Friday, November 20, 2015

SEHEMU YA NNE: BARAKA TANO ZA PETRO (KANUNI ZA KUTUMIA LEO YAKO)

MAISHA NI NINI

Hili ni zaidi ya swali, kila mtu anayeweza kupata mda wa kufikiri maisha yake (experience) atapata kusema kuhusu maisha.
Maisha ni neno gumu kujua.

“Unaweza kuwa na maana nyingi kuhusu maisha, ila mapito yatakwambia ukweli”

Hii ni sehemu ya nne ya somo letu, leo tutaangalia sana kuhusu maana ya leo, leo ni nini, pia tutaangalia fikra tofauti za watu na namna inavyoathiri kutumia leo yao.


Maisha ni mda, ni mda uliopimwa au usiopimwa, maisha hupimwa na mda. Na kama ni mda usiyoweza kuhesabika hayo ni maisha ya milele, na kama ni mda unaohesabika basi hiyo ni miaka ya kuishi.

Huwezi taja miaka ya Mungu, ila unaweza taja miaka yako, huwezi taja miaka ya mtu anayeishi milele.

Mda wa kuhesabu miaka ni ule unaokuwepo hapa duniani pekee, ukishaondoka na kufa basi sasa unaelekea kwenye maisha ya umilele, huwezi huko tena kuhesabu miaka. Maisha ya hapa duniani ya yanahesabika na kila mtu kapewa kwa kipimo maalumu

“Maisha ya hapa duniani ni mtihani wa kuona uwezo wetu wa kuishi milele”

Jinsi unavyotumia mda wako duniani, utavuna baada ya kufa” Hakimu wa Haki Yesu hatoangalia umeishi miaka mingapi, ataangalia umeishi vipi.

"Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe" Ayubu anazungumzia maisha ya mwanadamu kuwa siku zake zimeamriwa yaani zina kikomo na kikomo kimeshapangwa/kimeamriwa na tayari na kipo mikononi mwake.  "mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu, naye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa, hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe" Ayubu 14:1-2,5.

Nimetamani ujue kuwa siku zetu za kuishi hapa duniani zimepimwa, na zimeamriwa, zina mwanzo na zina mwisho.

Mwandishi wa Zaburi anamuomba Mungu "basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie hekima" Zaburi 90:12, alianza kusema "Bwana, unijulishe mwisho wangu, na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; nijue jinsi nilivyo dhaifu" Zaburi 39:4.

Hii yote yatuonesha maisha ya hapa duniani ni mda na kama mda una kipimo basi maisha yako yana kipimo na ipo siku yatafika mwisho,

Swali unaendaje na wakati huo uliopimwa, na unataka uwe umefanya nini ndani ya masaa hayo.

Nakuthibitishia kuwa wakati wako ukifika mwisho utaondoka tu hapa duniani
Usiwe kama Mfalme Hezekia, wakati wake ulipofika Mungu akamfata na kumwambia “atengeneze mambo ya nyumba yake, lakini Hezekia akatafsiri tofauti, Mungu hakuwa anamlaani bali anamtaarifu kiwa katika ugonjwa huo bado itakufa. Lakini alipoomba sana, Mungu ni msikivu akamsikia. Lakini kwa kuongeza siku hizo chache, Kwanza siku Hezekia akakosea, Biblia inasema baada ya kupona, hakumpa Mungu utukufu, akawaonesha wageni milki yote ya nyumba ya Israel, Sasa hezekia aliyeomba kuongezewa mda, unajua nini kilitokea tena, Hezekia akautumia ule mda kumzaa mtoto Manase, Manase akawa mfalme mbaya kuliko wafalme wote waliopita na waliyokuja katika israel.

Tumia mda wako vizuri...

“Nioneshe sababu nyingi za kushindwa maisha, mimi nitakuonesha moja, ni kughairisha.

Acha kughairi ghairi, kila siku nitafanya nitafanya. Sulemani anauliza E mvivu utaamka lini?
Anza kufanya leo jambo unaliona bado. Kuna wakati utafika hutoweza kufanya.

