Tuesday, October 20, 2015

SEHEMU YA PILI: BARAKA TANO ZA PETRO NA KANUNI KUMI ZA KUFIKIA MAFANIKIO YAKO.

Tunaendelea
Kwanza naomba amini maneno haya;

"Maadamu yu hai...
1. Unaweza songa mbere zaidi
2. Unaweza toka hapo ulipo
3. Unaweza kuwa mtu huru
4. Unaweza kuwa mtu uliyefikiri kuwa
5. Unaweza kuishi maisha ya mafanikio unayotaka kuishi
6. Unaweza kuacha historia nzuri katika ulimwengu huu
7. Unaweza kubadirika
8. Unaweza kubadiri tatizo lako kuwa neema
9. Unaweza kubadiri historia mbaya kuwa nzuri
10. Unaweza kuinua maono yako na kuyaanza tena na kuyatimiza.
11. Bado unaweza kuwa jasiri tena
12. Unaweza kuwa mtakatifu tena na mwenye haki
13. Unaweza kuwa mtumishi tena
14. Unaweza kufanya uliyowaza kuyafanya.

Bado unaweza....
Na "LEO" ndiyo siku pekee unayoweza kufanya maamuzi ya kufanya haya. Jana haikuwa siku sahihi, kesho haigusiki, na hatujui.


JANA IMEISHA, LEO NI SIKU MPYA,  KESHO YAWEZA NZURI ZAIDI YA LEO
Tangazo hili naomba liingie ndani yako. Soma mfululizo huu kwa umakini, soma kanuni kumi kwa umakini, baada ya kusoma vitabu vingi vya watu waliofanikiwa, na kuona, na kusikia wengi waliofanikiwa, kupitia Biblia na kusoma watu waliofanikiwa, na maisha yangu binafsi; nimekuja kugundua kanuni hufanya kazi kwa yeyote pasipo kujali kabila lake, dini yake, taifa lake, rangi yake, umri wake, nchi anayotoka, elimu yake, na wote waliofanikiwa waliishi maisha ya kushindwa kwanza, ila walipoamua kufata kanuni maisha yao yalibadirika, na nilichogundua hawakutumia miaka au miezi, walitumia siku moja kama dhahabu inayotoka kwa Mungu kwa neema, inaitwa leo.
Kanuni zikiheshimiwa huleta mafanikio, zikivunjwa huleta kushindwa, uamuzi ni wako, kazi ya karama ya mwandishi ni kupokea toka kwa Roho Mtakatifu na kuandika kwa utiifu wote bila kupunguza, kazi ya msomaji ni kusoma, kuamini na kutendea kazi.
Mimi naanza kufanya jukumu langu.

Wote tunakubali tunaishi kwenye dunia inayokubari mabadiriko, dunia inabadirishwa na wachache, dunia yenye wengi wanaoshangaa na kuhadithia mafanikio ya wengine, wachache ndiyo wamiliki wa mali za dunia, wengi ni watumishi na wateja wa hawa wachache, nani kazaliwa na kitu, hapana; wao wamevipata wapi? Hapa hapa duniani, na sisi twaweza kuvipata wapi? Hapa hapa duniani
Nianze kusema wote tumeumbwa ili tuwe wamiliki
Jambo la kwanza alilolifanya Mungu alipomuumba Adamu ni kumpa umiliki, akamwambia "ukataware" kutawara ni umiliki, huwezi kutawara vitu ambavyo havipo chini yako, soma mwanzo 9:2 Baada ya wanadamu kukosea na Mungu kuwaangamiza kwa Ghalika, Mungu anafanya agano jipya na Nuhu na neno la kwanza ni kummilikisha vitu vyote duniani, Mungu amekupa umiliki, lakini ni kumiliki kwa niaba yake, Yeye bado atabaki Bwana yaani Adon kwa Kiebrania, yaani mmiliki kwa kiswahili, Yeye yupo juu ya vyote, ila amempa mwanadamu ataware kwa niaba yake
Swali kwanini humiliki, kwanini umekuwa mteja na mfanyakazi wa hili kundi dogo la mabepari,
Ipo kanuni ya kuondoka ulipo na kurudi namna ya Mungu alivyokuumba.

