kunena kwa lugha ni muhimu sana kwa kila mkristo, haina maana mtu hatoenda mbinguni kwa kutonena kwa lugha, lakini kuna vitu vikubwa atavikosa.

- Wengi walio okoka hawaneni kwa lugha, moja ni kwa sababu hawajafundishwa umuhimu wa kunena kwa lugha wakaelewa, mbili ni kwa sababu hawajafika kujua umuhimu wake hata kunena kwa lugha. Siku wakijua watataka sana. 

       - Sababu nimeona watu wakijua, wanaanza kukesha mpaka kanisani wakitaka sana kujawa na Roho kiwango cha kunena kwa lugha.

- Isaya 28:11, 12 - Isaya alitabiri ya kuwa tutasema kwa lugha nyingine.

- Marko 16:17 - Yesu anasema kunena kwa lugha ni moja ya ishara ya mwamini.

- Mdo 2:4 - Unaona ishara ya kwanza ya mtu kujawa na Roho ni kunena kwa lugha.

- 1 Kor 14:18 - Paulo alimshukuru Mungu sababu alinena kuliko wote wakorintho, ambayo walisifika kwa kunena mpaka kupitiliza, ina maana Paulo aliwe msisitizo sana kunena kwenye maisha yake.


- Na kumbuka Biblia imesema "wakasema kwa lugha" na tena inasema "nikiomba kwa lugha" maana yake kunena kwa lugha kunakuwezesha wakati wowote mahali popote ukawa ukisema na Mungu wako, siyo lazima kwenye maombi, hata wakati unakula, unavaa, unatembea, unapiga stori.

UMUHIMU WA KUNENA KWA LUGHA

Tuone sasa umuhimu wa kunea kwa lugha, kwanini Mungu anataka tunene kwa lugha


1. Kunena kwa Lugha ndiyo ishara ya kwanza mtu akipokea Roho Mtakatifu.

- Mtu akipokea Roho Mtakatifu ishara ya kwanza ni kunena kwa lugha.

- Mdo 2:4 ; tunaona wanafunzi walipojawa na Roho mtakatifu, muujiza wa kwanza haukuwa kuinua kiwete au kuponya kipofu, bali walinena kwa lugha. Siku zote Mungu anacholeta kwanza ujue kinabeba vyote. Mfano katika uumbaji, Mungu alianza na kuumba "Nuru" sababu Nuru inabeba vyote - Mwanzo 1:3. 

- Kwahiyo Mungu alitangulia na Kunena kwa Lugha akiwa na maana Lugha mpya [Marko 16:17] inabeba vyote ambavyo Roho anakuja navyo.

   -  Mdo 10:45, 46 ; Utaona Katika nyumba ya Kornelia, wale watu waliokuja na Petro, Wayahudi walioamini, walijua kuwa mataifa nao wamepokea kipawa cha Roho kama wao walipowasikia wakinena kwa lugha; ina maana ishara ya kuwa mtu amepokea hiki kipawa cha Roho ni Kunena kwa lugha.

  -  Mdo 19:6 ; Utaona Paulo alipowawekea mikono wale wanaume kumi na wawili wa Efeso wapokee Roho Mtakatifu, walipopokea, cha kwanza walinena kwa lugha. 

2. Kunena kwa Lugha ni Njia ya Kuongea na Mungu.

- kunena kwa lugha kunamuwezesha mtu kuongea na Mungu kwa njia ya roho yake 

- 1 Kor 14"2

- kwa maana nyingine Mungu ametupa njia ya kiroho ya kuwasiliana naye kibinafsi, tena moja kwa moja [mazungumzo ya wawili na Mungu].

- Paulo anasema "anasema mambo ya siri" maana yake hakuna anayeelewa zaidi ya roho yako na Mungu, na hata shetani haelewi.

- ndiyo maana shetani anapinga sana kunena kwa lugha sababu anajua haelewi, anajua kuna ushindi mkubwa sana kwa mtu anayeomba kwa lugha.

- Mungu ni roho, na kunena kwa lugha ni kunena katika roho yako - maana yake roho kwa roho ndiyo zaweza kuelewana vizuri zaidi ya mwili kwa roho - Ndiyo maana Paulo anasema "akili hazina matunda [1 Kor 14:14]" 

- Yesu amesema "Mungu ni roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli - Yoh 4"24. Maana yake kumuabudu Bwana kwa kunena, kuomba kwa kunena ni muhimu zaidi [1 Kor 14:15]

- Mungu anataka sana roho yako, sababu inamuelewa zaidi ya mwili wako -  na sababu Roho Mtakatifu anakaa kwenye roho yako, basi Mungu anaelewa zaidi roho yako ikiomba zaidi ya maneno ya akili - Ndiyo maana Paulo alimshukuru Mungu kwa sababu ananena zaidi ya wote.

3. Kunena kwa Lugha Inakusaidia Kuomba kama Mungu atakavyo.

- Kwa sababu unponena ni Roho ambaye anayajua mapenzi ya Mungu - 1 Kor 2:11 anasema "vivyo hivyo mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu".

- Rum 8:26, 27 - Anasema hatujui kuomba jinsi itupasavyo.

- Maana yake "tunajua kuomba" ila siyo "itupasavyo"

- maana yake naweza omba kwa kiswahili, kwa lugha yangu, ila sitoweza kuomba inipasavyo. 

- Kwanini, Sababu;  ni Roho pekee ndiye anaweza jua mambo ya Mungu, hivyo ni Yeye Roho pekee anaweza kuomba ipasavyo, hata ukapata majibu.

- Kwahiyo kuomba katika roho kunamuwezesha mtu kuomba "impasavyo". siyo tu kuomba kukamilisha ratiba au kuonekana umeomba, maana kufanya isivyopasa wakati mwingine ni sawa na hujafanya.

- Sasa Paulo anasema "udhaifu wetu" ina maana [siku ukikubali huu udhaifu unao, kwamba huwezi kuomba ipasavyo], basi utataka kuomba kwa lugha saa zote, ili usi-miss kuomba ikupasavyo.

- Tena anasema "Yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho" maana yake Mungu anaijua nia ya Roho, maana yake anaanza kutazama nia ya Roho siyo nia yetu tena; ambayo mara nyingi haiwazi sawa sawa na mapenzi ya Mungu, sawa sawa na neno.

- Sasa "Kwanini anatazama nia ya Roho na siyo yako" anasema "Kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu" - maana yake kuna namna Mungu anapenda tuombe.

- Siyo kwamba hatuombi, ila tunaponena kwa Lugha tunaomba kama apendavyo Mungu.

- Nikupe mfano, unaweza ukawa unaomba kuhusu chakula, au kuolewa - kwa maneno utaomba chakula au kuolewa lakini katika roho hujui ya kesho, kunena kunaweza kuondosha nguvu za giza au sababu ambayo inazuia wewe kupata chakula, kunena kutakusaidia kuondoka na yoyote, maana mwenye uhitaji "anaweza kuja mtu ukaona muujiza kumbe siyo" sasa kunena kutamzuia huyo mtu na kuanza kupangua rohoni mpaka kumpata yule sahihi" ndiyo maana tunasema unatamka "siri" maana yake ni rohoni.


linaendelea wiki ijayo....

Kwa msaada wa Roho Mtakatifu

Wako Pastor Ulenje

+255 683 477 827 

Facebook kama Pastor Ulenje Online.


Tuesday, May 2, 2023

ROHO AKIJA ANAMBADIRISHA MTU NA MAISHA YAKE

ROHO MTAKATIFU ANABADIRISHA MTU NA MAISHA.

ROHO NI NANI?

- MUNGU anasema ni Roho yake - Yoel 2"28

- Yesu anakuja kusema Roho Mtakatifu - Yoh 14"26. 

- Ina maana utakatifu upo ndani yake, ndiyo sifa yale kuu [ Roho ni mtakatifu na ana nguvu ya kumfanya mtu kuwa mtakatifu]

○ Rum 15"16, 2 Thes 2:13, 1 Petro 1"2

- Roho anakuja ameonekana anakuja na nguvu - Luka 1"35, Mdo 1"8


ROHO ANABADIRISHA MTU NA MAISHA.

1 SAM 10"6,7

- Roho anakufanya kuwa mtu mwingine, tofauti na yule wa kwanza.

- Unapofanyika mwingine, unapewa uwezo, mamlaka ya kufanya chochote uonavyo vema.

- Kuokoka ni kufanywa upya kabisa, na Roho ndiye anahusika katika kukufanya upya

Tito 3"5 - si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;

Yesu alipojiliwa na Roho akawa mwingine.

- Yesu bila Roho alikuwa ni mtu wa kawaida, Sababu Yesu ni alichukua asili yetu, akawa kama mwanadamu.

- Ila ile Roho ndani yake ikamfanya kuwa Mungu yaani Kristo.

- Kilichofanya aseme Yeye na Baba yake ni sawa siyo muonekano wa nje, bali ni ndani.

- Alipojiliwa na Roho akawa mwingine kabisa na kuanza kufanya makubwa.


- 1 Sam 16"13

- Daudi alipojiliwa na Roho akawa mtu mwingine kabisa.

- Ndipo watu wakaanza kumfahamu Daudi, lakini hakuna aliyemjua hapo kwanza.

- Pasipo Roho unaweza tia bidii ila zikawa si kitu sababu unakuwa kama wanadamu wengine. 

