Monday, April 24, 2017

UBIZE NA MUEREKEO WA KANISA.

BUSY AND WORK...

Bila kupinga tunaishi dunia ya watu bize sana,
asubuhi baba kazini, akifika ni bize, hata mama anayebaki nyumbani pia ni bize_ ameshika kupiga deki, kuosha vyombo, mtoto n.k.

wafanyabiashara na wajasiliamari ni bize...

sasa kuja kwa simu za Smartphone na vipindi vizuri vya TV na siasa kuchukua sehemu kubwa ya maisha; basi ubize umeongezeka_ asubuhi lazima uguse Facebook, na kundi la whatsapp limesema nini, bado hujafika kutazama picha nzuri instagram,  na sentensi fupi twitter...

unaporudi jioni, mama ni kupika,  baba taarifa ya habari, huku anacheza na simu mkononi akicheka na marafiki fb, na whatsapp...

TUMEKUWA BIZE SANA...

MPAKA TUNASAHAU....kuomba, Kusoma neno, kutafakari sheria na hukumu za Mungu, na namna ya kutenda kazi ndani ya ufalme...

Dada mmoja (jina nahifadhi)  nilipomwambia kuna wakati sipokea simu, sijibu sms, wala whatsapp hata kama sms ni nzuri_ Alisema nalinga, LAKINI: Naijua faida ya kutenga masaa ya simu, whatsapp, insta na fb.

***Sasa Siku ya Jumapili si siku ya BWANA TENA, bali ndiyo siku ya KUPUMZIKA...

Hata kanisani tunaomba ibada iishe mapema, ili tukale na kupumzika na familia nyumbani, na kuna rafiki ndiyo siku ya kuja kukusalimu.

huwezi kukataa "NI MAMBO MENGI LEO YANACHUKUA MDA WETU MWINGI, ambao, TUNGETUMIA KUTAFAKARI, KUPANGA NA KUMJUA MUNGU ZAIDI.

- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa ni mda wamaombi?
- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa wa kusoma neno
- Ni kipi kimeiba mda wako wa kutafakari
- Ni kipi kimechukua shahuku yako ya kushuhudia

- Ni kipi kimechukua pesa yako ya sadaka na kuchangia injili_ ni vocha au bando...

***Unafikiri ni hekima kusoma neno Dk 30 na kukaa mtandao Saa 1.30 na zaidi....Kuomba lisaa 1, na kukaa mtandaoni usiku Masaa 2. IS NOT FAIR, kweli IS NOT FAIR....

NAAMINI
Ukitazama nyuma kabla huna smartphone kuna vitu ulikuwa hufanyi sasa unafanya
kuna udhaifu ulikuwa huna, sasa unao
kuna dhambi inakutesa na ilikuwa haikutesi
kuna mda unamwibia Mungu...

Tunapokuwa Bize tuangalie TUSIMSAHAU Mungu wetu,
tuangalie TUSITENDE dhambi

YESU aliposema "Upendo wa wengi utapoa, alimaanisha alichosema, na alimaanisha kama alivyosema.

Ujumbe kwa wote_ We must Refocus_
#ChurchBACKtoFocus.

Written by
Ev. Ulenje
Director CWGM

Inspire by the Holy Spirit.
fungua ulenje.blogspot.com kwa masomo zaidi.

No comments:

Post a Comment