Wana wa Israel walifurahi kwenda Misri wakati nchi yao ilipokumbwa na njaa yaani Kanaani, Yusuph akawapokea, Mungu alikuwa ameshaagana na Ibrahimu kuwa atakipeleka kizazi chake Misri na kuwa watumwa kwa miaka 400 kisha atawaokoa na kuwarudisha kwenye nchi aliyomwahidi Ibrahimu.
Wana wa Israel moja ya vitu ambavyo hawawezi kusahau ni kuwa watumwa ndani ya Misri kwa mda wa zaidi ya miaka 400.

Mtumwa ni mtu ambaye hufanya kitu pasipo kutaka/ pasipo kuwa na matakwa yake. Mtumwa huenda asipotaka, hufanya kazi asiyotaka, hula chakula asichotaka, hulala mda asiyotaka, hupumzika mda asiyotaka, huishi maisha asiyotaka, hulala mahari asipotaka, huvaa nguo asizotaka; kuwa mtumwa ni heri ya kutozaliwa.

Wana wa Israel najua walifika wakati wakasema ni heri tusingezaliwa.
Mtu asiyekuwa katika kundi la wamiliki wa mali na uchumi wa dunia hii; yawezekana ukawa mmoja wa hao, atakula chakula asichokitaka, atavaa nguo asizozitaka, atafanya kazi mpaka mda asiyoutaka, atafanya kazi asiyoitaka, atalala mahari asipopataka, atanunua vitu asivyovitaka, atalala mahari asipopataka, ataishi maisha asiyoyataka, huu ni utumwa, wengine katika sayari hii wamekuwa ni mtumwa wa kiwango kidogo cha pesa walichonacho; "Pesa ndiyo jawabubla mambo yote"

Mara ngapi umeingia kwenye mtihani wa shule au chuo, umejiandaa kwa kusoma, kila kifaa unacho, peni, rula, na umevaa nguo za kupendeza: unaingia ndani ya chumba cha mtihani, unakaa vizuri kwenye kiti, unafunua karatasi ya mtihani, na kukuta kichwani una asilimia 30 ya yale yaliyoulizwa, kati ya maswali 20 unayajua maswali saba tu, ina maana asilimia 70 ya mtihani hujui. Wewe unadhani majibu hayapo ya maswali hayo, ukitaka kujua majibu yapo, tazama wa kulia kwako utamuona anajibu mtihani kwa tabasamu akionesha kuyajua yote;
"si kwamba pesa kama haijibu mambo yote unayoyahitaji kwamba imepoteza uwezo wake wa kujibu, ila ni kwamba unazo chache, umekusanya chache, umezipata chache.
Kushindwa kujibu maswali yote hakuna maana kichwa chako hakina uwezo wa kujibu; ila hayo saba ndiyo ambayo uliyasoma na kuyaweka kichwani, kichwa hakiwezi kujibu zaidi ya uliyoyaweka ndani yake wakati unajisomea, ukilazimisha utakosa tu.
Ndivyo pesa ilivyo; siyo kwamba haiwezi kujibu mambo yote unayotaka; tatizo ni kwamba hizo ndizo ulizotafuta, hizo ndizo ulizopata, hizo ndizo ulizonazo.
Kama wenzio wananunua vitu vya gharama ya Laki tano, ndizo walizokusanya, wewe nguo ya 3000 ndiyo uliyokusanya, na huwezi zidi hapo. Kanuni ndani ya kitabu hiki zinataka kuondoka na utumwa huu wa na kuwa mmiliki na uwe na pesa zenye jawabu la mambo yote.
Mungu amenipa kanuni hizi ili tu utoke ulipo na uwe na kesho yenye furaha na ushuhuda.

