Thursday, December 31, 2015

2016 BWANA ANAKUWAZIA MEMA, WEWE JE?

WEKA ALAMA, JENGA JINA JEMA KATIKA UFALME WA MUNGU.

2016 ndiyo hii,
Mengi twaweza kuyafikiri kuyafanya, katika mwaka ujao.
Jambo la kufikiri, mwaka unapoisha, utakuwa umefanya jambo watu watazame au utakuwa unatazama watu waliyofanya.

Maana kuna watu hupokea mwaka kwa kufurahi kuongeza umri na wengine hutazama nini wamefanya.

Mfano: mtu mmoja alienda kwenye duka wanalouza ubongo. Muuzaji akamwambia kuna aina nne za ubongo. Akaanza kumuonesha aina:
Akamuonesha aina ya kwanza, ni bongo waliyofanikiwa kugundua Satelite, ndege, na magari, akamuonesha aina ya pili, ni wale waliyofanikiwa kugundua radio, simu, na television, akamuonesha aina ya tatu waliyofanikiwa kugundua kutengeneza majumba ya kufahari, madaraja na hoteri za kisasa, akamuonesha ubongo aina ya nne, ambao wao hawajafanikiwa kugundua chochote, wao hata kujenga vyoo vy ikulu huwaita watu toka nje kuwajengea
Mnunuzi akauliza bei, na kuambiwa bongo za kwanza mpaka namba tatu ni bei rahisi sana, ila ubongo wa mwisho ni aghari sana huwezi kununua, mnunuzi akashangaa inawezekanaje ubongo ambao hawajafanya chochote kuwa aghari zaidi ya bongo waliyofanya vitu vikubwa.
Akamwambia huu ubongo una uwezo mkubwa ndani yake, ambao bado haujatumika.

Mwanzo wa somo:
Dr Myles Munroe aliwahi sema, mari na utajiri haupo kwenye migodi, wala haupo kwenye visima vya mafuta.
Bali utajiri upo karibu na nyumba yako, utajiri upo kwenye makaburi.
Mungu akiyatazama makaburi anahuzunika, maana anaona nyimbo ambazo hazitoweza kuimbwa tena, anaona mahubiri hayatoweza kuhubiriwa tena, anaona vitabu havitaweza kuandikwa tena, anaona sadaka zilizo bank hazitoweza jenga makanisa tena, anaona vipawa havitaweza kutumika tena, anaona karama hazitaweza kutumiwa tena.
Hamu ya Mungu ni kuona kila mtu aliyemuumba na kumuokoa anafanya kazi aliyomuumba kuifanya.
Na ufahari wa Mungu ni pale mtu aliyemuumba na kumuokoa anafanya kazi aliyomuumba kuifanya.
Fahari ya Toyota inapofanya kazi kwa mtengeneza toyota, na toyota inakuwa na jina jema inapofanya kazi iliyoumbiwa kuifanya.
Vivyo hivyo na fahari ya simu inapofanya kazi, ni kwa mtengeneza simu, na simu hujenga jina jema pale inapofanya kazi iliyotengenezwa kuifanya.
Fahari ya Mungu ni pale bidhaa aliyoitengeneza inafanya kazi, aliyoiumba kufanya. Na jina jema hutengenezwa na mtu pale anapofanya kazi aliyoumbiwa kuifanya.

Mithari 22:1
Mhubiri 7:1
Sulemani anasema ni heri siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.
Watu wanaogopa hasa siku ya kufa. Na siku ya kuzaliwa huwa ni siku ya sherehe kwa kila mtu, watu hufurahi na kufanya na sherehe, lakini Suremani anasema hiyo siku si heri. Siku ya msiba watu wanalia na kuomboleza, Sulemani anasema hiyo siku ndiyo heri. Hapa kuna kitu Sulemani anajua sisi hatujui.
Paulo alipofika wakati wa kufa kwake, akasema vita nimevipiga mwendo nimeumaliza na imani nimeilinda, anasema mwendo ameumaliza. Hakuogopa kufa kwasababu alijua mwendo ameumaliza: kazi ameimaliza.
Yesu hakuogopa kufa, hata akasema imekwisha, kwanini hakuogopa kufa, sababu alijua kazi yake ameimaliza.
Ukiona kazi umeimaliza, kufa inakuwa ni sawa na kuingia ndani ya chumba, unahamia sehemu nyingine.

Kitu cha kwanza kwa mtoto kukishika ni jina lake, hata kama atakuwa hajui kuona au kuongea, hata kutambaa, mama atamrazimisha alijue jina lake, kwa kumuita kila wakati.
Hata akifika shule, ni ufahari kwa walimu na wazazi wanapoona mtoto wao anajua kuandika jina lake. Hii inanipa kukua kuwa jina lina umuhimu sana.
Nilipokuwa utotoni nilidhani maana ya jina ni herufi, kama I. M. A. N. U. E. L na kujua kuwa ni kutoka na jina lilipotokea mfano Mungu pamoja nasi kwa jina la Imanuel, ila baada ya kusoma vitabu, Biblia, kusikiliza mahubiri na maisha binafsi nikaja kugundua maana ya jina ni zaidi ya nilivyofikiri.
Kuna watu wenye majina mazuri kama John, Jane, Petro, Happy, Precious, Michael, wanakosa kazi na watu wenye majina kama Mwantumu, Mboneghe, Nailejileji, wanapata kazi.
Nikagundua maana ya jina inatokana na alama uliyoweka.

Kwanini watu wanapenda majina kama Mathayo, Petro, Yohana, Daudi, Sarah, prisca, Rahabu, au Mary.

Kwanini wasiwape watoto wao majina kama Goliath, Ahabu, Yezebeli, Nebukadreza, Pilato, Herode, Iddi Amini, Senokarebu au Mabutu
Kutokana na alama waliyoweka.

Mtu aliyeweza kufanikiwa kutumia kiasi kikubwa cha ubongo kuliko wanadamu wote Albert Eastern aliwahi sema "Jaribu kuwa siyo mtu wa mafanikio, bali mtu wa thamani...maisha yanayo ishi kwa ajili ya wengine ndiyo maisha ya thamani"

Matendo na utumishi wa mtu ndiyo hujenga alama, na alama inajenga jina.
Kwahiyo; alama ya mtu inajengwa kutokana na matendo aliyofanya na utumishi aliyotumika.

Mfano Luka 7:1-5.
Akida Mrumi, aliyepatwa na tatizo la mtumwa wake kuumwa. Alipowatuma wazee kwenda kumuomba Yesu amponye mtumwa wake, wale wazee wakamwambia Yesu, "amestahili mtu huyu kutendewa jambo hili, maana analipenda taifa letu, ametujengea na hekalu".

NAMNA YA KUWEKA ALAMA, ILI KUJENGA JINA JEMA KATIKA UFALME WA MUNGU.
Ziko njia nyingi, ila leo tuongelee utumishi.
1. Tambua maono ya kanisa, na ujiunganishe nayo.
Maono ni kuona mbere kwa hekima. Nini kanisa au mchungaji anatamani kufika, au anatamani kanisa lifike. Kuna maono ya mda mfupi na ya mda mrefu, jiunganishe nayo kuhakikisha yanatimia.
Usipotambua maono ya kanisa utajitafutia mambo yako mwenyewe, utatumika, na kuishia kufanya mambo yanayoonekana hayana maana.

2. Tambua wewe ni nani, Kwanini uko hapo, na Unaweza kufanya nini.
Usipojua wewe ni nani utajitumia vibaya. Utafanya yasiyo yako.
Usipojua kwanini uko hapo; utapoteza mda na usifanye ulichopaswa kufanya, na hautofurahia maisha ya kuwa hapo.
Usipojua unaweza kufanya nini; utajaribu kufanya kila kitu, na kujikuta mpaka siku yako yako ya kufa, bado hujafanya chochote.

3. Kuwa chanzo cha mabadiriko:
Kuna watu kanisani ni waanzisha mabadiriko, na wengine washangaa mabadiriko.
Wanaoshangaa mabadiriko hawatengenezi jina, wanaosababisha mabadiriko, huweka alama na kujenga jina jema.

4. Kuwa sababu ya suruhisho la matatizo kanisani.
Kuna watu kanisani husababisha matatizo, hujenga jina baya na wengine ni suruhisho la matatizo; hujenga jina jema.
Kumbuka kushindwa kutoa suruhisho na wewe unakuwa tatizo.
Kama tatizo ni keyboard kanisani na washirika hawawi suruhisho la kupatikana na wao wanakuwa tatizo. Wataitwa washirika wasiyotoa michango. Wanakuwa tatizo kwa mchungaji, akijiuliza awafanyaje ili watoe.

5. Jitoe sadaka: kuwa wa kujitolea
Wakisema tunahitaji mtu, usiwe mtu wa kurudi nyuma, songa mbele, wanaosonga mbele hujenga majina mema, wanaorudi nyuma hawajengi majina.
Filipi 1:23.

6. Ishi kwa ajili ya wengine: Jitoe kwa ajili ya wengine.
Fanya kuona wengine wananufaika
2 Timotheo 2:10
Kuwa sababu ya wengine kufurahia ibada.

7. Usisubiri fanya (Just Do It)
Kampuni ya Nike mwaka wa 1988 January ilikuwa na utajiri wa dola milioni 177 lakini kwa kuanzisha neno la Just Do It ikawafanya mwenzi December kuwa na utajiri wa dola bilioni 9.2 sawa na tilioni 18.4 za kitanzania.
Kuna siri ndani ya neno; fanya usisubiri.
Wale wanaoona kitu na kufanya bila kusubiri wengine watafanya hujenga majina mema, ila wale wanaosema fulani atafanya hujenga majina mabaya.

8. Tafuta sehemu sahihi na ujenge jina hapo.
Kama ni kusafisha kanisa, kutoa, kufuta viti, kumtumza mchungaji, kutembelea watu, injili au kufundisha.

9. Kuwa mtu wa maono
Mtu wa maono ni mtu anayewafanya wengine kuona. Wakati wengine wanasema haiwezekani, yeye husema hebu tujaribu hivi, inawezekana.

10. Jenga tabia njema
Tabia ni wewe halisi, ni wewe nje ya ibada, nje ya madhabahu. Unafanya nini unapokuwa peke yako, unafanya nini ukifanikiwa au tukikupa cheo.
Tabia ina nguvu kuliko kipawa chako, kuliko karama au huduma.

