Tuesday, May 2, 2023

ROHO AKIJA ANAMBADIRISHA MTU NA MAISHA YAKE

ROHO MTAKATIFU ANABADIRISHA MTU NA MAISHA.

ROHO NI NANI?

- MUNGU anasema ni Roho yake - Yoel 2"28

- Yesu anakuja kusema Roho Mtakatifu - Yoh 14"26. 

- Ina maana utakatifu upo ndani yake, ndiyo sifa yale kuu [ Roho ni mtakatifu na ana nguvu ya kumfanya mtu kuwa mtakatifu]

○ Rum 15"16, 2 Thes 2:13, 1 Petro 1"2

- Roho anakuja ameonekana anakuja na nguvu - Luka 1"35, Mdo 1"8


ROHO ANABADIRISHA MTU NA MAISHA.

1 SAM 10"6,7

- Roho anakufanya kuwa mtu mwingine, tofauti na yule wa kwanza.

- Unapofanyika mwingine, unapewa uwezo, mamlaka ya kufanya chochote uonavyo vema.

- Kuokoka ni kufanywa upya kabisa, na Roho ndiye anahusika katika kukufanya upya

Tito 3"5 - si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;

Yesu alipojiliwa na Roho akawa mwingine.

- Yesu bila Roho alikuwa ni mtu wa kawaida, Sababu Yesu ni alichukua asili yetu, akawa kama mwanadamu.

- Ila ile Roho ndani yake ikamfanya kuwa Mungu yaani Kristo.

- Kilichofanya aseme Yeye na Baba yake ni sawa siyo muonekano wa nje, bali ni ndani.

- Alipojiliwa na Roho akawa mwingine kabisa na kuanza kufanya makubwa.


- 1 Sam 16"13

- Daudi alipojiliwa na Roho akawa mtu mwingine kabisa.

- Ndipo watu wakaanza kumfahamu Daudi, lakini hakuna aliyemjua hapo kwanza.

- Pasipo Roho unaweza tia bidii ila zikawa si kitu sababu unakuwa kama wanadamu wengine. 

- unapofanyika mtu mwingine maisha yako yote yanabadilika, ndiyo maana kila aliyejiwa na Roho maisha yake yanabadilika kuanzia na hapo. Ukisoma mifano ya Yusufu, Musa, Daudi, Sulemani, Nabii Eliya, Yesu Mwenyewe, Wanafunzi wa Yesu, na hata leo tunaona mtu anapofika kiwango cha kujaa Roho maisha yake yanabadilika kabisa na kupata sura mpya.


Ubarikiwe kwa Kusoma

Mimi ni Pastor Ulenje 

Tiktok kama Pastor Ulenje 

Facebook kama Pastor Ulenje Online 

+255 683 477827


No comments:

Post a Comment