Friday, November 20, 2015

SEHEMU YA NNE: BARAKA TANO ZA PETRO (KANUNI ZA KUTUMIA LEO YAKO)

MAISHA NI NINI

Hili ni zaidi ya swali, kila mtu anayeweza kupata mda wa kufikiri maisha yake (experience) atapata kusema kuhusu maisha.
Maisha ni neno gumu kujua.

“Unaweza kuwa na maana nyingi kuhusu maisha, ila mapito yatakwambia ukweli”

Hii ni sehemu ya nne ya somo letu, leo tutaangalia sana kuhusu maana ya leo, leo ni nini, pia tutaangalia fikra tofauti za watu na namna inavyoathiri kutumia leo yao.


Maisha ni mda, ni mda uliopimwa au usiopimwa, maisha hupimwa na mda. Na kama ni mda usiyoweza kuhesabika hayo ni maisha ya milele, na kama ni mda unaohesabika basi hiyo ni miaka ya kuishi.

Huwezi taja miaka ya Mungu, ila unaweza taja miaka yako, huwezi taja miaka ya mtu anayeishi milele.

Mda wa kuhesabu miaka ni ule unaokuwepo hapa duniani pekee, ukishaondoka na kufa basi sasa unaelekea kwenye maisha ya umilele, huwezi huko tena kuhesabu miaka. Maisha ya hapa duniani ya yanahesabika na kila mtu kapewa kwa kipimo maalumu

“Maisha ya hapa duniani ni mtihani wa kuona uwezo wetu wa kuishi milele”

Jinsi unavyotumia mda wako duniani, utavuna baada ya kufa” Hakimu wa Haki Yesu hatoangalia umeishi miaka mingapi, ataangalia umeishi vipi.

"Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe" Ayubu anazungumzia maisha ya mwanadamu kuwa siku zake zimeamriwa yaani zina kikomo na kikomo kimeshapangwa/kimeamriwa na tayari na kipo mikononi mwake.  "mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu, naye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa, hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe" Ayubu 14:1-2,5.

Nimetamani ujue kuwa siku zetu za kuishi hapa duniani zimepimwa, na zimeamriwa, zina mwanzo na zina mwisho.

Mwandishi wa Zaburi anamuomba Mungu "basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie hekima" Zaburi 90:12, alianza kusema "Bwana, unijulishe mwisho wangu, na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; nijue jinsi nilivyo dhaifu" Zaburi 39:4.

Hii yote yatuonesha maisha ya hapa duniani ni mda na kama mda una kipimo basi maisha yako yana kipimo na ipo siku yatafika mwisho,

Swali unaendaje na wakati huo uliopimwa, na unataka uwe umefanya nini ndani ya masaa hayo.

Nakuthibitishia kuwa wakati wako ukifika mwisho utaondoka tu hapa duniani
Usiwe kama Mfalme Hezekia, wakati wake ulipofika Mungu akamfata na kumwambia “atengeneze mambo ya nyumba yake, lakini Hezekia akatafsiri tofauti, Mungu hakuwa anamlaani bali anamtaarifu kiwa katika ugonjwa huo bado itakufa. Lakini alipoomba sana, Mungu ni msikivu akamsikia. Lakini kwa kuongeza siku hizo chache, Kwanza siku Hezekia akakosea, Biblia inasema baada ya kupona, hakumpa Mungu utukufu, akawaonesha wageni milki yote ya nyumba ya Israel, Sasa hezekia aliyeomba kuongezewa mda, unajua nini kilitokea tena, Hezekia akautumia ule mda kumzaa mtoto Manase, Manase akawa mfalme mbaya kuliko wafalme wote waliopita na waliyokuja katika israel.

Tumia mda wako vizuri...

“Nioneshe sababu nyingi za kushindwa maisha, mimi nitakuonesha moja, ni kughairisha.

Acha kughairi ghairi, kila siku nitafanya nitafanya. Sulemani anauliza E mvivu utaamka lini?
Anza kufanya leo jambo unaliona bado. Kuna wakati utafika hutoweza kufanya.