- unapofanyika mtu mwingine maisha yako yote yanabadilika, ndiyo maana kila aliyejiwa na Roho maisha yake yanabadilika kuanzia na hapo. Ukisoma mifano ya Yusufu, Musa, Daudi, Sulemani, Nabii Eliya, Yesu Mwenyewe, Wanafunzi wa Yesu, na hata leo tunaona mtu anapofika kiwango cha kujaa Roho maisha yake yanabadilika kabisa na kupata sura mpya.


Ubarikiwe kwa Kusoma

Mimi ni Pastor Ulenje 

Tiktok kama Pastor Ulenje 

Facebook kama Pastor Ulenje Online 

+255 683 477827


Wednesday, January 25, 2023

SOMO MAALUMU LA KUINULIWA NA MUNGU #04

 SOMO LA NNE

KUMKUMBUKA HULINDA AGANO LA KUINULIWA


Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo. Kumb 8:18 

Ndiyo! Utainuliwa lakini unahitaji zaidi ya kuinuliwa unahitaji kubaki katika kuinuliwa. Maana mara nyingi tumeshuhudia kwenye maisha yetu up and down sasa ukiendelea kupanda na kushuka hautafika popote. Bali ili ufike mbali ni lazima ukiwasha ndege yako kupaa ni moja kwa moja.

Neno la leo ni neno la kulihifadhi, sababu Mungu anaanza kukuinua kidogo kidogo sasa, hili neno litakusaidia kubaki kwenye sehemu ya kuinuliwa, kuzidishwa na kuongezwa daima.

KUMB 8:1_ Musa anawaambia Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo BWANA aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.

KANUNI #04 MUHIMU ILI KUBAKI KUINULIWA BILA KUSHUKA CHINI

#01. KUMBUKA MUNGU ALIPOKUTOA NA NAMNA ALIVYOKUINUA.

Mungu aliwapa amri  ya kumkumbuka ili wabaki kwenye kuongezwa, sababu alijua mwanadamu huwa anakumbuka akiwa hana, ila akipata anasahau; anasahau alipotoka, anasahau namna alivyofika alipo, na hasa anasahau aliyemuinua, hata akijitazama anaona ni kwa uwezo wake na ubora wake amefika pale.

KUMB 8:2, 12-14 ___Musa anawaambia Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa,

12 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;

13 na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau BWANA, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

Watu wengi wasipokuwa na kazi wanamtafuta Mungu, wakiwa hawana biashara, hawana mume, lakini wakipata basi wanatumia kazi, mume, biashara kama kisingizio kuwa hawawezi tena kuja kanisani kumtafuta Mungu. Wanasahau kuwa Mungu aliyewapa alijua kuwa huwezi firisika kama utampa muda. 

Hakuna mtu anaweza firisika kwa kumpa Mungu muda.


#02. MUNGU ANATUPELEKA JANGWANI KUTUFUNDISHA UNYENYEKEVU.

Shika hili Mungu anatuongozwa njia ya jangwani ili kutupeleka kwenye mafanikio, ili tujue kuwa Yeye ndiye mpaji wetu. Kuna watu jangwani wanafikiri ni wakati ambao hauna kitu cha kula wala kuvaa, hapana huyo siyo Mungu ni shetani kemea kwa Jina la YESU.

Mungu anatupeleka jangwani ili atuonyeshe kuwa yeye ni mpaji ___yaani anatuongoza sehemu ambayo tunakuwa hatuna uwezo wa kupata chakula wala mavazi kwa uwezo wetu alafu yeye anatupatia vyote hivyo na kuzidi bila hata juhudi zetu. Anafanya hivyo ili tujue kuwa yeye ndiye mpaji wetu.

KUMB 8:2, 3 Musa anawaambia Israel__

2 Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.

3 Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.

Israel walichukua miaka 40 kujifunza kuwa Mungu ni mpaji sababu walitaka sana kutumia nguvu zao. 

Kama utajifunza mwaka huu kuwa Mungu wako ndiye mpaji, na ya kuwa utakumbuka amri zake na kumkumbuka wakati wa kuongezeka, utakumbuka kuwa wakati upo jangwani ndiye alikulisha na halo ulipofika si kwa uwezo wako, basi atakuinua, Musa anasema alikujaribu ayajue ya moyoni mwako,

Kumbe kuna wakati Mungu anatupeleka sehemu ambapo tutakosa vitu, lakini atafanya tule tuvae ili ajue mioyo yetu kama itasema asante na kumtazama yeye peke yake bila kulalamika bali kuamini kuwa Yeye ndiye mpaji wetu. 


#03. TUNATAKIWA KUMKUMBUKA MUNGU SABABU YEYE NDIYE ATUPAYE NGUVU YA KUPATA UTAJIRI.

Nguvu ya kupata utajiri ni pamoja na ufahamu, nguvu, baraka, neema, kibali, na afya. Vyote hivi ni Mungu ndiye atupaye. Maana yake unatakiwa kumkumbuka sababu yeye ndiye atoaye hizo nguvu za kupata utajiri. 

KUMB 8:13, 14 __Musa anasema;

13 na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau BWANA, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

Musa anaongea kuhusu kutuongeza, kumbe kuna wakati Mungu ataanza kutuongeza. Neno linasema usimsahau BWANA Mungu wako. Kwanini, kwa sababu maongezeko huwa yanasababisha ulevi wa vitu, majigambo, na ubize __ mali ikiongezeka ina tabia ya kuchukua nafasi ya Mungu.

Kwanza lazima ujue Mungu hayupo kinyume na wewe kuwa tajiri ndiyo maana anatoa nguvu ya kupata utajiri, ila hataki mali ichukue sehemu yake; ndiyo maana anayemkumbuka wakati wa kuongezwa huwa anamuongeza zaidi.

Mungu sasa anakuongeza ndiyo maana ulichonacho leo hukuwa navyo jana, sasa kama utamkumbuka Mungu kwa maongezeko madogo basi atakuongeza sana na sana. 


#04. KUMKUMBUKA KUNAFANYA IMARA AGANO LA KUINULIWA.

KUMB 8:18 Musa Anaweka wazi __Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Anasema ili alifanye imara agano lake. Kumbe kumkumbuka ndiko kunaleta kufanywa imara agano la kuongezeka. 

Kuongezwa ndiko kunaleta kuinuka. Ana maanisha anakuongeza sawa, lakini usiridhike, mkumbuke hapo atafanya imara zaidi hilo agano lake la kukuongeza. Maana yake ndipo utaendelea kuongezeka na kuongezeka.

Galatia 3:9 __ Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

Baraka ya Ibrahimu ni kuongezwa na kuzidishwa, lakini utaona Ibrahimu alishika agano, na kwa kushika kwake agano aliinuka siku zote bila kushuka chini.

2 Kor 9:8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Kumbe Mungu huwa anatujaza neema ili tukiwa na riziki tuzidi kuteda mema. Maana yake Mungu anakuongeza kidogo kwanza ili apime moyo wako, bidii yako ya kumkumbuka na kumuweka mbele inakupa kukuongeza siku hata siku.


Ubarikiwe Sana, Fanyia kazi haya uliyosoma hakika utaona Kubarikiwa Sana. 

MAOMBI

Eh! Mungu Baba nisaidie siku zote hata wakati nikiongezeka nisikusahau wewe, uniweke sehemu ya kuinuliwa na wewe siku zote. 

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827, pastorulenje@outlook.com 



Sunday, January 15, 2023

SIKIA SAUTI YA MUNGU, KUINULIWA NA BWANA NI FUMBO

 SOMO LA TATU LA KUINULIWA


SIKIA KWA BWANA, KUINULIWA NI FUMBO.


Mith 25:2, 

Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.

1 Sam 8:30

Daudi akauliza kwa BWANA, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote.


Nikupe Mifano Miwili, Uone Kuwa Kuinuliwa na Mungu ni fumbo...


1) HAUJUI SEHEMU YA KUINULIWA KWAKO.

Yusufu angeweza kudhania au yawezekana aliwahi kudhania kuwa atainuliwa kupitia Potifa, au yawezekana aliamini pale ameshainuliwa. Kwa sababu Potifa alikuwa akida wa Farao na mkuu wa askari, na kama aliweza kumfunga Yusuph kwenye gereza la mfalme maana yake alikuwa mtu mwenye cheo. 

Lakini Mungu anamuinua Yusufu kutokea gerezani na siyo kwa Potifa.

Usikate tamaa kwa sababu hujui mbinu ambayo Mungu anataka kuitumia ili akuinue, kwa sababu hujui sehemu gani Mungu anataka kukuinua, unaweza fikiri anakupeleka gerezani kumbe ndiyo anakupeleka sehemu ya kukuinua, unaweza fikiri anakupeleka chini kumbe anakupeleka sehemu ya kuinuliwa kwako.


2) KUNA WAKATI VITA NDIYO SEHEMU YA KUINUKA KWAKO.

1 Sam 15, 17, 27 (8-9), 30.

Ukisoma hiyo mistari utaona maadui ambao aliwaacha Sauli ndiyo Daudi anawapiga, Lakini kumbuka hawa ndiyo waliomshusha Suali, leo wanakuja kama Maadui. Daudi anauliza niwafute. Mungu anamwambia nenda. 

Daudi alipokewa na Sauli vizuri, akapendwa na Yonathani kama anavyopenda roho yake, lakini haikuwa sehemu ya kuinuka kwake, bali viliinuka vita, akachomewa nyumba, na wake zake wakatekwa. Kumbe Mungu alileta maadui zake, ambao Sauli aliwaacha ukiwapiga ni sehemu ya kuinuka kwako. 

Kupitia Amaleki Yoshua aliinuka na kujulikana kuwa anafaa, leo Daudi anainuka kupiga maadui ambao Sauli aliwaacha. 

