Wednesday, December 25, 2013

PURPOSE OF PRAYER AND CHRISTMASS


KUSUDI LA MAOMBI NA KRISMASS
Kusudi la Yesu kuzaliwa ilikuwa ni kurudisha utawara wa mwanadamu ulikuwa umeibwa na shetani amba mwanadamu alipewa na Mungu.
Mwanzo 1:26
Mungu anampatia mwanadamu utawara, anawaambia mkataware (Let them have dominion), lakini shetani anakuja kuchukua ule utawara kwa kumkosanisha mwanadamu na Mungu (kuondoa uhusiano wake na Mungu) Ambao ndiyo nguzo kuu ya utawara wake;maana hawezi kutawara pasipo kuwa na utawara na Mungu.
Shetani alipchukua ule utawara toka kwa mwanadamu, ndipo akachukua cheo cha mwanadamu kama mkuu wa ulimwengu huu na yeye kuwa ndiye mkuu wa ulimwengu huu, shetani akaanza kumtawara mwanadamu na kumuamrisha afanye anachokitaka yeye, na mwanadamu hakuweza kujizuia kwake, hata wafalme walimfata, Sauli alikosea, Mussa alikosea, Daudi alikosea, Sulemani alikosea, Yeroboam alikosea na wengine, machafuk, na dhambi zikaingia ulimwenguni, watu kuuwana wa kwa wao na kuuwa wanyama kwa kasi kubwa sana, uzinzi, ufiraji, ubakaji, ukahaba, ushoga na usagaji, wizi, udokozi, vita, unafki na umbea na magmvi ya kila aina.
Mungu akaleta mapigo mawili kwa kuamini wenda mwanadamu akamrudia yeye (sodomo na ghomola, na ile ya Nuhu) lakini mwanadamu akaendelea kutenda maovu kwasababu alikuwa chini ya mkuu wa ulimwengu huu shetani
Ndipo Mungu akasema sitomwangamiza mwanadamu tena, bali nitafanya nae agano jipya, Yeremia 31:31; 32:40
Yesu akazaliwa ili kuunda agano hilo jipya, na kuzaliwa Yesu ni ishara ya agano hilo jipya kama ilivyotabiliwa na nabii Isaya( Isaya 7:14, 9:6)
na ishara hiyo ilikuwa ni utawara; Hivyo Yesu alikuwa ni ishara ya kurejeshwa utawara unaotokana na uhusiano wa mwanadamu na Mungu. 
Yesu alipozaliwa akazaliwa kwa kusudi la kurejesha uhusian huo
ndio maana alipokufa pazia la hekalu(patakatifu pa patakatifu) na hivyo si makuhani tena bali kila mtu ana ruhusa ya kutengeneza uhusiano wake binafsi na Mungu na kupkea utawara ambao baba yetu na mama yetu Adam na Hawa waliupoteza.
na hivy kwa kuzaliwa kwake na kupigwa kwake basi hapo kwanza hatukuwa taifa lakini sasa tu taifa la Mungu, na tumefanyika wafalme na makuhani, watu wa milki ya Mungu (1petro 2:9, Ufunuo 5:10)
na sasa Ufalme wa Mungu si ufalme wa watu tena wa kawaida bali ni ufalme wa wafalme chini ya MFALME WA WAFALME
na si tena watu chini ya Kuhani bali ni ufalme wa makuhani chini ya Kuhani mkuu Yesu. 
Na hivyo utawara wetu umerejea tena.
Yesu akasema nimewapa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka na kazi zote za yule adui,
lakini pia aliwapa mamlaka juu ya pepo wabaya na magonjwa yote (Luka 10:18-19)
na Yesu alipoondoka wanafunzi wa Yesu wakaanza, kuwa na amri dhidi ya pepo, magonjwa, na hata wafu wakafufuliwa na viwete wakatembea, na hiy ni ishara ya kurudishiwa ufalme.
Hivyo krismass ni kurudishiwa uhusiano na utawara ambao Ibirisi aliuchukua kwa Adam na Hawa.
lakini kuupata utwara huu ni lazima uwe mwana mambi, sababu Mungu hawezi kufanya kitu chochote duniani kama Mwanadamu asipoomba na kuruhusu kifanyike kwa njia ya Maombi
Yoh 12:31, yoh 16:11
 
 


No comments:

Post a Comment