Usitumie mda wako mwingi kutaka kumpendeza kila mtu. Usitumie mda wako kujaribu kufanya kila kitu, jitambue wewe ni nani, umezaliwa kufanya nini na nini unapata hamasa kubwa unapofanya, pesa zitakufata mbele.
Kumbuka hadithi ya Martha na Mariamu. Martha akaanza kuhangaika hangaika akitaka kumpikia Kristo na kufanya kila jambo, Martha akatulia miguuni pa Yesu akimsikiliza; akaacha mengi na kushughulika na moja tu: Ufalme wa Mungu.

“Nioneshe sababu bilioni za mwanadamu kutotimiza kusudi lake, nitakuonesha moja tu, kujaribu kutaka kufanya kila kitu”

Tumia nusu ya miaka yako hapa duniani kufanyika mtu halisi uliyezaliwa kuwa, na tumia mda wako wa mwisho kufanya ulichozaliwa kuwa.

Andrew Carnegie baada ya kufa, walipoenda kwenye nyumba yake, wakapata karatasi ndogo. Mr Carnegie aliandika akiwa na miaka 20 “Nitatumia mda wangu wa mwanzo kuwa milionea, nitatumia nusu ya pili kugawa zote”.
Mr Carnegie alikusanya Dola za kimarekanj zaidi ya milioni 450 na anapokufa akawa amegawa zote.
Inaleta raha.

Usipoteze mda muhimu katika mambo yasiyo muhimu. Heshimu mda wako, watu wengi wanaotazama TV sana huwa hawaji kuonekana kwenye TV, wakoonekana si kwa mema.

Jim Rohn amewahi kumuuliza mtu, gharama ya TV, yule mtu akajibu $12 akamwambia hapana, gharama ya TV ni $12,000 kwa mwaka. Kwanini, watu wengi wanahesabau gharama ya kununua TV na siyo ya kutazama TV. Rafiki yangu kila kitu unachokipa mda, usisahau unakipa sehemu ya maisha yako. Maana mda ni maisha.

Twende pamoja, heshimu mda wako,  kwa maana ndogo kuheshimu dakika moja ni kuheshimu sehemu ya maisha yako.

Maisha yamegawanyika katika Jana, Leo na Kesho.

Lazima tuiheshimu jana, najua umefundishwa kutotazama jana. Lakini kutazama jana ni vema: tazama jana kwa namba ulizoongeza kwenye akaunti yako, thamani yako iliyoongezeka kwa Mungu na kwa jamii, tazama umefanya nini mpaka sasa, narudia tazama umefanya nini mpaka sasa?.

Kuna kanuni inasema utavuna ulichopanda. Kutazama jana inakusaidia kujua uliponda nini jana na ulipandaje na ulikuzaje; na maana ulivyo leo ni mavuno ya ulichopanda jana.

Tazama jana na ugeuze yote yaliyotokea kwako na yote uliyokosea na kupatia na kuyageuza kuwa falsafa na mbinu mpya ya mafanikio.

Yaliyotokea jana na uliyokosea jana yanaweza kufanywa na kuwa mbinu ya mafanikio ya leo. Unataka uthibitisho: jaribu.

Leo ni siku ya baraka: hakuna zawadi nzuri kama leo.

“Mtu anauliza, Je naweza kubarika, jibu rahisi; Ndiyo unaweza,
Anauliza lini sasa jibu rahisi siku utakayoamua kubadirika

Yaweza kuwa kesho; No! Mwambiye siku yoyote inayoitwa Leo.

Kesho ni ajabu; inaweza kuwa njema, inaleta tumaini, inaleta furaha.
Kwanini ukate tamaa wakati huijui kesho.

Tufatane pamoja ili tujue maana ya siku zote tatu: Jana, Leo na Kesho.

A. JANA
Jana ni sehemu ya mda ambao mtu ameutumia ndani ya kipimo cha maisha yake.
Jana ni marighafi au nguvu isiyoweza kurudi wala kuzalishwa tena. Jana ni sehemu ndogo sana ya mda uliyopewa na Mungu kuishi na kutimiza kusudi lake hapa duniani.
Wanafunzi wa chuo kikuu kimoja  cha hapa Tanzania, walijikuta kwenye wakati wa kununua moja ya vinywaji maarufu na vya gharama duniani kwa gharama ya kutupa, kwa bei ya hasara, kwanini zile bidhaa zilikuwa zinaelekea kuisha mda wake wa kuishi (expire date), baada ya mwezi mmoja zingekuwa zimeshaharibika. Jinsi bidhaa inavyokaa dukani ndivyo inavyozidi kutumia mda wake wa kuharibika na kutumika.

Jinsi binaadamu anavyotumia masaa 12 ya siku na kuingia masaa 12 ya siku nyingine ndivyo anavyozidi kuupunguza ule mda aliyowekewa au kuamriwa tayari na Mungu kama muandishi wa Zaburi alivyothibitisha, na ndivyo kweli.
Hivyo kama ulipewa siku 1000, 000 za kuishi hapa duniani, jana ulipoitumia sasa una 999,999, bila ubishi.

MAMBO YA MSINGI KUHUSU JANA
1. Huwezi kuigusa tena jana
2. Huwezi kufanya chochote ndani ya jana
3. Huwezi kusahihisha ulichofanya jana
5. Una nafasi ya kurekebisha matokeo ya uliyofanya jana pekee na si kufuta ulichofanya.
6. Jana ni historia, si hatima ya maisha yako.
7. Wakati wa msiba wako hawatakumbuka ulichotaka kufanya jana watakumbuka ulichofanya pekee.
8. Ulivyo leo ni matokeo ya uliyofanya jana
9. Kukumbuka na kuhuzunika ya jana ni kupoteza wakati, hekima ni kutazama nini unacho na unaweza fanya leo.
10. Jana inapaswa kutumika kama elimu tu ya leo, ulikosea wapi, ulikoseaje, na namna ya kurekebisha
11. Waliyokufanyia jana; unaweza kuyarekebisha leo
12. Leo ina nguvu zaidi ya jana.
13. Huwezi kuipata tena jana. Imepita

INAWEZEKANA...
Ndugu mpendwa inawezekana jana ulikuwa ni masikini sana, au hata leo, inawezeka jana umetenda dhambi, ninaposema jana nasema kwa wakati uliyopita iwe ni robo saa iliyopita au miaka kumi au hamsini iliyopita au sekunde moja iliyopita, inawezekana umekuwa mtumwa wa pesa, au inawezekana umekuwa ni yatima wazazi wamekufa, au una maisha hayo kwasababu ni mjane hivyo upo hivyo kwasabau ya uliyotebdewa jana, inawezeka upo hivyo kwasababu ya waliyokufanyia jana.
Inawezekana kampuni yako imeshuka kutoka na waliyokufanyia watu jana, washirika wa kampuni yako wamekusaliti, umepata hasara, umefanya uzembe fulani. Au namna yeyote ile.
Na sasa kuna maisha unayoishi, au kuna hari kampuni yako inapitia, lakini hiyo ni jana, tuzungumzie leo, itakusaidia kutoka maisha ya chini kuelekea maisha ya juu zaidi.

Usitazame jana, maadamu umeamka. Jifunze tu kanuni za kutumia leo yako vema.

Jifunze kanuni kuhusu leo.

Jana imepita achana nayo, jifunze tu ulikiseaje kupanda mbegu zako, au ulipanda mbegu gani. Panda mbegu njema sasa na uitunze na kuilinda mpaka iote na linda mazao mpaka uvune.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA


Karibu tena Siku sehemu inayofata, tutaona fikra tofauti kuhusu jana na kuenderea na somo letu.

Asante kwa kusoma
Mungu akubariki.
Ev.Ulenje.

Tuesday, November 17, 2015

SEHEMU YA TATU: BARAKA TANO ZA PETRO

SEHEMU YA TATU
BARAKA TANO ZA PETRO

JINSI PETRO ALIVYOTUMIA LEO.