11. Kuwa mtu wa kusadiki.
Mtu anayesadiki ni mtu anayeamini kitu kinawezekana na kushikiria kitu mpaka kinafanikiwa. Ni mtu anayeweza kuhangaikia maono ya kanisa zaidi hata ya mchungaji.

12. Tengeneza uhusiano mzuri na wengine
Tuwe furaha kwa watu wengine katika utendaji kazi.
Kuna baadhi ya kazi na maono ya kanisa huonekana ni magumu, si kwamba ni maono au kazi ngumu bali kuna tu fulani yupo.

13. Kuwa mtendaji kazi na si mfanyakazi.
Kuna mtumishi na anayetumika
Mtumishi yeye utumishi na utenda kazi upo moyoni.
Mtumishi anapotumika hufanya kwa moyo, na ni mtii hata kama mchungaji hayupo, hata kama hajatumwa, hata kama hakuna ujira, hakuna sifa alizopewa, hatazami aliyoyafanya, bali hutazama nini anapaswa kufanya.
Mfanyakazi: yeye kazi haipo moyoni, hufanya ili apate sifa, ujira au zawadi, hukwazika asiposifiwa, hukwazika akifanya peke yake, hukwazika akitoka kufanya kazi moja na kuambiwa afanye nyingine, hukwazika akikwazwa kazini, hupenda kuonekana afanyapo, si mti kiongozi asipokuwepo.

FAIDA ZA KUWEKA JINA JEMA.
1. Jina jema ni zaidi ya pesa na mali nyingi.
Maana pesa na mali huwa na kikomo, lakini jina jema hufungua milango na fulsa zaidi.

2. Jina jema hufungua mlango na kukupa kibari.
Kibari ni mlango uliyofunguka na kupitisha baraka.
Kibari huwavuta watu wa thamani kwako, kibari huvuta mafanikio na kuongeza thamani yako.
Mfano Yusuph na Daudi walipata kibari.

3. Hukupa ulinzi
Jina jema linakulinda, kila mtu atakuwa ni shahidi yako, kila mtu atapenda usishindwe na kanisa litahangaika unaposhindwa. Utakuwa kidonda kwa mchungaji, atakuita mwanae.

4. Hutakufa hakika.
Mtu mwenye jina jema kama Paulo hawezi kufa, huwezi kuhubiri injili na ujumbe uka kamilika pasipo kuchukua toka kwenye injili ya Paulo.

5. Kufanikiwa katika utumishi mdogo hukupa kufanikiwa katika utumishi mkubwa.
Hata leo unapowaona watumishi wakubwa, walianza kufanikiwa katika utumishi mdogo.

Kuna mifano ya watu waliyotumika na hawakuwa na vyeo kwenye kanisa la kwanza, maana kuna watu huamini kuwa kutumika mpaka uwe na cheo.

1. Epafra (mtu niliyempenda sana)
Huyu anapatikana kwenye kutabu cha Kolosai 4:12
Nimemuweka namba moja, kwasababu aliwabebea wenzake, na hakuna aliyemuona wakati huo, ila Paulo akaitambua huduma yake, na kuona wengine walistahimili na kuimarika kwa sababu yake.

2. Prisca na Akila.
Luka aliwandika kama Priscila na Akila kwenye kitabu cha matendo. Hawa walikuwa wakitumia pesa zao kusaidia huduma ya Paulo, walitumia nyumba zao kufundisha watu  Kristo, pale Paulo alipoenda kuhubiri injili. Na ndiyo wakiyotumiwa na na Paulo kuuza mahema aliyokuwa akiyatengeneza.

3. Luka tabibu. Huyu alitembea na Paulo popote alipoenda akiandika nini kinatukia na nini Paulo anasema.

4. Sira: aliyetembea na Paulo sehemu nyingi hata kukubali kufunga na Paulo.

5. Timotheo: kijana aliyekutwa Listra, Paulo na Sira walipo ona utumishi wake japo kuwa alikuwa ni kijana mdogo sana na baba yake hakuwa Myahudi, alikuwa na Myunani, Paulo akampenda, wazee wakamwekea mikono, akamtahiri kuogopa Wayahudi, na kuanza kutembea naye katika huduma.

6. Kreske, Tito, Tikiko, Karpo, Erasto, Trofimo, Eubulo, Pude, Lino, Klaudia: wengi kati ya hawa Paulo aliwa anzishia makanisa baaye.

7. Marko: paulo alisema kuwa anamfa sana.

NB: BADO WEWE... Chukua hatua, Inuka, Tumika, weka alama, Jenga jina jema.

MWISHO: Moja ya vitu ambavyo wapendwa wengi waliyofanikiwa kuwepo miaka ya 70 na 80, huwa vinawasikitisha ni mabadiriko ya kanisa.
Kanisa limebadirika
• tupo katika zama ambazo mabadiriko hatari yametokea kanisani
• utumishi umekuwa mtaji wa maisha
• karama za roho mtakatifu nyingi hazionekani
• huduma zimekuwa ni biashara
• sasa makanisani kuna utumishi wa matajiri na masikini. Mtu akishafanikiwa kuna baadhi ya kazi kanisani hafanyi tena.
• watu wanajenga majumba yao zaidi ya moja, na kuacha nyumba ya Bwana katika aibu.
• maombi yamekuwa ni ya watu fulani kanisani hasa wazee na wenye shida.
• mrundikano wa vijana kulima shamba la kanisa haupo tena, sasa  wachungaji ndiyo watumishi wa kazi zote.
• sadaka imekuwa ni ibada ya ziada.
• watu wanataka kuonekana na si kutumika.

Kama bahari inaweza kuhamisha vitu vyote ila si jiwe. Ni vyema wakati kanisa linabadirika, wewe usimame imara, kuweka alama na kujenga jina jema katika ufalme wa Mungu.

Kwa msaada wa Roho mtakatifu somo limeandaliwa na
ULENJE (Emanuel) MWAIPUNGU.

Monday, December 21, 2015



SEMINA DEC 2015 -DAY 1

FUMBO LA MAISHA NA KUFIKIA HATIMA NJEMA

Yer 29:11
Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho"

Bwana anakuwazia mema, mawazo ya amani, kukupa tumaini siku yako ya mwisho: swali wewe je?

Maisha yana mwanzo, kati na mwisho. Wote hapa bado hatujafika mwisho, kuna wengine wapo katikati, na wengine wanakaribia mwisho.

Lakini lipo tumaini: hata kama unakaribia mwisho au upo katikati unaweza kuyafanya maisha yako yaanze mwanzo.

Yesu alikuja ili mwanadamu apate fulsa ya kuanza tena mwanzo maisha. Hata kama alichezea kete anaweza kuanza tena mchezo na akashinda.

Ibrahimu alikuwa mwisho, Mungu anakamuita na miaka 70 na kuanza na mwanzo. Musa anaitwa akiwa anafikiri yupo katikati ya maisha, Mungu anamuita kuanza mwanzo mpya wa maisha yake. Petro vivyo hivyo na Paulo anaitwa akiwa katikati ya maisha, anaitwa na kuanza tena mwanzo.

Somo hili ni la muhimu sana kwenye maisha yako, muhimu sana. Maana Roho anakwenda kutufundisha namna ya kuutumia mwanzo wa maisha yetu kutengeneza katikati na namna ya kutumia katikati ya maisha yetu ili kujenga mwisho mzuri ambao Bwana Mungu ametuandalia.

Mungu alipokupa nguvu ya maamuzi; basi alikupa nguvu ya kuamua hatima ya maisha yako. Mungu anapanga mwisho wako, ila kuufikia au kutoufikia hayo ni maamuzi yako. Mfano Sauli Mfalme na Sulemani na Joashi.

Mungu kukuwazia mwisho mzuri haina maana kwamba Mungu anashuka na kuja kuishi kwa niaba yako. Yeye anakupa marighafi na vitendea kazi na kuwa na wewe na kukusaidia.

Na utakapojitoa na kusimama ndani ya mstari wa kufikia mwisho aliokuandalia basi atahakikisha unaufikia, lakini utakapotoka nje ya mstari basi anakuacha na kumfikiria mtoto wako au mtu mwingine kuufikia mwisho huo. Na atajitahidi kukurudisha siku zote hatochoka, mpaka siku zako za kuishi zitakapoisha. Sababu yeye ni wa rehema huwarudi wale wamrudiao, hupenda watu wamrudie.

MWANZO.
Tuanze sasa...
• Maisha yamejawa na matukio tusiyo yatarajia. Kila siku yanatokea yale ambayo hatukuyapanga wala kutarajia yatokee.
• Maisha yamejawa na hasa huendeshwa na matokeo tusiyoyatarajia. Tunapofanya vitu na kupanga mipango huwa tunataajia mema na kujikuta tunapata tofauti.

• Maisha yamejawa na matukio ya kushangaza sana.
   Watu wanakuwa tofauti na walivyotajia au kutarajiwa kuwa:
   Waliopanga kuwa madaktari wanaishia kuwa wachungaji, waliopanga kuwa maaskofu wanaishia kuwa wachungaji au mashemasi, waliopanga kuwa wanasiasa au wafanyabiashara wanaishia kuwa wafanyakazi wa kawaida, bodaboda, wakulima au walimu, na wengine kuwa walevi wa pombe, sigara au bangi na madawa ya kulevya.
   Mwanafunzi anapanga kufika chuo kikuu na mzazi anajitahidi ili kutimiza ndoto za mwanae, matokeo yake anaishia kukuletea mtoto nyumbani au kushindwa mtihani na kuishia kidato cha nne au cha tano.
   Wazazi wanashangaa wale watoto waliowapenda sana na kutarajia kuwa ndiyo watawasaidia na kuwaona kuwa ndiyo watoto wema ndiyo wanakuja kuwa hawafai na wale waliokuwa hawafai ndiyo baadae wanakuja kuwa wamaana.
     Pastors and bishop become prisoners, politician come from high ranks to prison, beautiful girls become prostitute, those we call bad girl, poor, ignorant, they become our boss, ministers, chief secretary and C. E. O.
     Those we love in public, we hate after we see them in private.

