Thursday, January 21, 2021

NAMNA HII HUPONYA NDOA MARA 100 ZAIDI.


Jambo hili likikosekana, mwanamke atachanganyikiwa, Mwanaume atakuwa wa lawama siku zote.

Nimetazama ndoa nyingi za mwanaume mvivu asiyejua majukumu yake.

Mwanamke akitazama kila kitu alichovaa ndani na nje, simu na vocha, na kila kitu alichonacho, kimetoka kwa mwanaume, Si tu, Atajivuna kwa marafiki, Lakini ATAKUHESHIMU na UTAMTAWARA.

MUNGU hakumpa Hawa Bustani, alimpa Adamu, Mungu hajawahi kumwambia Hawa ailime bustani, bali alimwambia Adamu, hata neno la kusema "matunda ya kila mti wa bustani waweza kula" MWA 2:16 hakumwambia Hawa, alimwambia Adamu.

Ina maana jukumu la kula na huduma, ni la Adamu kwenye familia, siyo Hawa. Ndiyo maana siku moja, siku moja tu, haikuhitaji nyingi, Adamu alipopumzika na kumuacha Hawa akajitafutie chakula, ndipo shetani anajitokeza, na ndipo anguko la familia ya kwanza linatokea, na madhara hadi sasa duniani tunayaona.

Nionyeshe familia ambayo, mwanamke anahusika kutafuta chakula, nitakuonyesha familia ambayo shetani amejenga nyumba karibu nao. Na ipo siku atawadondosha, as matter of time. GOD FORBID.

Hata uchumba ambao mwanamke ndiye chanzo cha pesa unahitaji mabadiliko.

Mwanaume asiyefanya kazi na kuhudumia mke wake na watoto, asitegemee kupata heshima na asiwe na tarajio la kumtawara mke wake. Biblia inasema...

Mithali 12 24
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.

Ukiwa na bidii, bila hata kumwambia "niheshimu" bali akitazama wewe ndiyo chanzo cha kupendeza kwake, chanzo cha kula yake, chanzo cha kila kitu alichonacho. ATAKUHESHIMU automatic. Mwanamke anaheshimu sana chanzo cha heshima yake, shika sana hili neno.

Nikiwa nasoma chuo kikuu cha Dar es Salaam, nilikuwa nasoma huku nafanya biashara stendi ya Ubungo, asubuhi naamka naenda Kariakoo kufata bidhaa, ndipo naenda chuo. Jioni naenda kanisani kuonyesha sinema watu waokoke, nikirudi moja kwa moja maktaba kusoma, nilikuwa naomba mara nne hata zaidi kwa siku. Nilikuwa sina mkopo lakini kuna watu wenye mkopo niliwakopesha pesa.

Kwa neema ya Mungu sijawa pata Disco, Wala sijawa Carry, Wala sijawahi fanya SAP, Na bado msimu wa mvua nilirudi Morogoro kulima, maana nilikataa kula unga wa dukani kwenye maisha yangu, na mchumba wangu alitumia Smartphone ambayo mimi nilinunua na nilimuongezea pesa za kutosha katika biashara yake. Kwanini nilikataa kuwa mvivu.

Nakumbuka watu waliniita speed man, sababu nilikuwa natembea speed ni hatari.

Vijana wa kizazi hiki Mungu atusaidie tuache uvivu. Tuhudumie familia zetu. Bila kujali mke anafanya kazi gani, usihesabu pesa yake, hesabu majukumu yako.

Kama bado hujapata kazi inayoendana na elimu yako nikutie moyo, 2021 Inuka "Kabla hujapata unachotafuta kufanya, fanya kilicho mbele yako" (before you find what you finding to do, do what you find"

Suleman anasema Mhubiri 9 10
"Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.

Kabla hujafa kama masikini, angalau ionekane umejaribu kuushinda umaskini, maana hakuna aliyeandikiwa umasikini. Wewe ni mzao mteule, umeumbwa kwa mfano wake anaye miliki mbingu na nchi. You're Born A Winner, God can never birth a failure, even once.

Mwanaume ambaye mke wake ndiye anahudumia kila kitu, ni ngumu hata kumuuliza mke wako "unaenda wapi?" maana atakujibu "nisipotoka tutakula nini!, acha nitoke ile tule"

Ukiona ukiulizwa Ada ndiyo unaanza kuwa rohoni, jua kuna shida mahali.

Mwanume kuhudumia familia ni utukufu kwa Mungu, maana ndivyo alivyoumba, mmoja mfanyakazi mmoja msaidizi.

Nimalize kusema, Mithali 13 4
Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

Ukiwa mvivu utatamani amani ya familia, utatamani uheshimiwe, lakini hutopata.

Na kuna wanaume ambao ni wachapakazi, wana pesa ila si wahudumiaji wa wake zao. Ndugu haijarishi kiwango cha pesa ulichonacho. Mwanamke anaheshimu sehemu ya chanzo chake cha heshimu. Mwanamke anapoishi na mwanaume asiyehudumia, hujiona ni bora kuishi na masikini.

Aliyekwambia kumpa zawadi mchumba wako dhambi nani, hata asipokumbuka sms zako, atakumbuka fadhila na utu wako.

Na mwanamke unayesoma ujumbe huu kumbuka...

Mke mwema... "Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato" MITH 31:11.

Mwanamke aliyejiweka kuwa mchumba au mke mwema ni, Biblia inasema hatakosa mapato. Hata kama hatofanya, lakini kama wewe ni mke mwema hutokosa mapato. Juhudi yako, ya kuhudumia familia yako, mume akiwa mbali, itaamsha akili yake, na atakuamini na hutokosa mapato.

Nionyeshe mwanamke mchapakazi na ni mwema kwa mumewe, huyo ndiye ambaye Mumewe atamwamini, na hatakosa mapato.

Ubarikiwe Sana.
Kwa Msaada wa Roho Limeandikwa na.
Pastor Ulenje EM.
0683-477827
2021 INAWEZEKANA.


3 comments:

  1. Naomba soft copy ya vitabu ulivyoandika mtumishi

    Email yangu ni fmponda.tz156@gmail.com

    ReplyDelete
  2. Sorry kwa kuona comment yako late. Nitafanya hivyo. Remind me via 0683 477827

    ReplyDelete