Lakini yatufundisha Sehemu ambapo wengine wanaacha wewe muulize Bwana kwanza, yawezekana hizo changamoto zinazofanya wengi waache ni Adui za Bwana, Bwana anataka ushinde ili akupe kuinuliwa.

Walichoshindwa wao ndiyo sehemu ya kuinuka kwako (I am your replacement) ukishindwa kuomba mimi naomba, ukishindwa wachawi mimi naondoa, ukishindwa kufunga mimi nafunga, wakati unalala mimi naomba…

NINI CHA KUFANYA ILI KUCHUNGUZA SIRI YA KUINULIWA


I. FUNGUA MOYO WAKO KWA ROHO MTAKATIFU

1 KOR 2:9-10

9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

Kama kuinuliwa ni fumbo, na Roho ndiye pekee anaweza kukujulisha siri hiyo, kwa sababu yeye anayajua mafumbo ya Mungu.

Katika siku yako, tenga angalau asilimia 10 ya masaa yako 24 ukae na Roho Mtakatifu, Yeye atakujulisha siri ya kuinuliwa kwako.

Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani. MWA 41:16

Yusuph alisaidiwa na Roho Mtakatifu kumtafsiria Farao ndoto, na ndiyo ikawa point yako ya kuinuliwa.

Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake? MWA 41:38


II. TAZAMA ISHARA YA KUINULIWA

1 FAL 19:19, MWA 40:1-3

Mungu anapotaka akuinue, kwanza anatuma ishara, alipotaka kumuinua Musa, kwanza alimtumia ishara ya kijiti kikiwaka moto bila kuteketea.

Mungu alipotaka kumuinua Elisha, kwanza alimtumia ishara, Eliya akamfata na kumtupia vazi lake. Na Elisha alipoona akajua kabisa kuwa ni ishara ya kuchukua nafasi ya Eliya ya kuwa nabii wa kimataifa. Kwa sababu watumishi wa Mungu walipewa vazi maalumu na Mungu kama ishara ya nafasi zao.


III. OMBA UNAJISIKIA AU HAUJISKII

YER 33:3

Hatuombi kwa sababu tunajisikia, bali unajisikia aua haujisikii inatakiwa kuomba. Yesu hajasema mtakapojisikia kuomba, bali alisema ombeni.

Biblia inasema

Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

Utakapoamua kumuita Mungu na kumuita zaidi, Mungu atakuonyesha makubwa na magumu usiyoyajua. Usiyoyajua ni sehemu ya fumbo la kuinuliwa kwako. Huwezi kuonyeshwa makubwa na Mungu alafu ukaishi maisha ya chini.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827 

pastorulenje@outlook.com 


Nifatirie zaidi katika mitandao ya kijamii kama...

Pastor Ulenje 


JITIE NGUVU KATIKA BWANA ILI KUINULIWA NA BWANA

 SOMO LA PILI LA KUINULIWA NA MUNGU


JITIE NGUVU KATIKA BWANA, INUKA


1 SAMWELI 30:1-8

Kujitia nguvu katika Bwana ni kukumbuka ya kwamba yupo Mungu ambaye naweza nikamtegemea, yupo Mungu ambaye nikimtafuta atanipigania na kunipa ushindi.


KWANINI UJITIE NGUVU KATIKA BWANA?


1. KWASABABU BWANA AMETUHIFADHI HAI.

Wakati wa changamoto zote, unachokihitaji hasa ni kuwa hai, kwa sababu ukiwa hai unaweza kugeuza yote uliyokutana nayo kuwa ushuhuda. Kwa sababu majaribu hayawezi kukuharibu kama bado una uhai wa kuendelea kujaribu. 

Pamoja na yote tuliyokutana nayo, ila Bwana alihakikisha yanatuliza, yanatuumiza, yanatuvunja moyo ila hayatuuwi. Siyo kwamba hayakuwa na nguvu ya kutuuwa, ila kwa sababu Bwana alikuwa upande wetu kuhakikisha tunaishi, ili siku moja tuje kusema Farasi na mpanda Farasi aliwatupa baharini. 1 Sam 27:8,9.

Pamoja na yote Daudi aliyokutana nayo, Bwana alihakikisha Suali hamuuwi, alihakikisha Wafilisti hamuuwi, alihakikisha Waamaleki hamuuwi_ kwanini kwa sababu Bwana alitaka kuyageuza yote aliyopitia kuwa kitabu cha SIFA CHENYE SURA nyingi kuliko zote kwenye Biblia 150. 

Biblia inasema Mhubiri 9:4 Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);

Maadamu Una Uhai, Bado Lipo Tumaini, Inuka Jitie Nguvu Katika Bwana.


2. KWA SABABU MACHOZI TULIYOLIA HAYAJATUTOA TULIPO TEKWA.

Daudi na wenzie mianne wakainua sauti zao na kulia, siyo tu walilia, bali waliinua sauti zao na kulia mpaka walipokuwa hawana nguvu za kulia tena; lakini majibu hayakutokea. Wakaanza kumlaumu Daudi lakini lawama hazikuwasaidia.

Mungu ameweka machozi ili kutujulisha kwamba kuna jambo la uchungu, ila siyo njia ya kututoa kwenye uchungu. Mungu ameweka machozi ili watu wajue kuwa upo matekani, ila siyo ya kukutoa kwenye mateka. Kama umeamua kulia ni bora ulie kuinuka kwa mkono wa Bwana ili siyo ulie kuonyesha namna unapitia. Adui amekuteka ili ulie, unapolia unampa sifa kuona amekuweza. Daudi akainuka, akajitia nguvu katika Bwana, ndipo ukombozi wao ukapatikana. 


Kama machozi hayajakupa matokeo, Leo inuka Jitie Nguvu katika Bwana, Mungu wako Anakusubiri umalize kulia na kulalamika ili Akusaidie. 

Wakati Daudi na wenzie wanalia, Mungu alikuwa akiwatazama, ila Daudi alipojitia nguvu, Mungu akainua mkono wake na kuwainua na hapo ukawa mwanzo wa Daudi kuwa Mfalme na wenzie kuwa majemedari wa jeshi na wakuu wa Israel ambao hapo kwanza walimfata Daudi sababu walikuwa na njaa na madeni.


3. KWA SABABU BWANA AMEHAKIKISHA TUNABAKIWA NA NAIVERA.

Wakati adui anateka vyote kuhani tulibakiwa naye, na naivera nayo ikabaki. Naivera lilikuwa ni vazi la kikuhani, ambalo kuhani alivaa anapojihudhurisha kwa Bwana, na ni vazi lilibeba majina ya makabila ya wana wa Israel. 

Adui ameiba vyote, ila damu ya Yesu bado tunayo, ambayo haishindwi kwa dhambi zetu, haishindwi kwa nguvu za adui, haishindwi kwa nguvu ya pesa, adui ataiba vyote ili naivera bado tunayo, vazi la damu ya Yesu bado tunalo ambalo kwa hilo tunasogea mbele za Mungu wetu na kupokea nguvu mpya ya kumshinda adui aliyetushinda.

Ebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

Maadamu bado una vazi la damu ya Yesu, Acha kubaki chini, Jitie nguvu katika BWANA 2023, inuka.


4. JITIE NGUVU KATIKA BWANA KWA SABABU UKIFUATA UTAYAPATA. 

Daudi alipoacha kulia na kujitia nguvu katika Bwana, ndipo Bwana anamwambia, Inuka_ Ukiwafuata utawapata na utawapokonya yote waliyoiba, yote waliyochukua. Kumbe tunayofikiri hayawezi kuisha, yanaweza kuisha, yale tunasema hatuwezi kupita, tunaweza kupita, yale tunawaza hayawezi kutuachia, yanaweza kutuachia; 

Lakini kama tutainua imani, na kujitia nguvu katika Bwana, basi tutavipata. Kwa nini, kwa sababu Bwana ameshaondoa nguvu zilizo juu yao.

Yoshua na Kalebu wakawaambia makutano; Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope. Hesabu 14:9.

Unayoyaogopa yameondolewa nguvu zake, unayosema yanakutesa, yanakuliza, ni magumu, huwezi kutoka; yameondolewa nguvu zake_ tatizo siyo yenyewe tena, tatizo ni wewe hutaki kuinuka na kuyafuatia. Ukiyafuatia utayapata_ Ukiinuka na kupigana utashinda.

Kumbe tunavyohofu hatuwezi kuvipata, hatuvipati kwa sababu tunahofu ya kutokuvipata, kumbe kesho tunayohofu itakuwa mbaya, siyo kwamba ilitakiwa kuwa mbaya, inakuwa mbaya ni kwa sababu hatujaifuta tumeacha siku zote itufate sisi, YESU anasema 

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Math 6:34.

Kesho imewekwa ijisumbukie yenyewe, wewe ifuate kwa imani, maovu ya leo yasikukatishe tamaa maana siku inatosha kwa maovu yake.

Bado Lipo Tumaini, Kama utajitia nguvu katika Bwana, Utawapata Hakika


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

pastorulenje@outlook.com 

Nifatirie kupitia mitandao ya Kijamii 

Tiktok, Facebook, Youtube na Instagram kwa Jina la Pastor Ulenje.



MAANA YA KUINULIWA NA MUNGU

SOMO LA KWANZA LA KUINULIWA NA MUNGU.