MYSTERY OF LIFE
• Life become mystery when we wonder Why we still doing what we hate (we do, what we don't wanna to do), and what we desire to do, we don't do.
"What you desire to do you're not doing and many-times you're even not able to carry them out, and what you hate you don't have the ability to stop yourself from doing.

"In fact every one has its fault that neither fear nor law can stop from doing"

• Life become mystery when we try harder and more harder to stop ourself from doing some action, and we fail. We try to stop some attitude and behavior and we fail.
Sometime we cry, explain to people, pray and asking God mercy and grace and we wonder why we still do what we pray and ask to stop.

• We know something is evil, and we try to stop our mind and our body to execute them, A force come from our heart, a force that we don't know  even its name that our body and our mind succumb to do what we truly hate to do.
  And what we know is right and is what God want us to do, we force our mind and body to do, we wonder we are not.
  Eg. I desire to wake up early in the morning to pray I don't, I plan to pray in mid night I fail, I desire to fast and pray but I don't, I desire to be more powerful and spiritual in the kingdom of God, but I'm not. We desire to have good relationship with God and doing what he want, but we wonder we don't, everyday instead of saying yes I win, we ask for mercy.

• And the mystery of all, Many of us we are not what we desire and wish to become when we're youth.

• This is mystery to more than 90% of the world population: Many folks they don't even know themselves.
  We pretend to, but we don't.

* We try to know God but not ourselves,
   Whilst is difficult to know God if you don't know yourself      what Make me wonder is that, Even God, has a desire to see all of us, to know ourselves. That why, He never call somebody without tell him who he is. Before telling Abraham Go! He first tell him, I call you be father of the nations, Before telling Moses Go! He first tell him, Saviour of His people, Before tell Jeremiah, he first tell him why he make his birth.
# In fact, Your purpose is what carry your real identity"

"You wander and wander doing everything because you don't know yourself"

* when you know yourself, will make you to know that you cant live without God, and God Joy is your Joy and strength.
* Many folks die, only they know they're names but not themselves.
* And some they don't even bothering, that they do not know they are. Only they care, is to make living.
* Some people they try harder and harder to know who they are, finding they're purpose. But they become old and die, without achieving they're desire, Why? They finding from wrong source. God is only source, because is one who created you. (Recommend Book : Purpose Driven Life By Rick Warren and The Power of Purpose By Dr Myles Munroe)
* Many Elites, They only know they're positions and they're bosses and not them self. That why most of them they die with stress and Blood Pressure.

• Life has no experts: We're all facing challenges, problem, thing we cant handle, unexpected and unplanned events, and unexpected results. But Those Who have Faith in God are always safe.

• Everyone need better life, better world, better marriage and better family. And this make human an Utopia

• we all want more and plenty money, while some they lie, pretending that they don't need money, they lie, they need more, and they want more than you.

"Money is not everything, but is important to everything" Robert Kiyosaki

But seek ye first the Kingdom of God and His Righteousness and Other Thing (including money) shall be added to you"

• We live life but we don't know the meaning of it
This is what I know "we can have many definitions about life, but experience will tell you the truth" #Ev.Ulenje

Kesho tunaendelea
Umbali si shida waweza kuwa karibu nasi.
Ubarikiwe Sana kwa kusoma.
Naamini kuna kitu umepata, pita soma tena na tena.

+255 718 721 848
imaf2b@gmail.com

Wednesday, December 9, 2015

SEHEMU YA SITA: BARAKA TANO ZA PETRO NA KUJENGA KESHO KWA HEKIMA

Asante kwa kusoma sehemu ya tano, kama bado nakuomba katika Jina la Bwana Yesu tenga mda na usome sehemu ya tano, sasa tuendelee... ulenje.blogspot.com

B. KESHO

Baada ya kujifunza kuhusu jana sasa ni vema tukajua zaidi kuhusu kesho na kuona namna Petro alivyoweza kutumia leo yake kutengeneza kesho yake.

Petro siku zote alifanya jambo pasipo kutazama jana, hakutazama makosa, kati ya wanafuzi 12 Petro alikuwa ndiye mwanafunzi aliyekaripiwa na Yesu mara nyingi na kukosolewa mara nyingi lakini ndiye aliyetumiwa na kuwekwa karibu sana na Yesu, si hivyo tu, baada ya Yesu kuondoka Petro ndiye maanafunzi aliyeachwa kuwa kiongozi kati ya watume, ndiye aliyeambiwa waimarishe wenzio, ndiye aliyeambiwa kisha kondoo wangu, unaona pamoja na makosa yake yote lakini Mungu aliyakusanya yote na kuyafanya mema kwa kutimiza kusudi lake duniani.

"Unataka kumjua mtu asiyekosea, mtafute mtu asiyetumia fulsa"

Unataka kumjua mtu anayekosea na kuibuka mshindi, mtafute Petro, anayeona fulsa na kuitumia, wakamuita kiherehere, wakamuita mnafki, wakamuita charismatic, wakamuita msariti, lakini ndiye huwezi taja maendereo ya kanisa la kwanza na kuacha jina lake, hata Paulo anajua hilo, hata wewe unayesoma unajua hilo.

Uanataka kuwa mtu wa mafanikio, jaribu sana, ukikosea umia tena umia sana ili usirudie kosa hilo, jisamehe jisamehe tena jisamehe sana, kisha jaribu tena, ukikosea jaribu tena usiache kujaribu, hata ukifika mbinguni, jaribu kuimba kila wimbo jaribu kila wimbo mpaka uwekwe kiongozi wa kuimba kama cheo hiko kipo, lakini kubwa usiache kujaribu.

Najua ungetamani leo iwe ya pili kuelezwa, lakini hapana, siku zote ni za muhimu lakini kwa mafanikio ya mwanadamu LEO ni kuu na muhimu kuliko zote.

Kesho ni mda wa mbere ambao bado haujafikiwa na kuanza kutumika"
Katika mda uliyopewa na Mungu, kesho ni mda ambao bado hujaufikia.
Yesu akasema "Basi msiyasumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe" Math 6:34. Yesu hapa alikuwa akizungumzia siku ya kesho, ambayo ipo mikononi mwako, ambayo katika mda uliyopewa kuishi, kesho ya kwako.
Mtu aliyekufa hana kesho, mtu aliye bado mzima ndiye pekee mwenye kesho. Hivyo kesho ni yako, ukiwa hujaamka kesho, ujue siku zako ziliisha.
Siku ya mkesha wa mwaka mpya wa mwaka 2014 mchungaji wa kanisa la CLC alitoa hadithi ya ajari ya mtu aliyegongwa na gari aina ya Toyota iliyotokea mda wa mchana wa tarehe 31/12/2013, siku moja kabla ya mwaka mpya wa mwaka huo, kisha akasema "fikiri kama tukirudisha dakika moja nyuma, wewe unadhani yule mtu atakuwa anawaza nini kichwani mwake?" Akajibu mwenyewe akasema "lazima atakuwa anawaza mipango ya kufanya baadae". Sijatoa hii hadithi kukwambia usipange ya kesho, nimetoa hii hadithi kukuonesha kuwa, kesho ni yako kama ukiifikia, usipoifikia si yako,

Hivyo kati ya siku tatu: jana, kesho na leo. Tunayoimiliki ni leo tu pekee, si jana wala si kesho. Na usiumize kichwa kwa habari ya kesho, panga tu kwa habari ya kesho, umiza kichwa kwa habari ya leo. Tukizungumzia leo, utanielewa.

"Weka mipango ya kesho na kuwa na dhamira dhabiti ya kuitimiza ila Usiumize kichwa kwa habari ya kesho, Wala usiwaze kwa habari ya jana, umiza kichwa nini unapaswa kufanya na usichopaswa kufanya Leo, maana leo ndiyo siku pekee tunayoimiliki"

Ndugu mpendwa leo ndiyo yenye nguvu kubwa ya kubadiri maisha yako, si jana, wala si kesho.

UTAENDA JEHANAMU SI KWA ULIYOFANYA JANA SI KWA UNAYOPANGA KUFANYA KESHO, ni kwa unayofanya LEO"

Kesho ni siku ndani ya mda tuliyopewa na Mungu ambayo hatujaifikia bado, tukiifikia inaitwa leo, hakuna mtu anayeimiliki kesho. Kama hatujui kuwa tutakufa lini ndivyo hatujui kuwa tuna kesho. Hivyo kesho ni miliki yetu ila ni milki hewa. Inaweza tokea au isitokee.
Kifupi ni kwamba: Mungu amempa kila mtu kusudi yaani kazi ya kufanya na kumpa mda ambao anajua hiyo kazi itakuwa imeisha, kuna wakati anaweza kuongeza, pia mwandamu anaweza kwa kuounguza mwenyewe, hasa pale mwanadamu anapotumia nguvu yake ya maamuzi kufanya jambo ambalo linaweza changia kuondoa uhai wake, Daudi alilia (paraphrase) "Bwana nipe kuzijua siku za kuishi kwangu ili tujue namna ya kuenenda"

1. Kesho ni siku mbere ya leo
2. Kesho ni siku ambayo bado haijatumika
3. Kila mwanadamu ni mjinga kuhusu kesho
4. Na ujinga huleta woga na hofu kwa kila mwanadamu kuhusu kesho.
5. Woga na hofu huleta watu kuisumbukia sana kesho.
6. Kesho ni makisio tu si kitu halisi.
7. Masikini wanahofu na kuacha ije inavyotaka, matajiri wanapanga wanavyotaka ije
8. Masikini wanaamini kutofika kesho, matajiri wanatumai kufika kesho bila kujari umri wao
9. Masikini wanajadiri kesho, matajiri wanawekeza kupata faida kesho.
10. Mabepari wanawekeza kesho kwa hofu ya watoto wao, wenye hekima wanawekeza kwa kizazi kijacho
11. Maisha unayoishi leo, ndiyo yatakuwa kesho yako; maisha ya kesho, yatakupa unachompa wewe leo.
12. Hakuna unachofanya leo, usivune kesho, na kile unachopanda leo, ndicho utakachovuna kesho
13. Maamuzi yako ya leo, ndiyo matokeo ya kesho.
14. Kesho hujaifika, iache siku itoshe kwa maovu yake
15. Usiseme nitafanya kesho hata mara moja, fanya sasa. Toa mchango sasa, panga mipango sasa, tekeleza sasa, kuwa muaminifu sasa, tenda mema sasa, jenga ndoa nzuri sasa, saidia watu sasa. Kuna watu wanatamani waume na wake zao wafufuke ili waweze kusema "nimekusamehe mume wangu, au nimekusamehe mke" ila haiwezi kutokea. Samehe leo, mpende mume au mke leo, fanya malenzi ya Mungu leo.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU KESHO.
Tengeneza picha kwenye kichwa chako, wewe ndiyo Yusuph upo gerezani kwa kosa la kusingiziwa. Unapelekwa kufanya kazi za gerezani, unateswa na mijeredi, unakula chakula cha gerezani, miaka mitano inafika na huoni hata wa kuja kukuona au ndugu yako kujua kuwa mzima. Futa wazo kuwa unajua nini kiliendelea kwa Yusuph, fikiria haupo kwenye hadithi  na si hadithi, fikiria ni tukio la kweri kwako; hivi nini mawazo yatakuja kichwani mwako mfano; "nitatoka kweri?, nitatokaje?, itakuwaje wakiniuwa?, au nimkane Mungu wangu?, au nijifanye Mmisri?" Maswari mengi najua yalikuwa ndani ya Yusuph mpaka kufikia hatua ya kuwaambia wale wafanyakazi wa Farao waliopata fursa ya kutoka "msinisahau..." Kwanini alikuwa akitafuta njia ya kutoka, alikuwa hajui kesho yake. Ukweli wa hadithi ni kwamba anayeifahami hadithi anafahamu nini kinaendereana nini kitatokea, tofauti na yule asiyejua hadithi au yule ambaye anaipitia hadithi hiyo.
Yusuph alikuwa hajui nini kitatokea, wewe unajua nini kilimtokea, sasa kuielewa zaidi hadithi hii inatakiwa uivae hadithi hii ya Yusuph na iwe kama wewe, ndipo utajua kuwa mtu anayepitia hajui kesho.
Masikini kwao kesho ni kitendawili kisichokuwa na majibu. Kwao kesho siyo siku yao, ni siku ya wengine, kwao kesho kufika ni 0/100. Na hivyo hakuna anayewaza kesho. Anapopata pesa ya kula siku hiyo, anafurahi na kuona siku hiyo ni ya bahati sana, anafunga kazi na kupumzika. Anafungua pochi mda wa kula ukifika, akimaliza kula analala, akingoja kesho apate tena wapi ya kula. Maisha yote ni mkono na mdomo. Kwanini hawazi kwa habari ya kesho.
Matajiri hawawazi kwa habari ya kesho sana japo hofu yao kubwa kwa habari ya kesho, ni kushuka kiuchumi na kurudi kuwa kama jana yaani wanaogopa kurudi kuwa masikini. Hivyo kundi hili ni kundi lisilojiamini na lenye hofu kubwa sana, kuhusu kesho, utofauti wao na masikini, wao hawawazi kutofika, bali wao wanawaza itakuwaje wakifika wakiwa wameshuka chini kiuchumi na kurudi kama jana. Na hii huwafanya kuwa watu waoga sana wanapokuwa katika siku ya leo. Uzuri wao ni watu wa kupanga sana kwa habari ya kesho. Mabepari wao kesho ni siku ya muhimu sana na hivyo hutumia pesa, nguvu na tekinolojia  kupanga kwa habari ya kesho, mabepari huwaza faida, huwaza masikini atabaki vipi kuwa masikini, siku zote anafikiri na kubashiri kinachowesa kutokea kesho.

Mabepari huwa ni watu wa kufikiri sana, nini kitatokea kesho: uchumi kushuka au kupanda, pesa kushuka au kupanda, biashara kushuka au kupanda. Siku zote wanawaza hayo ili wajue namna ya kushindana na soko.

Wajamaa, wao na serikari tu; mara zote hutumia mda kusoma magazeti na kutazama television kuona nini serikari imepanga kufanya kesho, huwa makini kujua mipango ya serikari ya mda mfupi na muda mrefu na hufatiria kama inatimia. Watu hawa hupatikana hata nchi za kibepari pia.
"Watu wajamaa huwa wanawaza sana serikari imefanya nini kuliko hata wao wamefanya nini"

Watu wa ufalme wa Mungu wao huwa hawakondi wala kukosa furaja kwasababu ya kesho. Wao hutafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, kisha haki yao waliyonayo katika ufalme wa Mungu humfanya mfalme wao ambaye ni Mungu Baba kuwatengenezea fulsa. Soma vizuri kuwatengenezea fulsa, huwaandalia mazingira, huwapa kibari, huwapa hekima na maarifa zitakazowasaidia kufanikiwa. Kama ndege wa angani alivyokuwa hana shamba, hana ghara la kuifadhi chakula, wala hana duka ila Baba wa mbinguni humlisha.
Ukifanya uchunguzi wa ndege utagundua kuwa, yeye hutoka kiotani akiwa na matumaini kuna sehemu nitakuta chakula, nitakula na kupata chakula cha watoto wangu. Tazama maua ya kondoni, hayalimi wala hayavuni ila hata Sulemani na fahari yake hajapata kuvikwa kama maua hayo. Mauwa ili yaoate chakula, huwa yanaamini yakishusha mizizi yake na kuchanua maua yake wakati wa mchana yatapata chakuka na mwanga.

Jambo la msingi kuhusu ndege, anatoka kiotani kwenda kuchukua chakula alipowekewa na Baba wa mbinguni.

Maua huwa yanatoa mzizi na kuchanua ili yapate chakula na mwanga.

Nini cha kujifunza Yesu hakusema watu wa Ufalme wa Mungu wasifanye kazi au wasitoke mlangoni mwao na kutazama fulsa na kuzitumia, Kama Ndege anavyotoka kiotani na kwenda sehemu ambapo anaamini Mungu wake wa Mbinguni amemuandalia chakula, ndivyo nawe pia utoke mlangoni ukatazame fulsa pale ambapo Baba yake wa mbinguni amekuandalia.
Kama vile mauwa yanavyotoa miziz yake na majani yake yakiamini kwamba Baba wa Mbinguni amewaandalia maji na mwanga wa jua kwa chakula. Tafuta mtandao tafuta mawazo tafuta marafiki tafuta watu ukiamini kuwa Baba yako wa mbinguni kuna fulsa amekuandalia.

Jifunze katika mfano wa Yesu, kama Baba wa mbinguni anayalisha maua na ndege wa angani, itakuwaje wewe ambaye alikubali mpaka hata kufa kwaajili yako. Kuna fulsa nyingi amekuandalia toka mlangoni si kwa hofu, toka nje kwa imani, ukiamini kuna fulsa amekuandalia leo kufikia mafanikio yako.
Tuma tema barua ya maombi ya kazi, nenda tena kuomba kazi, fanya juhudi mpya maana Baba wa Mbinguni amekuandalia fulsa za kutosha.

Acha hofu na kesho, tafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na mengine hayo Yesu amekuandalia, wewe tazama fulsa na usonge mbele.

Mfano; Mungu atatoa watu kutoka mashariki na magharibi ya mbali kukuletea fulsa. Mamajusi toka mashariki ya mbali ni uthibitisho tosha kuwa Bwana atafanya hilo.

Watu wa ufalme wa Mungu huwa hawana tatizo, kwasababu wao, wameamini Baba yao wa mbinguni anawajua wao, na anashughukika kuwa mema. Hivyo kwao kesho siyo kitendawili, bali Mungu wao ndiyo tumaini kuu na kati ya watu wanaowaza na kutumaini kesho njema ni watu wa kundi hili.

FIKRA HASI KUHUSU KESHO.
watu wengi wanaoishi maisha ya kushindwa huwa wanaangukia kwenye makundi haya mawili.
1. Wale wanaosema "nani anayajua ya kesho" hivyo wanaishi kama wanakufa usiku na wanaona kufika kesho ni asilimia 0, wanaona kesho ni kama makisio tu, ni kama siku isiyofikika. Cha ajabu wanajikuta wamefika, hawana hata pesa ya kuanzia, au hata sehemu ya kuanzia, wanatafuta pesa ya kula, wanakula wanalala huku wakiwa na asilimia 0 za kuamka, wanajikuta wanaamka. Maisha yao huwa ni ya kujaa taabu, utumwa, manung'uniko, kukosa tumaini, kuhangaika, hawana malengo, hawana akiba, wanakula wanalala na kuamka.

Nimewahi kuwa na rafiki yangu nikiwa O-Level: baba yake alikuwa ni mtu mwenye pesa, na kuwafanya kuishi sehemu za watu wenye pesa maarufu kama Kilakala kwa watu wanaotoka Morogoro. Baada ya baba yake kustaafu, maisha yao yalibadirika na kuwa maisha ya shida sana kipesa, siku moja alikosa fedha ya nauli ya kurudi nyumbani kwao kutokea na shule, akanifata na kuniomba nauli, kwa kicheko nikamjibu "tatizo baba zenu wanakumbuka kujenga kwa pesa za kustaafu, nyumba ikiisha na pesa zimekwisha mnakuwa masikini" siku ile hakunielewa lakini akisha kuwa mkubwa atanielewa.

Watu wengi wanatumia pesa zao za mshahara zote, na kuacha kupanga ya kesho, wakiona watakufa kesho, wanashangaa hawafi.
• Watu hawa hutafuta pesa za leo bila kupanga kuhusu kesho yao.
• Huwa hawafanyi majukumu yao, wakiamini kesho itawafanyia majukumu yao.
• hawana mipango
• hawana maono wala ndoto
 • hawana uwekezaji wowote
• hawasaidii watu wengine

2. Kundi la pili ni wale wanaoitafutia kesho maisha na siyo wao wenyewe".
Watu hawa huangaika na kuhangaika wakaiitafutia kesho chakula, mavazi, heshima na utukufu. Kumbuka nimesema "wakiitafautia kesho" siyo "wakijitafutia".