Mbali na hapo kuna watu ni watumwa wa hari zao za maisha, waweza kuwa tajiri lakini ni mtumwa wa ndoa, furaha, amani na huishi unavyotaka kuishi, huoni faida ya pesa yako katika maisha yako ya kawaida. Kanuni hizi zitagusa huko pia.
Na mfululizo huu ni maalumu kwa kila mtu, kama ni tajiri, mjasiliamari, muwejezaji, na yeyote, kama unayo leo, kitabu hiki kitakupa mwanga wa kufanya zaidi; kama unaishi bado waweza kufanya zaidi, soma mfululizo huu ili tumshinde adui wa kufanya zaidi ambaye ni mafanikio yako uliyonayo.

PART ONE
sehemu hii hasa tutaangalia msingi wa somo letu, maana ya siku tatu (leo, jana na kesho), pia tutaangalia watu tofauti jinsi walivyotumia leo yao, na tutazama makundi muhimu, hasa wale ambao leo yao, imesababishwa na historia, matukio au sababu fulani kama kukisa elimu, yatima, mjane, kilema, n.k

SEHEHEMU YA KWANZA
MSINGI WA NENO

KANUNI: kanuni ni imani na sheria ambazo mtu huziamini na kuzisimamia na kuzifanya mwongozo wa maisha yake.
Kanuni ni za asiri si za kubuni, kanuni zimefanikiwa kufanya kazi kila mahari kwasababu ni za asiri. Mwanadamu ameumbiwa, kuzifata si hiyari ni lazima, kanuni hazina jaji, usipofata zinakuhukumu zenyewe, hapa hapa duniani.
Yesu alisema, Mimi sitowahukumu ila maneno yangu ndiyo  yatakayowahukumu"
Nimewahi kuwa na rafiki yangu miaka ya 2005 mpaka 2008, alikuwa ni mtu anayefanya vizuri sana toka tukiwa shule ya msingi, tulipofika sekondari alifanya vema toka kidato cha kwanza mpaka cha pili na alikuwa mbere yangu kimasomo, nilishangaa kidato cha tatu akaanza kuwa nyuma yangu, nilipochunguza alikuwa amejenga mahusiano ya kimapenzi na binti fulani ambaye kwa pale shule alikuwa ana historia ya kutembea na wavulana wengi, nikamfata na kujaribu kumshauri lakini alinijibu kuwa "acha ushamba dogo" nilipomng'ang'aniza akanijibu kwa kebehi "niache, kwani haya si maisha yangu" nikamuacha ila siku ile ile nakumbuka hata mama yangu nilimshirikisha kuwa "rafiki yangu unayemjua amebadirika na sijui kama atafauru".

Ilikuwa ni rahisi kujua kuwa hawezi kufauru kidato cha nne hata kama si nabii, kwanini alienda kinyume na kanuni. Kanuni haziitaji hakimu wala jaji, bali zenyewe ni za asiri, unapovunja zinakuvunja.
Mfano usinywe sumu, usizini, usilewe, usinywe sumu, usiwe mvivu, hizi ni moja ya sheria za asiri, unapovunja haihitaji hakimu, zinakuvunja hapo hapo.
Kumbuka Yesu kasema, ni heri msingesikia, lakini sasa mmesikia hukumu i juu yenu.
Unapovunja kanuni, unatupa ruhusa ya kujua mwisho wako wa majuto, unapojitoa na kufata kanuni, unatupa furaha ya kujua mwisho wako mzuri.
Msingi wa kitabu hiki si kukupa mawazo, ila nataka upate kanuni.
Sihofu umesoma vitabu vingapi na ukabaki kama ulivyo, mimi najali kuwa, kwa kusoma mfululizo huu hutabaki kama ulivyo.
Na kwa waliofanikiwa naamini utafanya vizuri zaidi maadamu bado unayo leo.

Tuanze na mdano wa Mpakwa mafuta wa Bwana Mungu, kuwatoa Israel toka utumwani Misri kwenda Kanaani.
Anatoka kutoka maisha ya anasa ndani ya ikulu ya Farao mpaka kuwa masihi wa Bwana. Na kuandika vitabu vitano muhimu kwenye Biblia, Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na KumbuKumbu la Torati.

