Monday, April 24, 2017

UBIZE NA MUEREKEO WA KANISA.

BUSY AND WORK...

Bila kupinga tunaishi dunia ya watu bize sana,
asubuhi baba kazini, akifika ni bize, hata mama anayebaki nyumbani pia ni bize_ ameshika kupiga deki, kuosha vyombo, mtoto n.k.

wafanyabiashara na wajasiliamari ni bize...

sasa kuja kwa simu za Smartphone na vipindi vizuri vya TV na siasa kuchukua sehemu kubwa ya maisha; basi ubize umeongezeka_ asubuhi lazima uguse Facebook, na kundi la whatsapp limesema nini, bado hujafika kutazama picha nzuri instagram,  na sentensi fupi twitter...

unaporudi jioni, mama ni kupika,  baba taarifa ya habari, huku anacheza na simu mkononi akicheka na marafiki fb, na whatsapp...

TUMEKUWA BIZE SANA...

MPAKA TUNASAHAU....kuomba, Kusoma neno, kutafakari sheria na hukumu za Mungu, na namna ya kutenda kazi ndani ya ufalme...

Dada mmoja (jina nahifadhi)  nilipomwambia kuna wakati sipokea simu, sijibu sms, wala whatsapp hata kama sms ni nzuri_ Alisema nalinga, LAKINI: Naijua faida ya kutenga masaa ya simu, whatsapp, insta na fb.

***Sasa Siku ya Jumapili si siku ya BWANA TENA, bali ndiyo siku ya KUPUMZIKA...

Hata kanisani tunaomba ibada iishe mapema, ili tukale na kupumzika na familia nyumbani, na kuna rafiki ndiyo siku ya kuja kukusalimu.

huwezi kukataa "NI MAMBO MENGI LEO YANACHUKUA MDA WETU MWINGI, ambao, TUNGETUMIA KUTAFAKARI, KUPANGA NA KUMJUA MUNGU ZAIDI.

- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa ni mda wamaombi?
- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa wa kusoma neno
- Ni kipi kimeiba mda wako wa kutafakari
- Ni kipi kimechukua shahuku yako ya kushuhudia

- Ni kipi kimechukua pesa yako ya sadaka na kuchangia injili_ ni vocha au bando...

***Unafikiri ni hekima kusoma neno Dk 30 na kukaa mtandao Saa 1.30 na zaidi....Kuomba lisaa 1, na kukaa mtandaoni usiku Masaa 2. IS NOT FAIR, kweli IS NOT FAIR....

NAAMINI
Ukitazama nyuma kabla huna smartphone kuna vitu ulikuwa hufanyi sasa unafanya
kuna udhaifu ulikuwa huna, sasa unao
kuna dhambi inakutesa na ilikuwa haikutesi
kuna mda unamwibia Mungu...

Tunapokuwa Bize tuangalie TUSIMSAHAU Mungu wetu,
tuangalie TUSITENDE dhambi

YESU aliposema "Upendo wa wengi utapoa, alimaanisha alichosema, na alimaanisha kama alivyosema.

Ujumbe kwa wote_ We must Refocus_
#ChurchBACKtoFocus.

Written by
Ev. Ulenje
Director CWGM

Inspire by the Holy Spirit.
fungua ulenje.blogspot.com kwa masomo zaidi.

Sunday, April 23, 2017

Kanuni Moja MUHIMU, Kumtafuta Mungu Nyakati Hizi.

KUMTAFUTA MUNGU KATIKA NYAKATI HIZI

Kanuni MUHIMU,  Mimi naona ni muhimu sana, kwa kila mtu kuijua na kuiweka moyoni, na kuifanyia kazi.

Nianze na kusema, Mungu alisema kwa wana wa Israel "Mtanitafuta na 'kuniona', mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote" Ye

maana ya "kumtafuta kwa moyo wote" ukiipata, ndiyo mwanzo wa kuanza kumtafuta Mungu kama Mungu anavyotaka, na utakuwa ndiyo mwanzo wa kumpata.

NI KAMA HIVI...
Kijana mmoja akamfata mzee tajiri na kumwambia "nataka kuwa tajiri kama wewe", Yule tajiri akamwambia tuonane kesho saa nne asubuhi ufukweni mwa bahari.
kijana akashangaa " kuna uhusiano gani kati ya kutaka utajiri na kwenda ufukweni"
Tajiri akamsisitiza "unataka utajiri, kesho saa nne asubuhi njoo Ufukweni"
Kesho kijana akafika ufukwe wa bahari akiwa amevaa suti amependeza saa nne asubuhi, Tajiri akamwambia "anza kupiga hatua kuingia ndani ya bahari". Kijana akaanza kupiga hatua, maji yakafika magotini, Maji yakafika mabegani, yakafika mdomoni, tajiri anazidi kumwambia aende. Maji yalipofika puani, anashindwa kuhema, kijana akatoka haraka majini,  akasema "huyu mzee ana kichaa". Mzee akamfata kwa haraka na kumshika kichwa na kumzamisha kichwa ndani ya maji_ Kijana akaanza kuhangaika ajitoe,

maana alikuwa anashindwa kuhema. Tajiri akaendelea kumkandamiza ndani ya maji. kwa mda baada ya kijana kuhangaika sana, akamtoa. Kisha akamuuliza "Je! Unapokuwa ndani ya maji, nini hasa unataka?"
Kijana akajibu "nataka kuhema"
Tajiri akamjibu "Hadi utakapofika wakati wa kutaka utajiri kama unavyotaka kuhema, hapo utakuwa tajiri"

NINI MAANA YAKE...
Tuhamishe hii hadithi kwetu watu wenye fikra tofauti na ulimwengu,  sisi tumeagizwa kutafuta kwanza ufalme wa Mungu na mengine tutazidishiwa.

neno hili liki-ingia moyoni mwako,  KUMTAKA MUNGU KAMA UNAVYOTAKA PUMZI"

kati ya kitu muhimu sana kwetu ni pumzi, na tunahakikisha hatuipotezi_ na ndiyo HITAJI NAMBA MOJA KWETU.
Unapokuwa ndani ya maji, huwezi kutazama simu, TV, mama, Wala kumsikiliza mjomba, wala mume, au mke ila ni moja tu KUPATA KUHEMA..
Sidhani kama utakumbuka kula, au kuchati, kama unataka unatafuta pumzi, bali unachohitaji ni PUMZI TU.
UKIFIKA kumtaka Mungu namna hiyo_ Kuacha vyote na kushughurika na kumtaka kama unavyohitaji pumzi...
UTAKUWA UMEFIKA KUMTAKA KWA MOYO WOTE.

KANUNI YA PILI: Sema KANUNI namba 1 hata mara saba zaidi, asubuhi na jioni, mpaka uone inajisema yenyewe moyoni, hapo itakuwa imechukua maisha yako yote.
Sema nami
NIKIMTAKA MUNGU SANA KAMA NINAVYOTAKA KUHEMA NITAMPATA ZAIDI.
Ukifika kumtafuta Mungu, na kuona huwezi ishi pasipo Yeye, ukarudia kusema hata ikafika moyoni, itachukua moyo wako wote.
Jina la Bwana Libarikiwe

Contact: 0718721848