Kundi hili ni watu wenye hofu, mashaka, kuhangaika, na wengi huwa wanatumia mpaka njia ambazo si harari, njia hatarishi, dhuruma, ufisadi na rushwa, ili kutengeneza kesho yao. Watu hawa huishia kuitafutia kesho yao, na kusahau kujitafutia wenyewe maisha. Kuitafutia kesho haki na kusahau kujitafutia wewe haki, si mafanikio ni utumwa.
Mr Msofe alijitahidi kutafuta pesa kwa hari nyingi, aliuza bangi, madawa ya kulevya, akajiunga na rushwa za kuizurumu serikari na dhuruma nyingi akiihofu kesho yake, pesa nyingi alizopata aliweka akiba akiogopa kuteseka kesho yake; akajenga majumba na makampuni, alipomaliza kufanya yote sasa aanze kula faida, akavamiwa na majambazi wenzie akapigwa risasi akafa" Kesho inafaidika yeye ameenda na maji.

Patric the great kijana maarufu, akaenda kwa mganga ili apate utajiri, baada ya kupata utajiri, akaowa na kupata mtoto, baada ya miaka mitano akaumwa akafa, mke akapokonywa mari na ndugu wakatapanya mari zikaisha.

Mzee James ili kupata utajiri akaradhimika kuhudhuria kanisani siku ya jumaapili pekee na siku zingine alikataa kufunga duka lake ili aende kanisani, alipopata utajiri wa kuanza kufanya biashara nje ya nchi, akapata ajari akafa, ndugu wakatapanya mari na mke wake akaishi maisha ya shida.
Mr Tomson alipopata pesa zake za ajira yake ya kusafisha ofisi za watu, kufagia na kuzoa taka taka. Pesa alizopata aliziifadhi chini ya kitanda chake, akisema kesho nitazitumia katika uzee wangu. Siku moja akapata ajari ya gari kabla ya uzee wake, akafa. Hakuwa na ndugu maeneo yale, wakatangaza kwenye vyombo vya habari ili wapate ndugu zake, hakuna aliyejitokeza. Serikari ikachukua jukumu la kumzika. Walipoifungua nyumba yake, wakakuta Dola zaidi ya milioni kumi na tano. Mr Tomson aliishi maisha ya kimasikini sana, kila mtu aliyesikia habari ya kukutwa kwa pesa zile na maisha ya Tomson kila mtu alihuzunika. Kwanini alitafuta maisha ya kesho akasahau kuyatafutia maisha yake.
• Watu wa kundi hili hutumia pesa nyingi kuweka akiba na si kuzalisha pesa zingine
• watu hawa hutumia mda mwingi kujenga ya kesho kuliko kujenga maisha yao, wakihofu kushuka kiuchumi zaidi kuliko kushuka kwa maisha yao, wakihofu vipi fulani akinipita
• watu kama hao ni waoga sana kwa habari ya kesho. Huwa hawana amani siku zote. Wanahofu sana kuwa wasipotafuta leo kesho watateseka sana.
• watu kama hawa, huishi kama masikini wakihifadhi na kutafuta ya kesho. Husema moyoni mwao heri nilale njaa leo, kesho nitashiba na kusaza.
Robert Kiyosaki amewahi sema "haina maana kuishi masikini na kufa tajiri"

Watu wengi wanaishi kama masikini wakisema wanahifadhi, wanajikuta wanaishi masikini nankufa tajiri wakiwaacha watoto na ndugu zao kama Fisi wakigombea mari zao. Unahitaji kujipanga.

"Jenga ufalme wa mbinguni ambapo mwivi wala kutu haviwezi kuharibu"

Kesho ni mda wa mbere ambao Mungu ameundaa kwaajili yako. Na ana mpango na wewe, anachotaka ni wewe kutafuta ufalme wake na haki yake, kisha mengine utazidishiwa. Kwa maana ndogo fanya nafasi yako na umuache Mungu afanye nafasi yake.

FIKRA SAHIHI KUHUSU KESHO

Usikose sehemu ya sita tukizungumzi fikra sahihi kuhusu kesho.
Asante kwa kusoma naamini Roho mtakatifu hajakuangusha, neno hili ni ya hai na linaponya soma vema hata mara mbili ili uelewa
Uliza swali aunacha comment na share ili unisaidie somo hili kufika na kwa wengine.
MUNGU AKUBARIKI
From Holy Spiri

Monday, December 7, 2015

KUFIKIA UKAMILIFU WA YESU KRISTO

KUFIKIA UKAMILIFU WA KRISTO


Utofauti wa Mungu na wanadamu katika kuona vitu,
1. Mwanadamu anaona mwanzo kisha mwisho, Mungu anaona mwisho kisha anarudi mwanzo na kupanga namna ya kufika mwisho

2. Mwanadamu anaona nje na kuweka hitimisho, Mungu anatazama ndani kwanza kisha anafanya cha ndani kuonekana nje.

3. Mwanadamu anatazama kitu, Mungu anatazama matokeo ya kitu

4. Mwanadamu anatazama mwisho wa kitu Mungu anatazama baada ya mwisho.

5. Siku zote Mwisho wa mwanadamu ndiyo mwanzo wa Mungu

6. Ana heri yule ajuaye mawazo ya Mungu kuliko yule ajuaye matendo, ishara na miujuza ya Mungu
I.e ana heri yule amjuaye Mungu kuliko yule anayejua matendo ya Mungu.

7. Kila anayetaka kuwa hodari wa imani kwanza lazima ajue mawazo ya Mungu na Mungu mwenyewe

8. Imani huonekana tu mahari ambapo hapana majibu
Kama sehemu ina majibu hapo siyo imani

9. Imani ni kuamini kitu ambacho hujawai kuona kutokea.
Mfano wa Martha

10. Kufikia ukamilifu wa Kristo ni kufikia kwenye imani ya Kristo

11. Imani ni kufika wakati wa ulichosoma kwenye neno na kuhubiliwa unakuta ni tofauti kwenye maisha halisi

12. Mungu hufanya na huruhusu kila kitu kwa kusudi lake.

13. Mungu unayemtumikia hayupo kukuepusha usipate matatizo, mjaribu, kushindwa, udhaifu, na majaribu bali yupo ili akupitishe katika hayo kwaajili ya utukufu wake.

14. Unapombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.

Usiogope unapopitia hayo, maana ni Mungu wako amekupitisha.
Kama ukitaka kuwa na Mungu anayekuepusha na majaribu basi 80% ya Biblia ilipaswa tuitoe, maana asilimia zaidi ya asilimia 80 ya Biblia ni hadithi za watu waliopitia mateso na majaribu, kuanzia mwanzo mpaka ufunuo
Na kipimo cha wewe kuwekwa kwenye Biblia ni kupitishwa kwenye majaribu, mateso na udhaifu
Ibrahimu hazai
Mussa hajuo kuongea
Yakobo mwongo, mwizi
Esau mwoga wa njaa
Gideoni mwoga
Samson mdhaifu kwa wanawake
.......................

Yoh 16:33

Mara nyingi ndani ya ibada na makongamano mengi ya watu waliookoka tumekuwa tukifundishwa imani ya matendo ya Mungu
Yeye atafanya njia
Yeye atakuwa nawe
Yeye atakutetea
Ataponya nyumba yako
Hakuna uchawi wala uganga nyumba ya Israel
Atakuwa nawe daima
N.k

Lakini wengi tumeshangaa kuona tulichoamini na tunachokiona ni tofauti
Tulichosoma kwenye Biblia na kinachotokea kwenye maisha halisi ni tofauti
Tulichohubiliwa na tunachokiona ni tofauti

Unafika wakati
Familia uliyoamini inafunikwa na Mungu; mke anasumbua, mume anasumbua, mtoto anakuletea mimba
Ulivyoamini kuwa hatutakopa tutakopesha, unakuta ni tofauti, una madeni na mengine yanaongezeka

Uliamini hakuna uchawi juu ya Israel wala magonjwa ya kutisha, unashangaa anatoka kuumwa mume anakuja mtoto, usiku vita vya kichawi haviishi

Uliamini kutawara si kutawalia, unajikuta unatawaliwa na kuhama chini ya utawara wa bosi huyu na bosi huyu.

Uliamini kwa mikutano na kushuhudia na kulitangaza Jina la Yesu watu watajaa maelfu kwa maelfu kanisani unakuta katika maisha halisi hata mtoto haokoki na hata mtoto wako pia hajaokoka.

Leo tunaongelea imani ambayo unafika wakati hata neno uliloliamini halitokei
Mungu aliyemwamini humuoni
Mahubiri uliyoamini hayatokei

Maombi unaomba tena kwa kufanya kwa kujidhiki na kushirikisha na wengine lakini ndiyo kwanza mambo yanaongezeka kuwa magumu na majibu kutoonekana

Unaomba kwa ushahidi wa vifungu, lakini hakuna majibu

Imani wakati ambapo nini unaamini ni tofauti na unachoona katika maisha halisi.
..............................


Yesu anapowaaga wanafunzi wake,
Anaamua kuweka hitimisho/conclusion ya maisha yake yote toka anazaliwa mpaka anaenda kuteswa mpaka anapaa mbinguni, kwa kutumia sentensi moja tu

"Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu"

Luka 2:52 anamtambulisha Yesu tofauti na yeye anavyosema
Si kwamba alikosea Luka anamtambulisha Yesu wakati ana miaka 1-30

Luka anasema "naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu"

Katika umri wa miaka 1-30 Yesu akafurahia maisha yale, akaona ulimwengu huu mwema sana.

Hivyo ndivyo kwa wengi wetu, tulipozaliwa, wakati wa utoto tuliitazama dunia katika uwema sana, ukiamka asubuhi baba ameshaacha pesa ya kula shule nyumbani
Kitu kikiisha unasema tu mama au baba analeta
Ukaishi pasipo kujua ulimwengu halisi aliouongelea Yesu kwenye Yohana 16:33

Tambua kuna kuwa
1. NJE YA ULIMWENGU
2. Na kuwa NDANI YA ULIMWENGU

Wakati ule ulikuwa nje ya ulimwengu, wala ulikuwa hujui kinachowapata wazazi wako ndani ya ulimwengu

Wazazi Wakija sebureni wanacheka, unaona yes ngoja nikue kumbe maisha ni furaha, ukiongezeka umri unafurahi sana maana unatamani kufikia ukubwa kama wao ili ujitegemee.

Unapanda darasa na kumaliza shule unafurahi sana, unaolewa na kupata kazi unafurahi

Sasa mchezo unaanza unapotoka nje ya ulimwengu na kuingia ndani yake, na kukuta maisha ya ndani ya ulimwengu ni tofauti na ulivyokuwa unafikiri ukiwa mtoto kwa wazazi (nje ya ulimwengu)

Ulikuwa unasikia maisha magumu, sasa una yaishi hayo maisha.
Ulihadisiwa kuna kupitia majaribu sasa unapitia
Ulihadisiwa sana kwa habari za matatizo ya ndoa ya fulani na fulani na kuna wakati ukawaona wazembe sasa unapitia
Ukamuona mtu anafukuzwa kazi, ukasema mzembe, sasa unapitia

Ukamuona mtu hana kazi yuko nyumbani sasa unapitia

Ulikuwa ukiona tu baba anamfukuza mpangaji ukaona mpangaji mzembe anakunyimia fedha ya shule, leo ndiyo unaishi maisha ya kushindwa kulipa kodi

Hooooo
Unachanganyikiwa
Na kusema waoooh! This is the world

Yesu alipopitia maisha ya kukubaliwa, akawa akifurahi na kucheka na mama yake, na kuuliza je mkate si bora kuliko neno litokalo kwa Bwana?
Anakutana na Wakuu wa hekelu na kujadiri nao neno la Mungu akiwauliza maswali na wakimsifu sana.
Anafurahi kujenge meza na vitu na makochi akiwa seremara

Anafika miaka 30 na kuingia ndani ya ulimwenguni.

Anaona wao this is a world my mumy live?

Anaona walimu alioshiriki nao neno la Mungu hekaluni ndiyo hao hao anafika hekaluni wanamkataa

Watu walioona akiponya na kuwafanyia ishara na miujiza mbele yao ndiyo hao wanasema asurubiwe

Akaona waaooo! Kumbe nje ya ulimwengu ni tofauti na ndani ya ulimwengu.

Rafiki zako wa utotoni uliohisi watakutetea ndiyo hao watakusaidia mahakamani ndiyo hao wanasema afungwe, watu uliowahi hata kuwasaidia walipokuwa na shida leo kwako wanasema afungwe, watu walioona wema wako, leo wanasema mwongo mwizi huyo.

watu uliofikiri watakuwa ndiyo washirika wa kwanza kwenye kanisa ulilolianzisha, ndiyo hao wanakuwa wa kwanza kusema hukuitwa

Watu uliotegemea kukusaidia kutoka kimaisha leo wanasema hatuwezi, hata hawataki kuwa karibu na wewe.

Yesu anaona wanafunzi wake waliompenda sana na kumuita rabi, mfalme, na Mungu akawatambulisha ni mwanangu mpendwa, na kuwa naye mpaka kwenye dhiki na kuwafanyia miujiza baharini
Ndiyo hao hao wengine wanamsaliti, na wengine wanakimbia hawataki hata kuona anavyosurubiwa

Wanafunzi wengine waliomfata zaidi ya 15000 na kula mikate na samaki wa miujiza, hao ndiyo wa kwanza kupiga kerere msurubishe

Hii inatisha

Yesu anashangaa Baba yake yaani MUNGU BABA ambaye alipata kibari kwake na hata mara kadhaa akasema kuwa "Huyu Ni Mwanangu Mpendwa Msikilizeni Yeye" ambaye Yeye huwa tunategemea huonekana wakati wa mateso, hasa wakati ambapo tumechoka hatuna jibu, Yeye huleta jibu, huyo naye anafika katika hatima ya mwisho ya angalau kupata tumaini kwake au hata neno la kufariji, huyo naye anamuacha, Yesu akaseme "Eloi Eloi Lama Sabaktani"

"Ukifika wakati wa kukomazwa kiroho na Mungu, kuna wakati anakaa kimya ili kukufundisha imani ya kumtumaini na kumpenda Yeye na si vitu akupavyo"

Yesu anafika msalabani, hakuna tumaini tena ni kifo tu kinamngoja, anatazama kulia na kushoto haoni msaada zaidi ya mama yake tu analia, anaona kama hawa wameniacha sawa, anaamua kumtazama Baba yake juu

My God!!!!!!
Anaona afadhari hata ya hawa ambao wamejificha lakini angalau wanamuangalia, anamuona Baba yake amegeuza shingo hataki hata kumuangalia

Na kumbuka Yoh 16:31-32

Huyo ndiye Baba ambaye alijidai kwa wanafunzi wake na kuamini wakimuacha wao, Yeye  atakuwa naye

Huu ndiyo wakati wa kuonesha imani

Yesu anafikiwa Na wamama wanampa maji huku wakilia, Yesu anawatazama,

Tazama sasa baada ya Yeye kujionea huruma anawaonea huruma wao
WHY? Anatazama ikiwa Yeye Mungu na mwana wa Mungu na dunia imemuonesha dhiki namna ile, itakuwaje kwa mti mkavu. Twende pamoja usichukuzwe.

Yesu anawaambia msinililie mimi, mimi ndiyo naelekea mwisho na nikitoka mwisho naelekea upande wa pili wa ushindi na kuitwa mfalme wa wafalme
Jililieni ninyi na watoto wenu, ikiwa dunia wamenitenda mimi mti mbichi itakuwaje kwenu

Kwa maana nyingine Yesu anawaambia ndiyo mmenifata lakini kuna wakati mtaona mlichosikia na kuamini viko tofauti, mtaona dhiki, umasikini, uadui na kukataliwa

Yesu akiwa msalabani kwa machozi anaita Eloi Eloi Lama sabaktani, Mungu wangu mbona umeniacha

Yesu anafika wakati haoni jibu, anapanga kete na kupanga, weka mawazo na kuweka, panga na kupangua
Omba na machozi ya damu
Anatazama msaada wa wanafunzi wake haoni jibu, wote wamelala
Kuna wakati miimili ya kukusaidi watalala, watakuacha peke yako
Anarudi kuomba Mungu haji,

Luka 22:43-44 anasema akiwa katika dhiki, malaika akaja kumtia nguvu
Lakini baada ya uchungu kupotea, ndiyo kwanza unaongezeka baada ya machozi ya maji sasa machozi ya damu, anaomba na kuomba Baba amuepushie kikombe kile inashindikana, panga na kupangua

Alafu ebu fikiri, Yesu alikuwa anaomba kikombe kimuepuke, badala ya Mungu Baba kuepusha kikombe, eti anamtuma malaika aje kumtia nguvu. Lile halikuwa jibu Yesu aliloenda kuomba mwanzo, alitaka kikombe kimuepuke, malaika anakuja kumtia nguvu.

"Kuna wakati Mungu atataka upite jangwana ili akufundishe kitu, wakati huo hutohitaji kutoka, utahitaji kutiwa moyo, lengo ni umalize somo"

Yesu akasema "ikiwa ni mapenzi yako" wakati huo utahitaji kutiwa moyo na mapenzi ya Mungu lazima kutimia"

Je umewahi pitia jaribu, unaomba na kuomba Mungu alifanyie hata wepesi, unafika hata kufunga tatu mpaka nne kavu lakini wapi bora ungekula tu....
Ita na watu wanakusaidia kufunga, wanakushauri lakini wapi ndiyo kwanza linazidi come on... Machozi ya maji yanabadirika sasa unaamia kilio cha kwikwi moyo wako umekata tamaa

Unapanga kete hazipangiki, unapanga hazipangingi, shauriwa na kushauliwa kama wanakuchelewesha tu
Ita mke, marafiki, wachungaji hakuna msaada.

Hapo ndipo imani ninayoongelea hapa inatumika

Wakati ambapo Biblia inasema nitafanya mlango wa kutokea alafu ndiyo unaona hata dirisha dogo ulilokuwa unatazamia kupenya hapo nalo limefunga
Haleluya

Yesu alipoona hii ngoma nzito
Akaamua anyoshe mikono juu
Akasema kwa imani "Ee Baba ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu bali ni mapenzi yako yatendeka"

Nenda hapa utanielewa

Yoh 11:4
Yesu analetewa habari ya Lazaro kutoka kwa maumbu yake yaani Mariamu na Martha, Yesu anajibu tofauti na matarajio ya mwanadamu awaye yeyote duniani

Anawaambia "naye Yesu aliposikia, alisema Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwaajili ya utukufu wa Mungu, ili mwana wa Mungu atukuzwe"

Kumbuka Yesu ni mponyaji na Lazaro ni rafiki yake, na Lazaro anakujua kuwa Yesu ni mponyaji hivyo tu kujua kuwa ana taarifa ni faraja tosha.

lakini haendi

Cha kufurahisha hakuna aliyehoji, wala Martha hakuwatuma tena watu, wala hakuja mwenyewe
Lazaro rafiki yake Yesu aliyekuwa akishuudia Yesu akifufua wafu na kuponya viwete na kwa moyo wote akaamini

Leo Yesu anataka kumfundisha kumjua si kuona miujiza
Lazaro anaita msaada, lakini hauji mpaka anafika mwisho, anakufa

Najua umewahi kufika wakati, umemuita Bwana na kuona yu kimya hata unaoomba nao ukafika wakati ukawaambia Mungu amekaa kimya, pamoja na shutuma bado Mzee wa siku anakaa kimya
Nyumba unafukizwa, watoto wanarudi nyumbani, fedha ya kula tu ni tatizo, ada je
Unaomba sana, leo unazika huyu, kesho mwanao wa kike anakuletea mimba, na mtaa mzima wanajua ni mlokole na unajisifu kuhusu wokovu wa wanao
Yesu amekaa kimya

Nazungumzia imani ambayo hata wakati unaona mwisho wa mambo yote yenyewe bado inaamini, wewe siyo wa kwanza, kufika wakati kuchoka

Martha anafika wakati amechoka, Anamtazama Yesu, Yesu hatokei, anajipa moyo
Mwisho anaona ndugu yake hawezi kabisa na mwili unaacha roho, ohooo hapo ndipo anachoka na kuona sasa imekwisha

Najua umewahi fika wakati huo, wakati ambao unaamini na umesoma kwenye Biblia ndiyo wakati wa Bwana kutokea
Unaona ndiyo kwanza hata maombi hayana uwepo wake, ni makavu kama hujaokoka
Unajiona labda una dhambi, unaanza kutubu, yote pia ni kama unasema hewani
Hiyo ndiyo imani ninayoiongelea hapa

Lazaro amekufa, Martha anawaza Yesu atakuja kumfufua, mpaka wanazika haji
Come on, je bado unayo imani? Unapofika nyakati hizi.