MAANA YA KUINULIWA

 1. MTU ALIKUWA CHINI UNAMSIMAMISHA 

Mtu ambaye yupo chini  ni yule ambaye ni daraja la mwisho mbele ya wengine, katika uchumi, maisha yake, uzima wake au historia yake, au familia aliyotoka, Mungu anampeleka kiwango cha juu, anampa historia, anampa heshima na daraja la juu. 

Mfano mzuri ni Daudi alitoka kuchunga kondoo, akafika kuwa na jeshi la watu minne, akafika kuwa mfalme wa Yuda, akafika kuwa mfalme wa Israel, akakuwa kuwa baba wa mfalme wa wafalme na Mungu akamwambia jina lake litabaki milele katika Uflme wa Israel. 

Lakini Bwana alipomuita, aliinuka na kumpiga Goliathi, na BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Zaburi 78:70-71.


2. MTU ALIKUWA CHINI SANA UNAMSIMAMISHA. 

Kuna watu wako chini sana kiwango ambacho hata aliye chini anamuona yuko chini, kiwango ambacho hata wewe mwenyewe unajikatia tamaa, hata Mungu akitaka kukuinua unamcheka kuwa hutoweza kuniinua kwa kiwango hiki cha chini, kisha Mungu anakuja anakuinua. 

Mungu anawasimamisha. Mfano mzuri ni Musa, kwa sababu alikuwa kiwango cha chini sana kiwango cha kwenda kufanya kazi kwa baba mkwe, mwanaume kufanya kazi kwa baba mkwe, ni kiwango ambacho hata masikini atakuona upo chini na atakudhalau, 

Ndiyo maana Mungu alipokuja kumuinua alikataa hata Mungu, ikamlazimu Mungu atumie ishara nyingi kumthibitishia lakini bado hakuamini, ila alipoinuka na kwenda Mungu aliposema, BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Kutoka 3:14-15


3. MTU AMEDONDOKA UNAMSIMAMISHA. 

Mtu ambaye alikuwa amesimama, kila kitu kinaenda vema, na kila mtu anampa heshima na amekuwa mtu mkuu, kisha katika njia ya maisha anadondoka, watu wanamkatia tamaa, kisha Bwana anakuja anamuinua na kuwa na uwezo wake wa zamani.

Mfano mzuri ni Samsoni, alikuwa mtu mkuu katika nchi yake, ameuwa simba, kauwa majeshi ya wafilisti na nchi yake ikampa heshima kama mwamuzi wao, lakini akadondoka mpaka kuwa kiwango cha chini mpaka kuwa kipofu, ila alipoinuka na kuomba toba mbele za Mungu, BWANA AKAMUINUA.

Soma ___Waamuzi 16:28-29


3. WEWE MWENYEWE KUINUKA HUWEZI 

Kuna mtu yuko chini kiwango ambacho hawezi kuinuka pale anapopewa nafasi ya kuinuka, kwa sababu imefika ameshajihesabia kuwa yeye ni wa chini na wengine ni wa juu. 

Mfano ni yule mtu aliyekuwa kiwete toka tumboni, hajawahi kusimama kwenye maisha yake, alafu leo Petro anamwambia simama, naamini hakuamini_ mpaka Petro akaamua kumsaidia kuinuka, naamini kwako ambae unaona huwezi inuka, inuka kwa maneno haya na BWANA ATAKUINUA kwa sababu naamini amenituma kwa ujumbe huu uinuke.

Soma ____Mdo 3:1-8


4. MTU ALIYEKATA TAMAA KUINUKA ALAFU ANASIMAMISHWA. 

Kuna mtu amejaribu mara nyingi, mara nyingi na mara nyingi tena na tena kusimama na akashindwa, alafu Bwana anakuja kumuinua.

Mfano ni aliyekuwa hawezi katika birika la kwenye mlango wa kondoo, birika la Bethzatha, amejaribu kuinuka kwa miaka 38 ni miaka mingi sana, malaika anapokuja anajaribu kuinuka ajitupe kwenye birika hawezi, mpaka watu wamemkatia tamaa naye akajikatia tamaa kwa sababu amejaribu mara kwa mara, lakini Yesu anamwambi simama, jitwike godoro lako uende. Aliposimama, BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Yoh 5:1-8


5. MAANA YAKE NI KUWA CHINI SIYO MWISHO WA MAISHA. 

Kama Mungu alimuinua Daudi aliyekatiwa tamaa na baba yake, kama Mungu alimuinua Musa aliyejikatia tamaa yeye mwenyewe, Samsoni ambaye taifa lilimkatia tamaa, mtu ambaye hata kuinuka mwenyewe hakuweza, mtu dhaifa kiwango cha kujaribu kuinuka miaka 38 asiweze, Sarah aliyekaa bila mtoto miaka 85 mpaka alipoambiwa utazaa akacheka__ LIPO TUMAINI KWAKO LA KUINUKA.

Lakini pia mwambie mtu yeyote “Usinikatie tamaa tafadhali, BWANA ANAWEZA KUNIINUA. Lakini pia na wewe jiambie “Usijikatie tamaa tafadhali, BWANA ANAWEZA KUNIINUA. Waambie watu wasikuandika MWISHO, Wala wewe Usijiandika MWISHO… Maadamu unaishi BWANA ANAKUINUA. 


KANUNI ZA MSINGI KUINULIWA 2023

1. Mkumbuke BWANA MUNGU wako. 
     Mh 12:1, Kumb 8:18 

2. Kuwa na imani ya KUINUKA. 
    Math 9:6-7 

Mimi ni Pastor Ulenje 
+255 683 477827 
pastorulenje@outlook.com 

Follow me kupitia 
Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama Pastor Ulenje. 

Wednesday, January 11, 2023

 DHANA HALISI ZA MAFANIKIO

(PRECEPTS TO SUCCEED)

The Original Concepts for Personal Success


Dhana ni wa wazo kuhusu jambo fulani.

Natamani tuone wazo halisi kuhusu Mafanikio. 

Na wazo halisi kuhusu mafanikio tunalipata kwa Mungu. Wazo halisi ni la muhimu sana sababu ndilo linakupa mafanikio halisi.

Mafanikio unaweza kuyapata kwa namna yoyote, na watu wakahisi umefanikiwa na kumbe ni mafanikio feki, tutakuja kuona ufupi wa furaha ya maisha yako na mwisho wako.

Mwaka huu mpya natamani twende kwenye mafanikio halisi, mafanikio ambayo yanatokana na baraka ya Bwana, ambayo haichanganyikani na majuto ndani yake. Binafsi leo naweka agano la kuzifata.

Kwanza naomba ijurikane sisi wana wa Mungu, ni watoto wa Mungu ni mawakili wa ufalme wa Mungu, hivyo tupo duniani kumuwakilisha Mungu, tupo duniani kuwavuta watu wa duniani waje kwenye ufalme wetu. 

Na njia kuu ya kufanya hivyo, ni kutumia kanuni zetu za mafanikio kw usahihi na bidii ili watu wa ulimwengu huu wakiona, watamani kufata kanuni zetu na kuingia kwenye ufalme wetu. Lakini kama tutafanikiwa kwa njia zao, basi hatutakuwa na sababu yoyote ya kuwavuta wao kwetu.


Tunapomaliza mwaka 2022 kuingia mwaka 2023 dalili zimeonekana wazi kwa Tanzania na dunia kuwa uchumi unazidi kushuka, hata Oxford Economics yenye jopo la wachumi 300 wamefanyia utafiti nchi zaidi ya 200 na kuona uchumi unashuka toka pato la 3% mpaka 1.3%. kwa namna hii tunahitaji kanuni za Mungu ili kuwa salama


Jiandae kutembea na kanuni za Mungu ambazo hazitashindwa.


1.   MFANO WA MUNGU 

   ðŸ‘‰ ILI KUTAWARA

Biblia inasema katika 

Mwa 1:26 na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyaa, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho chini ya nchi 

na Sura ya 27 inaweka wazi kuwa Mungu akaumba mtu kwa mfano wake. 

Mungu alimpa mwanadamu cha kwanza ni mfano wake na sura yake, ndipo akasema wakatawale. 

Kutawala ndiyo siraha ya kwanza mwanadamu kufanikiwa, kama ukitawala katika huduma umefanikiwa, ukitawala katika biashara umefanikiwa, ukitawala kazini umefanikiwa. Kwa sababu ili ufanikiwe lazima watu wakujie, na ukitawala maana yake watu wanakujia kupokea bidhaa yako au huduma yako, hapo umefanikiwa


Lakini ili upate utawala wa kweli, sifa ya kwanza ni lazima ufanane na Mungu. Kufanana na Mungu ni katika nia ya ndani, katika nia ya matendo yake, na namna ya kuishi binafsi na watu wengine. Na hasa aliongelea utu wa ndani.

Paulo anasema katika 

Efeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Tuliumbwa katika Kristo, sababu kule kuumbwa kwa kwanza kwa lile kosa la adui kulitufanya kuharibika. Siyo muonekano wa nje, bali ndani. Na anaonyesha kuna matendo Mungu aliyaweka tangu awali, ambayo sababu ya anguko mwanadamu akawa hawezi tena kuyafanya.

Yesu anasema zamani haikuwa hivi, ila sababu ya ugumu wa mioyo yenu.

Ukisoma 

Efeso 4:24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. 

Ukisoma tena Kolosai 3:10 Paulo anasema mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

Kama tunataka kufanikiwa katika uchumi, dhana ya kwanza kabisa ni kuwa watawara, kutawala katika mauzo ya biashara zetu, kutawala kazini, kutawala katika huduma. 

Mwa 17:1-5 Mungu anamwambia Ibrahimu, Mimi ni Mungu mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. Abramu akanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi.  