Usitumie mda wako mwingi kutaka kumpendeza kila mtu. Usitumie mda wako kujaribu kufanya kila kitu, jitambue wewe ni nani, umezaliwa kufanya nini na nini unapata hamasa kubwa unapofanya, pesa zitakufata mbele.
Kumbuka hadithi ya Martha na Mariamu. Martha akaanza kuhangaika hangaika akitaka kumpikia Kristo na kufanya kila jambo, Martha akatulia miguuni pa Yesu akimsikiliza; akaacha mengi na kushughulika na moja tu: Ufalme wa Mungu.

“Nioneshe sababu bilioni za mwanadamu kutotimiza kusudi lake, nitakuonesha moja tu, kujaribu kutaka kufanya kila kitu”

Tumia nusu ya miaka yako hapa duniani kufanyika mtu halisi uliyezaliwa kuwa, na tumia mda wako wa mwisho kufanya ulichozaliwa kuwa.

Andrew Carnegie baada ya kufa, walipoenda kwenye nyumba yake, wakapata karatasi ndogo. Mr Carnegie aliandika akiwa na miaka 20 “Nitatumia mda wangu wa mwanzo kuwa milionea, nitatumia nusu ya pili kugawa zote”.
Mr Carnegie alikusanya Dola za kimarekanj zaidi ya milioni 450 na anapokufa akawa amegawa zote.
Inaleta raha.

Usipoteze mda muhimu katika mambo yasiyo muhimu. Heshimu mda wako, watu wengi wanaotazama TV sana huwa hawaji kuonekana kwenye TV, wakoonekana si kwa mema.

Jim Rohn amewahi kumuuliza mtu, gharama ya TV, yule mtu akajibu $12 akamwambia hapana, gharama ya TV ni $12,000 kwa mwaka. Kwanini, watu wengi wanahesabau gharama ya kununua TV na siyo ya kutazama TV. Rafiki yangu kila kitu unachokipa mda, usisahau unakipa sehemu ya maisha yako. Maana mda ni maisha.

Twende pamoja, heshimu mda wako,  kwa maana ndogo kuheshimu dakika moja ni kuheshimu sehemu ya maisha yako.

Maisha yamegawanyika katika Jana, Leo na Kesho.

Lazima tuiheshimu jana, najua umefundishwa kutotazama jana. Lakini kutazama jana ni vema: tazama jana kwa namba ulizoongeza kwenye akaunti yako, thamani yako iliyoongezeka kwa Mungu na kwa jamii, tazama umefanya nini mpaka sasa, narudia tazama umefanya nini mpaka sasa?.

Kuna kanuni inasema utavuna ulichopanda. Kutazama jana inakusaidia kujua uliponda nini jana na ulipandaje na ulikuzaje; na maana ulivyo leo ni mavuno ya ulichopanda jana.

Tazama jana na ugeuze yote yaliyotokea kwako na yote uliyokosea na kupatia na kuyageuza kuwa falsafa na mbinu mpya ya mafanikio.

Yaliyotokea jana na uliyokosea jana yanaweza kufanywa na kuwa mbinu ya mafanikio ya leo. Unataka uthibitisho: jaribu.

Leo ni siku ya baraka: hakuna zawadi nzuri kama leo.

“Mtu anauliza, Je naweza kubarika, jibu rahisi; Ndiyo unaweza,
Anauliza lini sasa jibu rahisi siku utakayoamua kubadirika

Yaweza kuwa kesho; No! Mwambiye siku yoyote inayoitwa Leo.

Kesho ni ajabu; inaweza kuwa njema, inaleta tumaini, inaleta furaha.
Kwanini ukate tamaa wakati huijui kesho.

Tufatane pamoja ili tujue maana ya siku zote tatu: Jana, Leo na Kesho.

