Monday, March 7, 2016

Part 5: MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

Bado Tunazidi kuchana Nyavu...
#SeminaKiganjaniMwako.

4.  Je upo Tayari Kubadirishwa, Kukosolewa, na Kuboreshwa

Moja ya hadithi niliyowahi kuisoma darasa la kwanza na  nisiyoisahau ni hadithi ya "Mti wa Mpapai uliogoma kwenda huku-na-huku kuufata upepo" upepo ulipozidi, mpapai ukaanguka.
Tunafahamu kuwa kila binaadamu ana udhaifu, ila Mungu ametupa uwezo wa kuwa wakamilifu: na hutumia watu wa karibu, matukio na majaribu katika maisha.
Naamini tunaingia kwenye ndoa si kushindana bali kukamilishana: ili kutimiza kusudi ambalo Mungu ameliweka katika maisha yetu.
1 Kor 11:11 "Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana"

Nikupe siri; Udhaifu wa mtu hugunduliwa na mtu mwingine hasa wa karibu yake sana" Dr Myles Munroe aliwahi toa mfano kusema "Ni vigumu kujua kuwa kiatu chako kinatoa harufu mpaka mtu mwingine akwambiye"

#Kama wote tupo kwenye safari ya kuelekea ukamilifu, na tunahitajiana ili kuwa wakamilifu, na tunafurahiana hasa pale tunapoonesha ukamilifu: basi kuwa tayari kuelimishwa, kupokea mafundisho mapya, fikra mpya, mipango mipya, na kuboreshwa baadhi ya tabia zako, ni MAANDARIZI YA MUHIMU SANA"

5. Je upo Tayari Kuacha Baadhi ya Vitu Unavyovithamini Kwaajili ya Mahusiano.

Idadi kubwa ya wachumba wameachana kutokana na kupishana na misimamo na mitazamo ambayo kila mmoja anathamini. Hata wanandoa wengi; mabishano yao makubwa mara nyingi, ni pale misimamo, mitazamo na fikra zinapogongana.
Misimamo; ni falsafa na mawazo ambayo mtu huamini kuwa ni sawa na yanapaswa kufatwa na wote ili kupata mafanikio.
#Kama hampo tayari kukaa chini na kujiandaa kupanga misimamo, mitazamo na falsafa ya pamoja na kuacha ya binafsi basi ni heri mkaomba pooooo! Kabla ya kusema ndiyo!! Na mkaendelea kukuza akiri zenu.

Maana mtakaposema ndiyo! Pasipo kuwa tayari kuacha baadhi ya misimamo ambayo inaweza kuwatenganisha, na kuunda misimamo ya pamoja; Itakuwa haina maana, sababu safari yenu itakuwa fupi.

6. Je Unaweza kulinda Maono yako; Huku Ukitimiza Kusudi la Pamoja.

Mwanzo 2:18;5:1
Hii ni mistari dhahiri inayoonesha kuwa Mungu ametuumba kutimiza kusudi moja pale tunapoungana na kuwa mtu mmoja; tofauti ni kwamba mmoja mjenzi, mwingine saidia.
Ila saidia asiyekuwa na maono, hafai, na mjenzi asiyekuwa na maono hafai kitu.
Saidia ni lazima maono yake yaendane na maono ya mjenzi, na kusaidia kusudi la pamoja kutimia.
Na mjenzi ni lazima maono yake yajulikane, yaendane na saidia wake; ili aweze kumsaidia.
Kusudi ni juu ya maono: Kusudi ni "Sababu ya wewe kuzaliwa" na maono ni "Kioo cha kutimiza kusudi lako na namna ya kufika kwenye kutimiza kusudi lako"

#Hivyo wote wawili muwe tayari kuunda maono yenu yaendane na safari ya kufika kwenye kusudi ambalo Mungu amewaumba kutimiza"
Haleluya!!!!

Sifa na Utukufu apewe Bwana
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu tunazidi kuenderea

1 comment: