Monday, March 3, 2014

WAMNGOJAO BWANA TUTAPAA KAMA TAI (Isaya 40:26-31)


Isaya 40:25-31(31)
Tai ni ndege wa tofauti na ndege wengine kabisa.

SIFA ZA TAI
1.      tai anatembea na tai wenzie
na sio ndege wengine yeyote; sio mwewe wala kunguru
Ø  watu wapenda mafanikio wanatembea na wapenda mafanikio
Ø  watakatifu na watakatifu.
2.      tai anapaa umbari mrefu zaidi ya ndege wengine.
Ø  Mungu ni lazima atupe nguvu za kufanikiwa zaidi ya wengine
Ø  Mafanikio kazini zaidi ya wengine
Ø  Biashara mafanikio na wateja wengi zaidi
Ø  Tenda nyingi zaidi
Ø  Max nyingi zaidi kwa wanafunzi
3.      Tai anatazama umbari mrefu zaidi (kilometa 5 mbere)
na akikiona kitoweo au kitu hukivuta na kuonekana karibu na kukifata mpaka akipate, hata kama vikitokea vizuizi huwa hajari na hupambana mpaka akipate.
Ø  Hata majaribu yajapo 2014 hatutojari bali tunatazama ahadi za Jehova mpaka tutakapozifikia
Ø  Hata kama wakitokea watu kupinga, kazi au mume lakini tunatazama ahadi za Bwana mpaka tuzipate
Ø  Majaribu yajapo tunafumba macho na kuzivuta ahadi za Bwana na kuzitazama hizo tu.
Ø  Lolote na hilo (piga uwa) kupaa kama tai lazima.
4.      Tai hali mizoga bali anakula chakula halisi (kipaya/flesh)
Ø  Tunatafuta taarifa mpya na sio za zamani.
Ø  Hatutotumia vitu vya kale; kuazima au kupewa bali 2014 ni mwaka mpya na mafanikio mapya.
Ø  Sisi sio watu wa kazi za kale
Ø  Sisi sio watu wa asiri tena; ugonjwa na mikosi ya babu ni ya babu sisi tunaanza upya.
5.      Tai anatumia kimbunga au upepo mkali kupumzisha mbawa na kupaa juu zaidi.(upepo mkali unaoambatana na radi, mvua, na ngulumo kali).
Wakati ndege wengine wanajificha kwenye miti na vichaka kuogopa
Ø  Wakati wengine wanalalamika matatizo na shida wewe unatumia majaribu na shida hizo kupaa zaidi angani.
Ø  Tumngojeao Bwana tunatumia dhiki, uchi na adha kupaa juu zaidi kimafanikio.
6.      Tai wanapotaka kukutana (kujenga ndoa).
·         Mwanaume humfata mwanamke juu, mwanamke agunduapo hushuka chini na kuchukua gome au ganda la mti na kupaa nalo juu.
·         Akifika juu analiachia lianguke chini; mwanaume analiata kwa kasi, na jinsi linavyoongeza kasi naye anaongeza kasi; akilipata anarudi nalo juu na kumpa mwanamke.
·         Mwanamke anapaa tena juu zaidi na kuliachia tena; na mwanaume kulifata kama mwanzo na kulirudisha kwa mwanamke
·         Na mwanamke hupaa tena juu
·         Kitendo hiko hufanyika zaidi ya saa moja
·         Mpaka pale mwanamke atakapoona umbari wa kwenda juu unatosha na baada ya kuona mwanaume amefauru mchezo ndipo anakubari.
Ø  Kabla mtu hujakubari urafiki au ukaribu naye mpime kwanza
Ø  Sisi ni wa thamani (tumngojeao Bwana)
Ø  Sisi sio watu wa kawaida
Ø  Sio watu wa chipsi na keki au soda
Ø  Hatupatikani kirahisi
Ø  Ni bidhaa hadimu
Ø  Thamani yetu ni kubwa makazini; wanatuhitaji na wakibaki wao tu mambo yote yanaharibika.
Ø  Dunia yatuhitaji; ndio maana tukiondoka tu na dunia ndio mwisho wa mchezo wake.
Ø  2014 ni kutafutwa kama lulu
7.      Wanashirikiana kwenye uzazi
·         Tai jike anapotaka kuzaa; jike na dume wanashirikiana kutafuta eneo la juu la ncha ya mlima ambapo mnyama na adui hawezi kufika.
·         Mwanaume anaenda kutafuta miba na kuweka sehemu hiyo na kushuka tena chini kuleta magome ya mti kujenga kiota juu ya ile miba
·         Na kushuka tena chini na kuchukua miba na kuweka juu ya yale magome; anashuka tena na kuchukua nyasi na kufunika ile miba
·         Kisha anashuka tena na kuchukua ngozi kufunika zile nyasi
·         Baada ya kumaliza kujenga kibanda anarudi tena chini kuchukua miba mingi zaidi na kufunika kile kiota; kuzuia maadui.
Ø  Mwanaume na wanawake lazima tushirikiane katika kujenga familia; familia tujenge pamoja.
Ø  Kanisa lazima tubebane: muujiza wa mtu upo mikononi mwetu
Ø  Nyumba zetu, familia zetu, maisha yetu ni lazima yalindwe na Damu ya Yesu.
Ø  Wako makini kufanya mambo yao nasi lazima tufanye mambo kwa umakini.
Ø  Baba anafanya jukumu kama kichwa na mama anakaa pembeni na kutia moyo
8.      Wakati wa kufundisha watoto.
·         Mama yao anawatoa kwenye kiota sababu ya uwoga wanarudi tena
·         Hivyo mama yao anatoa ngozi na kubakiza miba- hivyo wanaporudi tena ndani wanakutana na miba wanachomwa na kutokwa na damu
·         Wanashangaa baba na mama yao aliyewapenda sana leo amewageuka na kuwaumiza.
·         Na baadae mama yao anawasukuma pembeni ya ncha ya mlima na kuanza kuruka kwa hofu.
·         Kabla hawajaanguka chini baba yao anatokea na kuwabeba wasianguke na kuwarudisha mlimani
·         Kitendo hiko kinaendelea mpaka wahakikishe wote wanajua kuruka sawa sawa.
Ø  Wanapopatwa na mshangao wa mateso hayo- hapo hapo wanapata maarifa na mbinu mpya za kimaisha na kuishi
Ø  Mungu anakuwekea miba (shida, dhika, uchi na adha na mateso na majaribu) kwa mema; ili upate mafunzo na kukufanya uwe bora zaidi ya sasa.
Ø  Wakati mwingine anafanya kama amekuacha kumbe yupo pembeni akikutazama na kabla hujaanguka anakuja kukubeba
Ø  Tumngojao Bwana mwaka huu ni lazima tubebwe na Jehova katika Jina la YESU.
Ø  Na atakujaribu kwa kila hatua mpaka ufuzu mafunzo yote na kuitwa mkakamavu: ukifuzu level moja anakupeleka level nyingine mpaka uwe umekomaa ndipo anakuacha.
Ø  Tunapaswa kujifunza kutoka kwenye matatizo na sio kuraumu
Ø  Kawaida watu wanaopata mateso, magumu na matatizo magumu na mengi ndio ambao wanatoka na maarifa, hekima na uzoefu zaidi. MFANO DAUDI NA SULEMANI
9.      Tai anaishi miaka mingi zaidi
·         Anaishi miaka 70
·         Lakini kufika miaka hii, anapaswa kufanya uamuzi mgumu katika maisha yake.
·         Akifika miaka 40;
o   Mdomo wake unachoka/unazeeka na kushindwa tena kuchukua mawindo(ukari na uregu wa mdomo unapinda)
o   Kutokana na uzee na uzito wa mabawa, manyoya yanarundikana kifuani na kumfanya kushindwa kuruka.
·         Anabakiwa na maamuzi mawili tu
o   Kufa
o   Au kupitia mateso na maumivu ya siku 150 (miezi 5)
·         Kitendo hiko kitamtaka tai apande juu ya ncha ya mlima kwenye kiota chake na kujipiga kwenye mawe mpaka ncha ya mdomo wake ivunjike yote.
·         Na kukaa akisubiri mpaka ncha ya mdomo iote yote.
·         Baada ya hapo analazimika kutoa manyoya yake yote ya uzeeni mpka abaki pasipo hata na nyoya
·         Baada ya miezi 5 anapata manyoya mapya na kuishi tena miaka 30.
Ø  Anaonesha kwamba wamngojeao Bwana kumbe kumbe tuchakaapo kuna kuzaliwa upya na kufanya upya tena na kuishi miaka mingine zaidi tukiwa na nguvu mpya.
Ø  Ni lazima tukubari kubadirika hata kama mengine yanaumiza; kwenye ufalme wa Mungu
Ø  Kujitoa kwenye matatizo ya kale ni lazima tukubari kupoteza faida za sasa (vya thamani vya sasa) kwaajiri ya baadae
Ø  Tunapaswa kutoa mambo yote ambayo hayana umuhimu kwetu kwa sasa ili kufanyika upya; kwaajiri ya kesho yetu
Ø  Lazima tukubari mateso, majaribu na shida kwaajiri ya baadae
Ø  Wakati fulani twapaswa kutoa tamaduni zetu, tabia, na mazoea fulani ili kuweka tabia na ufahamu mpya
Ø  2014 Bwana anakwenda kurenew maisha yetu na kutupa mapya yenye raha zaidi.
Ø  Maombolezo 3:22
Ø  Ayubu 17:9