Martha anakata tamaa, wanamzika Lazaro
Martha amekwisha, tatizo sasa ni basi
Yesu ndipo anatokea
Martha anamwambia Bwana umechelewa kuja mtoto ameshafukuzwa shule,

mke wako ndiyo amepinda tayari asikii wala haambiliki, amesharudi kwao tayari, hata kitanda kila mtu na chake
Anaumwa kabaki mifupa
Biashara na fremu tumesharudisha
Chumba na vyombo tulitoa nje hukuja, sasa na kuuza tumeuza vyote tumerudi kwa wazazi kuomba hifadhi, kama ni aibu tumeshaipata
Wakati alisema atatufichia aibu, ni masikini tayari, na huduma nimeshaacha, chuo nimesha Disco, sina ada; Yesu ndiyo unakuja, umeshachelewa.

Je umewahi pita wakati Yesu anakuja kujibu maombi yako too late (ameshachelewa) na ulivyotarajia.

Yesu anamwambia

"Sikukwambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu".

Naongelea imani ambayo, bado unaamini wakati uliyosoma kwenye Biblia ni tofauti na unavyoona kwenye maisha halisi

Yesu alikuwa anataka Martha asiishie kumpima Yesu kwa vilema na viwete na wafu waliokufa asubuhi mchana anawafufua, alitaka asimpime katika ufufuo wa wafu pekee katika siku ya mwisho, kuna kiwango cha imani alitaka kumpeleka.

Jiulize Kiwango gani Mungu anataka kukupeleka?

Ipo level ambayo unamwamini Mungu, mruhusu Mungu akuonesha anaweza fanya zaidi ya hapo ulipo, zaidi ya aliyowahi kukufanyia, muache akuoneshe anaweza zaidi ya ulivyoona zaidi ya ulivyoamini.

Alitaka ajue Utukufu wa Mungu ni mkuu sana pale ambapo hakuna majibu, pale ambapo akiri za mwanadamu haziwezi endelea mbele tena. Anachoka

"Lolote linafanyika kwako ni kwa utukufu wa Mungu, ambao huonekana baada ya kufika mwisho"

Lazaro anateseka, Martha analia, kumbe Mungu anajua mwisho wa jambo kabla hata ya mwanzo na ameweka kwa utukufu wake.

Yesu anapotazama, mateso na machozi yale anakumbuka kuwa Baba yake huwa anatenda mwisho wa akili za wanadamu.

"Unapombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.

Yesu ananyosha mikono juu
Na kusema ikiwa ni mapenzi yako na yatendeke

Na hii ndiyo imani
Wakati ambao huna majibu ya mambo unayopitia,

kama kweli una imani na Mungu na si kanisa, si mchungaji
Unaona marafiki, washirika, ndugu na wote wamesimama kushoto wanakutaza na hawana msaada kwako wowote huo ndiyo wakati wa kuonesha imani yako
Wakati wa Kuacha Mapenzi ya Mungu na yatendeke

Biblia inasema katika
Ebrania 12:1-3

"Yesu kwajili ya furaha aliyowekewa mbele aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu"

Hivyo tunapoongelea ukamilifu wa Kristo tunaongelea pale mtu anapofika wakati hayatazami mateso yake, hatazami kushindwa, hatazami kukataliwa, bali anatazama furaha iliyoko mbele yake, furaha iliyo ndani ya jaribu hilo

Hivyo imani ni kutazama ya mbele na kuyafumbia macho ya sasa hata kama Mbele imefunikwa na kiza kinene, haionekani, inaona ulipo ndiyo mwisho
Uko tayari hata kufa hivyo hivyo ulivyo

"Imani ni kupika hatua pale ambapo huoni mwisho wa ngazi" Martin Luther King Jr

Na ukayafumbia macho na kutazama mbele, kwa kutokuitazama aibu ya sasa, hiyo ndiyo imani na ndiyo iliyokamilifu katika Kristo

1. Naongelea wakati ambao Yakobo amechoka, na Mbingu zinafunuka na kugundua kumbe pale alipo kuna Mungu
Wakati ambao katika hari ya kushindikana kabisa, na kuona Mungu amekuacha, unakuja kugundua kumbe Mungu yupo hapo ulipo

2. Wakati ambapo imani yako inagoma kuamini, na inakuradhimu kuanza kushindana na imani yako
1 Timothy 6:12
Imani yako inagoma kuamini, lakini wewe unashindana nayo na kuishinda mpaka inaamini

3. Wakati wa kutazama mwisho na kuona furaha uliyowekewa mbele kisha kurudi mwanzo na kuona unatokaje ulipo

4. Ni wakati wa kuwa na subira na saburi na kusubiri kuyaona mapenzi ya Baba wa Mbinguni
Huu ndiyo ukamilifu wa Kristo

Waooooo

Mungu alibariki neno lake
Kristo neema yako iwe nawe
Roho mtakatifu awe ushirika nawe unaposoma ujumbe huu
Mungu uwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja nami katika kuandaa ujumbe huu, kuufundisha makanisa kadhaa na leo kuuandika kwako.


From the Holy Spirit
Written by Ev. Ulenje Mwaipungu.

Saturday, December 5, 2015

SEHEMU YA TANO: BARAKA TANO ZA PETRO FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA

FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA

Unaweza kubadiri jana yako na ukawa tajiri wa kesho.
Fanya hivi

"Tendo unachopaswa kutenda, usitende usichopaswa kutenda"

FIKRA NNE TOFAUTI KUHUSU JANA

A. Kundi la Watu ambao Huamini wanaweza kufuta makosa ya jana kwa kufanya zaidi leo.
Jim Rohn anakutana na binti akiuza maandazi ya aina tofauti, binti anamuonesha tabasamu zuri na kutangaza maandazi yake, Jim anapenda sana tabasamu la yule binti, na kwasababu alikuwa ni mpenzi sana wa maandazi ya aina ile, na tabasamu la binti akajikuta anavutiwa kununua.

“Huwezi kufanya usichoweza kufanya, kama hukujiandaa kufanya, wenye maandarizi bora ndiyo pekee wanaweza kufanya kwa ubora”

Jim akauliza bei, binti akamjibu kwa dharau akijua ni kiasi kidogo sana cha pesa "yapo maandazi ya rangi tofauti, na yote nayauza Dola $2 pekee”
Jim pia akakubaliana na binti pia kuwa ni kiasi kidogo sana, lakini kilichomkwamisha, akajitazama mfukoni hana kiasi hiko kidogo. Ndiyo ni kiasi kidogo ila ndiyo hana, Jim akafikiri "ni mtu mzima, ana familia, ana mtoto, anaishi Amerika, kwa aibu akalazimika kumdanganya, ili tu afiche aibu, akajibu kwa ujasiri wa kutengeneza "Nina maandazi mengi tu nimenunua, yanatosha kwa familia yangu"

“Tatizo laweza kuendelea kuwa tatizo, kama halitashughulikiwa kama tatizo”

Ficha tatizo ila si kwa wote, maana unahitaji Mungu, Fikra chanya, Maono, Ndoto, Kuona mbali na Watu ili ufanikiwe”

Binti alipotazama ujasiri wa Jim akaamini, akaondoka.
Lakini baada ya binti kuondoka, Jim anaingia ndani na ghafla akiri zinamjia, na kufikiri “Siwezi kuendelea kuishi namna hii”

Tukio moja likabadirisha maisha ya Jim Rohn, Jim Rohn akanyanyuka siku na kuwa milionea, mwalimu mhamasishi (Motivation Speaker), akazunguka karibu dunia yote akifundisha namna ya kufanikiwa na kuongeza ubora wao, Kila mtu alipenda kusikia japo neno lake moja, na katika maisha yake alipenda kusema"

"Usitamani iwe rahisi, tamani uwe bora”

Haikuwa rahisi, ila aliponyanyuka siku hiyo akaongeza ubora wa fahamu zake kuhusu kesho yake, na kusema SIWEZI KUENDELEA KUISHI MAISHA HAYA.
Maisha yake yakabadirika.

“Namna unavyoiona kesho, Ndivyo utakavyokuwa”

SWALI: nini kinakutia hasira leo, ni tukio gani linakupa hasira leo, ni dharau ipo inakupa hasira, nani kakunyima kazi, nani kakufukuza kazi, nani kakuibia, nani amezina mafanikio yako. Jibu lipo...

"Kisasi kizuri ni kuwa na mafanikio makubwa"

TAARIFA MUHIMU
Dunia imejaa matajiri ambao ni masikini wa jana. Na KESHO dunia itajaa matajiri ambao ni masikini wa leo" kama hauamini, Omba uhai, utaona. Lakini nakuombea uje kuwa wewe.

Nikupe siri kabla ya kusonga mbele: Kutafuta mafanikio ni kazi ngumu, ila kuwa masikini ni kazi ngumu zaidi"

Dunia imejawa na watu wenye furaha ya maisha, ndoa, kazi, wamejawa na maisha wanayopenda kuyaishi, lakini jana walikuwa wanaishi katika maisha wasiyoweza hata kuyahadithia. Yamejawa na aibu na matukio ya huzuni.
Pamoja na shuhuda za watu hawa ambao walikuwa masikini jana leo ni matajiri lakini nashangaa  bado bilioni ya watu duniani wanaishi maisha yao ya jana na kuiabudu leo hata kukata tamaa na kesho yao.

Jibu ni dogo... Kwanini unakata tamaa, kwani una hofu kama utafika, kwanini unaanza na kuanguka, unainuka na kuanguka...

JE WAJUA
1. Historia nyingi za watu waliofanikiwa zipo kwenye vitabu, na namna walivyofanikiwa, Cha ajabu matajiri ndiyo wanaosoma vitabu na vipeperushi, masikini hawasomi, na wengine wamebakia vile vile, walivyo jana ndivyo walivyo leo, kwanini?

2. Fikra za masikini kuwa jana yao ni matokeo ya mambo waliyofanyiwa na wengine, matokeo ya jinsi walivyo; "sina akiri, mimi ni kilema, mimi ni kipofu, mimi ni yatima, nilikosea kuowa, nilikosea kuchagua elimu hii, nilikosea kuchagua mtu wa kufanya naye biashara, serikari ilikuwa mbovu". Kundi hili huwa halikosi sababu.
Watalaumu serikari, wazazi walikuwa masikini, sina elimu, walimu walikuwa hawafundishi, wazazi hawakunipa mtaji, ndugu hawakunijari, uchaguzi haukuwa huru na haki, barabara mbovu.