Mungu alipomwambia awe mkamilifu alimaanisha awe afanane na yeye, awe tofauti na wanadamu. Na Ibrahim alipoanguka kifudifudi ishara kukubali, Mungu akwambia sasa nitafanya agano la kukupa kutawara.

Na Yesu anatuamuru tuwe tofauti na watu wengine katika Math 5:48 ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu


2.   PUMZI YA UHAI.

  👉 HAPO UTAWEZA FANYA CHOCHOTE.


Biblia inasema 

Mwa 2:7 Bwana akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Neno la msingi hapo ni mwanadamu akawa nafsi hai. Maana yake ile pumzi ya uhai ndiyo ikamfanya kuwa nafsi hai. Mtu asiye hai hawezi kufanya chochote. Adamu alipokufa kiroho ndipo mahangaiko ya mwanadamu yalianza. 

Lakini inaonyesha uhai wa mwanadamu unatoka kwa Mungu, mwanadamu hawezi chochote pasipo Mungu, mwanadamu pasipo Mungu kinachofata ni mahangaiko tu. 

Utaona mwanadamu alipopewa pumzi ya uhai akawa nafsi hai ndipo Bwana anampa kazi sasa ya kufanya. Kazi ni jukumu la kukuletea pesa, kukuletea mafanikio lakini huwezi fanya kazi pasipo ile pumzi ya uhai, mwisho wake ni mahangaiko,  

Kinachofanya wengi wasipate mafanikio ni kwa sababu wanahangaika na kazi, wanaacha walichopewa ili kufanikisha kazi. Na wengine wanapata mafanikio feki ambayo mwisho wake ni mauti.

Ibrahimu baada ya kutembea sana kuendea nchi ambayo Bwana atamuaonyesha. Mwanzo 12:7 Bwana anamwambia uzao wako nitawapa nchi hii. Kabla hata ya kuanza kuilima wala kujenga hema, akamjengea Madhabahu BWANA aliyemtokea, mstari wa 8 unasema ...akaliitia jina la BWANA.

Hii ilimaanisha Ibrahimu alijua, sawa Mungu amenipa sehemu ila lazima nimtake Yeye kwanza ambaye ndiye pumzi ya uhai ili nifanikiwe katika hii nchi...

Yesu amekaa miaka 30 bila kuanza kazi aliyoijia mpaka aliposhukiwa na Roho mtakatifu Luka 3:22-23. Neno la Bwana linamjia Zakaria kwa Zerubabeli Zekaria 4:6 kusema Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.

Wakati kanuni za dunia zimeshindwa, na umezijaribu sana, 2023 kaa chini na Roho Mtakatifu kwanza muulize nini nifanye, pili mshirikishe katika kila unalofanya. Ufanye 2023 siyo mwaka wa kujaribu bali wa kufanya. Baada ya Israel kuzunguka miaka 40 mlima Seiri, sauti ya Bwana ikamjia Musa peteni njia hii (Kumb 2:1-3). 

Weka mkazo sana katika kumtaka Bwana 2023 zaidi ya miaka yote, taka sana ufalme wake na haki yake, yale ambayo wengine wanayasumbukia hawayapati au wanatumia njia ya udhalimu kuyapata, wewe Mungu atakupa kibali na kukuweka katika nafasi ya kuyapata.


3.   BARAKA ZA BWANA.

 ðŸ‘‰ ILI UONGEZEKE


Baada tu ya mwanadamu kuwa nafsi hai, Mungu akambariki. 

Mwanzo 1:28 Biblia inasema Mungu akawabarikiwa, Mungu akawaambia Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini,na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Nikwambie tu wazi unahitaji baraka za Bwana kuliko unavyoweza ukafikiri. 

Watu wengi wanapenda kuongezeka, wanapenda kuzaa vitu, kuanzisha biashara, kampuni na wanataka waende dunia nzima pasipo baraka za Bwana. 

Baraka ni uwezesho wa Mungu ndani ya mtu wa kufanikiwa. Baraka ni kibali cha Mungu, ni neema.

Mtu aliyebarikiwa, ile baraka inampa kufanikiwa katika kila analogusa. Haina maana hatokutana na changamoto, ila ile baraka inampa ulinzi na kushinda.

Biblia inaweka wazi mtu aliyebarikiwa atakuwa tajiri, Mith 10:22 inasema Baraka ya Bwana hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo. 

Katika agano jipya 

Efeso 1:3, 4, Paulo anasema Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo. Kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo

Hilo neno kama na neno ili tuwe linaunganisha kuonyesha Kumbe kuwa mtakatifu, kuwa mtu usie na hatia mbele zake inaambatana kabisa na baraka zetu kutenda kazi, ndiyo maana hata Adamu utakatifu ndiyo ulilinda baraka yake.  

Ndiyo maana utaona baada ya Bwana kumaliza kumuumba mtu, na kumpatia baraka zote akampa Discipline. Adabu, akamwambia utaishi ndani ya bustani lakini kwa mipaka, kula miti yote lakini miti fulani usile. 

2023 jiandae kuishi kwa mipaka, ishi maisha ukifanya unayopaswa kufanya, achana na yale ambayo yanakuondoa kwenye reli, kwa maana yaliyofanya mpaka sasa una struggle ni kutoishi kwa mipaka.

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827 

FOLLOW ME KWA; 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram 

Kama Pastor Ulenje.


 



MAANA YA KUJITIA NGUVU KATIKA BWANA, INUKA

JITIE NGUVU KATIKA BWANA, INUKA.


1 SAMWELI 30:1-8

Kujitia nguvu katika Bwana ni kukumbuka ya kwamba yupo Mungu ambaye naweza nikamtegemea, yupo Mungu ambaye nikimtafuta atanipigania na kunipa ushindi.


KWANINI NIJITIE NGUVU KATIKA BWANA.


1.     KWASABABU BWANA AMETUHIFADHI HAI

Wakati wa changamoto zote, unachokihitaji hasa ni kuwa hai, kwa sababu ukiwa hai unaweza kugeuza yote uliyokutana nayo kuwa ushuhuda. Kwa sababu majaribu hayawezi kukuharibu kama bado una uhai wa kuendelea kujaribu. Pamoja na yote tuliyokutana nayo, ila Bwana alihakikisha yanatuliza, yanatuumiza, yanatuvunja moyo ila hayatuuwi. Siyo kwamba hayakuwa na nguvu ya kutuuwa, ila kwa sababu Bwana alikuwa upande wetu kuhakikisha tunaishi, ili siku moja tuje kusema Farasi na mpanda Farasi aliwatupa baharini. 1 Sam 27:8,9.

Pamoja na yote Daudi aliyokutana nayo, Bwana alihakikisha Suali hamuuwi, alihakikisha Wafilisti hamuuwi, alihakikisha Waamaleki hamuuwi_ kwanini kwa sababu Bwana alitaka kuyageuza yote aliyopitia kuwa kitabu cha SIFA CHENYE SURA nyingi kuliko zote kwenye Biblia 150. 

Biblia inasema Mhubiri 9:4 Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);


Maadamu Una Uhai, Bado Lipo Tumaini, Inuka Jitie Nguvu Katika Bwana.


2.     KWA SABABU MACHOZI TULIYOLIA HAYAJATUTOA TULIPO TEKWA.

Daudi na wenzie minne wakainua sauti zao na kulia, siyo tu walilia, bali waliinua sauti zao na kulia mpaka walipokuwa hawana nguvu za kulia tena; lakini majibu hayakutokea. Wakaanza kumlaumu Daudi lakini lawama hazikuwasaidia.

Mungu ameweka machozi ili kutujulisha kwamba kuna jambo la uchungu, ila siyo njia ya kututoa kwenye uchungu. Mungu ameweka machozi ili watu wajue kuwa upo matekani, ila siyo ya kukutoa kwenye mateka. Kama umeamua kulia ni bora ulie kuinuka kwa mkono wa Bwana ili siyo ulie kuonyesha namna unapitia. Adui amekuteka ili ulie, unapolia unampa sifa kuona amekuweza. Daudi akainuka, akajitia nguvu katika Bwana, ndipo ukombozi wao ukapatikana. 

Kama machozi hayajakupa matokeo, Leo inuka Jitie Nguvu katika Bwana, Mungu wako Anakusubiri umalize kulia na kulalamika ili Akusaidie. Wakati Daudi na wenzie wanalia, Mungu alikuwa akiwatazama, ila Daudi alipojitia nguvu, Mungu akainua mkono wake na kuwainua na hapo ukawa mwanzo wa Daudi kuwa Mfalme na wenzie kuwa majemedari wa jeshi na wakuu wa Israel ambao hapo kwanza walimfata Daudi sababu walikuwa na njaa na madeni.


3.     KWA SABABU BWANA AMEHAKIKISHA TUNABAKIWA NA NAIVERA.

Wakati adui anateka vyote kuhani tulibakiwa naye, na naivera nayo ikabaki. Naivera lilikuwa ni vazi la kikuhani, ambalo kuhani alivaa anapojihudhurisha kwa Bwana, na ni vazi lilibeba majina ya makabila ya wana wa Israel. 

Adui ameiba vyote, ila damu ya Yesu bado tunayo, ambayo haishindwi kwa dhambi zetu, haishindwi kwa nguvu za adui, haishindwi kwa nguvu ya pesa, adui ataiba vyote ili naivera bado tunayo, vazi la damu ya Yesu bado tunalo ambalo kwa hilo tunasogea mbele za Mungu wetu na kupokea nguvu mpya ya kumshinda adui aliyetushinda.

Ebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.


Maadamu bado una vazi la damu ya Yesu, Acha kubaki chini, Jitie nguvu katika BWANA 2023, inuka.


4.     UKIFUATA UTAYAPATA. 

Daudi alipoacha kulia na kujitia nguvu katika Bwana, ndipo Bwana anamwambia, Inuka_ Ukiwafuata utawapata na utawapokonya yote waliyoiba, yote waliyochukua. Kumbe tunayofikiri hayawezi kuisha, yanaweza kuisha, yale tunasema hatuwezi kupita, tunaweza kupita, yale tunawaza hayawezi kutuachia, yanaweza kutuachia; Lakini kama tutainua imani, na kujitia nguvu katika Bwana, basi tutavipata. Kwa nini, kwa sababu Bwana ameshaondoa nguvu zilizo juu yao.

Yoshua na Kalebu wakawaambia makutano; Hesabu 14:9. Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope. 

Unayoyaogopa yameondolewa nguvu zake, unayosema yanakutesa, yanakuliza, ni magumu, huwezi kutoka; yameondolewa nguvu zake_ tatizo siyo yenyewe tena, tatizo ni wewe hutaki kuinuka na kuyafuatia. Ukiyafuatia utayapata_ Ukiinuka na kupigana utashinda.

Kumbe tunavyohofu hatuwezi kuvipata, hatuvipati kwa sababu tunahofu ya kutokuvipata, kumbe kesho tunayohofu itakuwa mbaya, siyo kwamba ilitakiwa kuwa mbaya, inakuwa mbaya ni kwa sababu hatujaifuta tumeacha siku zote itufate sisi, YESU anasema 

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Math 6:34.

Kesho imewekwa ijisumbukie yenyewe, wewe ifuate kwa imani, maovu ya leo yasikukatishe tamaa maana siku inatosha kwa maovu yake.


Bado Lipo Tumaini, Kama utajitia nguvu katika Bwana, Utawapata Hakika.


Mimi ni Pastor Ulenje 

 +255 683 477827 

FOLLOW ME 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama 

PASTOR ULENJE


Tuesday, January 10, 2023

UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU

 UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU


1.    Roho ndiye analishuhudia neno ndani yetu.


Yoh 15:26 Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia

1 Yoh 5:7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli

Tena kuhusu kuokoka Yoh 3:5 Yesu anasema Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, maana yake siyo neno peke yake, Roho lazima awepo ili neno kumuokoa mtu.


2.    Roho ndiye analisema neno la Mungu midomoni mwetu.


Yesu anasema Marko 13;11 msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni; kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu

Kwenye Mathayo 10:20 anasema kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu

Siri ya kufikia hapa ni kujaa Roho Mtakatifu, Biblia inasema kwenye Mdo 4:8 Petro akijaa Roho Mtakatifu, alipoongea wazee wakashangaa mbona hawa watu hawajasoma wametoa wapi ujasiri huu.


3.    Roho ndiye anayekupa uwezo wa kuisikia sauti ya Mungu.


Ufu 1:10 Yohana anasema Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu

Ukisoma Eze 2:2 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami. 

Kumbe muda wote alikuwa hamsikii Yeye aliyesema naye.

Ukisoma Efeso 3:1-6

1 Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;

2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.

5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo 


4.    Roho ndiye anayetupa kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.


Ukisoma 1 Kor 2:9-12 

9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Kumbe yapo ambayo Mungu amekuandalia lakini kuyapata ni lazima Roho apate kukufunulia, la sivyo utaendelea kuteseka ikiwa uliyokirimiwa yapo.

Na siri kubwa ili Roho akufunulie ni kuwa mtu wa Rohoni, anasema katika mstari wa mwanadamu wa tabia ya asili yaani tabia ya mwilini hayapokei mambo ya Roho wa Mungu, kwake ataona ni upuuzi, kwanini kwa sababu yanatambulikana kwa jinsi ya Rohoni.


5.    Roho ndiye anatusaidia kulishika Neno


Eze 36:27 anasema Nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu,nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. 

Ni baada ya Mungu kuona mwanadamu ameshindwa kuenenda katika sheria zake wala kushika hukumu zake wala kuzitenda, ndipo akaweka roho yake ndani yako.

Ukisoma Warumi 7:23-25 Paulo anaonyesha wazi akipambana kuushinda mwili, lakini jibu anasema ni Roho mtakatifu ndiye anaweza kumuweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.


6.    Roho ndiye analithibitisha neno linapofika wakati wake.


Kila ahadi ya Mungu inapofika wakati wa kutimia unaona Roho anatokea kwenye tukio. Kuzaliwa kwa Yesu unaona mariamu anashika ujauzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Luka 1:35.

Ukisoma Mdo 13:2 Paulo anaitwa kuwa mtume wa mataifa, lakini anakaa miaka 11 Antiokia bila kufanya wito mpaka Roho anashuka na kusema sasa ndiyo wakati Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi niliyowaitia.

Siri kubwa waliingia kufunga na kumsifu Mungu, waliingia rohoni, kama wasingeingia rohoni wakati ungewapita. Acha kujichelewesha kwa kupenda sana kuwa ubize, tenga muda wa kuwa rohoni huu ndiyo wakati wa kupiga hatua uliyoisubiri.


7.    Roho ndiye anathibitisha Neno kwa Ishara na Nguvu.


Watu walipoona Yesu anafanya ishara nyingi wakasema akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote... Math 8:16, 

Lakini Yeye anakuja anasema kwenye Sura ya 12 hiyo Math 12:28 Lakini nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu. Kumbe wao waliona neno lake pekee, kumbe neno lake lilichanganyika na Roho Mtakatifu.

Mdo 13:9 Inasema Sauli, ambaye ndiye Paulo akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho yule mchawi akamwambia angalia mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu. Ikawa, kwanini kwa sababu neno lake lilichanganyika na nguvu za Roho.

Ndipo anasema kwenye 1 Thes 1:5 Injili haikuwafikia katika maneno tu, bali katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu.

Kama unataka neno lako liwe na nguvu unapotamka katika maombi, siri ni Roho Mtakatifu, Unataka Neno litokee kwenye maisha yako, Roho ndiye anafanya neno litokee kwako pale unapolitenda.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

Follow me 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama Pastor Ulenje... hakika Utabarikiwa



Tuesday, November 22, 2022

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KWA MKRISTO

 KWANINI TUNAMHITAJI ROHO MTAKATIFU?

Somo la Kwanza


Luka 24:45, Mdo 1:4-5

Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasitoke mjini mpaka wapokee Roho mtakatifu, maana yake ni muhimu sana kwa Mkristo. Yesu alileta ufalme wa Mungu, na alitaka watu kuingia ndani ya ufalme huo. Wanafunzi walipotaka kujua lini atawaletea ufalme, Yesu anasema kuhusu Roho Mtakatifu.

Yesu anamaanisha ili mfanikiwa ndani ya huu ufalme muhimu sana ni Roho mtakatifu.

  • Utaona kabla Yesu hajafanya chochote kwanza alipata Roho mtakatifu

  • Pia utaona anaawaacha wanafunzi wake, pia anawaambia wasitoke mpaka wapokee Roho

  • Na wanafunzi wake, utaona katika mahubiri yao, cha kwanza kabisa mtu akiokoka ni Roho mtakatifu, na ishara yao kubwa kama mtu amepokelewa na Mungu basi ni kupokea Roho Mtakatifu. Mfano mzuri ni habari ya Kornelio


KWANINI TUNAMHITAJI ROHO MTAKATIFU/ UMUHIMU WA RMT

  • ROHO NI MUHIMU KATIKA WOKOVU WETU.

Tunaokoka kwa njia ya Roho mtakatifu.

  • Yoh 3:5-6 tunazaliwa mara ya pili kwa njia ya Roho mtakatifu.

Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

  • Tito 3:5 Roho ndiye anayetufanya upya.

si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;

Roho ndiye anashuhudia kuwa sisi tu watoto wa Mungu

  • Rum 8:16 ndiye anashuhudia pamoja na roho zetu

Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;

Roho ndiye arabuni ya wokovu wetu

  • 2 Kor 1:22 Naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu. Arabuni ni ishara ya kitu kijacho. Muhuri ni dhamana au uthibitisho.

naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.

Tunatunza yale mazuri Mungu aliyotupatia kwa Roho Mtakatifu

  • 2 Tim 1:14 Tunalinda ile amana nzuri kwa RMT. Amana ni akiba nzuri au ya thamani. Pasipo Roho utapoteza kila kitu.

Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu.

Tunamshinda adui kwa Roho Mtakatifu

  • Mdo 1:8 mtapokea nguvu akishawajilia juu yenu RMT. Mfano wa Skewa Mdo 19:14-16. Hawa watu hawakuwa wameokoka, wakatamka jina la Yesu wakijaribu lakini hawakuwa na nguvu.

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

  • Mdo 8:5-7, 5:3-5. Filipo kwa sababu alijaa Roho mtakatifu akashinda nguvu zote za giza, mpaka mganga akasalimu amri.

Tunashinda tamaa za dunia na za mwili kwa RMT

  • Rum 8:13 

kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.

Tunakuwa imara katika wokovu kwa sababu ya Roho Mtakatifu

  • Mdo 4:8, 13 walipotikiswa Roho akawapa hekima ya kujibu kwa ujasiri mpaka mafarisayo wenyewe wakashangaa.

Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli,

Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Pastor Ulenje

+255 683 477827

MOROGORO, TZ.