Leo tuangalie kiundani kuhusu Petro na uhusika wake katika maisha ya Yesu akiwa duniani. Na pia tuone namna Petro alivyoweza kutumia leo yake aliyopewa na Mungu kwa neema. Na tuone namna alipotoka na namna alivyoweza kubadiri maisha yake na namna alivyoweza kuendana na baraka alizopewa hata zikaweza kutimia.

UHUSIKA WA PETRO

Petro alikuwa Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi na muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.

Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvua samaki na si kukaa na familia.

2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.

3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.

4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumuokoa Kristo asiteswe na Wayahudi na kufa japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.

5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanazungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuwa hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.

6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20

7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 11 waliobaki. Siku zote alitazama “maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari”.

8. Petro aliwaza chanya siku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwahi ona kitendo hiko toka azaliwe, akaamini akaenda, alipoambiwa habari za wokovu kwa mataifa katika maono, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ya jana, na kuwaza positive.

9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.

10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.

11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
“Tunashinda woga kwa kufanya tunachokiogopa kufanya”
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
“Unataka uijue siku ya kuanza kufanikiwa KiMungu, ni siku utakayoanza kufikiri kwa habari ya wengine”

5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
Akimaanisha “mwanaume shujaa ni yule mwenye uwezo wa kusimama peke yake”

7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa za leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15

Zote hizi tutaziangalia kiundani na kuzichambua kiurahisi zaidi ili kila mtu afahamu.
Namna alivyozipata na namna zilivyomfikia na namna zilivyotimia kwake.
Ila kwanza tuangalie maana ya jana, leo na kesho kiundani na kimafunuo zaidi.


MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, rafiki yangu mmoja akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika na hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana,
Akanitazama kwa makini na kuniambia "unajua Ulenje nilikuwa na akiri zaidi hata yako", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Yule rafiki hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.

MDA NI NINI...
Mda una maana nyingi ila huwezi kupinga hii.
Kifupi Mda ni maisha
Mda ni maisha yenye mwanzo na mwisho.
Mda si wa milele kama maisha ya milele, maisha ya milele hayana mda, huwezi kuyapima, yenyewe ni ya milele, yapo na yanaendelea kuwepo.
Unapotamka mda unazungumzia kipimo chenye mwanzo na mwisho. Unapotamka maisha niliyokaa shule, unatamka mda uliyokaa shule, ukihesabu kuna kipimo. Unapotamka nina miaka sabini unatamka mda uliyokaa duniani ni miaka sabini. Hivyo mda ni maisha, yana kipimo, yana mwisho.
Yesu anasema "imetupasa kufanya kazi zake yeye aliyenipeleka (nani?, Mungu) maadamu ni mchana; usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi"

"Yesu alipokuja alipewa mda wa kukaa ulimwenguni, na ilimradhimu kukimbizana nao: kwanini mda una kipimo”.
Ukipewa kazi ya kufanya kwa siku moja, maana yake yake ni masaa 12.
Moja ya huzuni ambayo huwa naisikia kwa wazee na watu wazima wenye miaka juu ya 50 wengi kila ninapopata mda wa kukaa nao, huwa wanasema "tulitamani kufanya mengi sana, tulipokuwa vijana kama ninyi, ila mambo yakawa mengi tukashindwa". Kwanini mda umeisha, kwa wao kufanya hayo, walipewa mda wakajisahau wakadhani wana umilele. Ila lipo tumaini toka kwenye kitabu hiki, kuwa hata kama una miaka 80 bado inawezekana.
Bado kwako unayesoma kitabu hiki, una miaka 20, 30, 35,  40, 45, 50, 55, 60, 65, 70, au yeyote ndani ya hiyo; jua kuna wakati utafika hayo unayoyafikiri hutoweza kuyafanya, na yataishia kwenye fikra zako tu.

MAISHA NI NINI...



Fatana nami tutenderea...
UBARIKIWE KWA KUSOMA.
By EV.ULENJE MWAIPUNGU