Sunday, January 17, 2021

USIOGOPE, AMINI TU. MARKO 5:36.

 Mathayo 19 26 

 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.



Mungu anataka tufanikiwe,


Kumbukumbu la Torati 30 15 

 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;



Mafanikio siyo karama, mafanikio ni uchaguzi. Mungu amekupa kuchagua kufanikiwa au kushindwa. Ila amekupa ushauri, chagua mafanikio.


INAWEZEKANA


1. Ni Kumwambia Mtu, Kuna Njia ya Kufanya ili Hilo Jambo Lifanikiwe.


Inawezekana alijaribu akashindwa kama Musa. Au wenda amejaribu mara nyingi sasa ameona haiwezekani. Au mbele yake anaona giza, hakuna kitu anaona anaweza fanya tena.


Sasa unamwambia INAWEZEKANA.


Katika kila jambo ambalo Mungu anaruhusu litokee kwenye maisha yako, kila mpango una njia ya kufanya. Kuna kitu hujajua tu bado ndiyo maana hujafanikiwa mpaka sasa.


Kuna mambo siyo kwamba hatuwezi ila kuna sehemu, kuna kanuni bado hatuijui.


Katika kila jambo linaloonekana haliwezekani, ni kweli kwamba kuna njia ya kulifanya liwezekane. Hata unayoyaona leo yamefanyika, mwanzo yalionekana hayawezekani.  Mwaka 1904 wana sayansi walikutana Uingereza kuthibitisha kuwa hakuna kitu kinaweza tembea angani. Lakini Ndugu wawili watoto wa Wright maarufu kama Wright Brothers, waligomea maamuzi yale, wakasema inawezekana. Mwaka 1910 wakatembeza ndege kwa mara ya kwanza.


Siyo kwamba haiwezekani, Tatizo umekata tamaa, kutafuta nini unatakiwa ufanye. Bado ipo Njia.


Marko 5:

Mwanamke alitokwa na damu miaka mingi na kuteswa na madaktari wengi, lakini alipogundua njia ya uzima wake. Kuwa nikigusa pindo la Yesu nitapona, akapona. Usikate tamaa, bado kuna kitu unaweza fanya ukafanikiwa.


Si kwamba haiwezekani, ila hujapata mbinu ya Kufanya. Unajua kujua namna ya kufanya mambo kunaondoa miaka mingi ya mateso ba kutoa jasho.


Kumb 2:1-3 Israeli walizunguka miaka mingi ndani ya jangwa wasiione njia. Siku moja Mungu akasema mlivyozunguka mlima huu vyatosha, geukeni upande wa kaskazini.


Israel wakakata tamaa, kuzunguka mda mrefu, siyo kwamba njia ya kufika haikuwepo, ila hawakuijua.


2021 Mungu anakwenda kukupa njia ya kufanya katika Jina la Yesu. Pokea.


Israel walipata neno la Mungu, neno likawaonyesha cha kufanya. Petro alifanya kazi ya kuchosha neno liliposhuka likampa cha kufanya, Mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12 alisikia habari za Yesu.


Kuna neno unalihitaji likupe cha kufanya...


A. Soma neno, Yoshua 1:8

B. Omba, Yoshua aliomba. Yoshua 7:6

C. Tafakari, kaa chini fikiri... Mda unaotumia kulia, ungekaa na kufikiri Neno La Mungu linasema nini kuhusu jambo lako na mpango wako, ungekuwa umeshapata njia.

D. Omba ushauri. MITH 13:10.


2. Unamwambia mtu Ambaye Anaona Jambo Au Mpango Hauwezekani.


Wakwanza anaona hakuna njia, huyu wa sasa anaona haliwezekani kabisa. Anaona ni jambo kubwa sana. Anaona ni mpango mkubwa kumzidi. Anaona Ha! Ngoja niwaze mengine, hii ni ndoto tu ya utotoni. Au watu wengi ameona hawajaweza na wengine wamemwambia haiwezekani.


Lakini naomba sikia....


Hakuna jambo haliwezekani kwa mtu aliyeokoka isipokuwa jambo lile ameliona yey mwenyewe kuwa haliwezekani.


Yesu anasema anabisha yupo mlangoni anabisha hodi mtu akifungua nitaingia ndani yake UFUN 3:20.


Aliyeingia ndani yako, Yeye anaweza yote. MATH 19:26 hilo kwa wanadamu haliwezekani ila kwa Mungu yote yanawezekana.


Yoh 14:10 Yesu anasema "bali ni Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake"


Kol 1:29 Paulo anasema "nikijitahidi kwa kadiri ya kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu. 


Tangu ulipookoka Mungu anafanya kazi ndani yako.


Fil 2:13 Neno linasema "Ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, katika kulitimiza kusudi lake jema.


Mungu yupo ndani yako kufanya hilo jambo liwezekane, Mungu aliye ndani yako, kwake yote yanawezekana.


Math 17:20 anasema "

Mathayo 17 20 

 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.


Maana yake, Ukiona ugumu unaongezeka, badala ya kukata tamaa, wewe amini sana.


Kuona inawezekana ndiyo mwanzo wa kushinda mambo yanayoonekana hayawezekani.