A. JANA
Jana ni sehemu ya mda ambao mtu ameutumia ndani ya kipimo cha maisha yake.
Jana ni marighafi au nguvu isiyoweza kurudi wala kuzalishwa tena. Jana ni sehemu ndogo sana ya mda uliyopewa na Mungu kuishi na kutimiza kusudi lake hapa duniani.
Wanafunzi wa chuo kikuu kimoja  cha hapa Tanzania, walijikuta kwenye wakati wa kununua moja ya vinywaji maarufu na vya gharama duniani kwa gharama ya kutupa, kwa bei ya hasara, kwanini zile bidhaa zilikuwa zinaelekea kuisha mda wake wa kuishi (expire date), baada ya mwezi mmoja zingekuwa zimeshaharibika. Jinsi bidhaa inavyokaa dukani ndivyo inavyozidi kutumia mda wake wa kuharibika na kutumika.

Jinsi binaadamu anavyotumia masaa 12 ya siku na kuingia masaa 12 ya siku nyingine ndivyo anavyozidi kuupunguza ule mda aliyowekewa au kuamriwa tayari na Mungu kama muandishi wa Zaburi alivyothibitisha, na ndivyo kweli.
Hivyo kama ulipewa siku 1000, 000 za kuishi hapa duniani, jana ulipoitumia sasa una 999,999, bila ubishi.

MAMBO YA MSINGI KUHUSU JANA
1. Huwezi kuigusa tena jana
2. Huwezi kufanya chochote ndani ya jana
3. Huwezi kusahihisha ulichofanya jana
5. Una nafasi ya kurekebisha matokeo ya uliyofanya jana pekee na si kufuta ulichofanya.
6. Jana ni historia, si hatima ya maisha yako.
7. Wakati wa msiba wako hawatakumbuka ulichotaka kufanya jana watakumbuka ulichofanya pekee.
8. Ulivyo leo ni matokeo ya uliyofanya jana
9. Kukumbuka na kuhuzunika ya jana ni kupoteza wakati, hekima ni kutazama nini unacho na unaweza fanya leo.
10. Jana inapaswa kutumika kama elimu tu ya leo, ulikosea wapi, ulikoseaje, na namna ya kurekebisha
11. Waliyokufanyia jana; unaweza kuyarekebisha leo
12. Leo ina nguvu zaidi ya jana.
13. Huwezi kuipata tena jana. Imepita

INAWEZEKANA...
Ndugu mpendwa inawezekana jana ulikuwa ni masikini sana, au hata leo, inawezeka jana umetenda dhambi, ninaposema jana nasema kwa wakati uliyopita iwe ni robo saa iliyopita au miaka kumi au hamsini iliyopita au sekunde moja iliyopita, inawezekana umekuwa mtumwa wa pesa, au inawezekana umekuwa ni yatima wazazi wamekufa, au una maisha hayo kwasababu ni mjane hivyo upo hivyo kwasabau ya uliyotebdewa jana, inawezeka upo hivyo kwasababu ya waliyokufanyia jana.
Inawezekana kampuni yako imeshuka kutoka na waliyokufanyia watu jana, washirika wa kampuni yako wamekusaliti, umepata hasara, umefanya uzembe fulani. Au namna yeyote ile.
Na sasa kuna maisha unayoishi, au kuna hari kampuni yako inapitia, lakini hiyo ni jana, tuzungumzie leo, itakusaidia kutoka maisha ya chini kuelekea maisha ya juu zaidi.

Usitazame jana, maadamu umeamka. Jifunze tu kanuni za kutumia leo yako vema.

Jifunze kanuni kuhusu leo.

Jana imepita achana nayo, jifunze tu ulikiseaje kupanda mbegu zako, au ulipanda mbegu gani. Panda mbegu njema sasa na uitunze na kuilinda mpaka iote na linda mazao mpaka uvune.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA


Karibu tena Siku sehemu inayofata, tutaona fikra tofauti kuhusu jana na kuenderea na somo letu.

Asante kwa kusoma
Mungu akubariki.
Ev.Ulenje.

Tuesday, November 17, 2015

SEHEMU YA TATU: BARAKA TANO ZA PETRO

SEHEMU YA TATU
BARAKA TANO ZA PETRO

JINSI PETRO ALIVYOTUMIA LEO.