KUTOKA14:13-14
"Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. 14. Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Maneno ya msingi ya kuyakumbuka kila unaposoma mfululizo wa somo hili ni:
• msiogope simameni tu
• mkaone wokovu
• Bwana atakaowafanyia
• Wamisri mliowaona leo
• hamtawaona Wamisri tena milele
• mtanyamaza kimya

Toka hapa tunapata maneno ya msingi;
Mafanikio hutokana na...
• uhusika wa Mungu (atawapigania)
• uhusika wetu (simameni)
• waleta utumwa (wamisri)
• utumwa (kutofanya unayopenda)
• mafanikio ni vita (atawapigania)
• kusonga mbere hata kama umetoka utumwani/umefanikiwa
• no retreat no surrender/ hakuna kurudi nyuma wala kunyosha mikono juu ya kushindwa.
• maisha yanahitaji kukubari kwa imani ya wengine juu yako na juu ya unachokifanya,. Musa ilimradhimu kuwashawishi kwa maneno ya imani wana wa Israel ili tu wakubali jambo analotaka kulifanya.
• Watu ndiyo wa muhimu sana katika jambo lolote unalotaka kulifanya. Ishi na watu vizuri, sema nao vema, chukuliana nao vizuri, ishi nao kwa hekima, uhakikishe unapata wengi wa kukuunga mkono,
 “ni ngumu kukupenda wote, ila tu unawahitaji watu sahihi”.
• muache Mungu afanye sehemu yake, na usingoje afanye sehemu yako.
• usimuingilie Mungu sehemu yake na usingoje aingilie sehemu yako.
• Mungu akisema 'nenda' wewe nenda.
• ukianza safari usifikiri kurudi nyuma/ ukiaga kwenu usirudi.

Pia tunajifunza namna ya kutumia tatizo na kulifanya kuwa baraka na siyo tatizo;
Huwa napenda kuwaambia INAWEZEKANA... watu walipita kwenye sehemu ya mkwamo wa kusonga mbere kufanya jambo ambalo kwa mda huo li juu ya uwezo wao (impossible).
Rafiki yangu wa karibu nikiwa mtoto Mama mmoja, siwezi kumsahau, mume wake alipomuacha, na kumuachia mtoto mchanga na kwenda kuowa msichana mwingine, mda mwingi nilimuona na tabasamu na mwenye maneno ya kufariji na si mwenye uhitaji wa faraja, ukienda kumfarini utaishia kufarijiwa wewe, alikuwa ni mtu aliyeumba kichwa chake kuwa tayari kujifariji na kukabiri haiwezekani kuwa inawezekana, sasa yupo Kenya ana maisha mazuri.

Tunajifunza nini toka kwa Musa aliibadiri "haiwezekani kuwa inawezekana” ndani ya fikra yake na ya team yake yaani wana wa Israel, na imani iliyochipuka ikaungana na nguvu za Mungu na bahari ikagawanyika.

“Imani ndiyo njia pekee ya kutuunganisha na nguvu za Mungu”

1. Tambua tatizo mpaka hapo ulipo: Wamisri

2. Tambua kikwazo cha kufika unapotaka kufika: Bahari

3. Weka akiri zaidi kupata uhitaji, na uache kupoteza akiri kwenye tatizo, bali nini unataka; Musa alifikiri kuvuka ng'ambo si kurudi Misri.

4. Badiri fikra: ondoa hofu weka ujasiri

5. Tambua fikra za team yako na kuzishughulika: woga

6. Peleka akiri pa kupata usaidizi: Mungu

7. Tambua ushiriki wako, katika kuliondoa tatizo, ushiriki wa Mungu na wa timu yako: piga fimbo

8. Yakusanye matatizo yote na uyajue yote : Wamisri, Bahari, hofu yake na ya Waisrael, jangwa, hawana msaada.

9. Yatenge kwa utofauti wake na uyatatue kwa upekee wake: akaanza na Wana wa Israel kisha akaja Wamisri, akamalizia bahari, wakavuka.