__Yesu alimwambia Yairo (Marko 5:36) "Usiogope, Amini Tu"


Kumbe 2021 Mungu anaposema Yote Yanawezekana, anasema "Usiogope, wewe inua imani yako"


A. Kula chakuka cha imani_ Neno. RUM 10:17

B. Meng'enya hiko chakula_ Tafakari YOSH 1:8

C. Tendea kazi_ Tumia hilo neno. YAK 1:22

D. Usiyumbishwe_ EBR 10:34 usiyumbishwe kile umeamini unapoona ugumu unaongezeka au kwa maneno ya watu.... Yesu hana too late.



3. Unamwambia Mtu Anayeona Hana Uwezo Wa Kufanya.


Anajiona hana uwezo. Hana uwezo wa kifedha, elimu, ndugu, mtaji, upako.


Hakuna mlima mrefu kwa mwanadamu, mlima ni jinsi wewe unavyouona. Maana hata mlima mrefu kuliko yote duniani, watu wameupanda.


Mungu bado hajaumba mwanadamu ambaye hawezi kitu. Alipoumba akasema "ni chema sana" vingine vyote alipotazama akasema ni vema, lakini kwa mwanadamu akasema chema sana.


Mafanikio yana siri hii, Ukijiona huwezi hutoweza. Ila ukijiona unaweza utaweza. Simba siyo mnyama mwenye nguvu kuliko wanyama wote, siyo mnyama mrefu kuliko wanyama wote, wala siyo mnyama menene kuliko wote.... Ila yeye ndiye mfalme wa mwitu.


Kwanini anapokutana nao, wao wanaogopa, ila yeye haogopi yoyote. Hata wale wenye nguvu zana. Tembo anaangusha mti, ila anakutana na simba analiwa, kwanini simba anaona "pamoja ni mnene wewe ni chakula"


Ukiona huwezi hutoweza, kwanini "siku ukisema naweza, basi utatafuta njia kwa kila hari, na utaweza"


Mwanamke mjamzito miezi 8, ilipotokea hatari aliruka ukuta. Aliambiwa rudia alishindwa. Kwanini, mwanzo alipoona hatari, kuna kitu kilisema ndani yake. UNAWEZA.


HESABU 13 MUSA anatuma wapelelezi, Wanarudi wanasema nchi ni nzuri, ila wanajiona hawana uwezo wa kuitamalaki. Wote wanafia jangwani.


Lakini Yoshua na Karebu wakasema "twaweza kushinda bila shaka HES 13:30.


Wengi wanapishana na mafanikio yao, uponyaji wao, majibu ya maombi yao, na kushindwa changamoto sababu wanaona haiwezekani. Inuka sema INAWEZEKANA.


Wanasema "Hakuna cha kufanya" No "Kipo cha Kufanya"


Wanasema "Hakuna Njia" No "Njia ipo" 


Unajua kwanini wanaosema hatuwezi huwa hawawezi "Sababu huwa hawafanyi hiko kitu"


Wanajeshi wa Israel walipoona hawawezi kunshinda Goloathi hata kumfata hawakumfata... Lakini Daudi aliona anaweza, AKAMFATA.... Kwa Jiwe tu Down.


Unachokiogopa na kukiona ni kigumu.... Ni kidogo sana.


Tengeneza ufahamu kuwa Unaweza. Aliye ndani yako ni Mkuu Kuliko Chochote. 


Mungu anatembea na watu wanaosema "Haijalishi Ugumu, Itafanyika"


_________________________



LAKINI KUMBUKA....


Neno linasema "bali kwa Mungu yote yawezekana" 


Maana yake_ Lazima Mungu ahusike. Biblia ya Kingereza inasema "with God, All things are possible"


Mungu hawezi husika mpaka umeomba. Paulo alifanya mambo makubwa ambayo wengine walishindwa, siri yake anasema...


Filipi 4:13 "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu"


Mungu akikutia nguvu yote yatawezekana kwako.


Maombi, Maombi, Maombi.


Lazima 2021 Tuombe Zaidi ya Miaka Mingine, kama tunataka kufanya yaliyoshindikana yawezekane.


Unapoomba  Unapata Vitu Viwili.


1. Uso wa Mungu_ Unakutana na uso wa Mungu kukupa njia ya kufanya, na nguvu zake.

2. Mkono wake_ wa kukusaidia unapokwama. Israel walikwama Misri na kufanywa watumwa lakini kwa Mkono wake aliwatoa.

3. Roho Mtakatifu_ kusafisha njia na kukufanya iwe unstoppable, uwe na ujasiri, uwe na imani, kukufanya ufanye mambo ambayo wanadamu wa kawaida hawawezi.


Unabii unapotoka unatoka kwa wote, lakini ni maamuzi ya mtu binafsi kufanya unabii utokee kwenye maisha yake. Hauji kuomba kumridhisha mchungaji, ila ni kwa ajili yako, ili upige hatua.


Leo unaona unaenda, ila kuna hatua ili upige ni lazima uombe leo. Kila mtu anakutana na hatua zisizowezekana, na ni hatua zisizowezekana zinawafanya watu wakuzidi kiuchumi na kiroho.


0718 721848

0683 477827

Pastor Ulenje EM



No comments:

Post a Comment