Saturday, November 19, 2022

MAANA HALISI YA MAOMBI 01.

Mpaka tumejua maombi ni ‘serious task’ kwetu tulio-amini, Hapo tutaanza kuomba. 


 Yesu anasema tukiomba tusipayuke-payuke.

Kupayuka si maneno mengi, kupayuka ni kurusha maneno pasipo shabaha. haikuwa na maana ya kukataa kuomba kwa sauti, ila usifanye hivyo kwa kuamini kuwa sauti huleta ufanisi wa maombi au ndiyo maombi yanakuwa na matokeo. 

Sauti haileti matokea, sauti ni sauti tu. Bali kuomba bila shabaha, bila imani, bali kutamka maneno mengi tu ukifikiri ndiyo kupata majibu, hiyo ndiyo kupayuka. Bali maombi lazima yawe na shabaha, yawe na matarajio. 

Pasipo matarajio hakuna uhakika, pasipo uhakika hakuna imani, pasipo imani hakuna majibu ya maombi, pasipo majibu ya maombi, maana yake bado hujaomba. 

 Swali kwanini Yesu alisema tusipayuke? 

Yesu alitamani tuombe kwa shabaha. Na hii ndiyo siri ya kuombea jambo la mda mrefu, ng’ang’anizi, lililokufata mda mrefu. Unapoingia kuomba ni muhimu kujua kuwa, hitaji lako Yesu alilijua kabla hata ya hitaji kukufikia (Math 6:8, Zab 139: 16), maana Yeye ndiye aliyeziamuru siku kabla hata hazijaja bado. Ndiyo maana akasema “...Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba”

 Mjumuisho wa maneno yote ya mwanzo ndipo tunapata maana ya maombi. Maombi yana nguvu sana kama yakiombwa kwa shabaha. Yaani kuomba ukiwa na matarajio ya kitu fulani kitokee, na ukaomba mpaka kitokee. 

Majibu ya Mungu ni kama bahari, cha kushangaza wengine wanaenda na vijiko, nenda kwa Mungu na matarajio makubwa, matarajio yasiyo na kizuizi cha kutazama uwezo wako bali uwezo wa Mungu usio na kipimo.

 MAANA YA MAOMBI

Kama Yesu anasema Baba Yetu anajua haja zetu kabla hata hatujaomba, kwanini hayashuki TU!?

 Yesu akasema “Basi ninyi salini hivi; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni” (Math 6:9-10). 

 Hivyo tunapoingia kwenye maombi tunaingia kwenye very serious business of God’s Kingdom, kushusha mapenzi ya Mungu ambayo yalishakuwa tayari mbinguni hata kabla siku hizi hazijafika, Mungu alikuwa anakusubiri wewe uyashushe duniani (Muhimu 1Kor 2:9). 

Yesu anawaambia wanafunzi wasalipo, wamwambie MUNGU mapenzi yake yatimizwe, kwanini wakati Mungu si mwanadamu hata a-amuriwe na mtu. 

Hapana “Mungu pasipo mtu hafanyi, na Mtu pasipo Mungu hawezi”. 

Usipotamka nini kitokee duniani Mungu hafanyi bali anasubiri mtu mmoja/wawili/zaidi “aliyeitwa kwa jina lake, ajinyenyekeshe na kuomba, na kumtafuta uso, na kuziacha njia mbaya; basi atasikia toka mbinguni na kuwaamehe dhambi yao, na kuponya nchi yao” (2 Nya 7:14) 

Hivyo; Maombi ni kumruhusu Mungu kuingilia jambo duniani 

Kifupi: Maombi ni kushusha mapenzi ya Mungu duniani.

Usikose Sehemu ya pili ya Somo hili kwenye Blog hii ya ulenje.blogspot.com. 

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827

Morogoro, TZ.


Saturday, November 12, 2022

LAZIMA UWE NA SHAHUKU YA KUKUA NA KUONGEZEKA

Bila shahuku ya kukua hakuna mtu aliyewahi kukua.

Shika sana hili_ Wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo na unaweza kuwa zaidi ya ulivyo leo.

📌 Kwa Mungu inatakiwa tukue, na Mungu anategemea tukue. Eph 4:13,14

Mungu ametupa nguvu ndani yatu, ikiwa na kazi ya kutufanya tukue. Kuna vitu Mungu hawezi kukupa, ijapokuwa ni vyako, mpaka ukue. Galatia 4:1-7.

Hata chakula, mafanikio, karama, vipawa, nafasi, fulsa na cheo, ambacho Mungu anakupa, kinatokana na ukuaji wako.


MAENEO MUHIMU UNAHITAJI KUKUA NA KUONGEZEKA.


1. Kua kwenye Kuomba

Math 26:40_ Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja.

Yesu alitaka wanafunzi wake wakue katika muda na stamina yao ya kuvumilia usingizi na kuomba.


2. Kukua kwenye kufunga

Math 9:15

Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga.

Yesu alimaanisha, siku atakayopaa basi lazima tuanze kuutisha mwili kuacha chakula kwa ajili ya Bwana kwa muda fulani.


3. Kukua kwenye imani

Math 17:16, 19-21

Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu.

Yesu alitegemea kwa muda aliokaa na wanafunzi wake, unatosha kukua imani, wakamvunja moyo alipoona kumbe bado wana mashaka hata kutoa pepo. Yesu anategemea kwa muda huo ulio kaa kwenye wokovu, uwe tayari una imani ya kutoa pepo na zaidi.


4. Kukua kwenye Neno.

Ebr 5:12

Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 

Kolosai 1:10 anasema "mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu"

Muda huu inatakiwa uwe tayari unaweza kufundisha siyo tena hata maziwa hujui, weka bidii kusoma neno ili ukue katika maarifa ya Mungu. 


5. Kukua katika kumtumikia Mungu.

Luka 5:10

Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu. 

Mungu anataka ufike hatua ya kuanza kuvua watu.

Yoh 15:16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Mengine yote ni mema, ila kusudi moja la kuokolewa ni ili ukazae matunda, uokoe wengine. "Mungu ametutuma kila sekta ili kuokoa watu kila sekta" huu ndiyo msemo wangu naupenda.


6. Kukua kwenye kiasi.

1 Thes 5:6-8

Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 

Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. 

Chochote fanya kwa kiasi, fanya kwa ratiba, ili ufanye kingine pia.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

MOROGORO. TZ.

Saturday, April 23, 2022

JUA UNDANI KUHUSU MAISHA YA MILELE

 *** MAISHA YA MILELE NA MWAMINI 


-( 1 Wathesalonike 4:13-18)

-Kwanini tunajifunza maisha ya milele? Ni muhimu sababu mtu ataweza ishi kwa kujizuia (mithali 29-18).

-Mtu anaejua Kuna maisha ya milele ataishi kwa umakini Sana

-MUNGU ametupa maisha ya sasa ili tujiandae na maisha ya milele


- MUNGU ametupa maisha ya sasa ni mchujo na kigezo kikubwa alichoweka ni utii Yani unae mtii ndie BWANA  wako

- Tamaa za shetani ni 

1)Tamaa ya mwili

2)Tamaa ya dunia

3)Kiburi Cha uzima


*Mwanadamu akifa anaenda wapi ??

- katika Agano la kale neno walilopata ni kuzimu (Zaburi 49-14) Yani walio haki na wasio haki wote wanaenda kuzimu ( Zaburi 88-3)

-YESU anakuja kutuonyesha kuwa kule kuzimu walitenganishwa walio haki na wasio haki ( Luka 16-19) YESU anatuletea neno peponi na jehanamu.


-Mtu asiyeokoka akifa anaelekea jehanamu ( Marko 9-45)

-Mwenye haki akifa anaelekea peponi( luka 23-43)

- peponi sio mbingu mpya peponi ni Mahali pa kufarijiwa

-Jehanamu sio Mahali pa mwisho kwa wasio haki Mahali pa mwisho ni kwenye ziwa la moto ( ufunuo 21-13)

- Walio haki wakifa wanaelekea peponi wakisubili pia hukumu kwa matendo ya mwili waliofanya baada ya kuokoka .

- peponi sio Mahali pa mwisho kwa waliokoka Bali ni mbingu mpya ama yerusalem mpya biblia inasema Mahali huko  ni pazuri hamn mfano Kuna Kuna dhahabu Safi Kama bilauri pia Kuna kuta nne ambazo marefu na mapana yake zimefanana kuta zimepambwa na madin Kama zumaridi  ,yakuti nk

- katika yerusalem mpya hutokumbuka maumivu 


* Nini maana ya kufa kwa mwamini ???

-Ni kuondoka toka mwili huu wa batili na kwenda kukaa na BWANA(2 Wakorinto5-6)

- Paulo alitamn kukaa na BWANA (wafilipi 1-21)

-Paulo anasema tuziweke kando zile dhambi zinazotuzuia( waebrania 12-1)


* Unaishi kwa ajili ya Nani???

