Friday, July 16, 2021

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI BORA WA YESU

25/06/2021, PREACHED 27/06/2021 AT VICTORY EMPOWERMENT TEMPLE 

FANYIKA MWANAFUNZI

WEWE NI ZAIDI YA JINSI ULIVYO. UNAWEZA KUWA ZAIDI YA JINSI ULIVYO LEO.


Yesu aliwakuta wanafunzi wake wakiwa wavuvi, hata Galilaya walikuwa hawafahamiki, lakini walipofanyika wanafunzi, wakafika mpaka kwa Wayunani, mpaka Asia. 
Unaweza kufanyika zaidi ya jinsi ulivyo leo, kwa sababu unaweza kufanyika mwanafunzi. Kufanyika mwanafunzi wa Yesu ni daraja la kukuvusha daraja la maisha, ni ngazi ya kupanda ngazi nyingine ya maisha. Kama unawaza wapi pa kuanzia ili upae kimaisha, basi anzia na kufanyika mwanafunzi wa Kristo.

Kusudi la Kristo ni Kujipatia Watumishi.

Math 28:19, Yesu anasema, “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Yesu anaweka wazi, anataka wanafunzi. Na ukweli hajatutuma kukufundisha bali kukufanya mwanafunzi. Yesu amekuokoa ili uwe mwanafunzi.
Yesu anasema “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; MATH 11:29.

Ukisoma mstari wa juu yake ‘28’ anasema “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”. Kusumbuka iwe mwisho_ umekopa sana kufanikisha mipango, umeomba, umetafuta, umelia_ leo nenda kwa Yesu_ kanunue Biblia sema “nitajifunza kwa Mungu nami nipumzike, nipate raha”

Kwanini uwe mwanafunzi?

1. Sababu mwanafunzi pekee ndiye unaweza kumbadirisha. 
Anayekufundisha anakufanya uwe mtu fulani_ na hasa anakufanya yeye alivyo. 
Yesu hataki ujifunze kwa dunia, kwa sababu ukijifunza kwa dunia utakuwa kama dunia. Ila ukijifunza kwa Yesu utakuwa kama Yeye. Yesu anasema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake”. LUKA 6:40. 
Yesu anataka uwe kama yeye. Na dunia wanataka uwe kama wao_ lakini wote hao ni wageni hapa duniani, Yesu ni zamani kuliko wote_ wote wameikuta Biblia_ na ina shuhuda ya kufanikisha wengi_ ni bora leo ukachagua kuwa mwanafunzi wa Yesu. 
Unapofungua Biblia na kusoma, unafanyika neno, unafanyika kama Yesu.

     ✅ Yesu Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu” MATH 4:19. Yesu anataka akubadirishe kutoka mtu fulani uwe mtu mwingine, 
Kila aliyeamua kufanyika mwanafunzi_ baada ya mda fulani, watu wakasema “siyo yule tunayemjua” wengine kwa mshangao wanasema “ni wewe kweli, au mwingine”
  Paulo anasema “Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ROM 8:30. TENA Anasema “tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 KOR 3:18.
Usijipime leo, Hayo unayopitia ni milima na mabonde tu ya njiani_ fanyika mwanafunzi_ wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo. Kuna mtu Yesu anamtengeneza mwenye utukufu zaidi ya ulio nao leo. 

2. Sababu anataka akujulishe siri za ufalme.
Ukishasikia siri, maana yake kuna watu maalumu wanaostahili kujua. Yesu hakuja kumwambia kila mtu siri za ufalme wake, bali wanafunzi wake pekee. Yesu anawaambia wanafunzi wake “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa” MATH 13:11. 


3. Sababu anataka akutumie.
Yesu hajawahi kutumia mtu ambaye hajafanyika mwanafunzi. “watu wengi walimwamini…lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; YOH 2:23, 24. Kumwamini haina maana yeye amekuamini, na sifa ya kumuamini siyo kuwa mkamilifu, bali kuwa mwanafunzi. Pamoja na udhaifu alio nao Petro, lakini Yesu alimvumilia na akamuachia kanisa, kwanini_ wakati wengine wamekimbia, yeye akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, YOH 6:68.
Mungu sasa anataka kutumia watu wa kila sekta, wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, waimbaji ili kujipatia mavuno na kutangaza jina lake_ ili kuipa aibu dunia… wewe fanyika mwanafunzi. Naye atakutumia. 

Siyo Kila Mtu ni Mwanafunzi.