Na hii huwafanya kutofikiri nini wanaweza kufanya leo.

3. Matajiri na watu waliofanikiwa hutumia semina na makongamano kufundisha masikini namna walivyofanikiwa. Cha ajabu hawaendi, ni matajiri tu ndiyo huenda.
"Unaweza kuifanya kesho yako kuwa njema, kama utaamua kuitumia leo yako vema.
Petro alitumia kila fulsa ya kuongea aliyoipata kutengeneza kesho yake njema.
Jibu la swali ni rahisi
Tajiri ana kuwa tajiri na masikini masikini, kwasababu tajiri ameamua kuwa tajiri na kujenga tabia ya kuwa tajiri.
Kutumia mda vizuri, kujifunza mbinu za kufanikiwa, kuona leo kama siku iliyipita na jana kama historia.
Wanatumia mda wao vema, wako smart.

B. Kundi la Watu ambao bado wanaishi Jana Yao.
Kundi la pili ni...
Kuna watu wengine wapo kwenye kundi lapili, wao wapo  dunia ya leo lakini bado wanaishi dunia ya jana. Bila kujari kipato ulicho nacho, hata kama ni tajiri ila kama bado unawaza yaliyotokea jana na kukufanya kuona leo huwezi fanya kitu basi bado unaishi jana, una fikra za masikini.
Kundi la watu wachache na waliofanikiwa, wanaoitwa matajiri,

"Hivi unadhani naweza kuwa mtakatifu? Huyu ni kijana anayejiuliza. Watu wengi bado wanaishi kwenye makosa waliyofanya jana, bado wanaishi kwa  kukumbuka waliyofanyiwa jana. Bado wanakumbuka yaliyotokea jana.
Na fikra hii huzaa maisha ya tabu, wanashindwa kufanya kitu chochote,  wanashindwa kutafuta fulsa, na hata zinapotokea wanashindwa kuzitumia, kwanini, bado wanawaza jana.
Asingeniibia fedha ningekuwa tajiri, haya ni mawazo ya kijana wa miaka 24-30, "mimi ni kijana mwema, nasari, natoa zaka, nasaidia masikini, nafanya kazi kwa bidii, lakini ni masikini. Muulize kwanini? Anajibu: "ndugu zangu hawanisaidii, baba yangu alikuwa masikini.
Haya yote ni mawazo ya jana. Badirika.
Acha kuwaza sababu toka nje, mafanikio yako ni kazi yako.

"Usisubiri wengine, fanya nafasi yako, na muache Mungu afanye nafasi yake"

Siku moja nimewahi kukutana na tajiri mmoja Mr. Mwacha nikapata fulsa ya kumshirikisha habari ya kumaliza chuo,  "mzee natafuta kazi ila kazi nyingi mshahara wake upo chini kweli" alinitazama, akacheka na kunijibu kwa ujasiri, neno lililobadirisha fikra yangu, akasema "hata ndege ili iruke lazima ianzie nyuma". Nikacheka ila nikaweka akirini. Baadae nikagundua, tajiri huwa anawaza jana alikuwa anarudi nyuma ili apae juu zaidi, huwa wao hawakati tamaa hata kama leo hana hata dola centi 25, bado anawaza kufanikiwa.

“Kufanikiwa ni kiwango unachoweza kwenda juu pale unapodondoka chini”

Masikini anawaza jana alirudi nyuma kwasababu yeye ni masikini, watu wanamuonea, jinsi alivyo: utaifa wake, rangi yake, ni kilema, ni Mwafrika mweusi, baba ni masikini.

C. Watu wengine Wao wanatazama tu serikari imefanya nini,
hawa ni watu wa takwimu na makabrasha, na mabingwa wa kusoma taarifa na si kanuni. Macho yao ni serikari ilifanya nini mpaka tupo hapa na haya yanatupata.

"Taarifa haiwezi kukuweka huru, kweli itakuweka huru"

Watu hawa Macho yao hutazama serikari ilitenda nini siyo wao walitenda nini. Petro hakuitwa Zelot kama Simoni, yeye hakutaka kupambana na Warumi, alihangaika kuongeza uwezo wake wa kuvua samaki, kuvua watu, kuhubiri injili, kufanya miujiza na mafanikio yakamfata. Haa walipopambana naye, hakupambana, alilinda tu Jina la Bwana.
Acha mambo ya kuifanya serikari mzazi; kutegemea ikurishe na kukupa maisha bora, kuwa mzazi wako binafsi na mhusika mkuu wa mafanikio yako.

"Hukumbukwa wale wanaotoa msaada kwa dunia, husahaulika wale wanaosaidiwa na dunia"

Martin Luther, Martin Luther King Jr, John Bunyan, Dr Living Stone, Abraham Lincolin, Mother Teresa, Albert Einstein, Musa, Yohana Mabatizaji, Paulo na Mkuu wa wote wa rohoni na wenye mwili Yesu Kristo:

Walipojitoa kuisaidia dunia hawakusahaulika. Acha kumlaumu mtu kushindwa kwako, angalia umekosea wapi, hata kama wamekutenda nini, bado unaweza kutumia hayo kwa mafanikio yako.

D. Kundi la Wafikiri Chanya.
Petro alifikiri chanya kila siku: akasema Bwana tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kingine cha Eliya na kingine cha Musa. Aliamini kuna kitu kitabadirika. Amini ukioata siku moja kukaa na Bwana kama Sulemani mambo yatabadirika.
Watu wa kundi hili ni watu watakaofanikiwa, kundi hili huwa wana amani na ni wakomboa mda saa zote, husahau waliyotenda jana na kutazama fulsa ya leo, na hutenda wakitazama nini wanapaswa kutenda leo.
Ni wachapa kazi wasiyopumzika, maana kwao jana hutosha kwa maovu yake, na faida zake, hata kama alifanya mambo makubwa ya kuushangaza ulimwengu, yeye anasahau na kutazama anayopaswa kuyatenda leo.
Hata kama jana alishindwa, yeye huamini leo ni SIKU MPYA NA FULSA MPYA. Wanatoka nje ya milango ya nyumba au geto zao na kwenda kutafuta fulsa, wanazitumia na kufanikiwa, hata kama watashindwa tena. Huendelea kuzitafuta fulsa zingine. Yaani wao hawakomi kutafuta na kuzitumia wanapozipata.

Mstari wa maisha: jana imeshapita, leo ni siku mpya na fulsa mpya, kesho yaweza kuwa nzuri zaidi ya jana.

FIKRA NZURI KUHUSU JANA
Nini kinatupa utofauti kuhusu jana, Tabia ndiyo inatupa utofauti wa fikra kuhusu jana. Fikra sahihi ni kufikiri:
1. Jifunze kutoka jana yako.
• Wapi ulikosea; usifanye tena
• Nini ulifanya kikakupa hasara: usifanye tena
• nini ulishindwa: ongeza uwezo na ufanye

“Usitamani ingekuwa rahisi, tamani uwe na uwezo" Jim Rohn.

2. Kubali ukweli
Kubali kuwa ulikosea, usipinge kila kitu, na ubadirike.

3. Usiruhusu jana kukuadhibu, itumie kwa faida yako.
Kwanini una huzunika, kwanini unasikitika, achana na hayo. Usiruhusu ikuadhibi, tumia mapito hayo kwa kufanya zaidi, hiyo ndiyo bora zaidi.

"Ana heri anaejari mwisho wake kuliko anayesumbuka na mwanzo wa shida”

4. Usihamishe uhusika wako kwa yeyote
Usiwaze kama ingekuwa hivi ningekuwa, waza kama ungekuwa hivi ingekuwa hivi. Usiseme baba angekuwa tajiri, ningekuwa tajiri, sema ningekuwa nina mipango na kusimamia mipango yangu ningekuwa tajiri. Petro hakusema Yesu bahari ni chafu hatujapata kitu, alisema Tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitazisha nyavu.

5. Ongeza uwezo
Petro aliposema kwa neno lako nitashusha nyavu, alimaanisha kukubali uwezo wake wa ndani ulikuwa mdogo, na kukubali kuwa uwezo wa Yesu ulikuwa mkubwa, hivyo kwa neno lake anashusha nyavu.
Ni mara ngapi katika jana yako umefanya kazi ya kuchosha pasipo matokeo chanya, kwanini ulishindwa, UWEZO WAKO WA NDANI ULIKUWA MDOGO.
Soma vitabu, sikiliza mafundisho, hudhuria semina, jifunze  kwa waliofanikiwa na kwa walioshindwa, ongeza uwezo wako wa ndani, kaaa karibu na waliofanikiwa, omba msaada kwako, kwa nguvu zao utafanikiwa.
Kumbuka Yesu alimwambia nini Petro "nitakufanya kuwa mvuvi wa watu"
Yesu hakutaka kumwambia Petro tatizo ni serikari ya Rumi, tatizo ni upepo au uwepo wa Mafarisayo na Masadukayo, akamwambia tatizo ni wewe, tatizo ni uwezo wako wa ndani, Yesu akatumia miaka mitatu kumfundisha Petro na kuongeza uwezo wake wa ndani, na akawa mtume kiongozi. Siku nilipoiona nyumba ya Petro kwenye dokomentari kuhusu maisha yake nilishangaa.

"Usitamani jana ingekuwa rahisi, tamani ungekuwa bora" Jim Rohn.

Leo nimemtumia sana Jim Rohn kwasababu natamani ujifunze kwake, mtu aliyeweza kupatwa na hasira na maisha yake ya jana, na kuweka ahadi ya kuibadirisha.

Tutaenderea...

Unafikiri ufanye nini kasahihisha jana yako
"Tenda unachotakiwa kutenda, Usitende usichotakiwa kutenda"

Somo lijalo tutaangalia hasa maana ya kesho na namna watu wanavyoitazama kesho. Na mwisho tutaangalia kuhusu leo, ambayo ndiyo lengo hasa la somo hili.

Tutajifunza Kanuni nyingi za msingi za namna ya kutumia leo.

Asante kwa kusoma, Mungu akubariki kwa mda wako.
Naamini ROHO MTAKATIFU AMEKUSAIDIA KWA SEHEMU.