- MUNGU anasema mbele yenu nimeweka uzima na mauti Ila chagueni uzima ( kumbukumbu la torati 30-19)

-(wafilipi 1-21)

-(warumi 6-21)


* Kiti Cha hukumu Cha KRISTO 

- Kwa walio haki

-wafu watafufuliwa kuungana na walio hai siku ile ya parapanda kuu ( 1wakorinto 15:50-53)

-(warumi 14-10)

-(2 wakorinto 5-10)

- sisi tuliokoka hatutahukumiwa pamoja na wasiokoka sisi tutahukumiwa maisha yetu baada ya kuokoka 

- Paulo anasema wengine kazi zao zitaungua Kama nyasi anasema wataokoka Ila kwa Moto 

 

* Vitu ambavyo tutatolea hesabu 

1)namna gani umeshiriki kuleta watu kwa KRISTO ( Daniel 12-3)

2) kwa habari ya ulimi 

3) kwa habari ya kushindwa dhambi( warumi 6:1-4)


-From pastor ulenje EM

Written by kayombo jr

Friday, July 16, 2021

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI BORA WA YESU

25/06/2021, PREACHED 27/06/2021 AT VICTORY EMPOWERMENT TEMPLE 

FANYIKA MWANAFUNZI

WEWE NI ZAIDI YA JINSI ULIVYO. UNAWEZA KUWA ZAIDI YA JINSI ULIVYO LEO.


Yesu aliwakuta wanafunzi wake wakiwa wavuvi, hata Galilaya walikuwa hawafahamiki, lakini walipofanyika wanafunzi, wakafika mpaka kwa Wayunani, mpaka Asia. 
Unaweza kufanyika zaidi ya jinsi ulivyo leo, kwa sababu unaweza kufanyika mwanafunzi. Kufanyika mwanafunzi wa Yesu ni daraja la kukuvusha daraja la maisha, ni ngazi ya kupanda ngazi nyingine ya maisha. Kama unawaza wapi pa kuanzia ili upae kimaisha, basi anzia na kufanyika mwanafunzi wa Kristo.

Kusudi la Kristo ni Kujipatia Watumishi.

Math 28:19, Yesu anasema, “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Yesu anaweka wazi, anataka wanafunzi. Na ukweli hajatutuma kukufundisha bali kukufanya mwanafunzi. Yesu amekuokoa ili uwe mwanafunzi.
Yesu anasema “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; MATH 11:29.

Ukisoma mstari wa juu yake ‘28’ anasema “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”. Kusumbuka iwe mwisho_ umekopa sana kufanikisha mipango, umeomba, umetafuta, umelia_ leo nenda kwa Yesu_ kanunue Biblia sema “nitajifunza kwa Mungu nami nipumzike, nipate raha”

Kwanini uwe mwanafunzi?

1. Sababu mwanafunzi pekee ndiye unaweza kumbadirisha. 
Anayekufundisha anakufanya uwe mtu fulani_ na hasa anakufanya yeye alivyo. 
Yesu hataki ujifunze kwa dunia, kwa sababu ukijifunza kwa dunia utakuwa kama dunia. Ila ukijifunza kwa Yesu utakuwa kama Yeye. Yesu anasema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake”. LUKA 6:40. 
Yesu anataka uwe kama yeye. Na dunia wanataka uwe kama wao_ lakini wote hao ni wageni hapa duniani, Yesu ni zamani kuliko wote_ wote wameikuta Biblia_ na ina shuhuda ya kufanikisha wengi_ ni bora leo ukachagua kuwa mwanafunzi wa Yesu. 
Unapofungua Biblia na kusoma, unafanyika neno, unafanyika kama Yesu.

     ✅ Yesu Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu” MATH 4:19. Yesu anataka akubadirishe kutoka mtu fulani uwe mtu mwingine, 
Kila aliyeamua kufanyika mwanafunzi_ baada ya mda fulani, watu wakasema “siyo yule tunayemjua” wengine kwa mshangao wanasema “ni wewe kweli, au mwingine”
  Paulo anasema “Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ROM 8:30. TENA Anasema “tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 KOR 3:18.
Usijipime leo, Hayo unayopitia ni milima na mabonde tu ya njiani_ fanyika mwanafunzi_ wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo. Kuna mtu Yesu anamtengeneza mwenye utukufu zaidi ya ulio nao leo. 

2. Sababu anataka akujulishe siri za ufalme.
Ukishasikia siri, maana yake kuna watu maalumu wanaostahili kujua. Yesu hakuja kumwambia kila mtu siri za ufalme wake, bali wanafunzi wake pekee. Yesu anawaambia wanafunzi wake “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa” MATH 13:11. 


3. Sababu anataka akutumie.
Yesu hajawahi kutumia mtu ambaye hajafanyika mwanafunzi. “watu wengi walimwamini…lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; YOH 2:23, 24. Kumwamini haina maana yeye amekuamini, na sifa ya kumuamini siyo kuwa mkamilifu, bali kuwa mwanafunzi. Pamoja na udhaifu alio nao Petro, lakini Yesu alimvumilia na akamuachia kanisa, kwanini_ wakati wengine wamekimbia, yeye akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, YOH 6:68.
Mungu sasa anataka kutumia watu wa kila sekta, wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, waimbaji ili kujipatia mavuno na kutangaza jina lake_ ili kuipa aibu dunia… wewe fanyika mwanafunzi. Naye atakutumia. 

Siyo Kila Mtu ni Mwanafunzi.

Kwenye biblia kuna makutano na wanafunzi. Kuhudhuria kanisani na kuokoka haina maana wewe ni mwanafunzi.
Unaweza ukahudhuria kanisani miaka 40 lakini usiwe mwanafunzi, kwasababu uwanafunzi siyo miaka uliyookoka, wala uliyohudhuria kanisani, uanafunzi ni maamuzi, siyo kuhudhuria. Wote ni mashahidi hasa kwa walimu ambao wanachapa sana, tulikuwa tunahudhuria darasani lakini tunasikia lakini hatusikilizi. 
Yesu anasema “Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. MATH 13:14, 15.
15. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Tunajuaje kuwa wewe ni mwanafunzi?

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI WA YESU.

Tuone sasa namna, unaweza kuwa mwanafunzi. Ni vigezo gani mwanafunzi anavyo.

1. Mwanafunzi Analiamini na Kulikubali Neno Lote.
Siyo nusu, siyo moja_ yote. 
Yesu siku zote alitumia maneno magumu ili kuchambua wanafunzi na makutano. Biblia inasema “wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena” wakakimbia wote, wakabaki wanafunzi tu. YOH 6:64-69. 
 Nao akawauliza “Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Petro akajibu akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, Nasi tumesadiki, tena tumejua wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu”. Mwanafunzi anaamini yote. Paulo anasema “…nikiyaamini yote…” MDO 24:14. 
Na huwezi sema umeamini mpaka umekubali ulichosikia, umekipokea na kukitendea kazi ulichosikia. 
Huwezi sema ni mwanafunzi mpaka umekubali, na kukishika kile mwalimu amesema. Na mwalimu wetu ni Yesu, na shule yake ni Biblia. Na anatumia watumishi wake kukueleza alichoandika. Paulo hajaandika Biblia, Mathayo hajaandika Biblia, mimi sijaandika Biblia_ wote waliandika yale Roho Mtakatifu amesema, nami nahubiri yale Biblia imesema. Nami natenda hayo hayo na naona matokeo, na Mungu amenituma nisema nawe, ili tuinuke pamoja.


2. Moyo wa unyenyekevu.
Pasipo moyo wa unyenyekevu huwezi kumfundisha mtu yeyote. 
Mtu mwenye kiburi anajua kila kitu, hata ambacho yeye mwenyewe anajua kuwa hajui. Lakini atalazimisha kwa maneno mengi kuwa anajua. 
Watu kama hao_ hawawezi kuwa wanafunzi. Sababu wanaenda kwa Mungu, huku wakiwa na ya kwao. 
Wanasema Mungu tufundishe, lakini kama ni kinyume na aliyosema mjomba, bwana vicoba, hatuwezi kukusikiliza.
Hakuna kazi ngumu kama kumfundisha mwanafunzi mwenye tution nyingi.
 
Yesu anasema “kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa” LUKA 14:11. Unafikiri kwanini Mungu anainua wanyenyekevu, kwa sababu mnyenyekevu ni kama mtoto anabebeka (Math) anafundishika,
Mungu anasema “…Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. ISAYA 48:17

Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko. MITH 16:18.

3. Mwanafunzi wa Yesu  Anakuwa.

Sifa ya mwanafunzi ni kukuwa. 
Kila mwalimu anapima mwanafunzi wake kwa kukuwa katika kile anamfundisha. 
Haijarishi umetokeo wapi kwenye wokovu, lakini kila siku inabidi ukue kila eneo_ kuomba, kusoma neno, kuhudhuria ibada, kufunga, kushuhudia.
Yesu anasema “Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini. MATH 13:23.

4. Mwanafunzi lazima awe ametubu.

Yesu anapoanza injili yake tu_ akasema nini ufanye ili uwe mwanafunzi wake.
Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. MATH 4:17

Kutubu siyo kuomba msamaha, ni zaidi ya hapo. Kutubu ni kubadiri unavyowaza, kubadiri mfumo wa maisha.

Yesu anaweka wazi, nimewakuta mna ufalme wa dunia hii, sasa geukeni acheni kuwaza na kufanya kama dunia, sasa muwaze na kufanya mambo kama ufalme wa mbinguni unavyotaka.

Others
5. Usiogope watu
Huwezi kuwa mwanafunzi kama unaogopa watu wanasema nini. Sababu siku zote Yesu anakwambia mambo ambayo watu hawataki, ni kinyume na wanavyojua, ni kinyume na wanavyotaka uishi. Kilichomponza Sauli ni kuogopa watu, akaacha kufanya Mungu alichomfundisha.
Yesu akasema 
6. Jikane mwenyewe_ luka 14:26
7. Beba msalaba wako_ luka 14:27

Hitimisho.
Omba unyenyekevu na maombi ya agano_ kuwa wanafunzi. Na weka agano kutenda nini neno linasema.

Ushauri au maombi.
0683 477 827 
0718 721848