10. Tengeneza mpango na mbinu nzuri ya kuyamaliza: Mungu akamtoa malaika aliyekuwa mbere yao na kumuweka nyuma, akaweza kiza kati ya Wamisri na mwanga kwa Israel ili kuwatenganisha.

11. Tembea katika imani huku ukimtazama Mungu; Musa alimwita Mungu na si mtu wa karibu, si Haruni wala Miriam, wala hakuanza kulia na kumueleza kila mtu.

12. Matatizo yasikufanye ukapunguza juhudi yako ya kusonga mbere: Musa hakupunguza munkari wa kwenda Kanaani, akaamnini Mungu atafanya lolote, saa yeyote.

13. Amini Fulsa, na jawabu inaweza kutokea saa yeyote na kwa namna yeyote: hawakufikiri kupasuka kwa bahari

14. Amini unaweza songa mbere zaidi: waliposikia wakapata moyo na nia, bahari ilipopasuka wakasonga mbere zaidi

15. Amini Mungu anaweza tokea mda wowote na kwa namna yeyote.

Alifanya kwa namna isiyoweza kufikilika kama angefanya vile, unaweza waza angeleta mtu alete maboti, au meri, au awauwe wa Wamisri kwa moto, hapana akawafanyia wasichofikiri.
Leo atafanya kwako. Kwa Jina la Yesu Kristo.

16. Weka suruhisho na siyo kukazana na ukubwa wa tatizo: Mungu alinishangaza hakuanza kuwakazia macho Wamisri, bali alikazia macho wao kusonga mbere, alikazia macho nini kinahitajika, na nini kifanyike wasonge mbele, hakutazama Wamisri.
Mungu akawapasulia njia, ndipo akawauwa Wamisri, kwa haraka utafikiri kwanini asingewauwa Wamisri, lakini alijua sasa akiwauwa, “enhee kwa wingi wao, wangepita wapi.
Leo hii Wamisri wanafananisha na utumwa wa pesa waliyokuwa nao wengi, na matatizo na changamoto nyingi ulizonazo.
Na kupasuka kuna maana ya usisimame ukaona umefika, bado hujammaliza adui, songa mbere, uhai wako, fulsa na nguvu ni kwamba bado unaweza songa mbere; shinda ugomvi wako na mafanikio uliyonayo ambayo yanakufanya usisonge mbere.

17: nini unahitaji kumaliza tatizo: Musa alihitaji fimbo ya kupiga maji yagawanyike. Na usiangalie mbali kwanza kupata kitu cha kumaliza tatizo, tazama kwanza nini unacho mkononi, nini unacho, kama ni kipawa, karama, au fedha kidogo, ndugu au rafiki wa karibu au watu sahihi. Tumia ulichonacho kwanza, na hivyo ulivyonavyo vitaleta unavyovihitaji kumaliza tatizo lako.
"Nyoka hatuanzi kummulika mbali, tunaanzia miguuni"

Tuendelee tena siku nyingine...
Karibu na ufurahie ufunuo wa siri za mbinguni kwa msaada wote wa Roho Mtakatifu.
Mungu awe nawe...

NAAMINI UMEBARIKIWA.
Bado tunaendelea
Fatana nami zaidi...

Saturday, October 17, 2015

BARAKA TANO ZA PETRO: JANA IMEKWISHA LEO NI SIKU MPYA, KESHO ITAKUWA NJEMA ZAIDI YA LEO.

BARAKA TANO ZA PETRO NA MAANA YA LEO, KESHO NA JANA.

