Saturday, April 23, 2022

JUA UNDANI KUHUSU MAISHA YA MILELE

 *** MAISHA YA MILELE NA MWAMINI 


-( 1 Wathesalonike 4:13-18)

-Kwanini tunajifunza maisha ya milele? Ni muhimu sababu mtu ataweza ishi kwa kujizuia (mithali 29-18).

-Mtu anaejua Kuna maisha ya milele ataishi kwa umakini Sana

-MUNGU ametupa maisha ya sasa ili tujiandae na maisha ya milele


- MUNGU ametupa maisha ya sasa ni mchujo na kigezo kikubwa alichoweka ni utii Yani unae mtii ndie BWANA  wako

- Tamaa za shetani ni 

1)Tamaa ya mwili

2)Tamaa ya dunia

3)Kiburi Cha uzima


*Mwanadamu akifa anaenda wapi ??

- katika Agano la kale neno walilopata ni kuzimu (Zaburi 49-14) Yani walio haki na wasio haki wote wanaenda kuzimu ( Zaburi 88-3)

-YESU anakuja kutuonyesha kuwa kule kuzimu walitenganishwa walio haki na wasio haki ( Luka 16-19) YESU anatuletea neno peponi na jehanamu.


-Mtu asiyeokoka akifa anaelekea jehanamu ( Marko 9-45)

-Mwenye haki akifa anaelekea peponi( luka 23-43)

- peponi sio mbingu mpya peponi ni Mahali pa kufarijiwa

-Jehanamu sio Mahali pa mwisho kwa wasio haki Mahali pa mwisho ni kwenye ziwa la moto ( ufunuo 21-13)

- Walio haki wakifa wanaelekea peponi wakisubili pia hukumu kwa matendo ya mwili waliofanya baada ya kuokoka .

- peponi sio Mahali pa mwisho kwa waliokoka Bali ni mbingu mpya ama yerusalem mpya biblia inasema Mahali huko  ni pazuri hamn mfano Kuna Kuna dhahabu Safi Kama bilauri pia Kuna kuta nne ambazo marefu na mapana yake zimefanana kuta zimepambwa na madin Kama zumaridi  ,yakuti nk

- katika yerusalem mpya hutokumbuka maumivu 


* Nini maana ya kufa kwa mwamini ???

-Ni kuondoka toka mwili huu wa batili na kwenda kukaa na BWANA(2 Wakorinto5-6)

- Paulo alitamn kukaa na BWANA (wafilipi 1-21)

-Paulo anasema tuziweke kando zile dhambi zinazotuzuia( waebrania 12-1)


* Unaishi kwa ajili ya Nani???

- MUNGU anasema mbele yenu nimeweka uzima na mauti Ila chagueni uzima ( kumbukumbu la torati 30-19)

-(wafilipi 1-21)

-(warumi 6-21)


* Kiti Cha hukumu Cha KRISTO 

- Kwa walio haki

-wafu watafufuliwa kuungana na walio hai siku ile ya parapanda kuu ( 1wakorinto 15:50-53)

-(warumi 14-10)

-(2 wakorinto 5-10)

- sisi tuliokoka hatutahukumiwa pamoja na wasiokoka sisi tutahukumiwa maisha yetu baada ya kuokoka 

- Paulo anasema wengine kazi zao zitaungua Kama nyasi anasema wataokoka Ila kwa Moto 

 

* Vitu ambavyo tutatolea hesabu 

1)namna gani umeshiriki kuleta watu kwa KRISTO ( Daniel 12-3)

2) kwa habari ya ulimi 

3) kwa habari ya kushindwa dhambi( warumi 6:1-4)


-From pastor ulenje EM

Written by kayombo jr

No comments:

Post a Comment