Kwenye biblia kuna makutano na wanafunzi. Kuhudhuria kanisani na kuokoka haina maana wewe ni mwanafunzi.
Unaweza ukahudhuria kanisani miaka 40 lakini usiwe mwanafunzi, kwasababu uwanafunzi siyo miaka uliyookoka, wala uliyohudhuria kanisani, uanafunzi ni maamuzi, siyo kuhudhuria. Wote ni mashahidi hasa kwa walimu ambao wanachapa sana, tulikuwa tunahudhuria darasani lakini tunasikia lakini hatusikilizi. 
Yesu anasema “Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. MATH 13:14, 15.
15. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Tunajuaje kuwa wewe ni mwanafunzi?

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI WA YESU.

Tuone sasa namna, unaweza kuwa mwanafunzi. Ni vigezo gani mwanafunzi anavyo.

1. Mwanafunzi Analiamini na Kulikubali Neno Lote.
Siyo nusu, siyo moja_ yote. 
Yesu siku zote alitumia maneno magumu ili kuchambua wanafunzi na makutano. Biblia inasema “wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena” wakakimbia wote, wakabaki wanafunzi tu. YOH 6:64-69. 
 Nao akawauliza “Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Petro akajibu akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, Nasi tumesadiki, tena tumejua wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu”. Mwanafunzi anaamini yote. Paulo anasema “…nikiyaamini yote…” MDO 24:14. 
Na huwezi sema umeamini mpaka umekubali ulichosikia, umekipokea na kukitendea kazi ulichosikia. 
Huwezi sema ni mwanafunzi mpaka umekubali, na kukishika kile mwalimu amesema. Na mwalimu wetu ni Yesu, na shule yake ni Biblia. Na anatumia watumishi wake kukueleza alichoandika. Paulo hajaandika Biblia, Mathayo hajaandika Biblia, mimi sijaandika Biblia_ wote waliandika yale Roho Mtakatifu amesema, nami nahubiri yale Biblia imesema. Nami natenda hayo hayo na naona matokeo, na Mungu amenituma nisema nawe, ili tuinuke pamoja.


2. Moyo wa unyenyekevu.
Pasipo moyo wa unyenyekevu huwezi kumfundisha mtu yeyote. 
Mtu mwenye kiburi anajua kila kitu, hata ambacho yeye mwenyewe anajua kuwa hajui. Lakini atalazimisha kwa maneno mengi kuwa anajua. 
Watu kama hao_ hawawezi kuwa wanafunzi. Sababu wanaenda kwa Mungu, huku wakiwa na ya kwao. 
Wanasema Mungu tufundishe, lakini kama ni kinyume na aliyosema mjomba, bwana vicoba, hatuwezi kukusikiliza.
Hakuna kazi ngumu kama kumfundisha mwanafunzi mwenye tution nyingi.
 
Yesu anasema “kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa” LUKA 14:11. Unafikiri kwanini Mungu anainua wanyenyekevu, kwa sababu mnyenyekevu ni kama mtoto anabebeka (Math) anafundishika,
Mungu anasema “…Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. ISAYA 48:17

Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko. MITH 16:18.

3. Mwanafunzi wa Yesu  Anakuwa.

Sifa ya mwanafunzi ni kukuwa. 
Kila mwalimu anapima mwanafunzi wake kwa kukuwa katika kile anamfundisha. 
Haijarishi umetokeo wapi kwenye wokovu, lakini kila siku inabidi ukue kila eneo_ kuomba, kusoma neno, kuhudhuria ibada, kufunga, kushuhudia.
Yesu anasema “Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini. MATH 13:23.

4. Mwanafunzi lazima awe ametubu.

Yesu anapoanza injili yake tu_ akasema nini ufanye ili uwe mwanafunzi wake.
Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. MATH 4:17

Kutubu siyo kuomba msamaha, ni zaidi ya hapo. Kutubu ni kubadiri unavyowaza, kubadiri mfumo wa maisha.

Yesu anaweka wazi, nimewakuta mna ufalme wa dunia hii, sasa geukeni acheni kuwaza na kufanya kama dunia, sasa muwaze na kufanya mambo kama ufalme wa mbinguni unavyotaka.

Others
5. Usiogope watu
Huwezi kuwa mwanafunzi kama unaogopa watu wanasema nini. Sababu siku zote Yesu anakwambia mambo ambayo watu hawataki, ni kinyume na wanavyojua, ni kinyume na wanavyotaka uishi. Kilichomponza Sauli ni kuogopa watu, akaacha kufanya Mungu alichomfundisha.
Yesu akasema 
6. Jikane mwenyewe_ luka 14:26
7. Beba msalaba wako_ luka 14:27

Hitimisho.
Omba unyenyekevu na maombi ya agano_ kuwa wanafunzi. Na weka agano kutenda nini neno linasema.

Ushauri au maombi.
0683 477 827 
0718 721848