UTANGULIZI
Jana Imekwisha, Leo ni Siku Mpya Kesho Yaweza kuwa Nzuri Zaidi ya Leo.
Huu ni mfulizo wa somo la muhimu sana kwa kila mtu, litakusaidia kutambua uko wapi na unaenda wapi, ni somo lililojaa kanuni za namna ya kuitumia leo yako kwa hekima na kuwa na Kesho nzuri. Somo litakupa kuelewa sehemu ya Mungu katika maisha yako na sehemu yako. Litaondoa maswali mengi kuhusu matumizi ya neema ya Mungu.
Mfululizo huu utamtazama Petro kwa kina: tabia zake, mitazamo yake, ucheshi wake, udhaifu na uimara wake na kutazama namna yote hayo alivyoweza kuyatumia hata kumfanya Yesu kwa neema akampa Baraka Tano na zote zikatimia. Na kutazama namna zinavyohusiana na maisha yetu ya leo na kujenga kesho yetu njema.

Nimetumia miaka mitatu sasa kuandaa somo hili. Na nitakayosema na wewe humu ni rasha rasha tu ya somo lenyewe ambalo lipo jikoni likioikwa zaidi kama kitabu.
Kwa msaada wa Roho mtakatifu mafunuo haya ya muhimu yameandikwa na kupewa uvuvio wa hari ya juu kubadiri maisha yako.
Fatana nami.

Tuanzie hapa, Safari ya kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine kwa kutumia gari la abiria ni wakati mzuri sana. Ni fanani ya safari maisha, MAISHA YANAENDA KASI SANA, hata kuzidi uwezo wetu wa kuyamudu".
Jinsi gari linavyoenda mbere ndivyo barabara, nyasi za pembezoni mwa barabara na vyote vya nje ya gari utaona vikirudi nyuma, jinsi gari linavyoongeza kasi ndivyo vitu pia vinaongeza kasi ya kurudi nyuma. Pekee huwa napenda kutazama uzuri wa tendo hili, maana jinsi unavyosonga mbere ndivyo unavyokutana na nyasi zingine, miji mingine, barabara nyingine, na wote wanarudi nyuma kwa kasi. Nikiwa mtoto nilifikiri kuwa ni kweri vinarudi nyuma, ila shule na ukubwa ukachangia kujua kuwa kwenda mbele kwa gari ndiko husababisha vionekane kurudi nyuma, ila vyenyewe huwa tunaviacha palepale.

Maisha ni safari, maisha ni safari, maisha ni safari, huu ndiyo msemo niliousikia tangu miaka yangu ya utambuzi wa mema na mabaya. Leo naandika kitabu hiki nikiwa na ufahamu napata nguvu ya kuhoji na kuandika, kama maisha ni safari basi kuna gari la abiria tumepanda, na kama lipo basi lazima litakuwa na lina jina, na kama lipo kweri basi kuna barabara, kuna nyasi tunazoziacha nyuma kila siku, kuna miji na vijiji tunaviacha nyuma, kuna vituo tunaviacha nyuma, kuna watu wanashuka njiani nasi tunaendelea mbere, tunafika pia tunashuka wengine wanaendelea, kuna wakati tunafika hata mwisho wa safari.

Kama ni kweri; maisha ni safari, mda ndiyo kipimo cha safari yetu, kila mtu ana mda amewekewa kuishi, na kikomo cha mda wake ndiyo mwisho wa safari yake inayoitwa maisha, wapi tunaenda, tunaelekea kwenye mafanikio na kushindwa, tunaelekea kwenye furaha au huzuni, tunaelekea kwenye utajiri au umasikini, tunaelekea kwenye kuleta mabadiriko au kukubari mabadiriko, tunaelekea kwenye kuwa mfanyakazi au kuwa muajiri, tunaelekea kuwa muwekezaji au mteja, tunaelekea kuwa mtumwa au mtu huru, tunaelekea kufa unafahamika au hufaamiki, tunaeleka mbinguni au jehanamu.
Basi tulilopanda linaitwa ulimwengu;  ni tofauti na nchi au dunia, hivi ni sayari, lakini ulimwengu ni hari ya uathiri (influence), ni hari ya kitWu, mtu/watu kuwa na nguvu ya kufanya wengine kufanya kitu fulani kwa kupenda au kutopenda,
Hivyo tupo kwenye basi la kila mtu akitafuta nguvu ya kuwa na uwezo wa kuwafanya wengine wafanye anachotaka, ulimwengu umpe anachotaka, apate anachotaka, aishi anavyotaka, aende anapotaka, ale na kuvaa anavyotaka. Ukitazama kwa makini; utaona ni wachache ndani ya gari hili ulimwengu wamefanikiwa kufikia hapo, tunawaita matajiri/mabepari/wawekezaji/wajasiriamari, ila kundi kubwa; mabilioni na mabilioni ya watu bado wapo hawajafanikiwa; bado hawajafanikiwa kupata nguvu hizo, za kufanya unachotaka, kwenda unapotaka, kuwekeza unapotaka, kula unavyotaka, kusoma na kusomesha unapotaka, kufanya starehe unayotaka n.k.