THANKS ALMIGHTY GOD, Please my Dear God go and teach your people yourself; but I give all my body to use me as a tools, For Your Glory. In Jesus Name... Amen


                       




                       


                       

  

Wednesday, December 25, 2013

PURPOSE OF PRAYER AND CHRISTMASS


KUSUDI LA MAOMBI NA KRISMASS
Kusudi la Yesu kuzaliwa ilikuwa ni kurudisha utawara wa mwanadamu ulikuwa umeibwa na shetani amba mwanadamu alipewa na Mungu.
Mwanzo 1:26
Mungu anampatia mwanadamu utawara, anawaambia mkataware (Let them have dominion), lakini shetani anakuja kuchukua ule utawara kwa kumkosanisha mwanadamu na Mungu (kuondoa uhusiano wake na Mungu) Ambao ndiyo nguzo kuu ya utawara wake;maana hawezi kutawara pasipo kuwa na utawara na Mungu.
Shetani alipchukua ule utawara toka kwa mwanadamu, ndipo akachukua cheo cha mwanadamu kama mkuu wa ulimwengu huu na yeye kuwa ndiye mkuu wa ulimwengu huu, shetani akaanza kumtawara mwanadamu na kumuamrisha afanye anachokitaka yeye, na mwanadamu hakuweza kujizuia kwake, hata wafalme walimfata, Sauli alikosea, Mussa alikosea, Daudi alikosea, Sulemani alikosea, Yeroboam alikosea na wengine, machafuk, na dhambi zikaingia ulimwenguni, watu kuuwana wa kwa wao na kuuwa wanyama kwa kasi kubwa sana, uzinzi, ufiraji, ubakaji, ukahaba, ushoga na usagaji, wizi, udokozi, vita, unafki na umbea na magmvi ya kila aina.
Mungu akaleta mapigo mawili kwa kuamini wenda mwanadamu akamrudia yeye (sodomo na ghomola, na ile ya Nuhu) lakini mwanadamu akaendelea kutenda maovu kwasababu alikuwa chini ya mkuu wa ulimwengu huu shetani
Ndipo Mungu akasema sitomwangamiza mwanadamu tena, bali nitafanya nae agano jipya, Yeremia 31:31; 32:40
Yesu akazaliwa ili kuunda agano hilo jipya, na kuzaliwa Yesu ni ishara ya agano hilo jipya kama ilivyotabiliwa na nabii Isaya( Isaya 7:14, 9:6)
na ishara hiyo ilikuwa ni utawara; Hivyo Yesu alikuwa ni ishara ya kurejeshwa utawara unaotokana na uhusiano wa mwanadamu na Mungu. 
Yesu alipozaliwa akazaliwa kwa kusudi la kurejesha uhusian huo
ndio maana alipokufa pazia la hekalu(patakatifu pa patakatifu) na hivyo si makuhani tena bali kila mtu ana ruhusa ya kutengeneza uhusiano wake binafsi na Mungu na kupkea utawara ambao baba yetu na mama yetu Adam na Hawa waliupoteza.
na hivy kwa kuzaliwa kwake na kupigwa kwake basi hapo kwanza hatukuwa taifa lakini sasa tu taifa la Mungu, na tumefanyika wafalme na makuhani, watu wa milki ya Mungu (1petro 2:9, Ufunuo 5:10)
na sasa Ufalme wa Mungu si ufalme wa watu tena wa kawaida bali ni ufalme wa wafalme chini ya MFALME WA WAFALME
na si tena watu chini ya Kuhani bali ni ufalme wa makuhani chini ya Kuhani mkuu Yesu. 
Na hivyo utawara wetu umerejea tena.
Yesu akasema nimewapa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka na kazi zote za yule adui,
lakini pia aliwapa mamlaka juu ya pepo wabaya na magonjwa yote (Luka 10:18-19)
na Yesu alipoondoka wanafunzi wa Yesu wakaanza, kuwa na amri dhidi ya pepo, magonjwa, na hata wafu wakafufuliwa na viwete wakatembea, na hiy ni ishara ya kurudishiwa ufalme.
Hivyo krismass ni kurudishiwa uhusiano na utawara ambao Ibirisi aliuchukua kwa Adam na Hawa.
lakini kuupata utwara huu ni lazima uwe mwana mambi, sababu Mungu hawezi kufanya kitu chochote duniani kama Mwanadamu asipoomba na kuruhusu kifanyike kwa njia ya Maombi
Yoh 12:31, yoh 16:11