Leo tuangalie kiundani kuhusu Petro na uhusika wake katika maisha ya Yesu akiwa duniani. Na pia tuone namna Petro alivyoweza kutumia leo yake aliyopewa na Mungu kwa neema. Na tuone namna alipotoka na namna alivyoweza kubadiri maisha yake na namna alivyoweza kuendana na baraka alizopewa hata zikaweza kutimia.

UHUSIKA WA PETRO

Petro alikuwa Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi na muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.

Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvua samaki na si kukaa na familia.

2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.

3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.

4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumuokoa Kristo asiteswe na Wayahudi na kufa japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.

5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanazungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuwa hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.

6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20

7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 11 waliobaki. Siku zote alitazama “maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari”.

8. Petro aliwaza chanya siku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwahi ona kitendo hiko toka azaliwe, akaamini akaenda, alipoambiwa habari za wokovu kwa mataifa katika maono, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ya jana, na kuwaza positive.

9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.

10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.

11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
“Tunashinda woga kwa kufanya tunachokiogopa kufanya”
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
“Unataka uijue siku ya kuanza kufanikiwa KiMungu, ni siku utakayoanza kufikiri kwa habari ya wengine”

5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
Akimaanisha “mwanaume shujaa ni yule mwenye uwezo wa kusimama peke yake”

7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa za leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15

Zote hizi tutaziangalia kiundani na kuzichambua kiurahisi zaidi ili kila mtu afahamu.
Namna alivyozipata na namna zilivyomfikia na namna zilivyotimia kwake.
Ila kwanza tuangalie maana ya jana, leo na kesho kiundani na kimafunuo zaidi.


MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, rafiki yangu mmoja akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika na hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana,
Akanitazama kwa makini na kuniambia "unajua Ulenje nilikuwa na akiri zaidi hata yako", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Yule rafiki hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.

MDA NI NINI...
Mda una maana nyingi ila huwezi kupinga hii.
Kifupi Mda ni maisha
Mda ni maisha yenye mwanzo na mwisho.
Mda si wa milele kama maisha ya milele, maisha ya milele hayana mda, huwezi kuyapima, yenyewe ni ya milele, yapo na yanaendelea kuwepo.
Unapotamka mda unazungumzia kipimo chenye mwanzo na mwisho. Unapotamka maisha niliyokaa shule, unatamka mda uliyokaa shule, ukihesabu kuna kipimo. Unapotamka nina miaka sabini unatamka mda uliyokaa duniani ni miaka sabini. Hivyo mda ni maisha, yana kipimo, yana mwisho.
Yesu anasema "imetupasa kufanya kazi zake yeye aliyenipeleka (nani?, Mungu) maadamu ni mchana; usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi"

"Yesu alipokuja alipewa mda wa kukaa ulimwenguni, na ilimradhimu kukimbizana nao: kwanini mda una kipimo”.
Ukipewa kazi ya kufanya kwa siku moja, maana yake yake ni masaa 12.
Moja ya huzuni ambayo huwa naisikia kwa wazee na watu wazima wenye miaka juu ya 50 wengi kila ninapopata mda wa kukaa nao, huwa wanasema "tulitamani kufanya mengi sana, tulipokuwa vijana kama ninyi, ila mambo yakawa mengi tukashindwa". Kwanini mda umeisha, kwa wao kufanya hayo, walipewa mda wakajisahau wakadhani wana umilele. Ila lipo tumaini toka kwenye kitabu hiki, kuwa hata kama una miaka 80 bado inawezekana.
Bado kwako unayesoma kitabu hiki, una miaka 20, 30, 35,  40, 45, 50, 55, 60, 65, 70, au yeyote ndani ya hiyo; jua kuna wakati utafika hayo unayoyafikiri hutoweza kuyafanya, na yataishia kwenye fikra zako tu.

MAISHA NI NINI...



Fatana nami tutenderea...
UBARIKIWE KWA KUSOMA.
By EV.ULENJE MWAIPUNGU

Tuesday, October 20, 2015

SEHEMU YA PILI: BARAKA TANO ZA PETRO NA KANUNI KUMI ZA KUFIKIA MAFANIKIO YAKO.

Tunaendelea
Kwanza naomba amini maneno haya;

"Maadamu yu hai...
1. Unaweza songa mbere zaidi
2. Unaweza toka hapo ulipo
3. Unaweza kuwa mtu huru
4. Unaweza kuwa mtu uliyefikiri kuwa
5. Unaweza kuishi maisha ya mafanikio unayotaka kuishi
6. Unaweza kuacha historia nzuri katika ulimwengu huu
7. Unaweza kubadirika
8. Unaweza kubadiri tatizo lako kuwa neema
9. Unaweza kubadiri historia mbaya kuwa nzuri
10. Unaweza kuinua maono yako na kuyaanza tena na kuyatimiza.
11. Bado unaweza kuwa jasiri tena
12. Unaweza kuwa mtakatifu tena na mwenye haki
13. Unaweza kuwa mtumishi tena
14. Unaweza kufanya uliyowaza kuyafanya.

Bado unaweza....
Na "LEO" ndiyo siku pekee unayoweza kufanya maamuzi ya kufanya haya. Jana haikuwa siku sahihi, kesho haigusiki, na hatujui.


JANA IMEISHA, LEO NI SIKU MPYA,  KESHO YAWEZA NZURI ZAIDI YA LEO
Tangazo hili naomba liingie ndani yako. Soma mfululizo huu kwa umakini, soma kanuni kumi kwa umakini, baada ya kusoma vitabu vingi vya watu waliofanikiwa, na kuona, na kusikia wengi waliofanikiwa, kupitia Biblia na kusoma watu waliofanikiwa, na maisha yangu binafsi; nimekuja kugundua kanuni hufanya kazi kwa yeyote pasipo kujali kabila lake, dini yake, taifa lake, rangi yake, umri wake, nchi anayotoka, elimu yake, na wote waliofanikiwa waliishi maisha ya kushindwa kwanza, ila walipoamua kufata kanuni maisha yao yalibadirika, na nilichogundua hawakutumia miaka au miezi, walitumia siku moja kama dhahabu inayotoka kwa Mungu kwa neema, inaitwa leo.
Kanuni zikiheshimiwa huleta mafanikio, zikivunjwa huleta kushindwa, uamuzi ni wako, kazi ya karama ya mwandishi ni kupokea toka kwa Roho Mtakatifu na kuandika kwa utiifu wote bila kupunguza, kazi ya msomaji ni kusoma, kuamini na kutendea kazi.
Mimi naanza kufanya jukumu langu.

Wote tunakubali tunaishi kwenye dunia inayokubari mabadiriko, dunia inabadirishwa na wachache, dunia yenye wengi wanaoshangaa na kuhadithia mafanikio ya wengine, wachache ndiyo wamiliki wa mali za dunia, wengi ni watumishi na wateja wa hawa wachache, nani kazaliwa na kitu, hapana; wao wamevipata wapi? Hapa hapa duniani, na sisi twaweza kuvipata wapi? Hapa hapa duniani
Nianze kusema wote tumeumbwa ili tuwe wamiliki
Jambo la kwanza alilolifanya Mungu alipomuumba Adamu ni kumpa umiliki, akamwambia "ukataware" kutawara ni umiliki, huwezi kutawara vitu ambavyo havipo chini yako, soma mwanzo 9:2 Baada ya wanadamu kukosea na Mungu kuwaangamiza kwa Ghalika, Mungu anafanya agano jipya na Nuhu na neno la kwanza ni kummilikisha vitu vyote duniani, Mungu amekupa umiliki, lakini ni kumiliki kwa niaba yake, Yeye bado atabaki Bwana yaani Adon kwa Kiebrania, yaani mmiliki kwa kiswahili, Yeye yupo juu ya vyote, ila amempa mwanadamu ataware kwa niaba yake
Swali kwanini humiliki, kwanini umekuwa mteja na mfanyakazi wa hili kundi dogo la mabepari,
Ipo kanuni ya kuondoka ulipo na kurudi namna ya Mungu alivyokuumba.

Wana wa Israel walifurahi kwenda Misri wakati nchi yao ilipokumbwa na njaa yaani Kanaani, Yusuph akawapokea, Mungu alikuwa ameshaagana na Ibrahimu kuwa atakipeleka kizazi chake Misri na kuwa watumwa kwa miaka 400 kisha atawaokoa na kuwarudisha kwenye nchi aliyomwahidi Ibrahimu.
Wana wa Israel moja ya vitu ambavyo hawawezi kusahau ni kuwa watumwa ndani ya Misri kwa mda wa zaidi ya miaka 400.

Mtumwa ni mtu ambaye hufanya kitu pasipo kutaka/ pasipo kuwa na matakwa yake. Mtumwa huenda asipotaka, hufanya kazi asiyotaka, hula chakula asichotaka, hulala mda asiyotaka, hupumzika mda asiyotaka, huishi maisha asiyotaka, hulala mahari asipotaka, huvaa nguo asizotaka; kuwa mtumwa ni heri ya kutozaliwa.

Wana wa Israel najua walifika wakati wakasema ni heri tusingezaliwa.
Mtu asiyekuwa katika kundi la wamiliki wa mali na uchumi wa dunia hii; yawezekana ukawa mmoja wa hao, atakula chakula asichokitaka, atavaa nguo asizozitaka, atafanya kazi mpaka mda asiyoutaka, atafanya kazi asiyoitaka, atalala mahari asipopataka, atanunua vitu asivyovitaka, atalala mahari asipopataka, ataishi maisha asiyoyataka, huu ni utumwa, wengine katika sayari hii wamekuwa ni mtumwa wa kiwango kidogo cha pesa walichonacho; "Pesa ndiyo jawabubla mambo yote"

Mara ngapi umeingia kwenye mtihani wa shule au chuo, umejiandaa kwa kusoma, kila kifaa unacho, peni, rula, na umevaa nguo za kupendeza: unaingia ndani ya chumba cha mtihani, unakaa vizuri kwenye kiti, unafunua karatasi ya mtihani, na kukuta kichwani una asilimia 30 ya yale yaliyoulizwa, kati ya maswali 20 unayajua maswali saba tu, ina maana asilimia 70 ya mtihani hujui. Wewe unadhani majibu hayapo ya maswali hayo, ukitaka kujua majibu yapo, tazama wa kulia kwako utamuona anajibu mtihani kwa tabasamu akionesha kuyajua yote;
"si kwamba pesa kama haijibu mambo yote unayoyahitaji kwamba imepoteza uwezo wake wa kujibu, ila ni kwamba unazo chache, umekusanya chache, umezipata chache.
Kushindwa kujibu maswali yote hakuna maana kichwa chako hakina uwezo wa kujibu; ila hayo saba ndiyo ambayo uliyasoma na kuyaweka kichwani, kichwa hakiwezi kujibu zaidi ya uliyoyaweka ndani yake wakati unajisomea, ukilazimisha utakosa tu.
Ndivyo pesa ilivyo; siyo kwamba haiwezi kujibu mambo yote unayotaka; tatizo ni kwamba hizo ndizo ulizotafuta, hizo ndizo ulizopata, hizo ndizo ulizonazo.
Kama wenzio wananunua vitu vya gharama ya Laki tano, ndizo walizokusanya, wewe nguo ya 3000 ndiyo uliyokusanya, na huwezi zidi hapo. Kanuni ndani ya kitabu hiki zinataka kuondoka na utumwa huu wa na kuwa mmiliki na uwe na pesa zenye jawabu la mambo yote.
Mungu amenipa kanuni hizi ili tu utoke ulipo na uwe na kesho yenye furaha na ushuhuda.

Mbali na hapo kuna watu ni watumwa wa hari zao za maisha, waweza kuwa tajiri lakini ni mtumwa wa ndoa, furaha, amani na huishi unavyotaka kuishi, huoni faida ya pesa yako katika maisha yako ya kawaida. Kanuni hizi zitagusa huko pia.
Na mfululizo huu ni maalumu kwa kila mtu, kama ni tajiri, mjasiliamari, muwejezaji, na yeyote, kama unayo leo, kitabu hiki kitakupa mwanga wa kufanya zaidi; kama unaishi bado waweza kufanya zaidi, soma mfululizo huu ili tumshinde adui wa kufanya zaidi ambaye ni mafanikio yako uliyonayo.