Kumbuka hii ni sehemu ya kwanza wiki ijayo tunaendelea...

"Maisha yanaenda kasi, zaidi hata ya uwezo wetu wa kuyamudu"

Kama gari ni ulimwengu, nyasi, na vingine ambavyo huwa tunaviona vikipita na kurudi nyuma kwa kasi ni nini?. Shetani na dunia haijawahi kuwa na jipya, siku zote ni yale yale, dhambi iliyomwangusha huyu, kesho inamwangusha yule, baada ya miaka kadhaa inamwangusha mwingine, jaribu na changamoto iliyomkumba huyu ndiyo hiyo kesho humkumba yule; nimekuwa mshauri wa watu wa rika tofauti kwa miaka kadhaa sasa, sijawahi sikia tatizo ambalo ni jipya, yote yanafanana, tofauti ni mtu na aina ya watu waliyopatwa basi. Nyasi na miji tunaipita huwa havitembei viko pale pale, gari la mbere na gari la nyuma watazikuta palepale na kuzipita, ukipita jana, leo na kesho utazikuta pale pale, hata zikikatwa, miji na vijiji vitabaki, katika safari hii kila mtu atapitia changamoto, majaribu, vikwazo, na makosa kadhaa. Na yote huwa yanafanana.
Cha ajabu, kwanini watu wanashindwa, yaani aliloshindwa huyu kesho yule naye anashindwa; watu hawataki taarifa na kujifunza.

Mfululizo wa somo hili la BARAKA TANO ZA PETRO ni kukusaidia kujua kanuni za kuwa salama katika safari, kujua kuitumia leo yako vema na namna ya kuandaa na kutumaini kesho yako, na pia kukusaidia kufika salama mahari unapotaka ufike katika safari ya maisha uliyoianza, na  kuwa moja ya kundi dogo lenye nguvu ya kuongoza na kuathiri ulimwengu uende wanapotaka, kufanya zaidi, kushinda adui yako mkubwa ambaye ni mafanikio yako ya sasa, kuishi maisha ya mafanikio na amani ya furaha, kuondokana na utumwa wa pesa.
Daniel aliishi nchi ya utumwa lakini aliifanya Babel iende yeye anakokutaka, akainuliwa na kuwa sehemu ya juu ya maliwali wote wa Babeli na juu ya Uliwali wote wa Babeli. Leo ni zamu yako, tumechoka kuishi kama watumwa katika nchi zetu wenyewe. Tumechoka kuishia katikati ya mafanikio yetu wakati Mungu ametuumba kufanya zaidi ya tuliyofanya.

PETRO MWANAFUNZI WA KIPEKEE
Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi, muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.
Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvu samaki na si kukaa na familia.
2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.
3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.
4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumwomo Kristo japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.
5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanasungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapi hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuw hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa. Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.
6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20
7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 12. Siku zote alitazama maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari.
8. Petro aliwaza chanya siku ziku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwa ona, akaamini akaenda, alipoambiwa wokovu kwa mataifa, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ni ya jana, sasa si wakati uliyopita.
9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.
10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.
11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa sa leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15


SEHEMU YA TATU
MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, Mr. Maneno akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana, akanitazama "unajua nilikuwa na akiri sana zaidi hata yako dogo", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Mr Maneno hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.