PART ONE
sehemu hii hasa tutaangalia msingi wa somo letu, maana ya siku tatu (leo, jana na kesho), pia tutaangalia watu tofauti jinsi walivyotumia leo yao, na tutazama makundi muhimu, hasa wale ambao leo yao, imesababishwa na historia, matukio au sababu fulani kama kukisa elimu, yatima, mjane, kilema, n.k

SEHEHEMU YA KWANZA
MSINGI WA NENO

KANUNI: kanuni ni imani na sheria ambazo mtu huziamini na kuzisimamia na kuzifanya mwongozo wa maisha yake.
Kanuni ni za asiri si za kubuni, kanuni zimefanikiwa kufanya kazi kila mahari kwasababu ni za asiri. Mwanadamu ameumbiwa, kuzifata si hiyari ni lazima, kanuni hazina jaji, usipofata zinakuhukumu zenyewe, hapa hapa duniani.
Yesu alisema, Mimi sitowahukumu ila maneno yangu ndiyo  yatakayowahukumu"
Nimewahi kuwa na rafiki yangu miaka ya 2005 mpaka 2008, alikuwa ni mtu anayefanya vizuri sana toka tukiwa shule ya msingi, tulipofika sekondari alifanya vema toka kidato cha kwanza mpaka cha pili na alikuwa mbere yangu kimasomo, nilishangaa kidato cha tatu akaanza kuwa nyuma yangu, nilipochunguza alikuwa amejenga mahusiano ya kimapenzi na binti fulani ambaye kwa pale shule alikuwa ana historia ya kutembea na wavulana wengi, nikamfata na kujaribu kumshauri lakini alinijibu kuwa "acha ushamba dogo" nilipomng'ang'aniza akanijibu kwa kebehi "niache, kwani haya si maisha yangu" nikamuacha ila siku ile ile nakumbuka hata mama yangu nilimshirikisha kuwa "rafiki yangu unayemjua amebadirika na sijui kama atafauru".

Ilikuwa ni rahisi kujua kuwa hawezi kufauru kidato cha nne hata kama si nabii, kwanini alienda kinyume na kanuni. Kanuni haziitaji hakimu wala jaji, bali zenyewe ni za asiri, unapovunja zinakuvunja.
Mfano usinywe sumu, usizini, usilewe, usinywe sumu, usiwe mvivu, hizi ni moja ya sheria za asiri, unapovunja haihitaji hakimu, zinakuvunja hapo hapo.
Kumbuka Yesu kasema, ni heri msingesikia, lakini sasa mmesikia hukumu i juu yenu.
Unapovunja kanuni, unatupa ruhusa ya kujua mwisho wako wa majuto, unapojitoa na kufata kanuni, unatupa furaha ya kujua mwisho wako mzuri.
Msingi wa kitabu hiki si kukupa mawazo, ila nataka upate kanuni.
Sihofu umesoma vitabu vingapi na ukabaki kama ulivyo, mimi najali kuwa, kwa kusoma mfululizo huu hutabaki kama ulivyo.
Na kwa waliofanikiwa naamini utafanya vizuri zaidi maadamu bado unayo leo.

Tuanze na mdano wa Mpakwa mafuta wa Bwana Mungu, kuwatoa Israel toka utumwani Misri kwenda Kanaani.
Anatoka kutoka maisha ya anasa ndani ya ikulu ya Farao mpaka kuwa masihi wa Bwana. Na kuandika vitabu vitano muhimu kwenye Biblia, Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na KumbuKumbu la Torati.

KUTOKA14:13-14
"Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. 14. Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Maneno ya msingi ya kuyakumbuka kila unaposoma mfululizo wa somo hili ni:
• msiogope simameni tu
• mkaone wokovu
• Bwana atakaowafanyia
• Wamisri mliowaona leo
• hamtawaona Wamisri tena milele
• mtanyamaza kimya

Toka hapa tunapata maneno ya msingi;
Mafanikio hutokana na...
• uhusika wa Mungu (atawapigania)
• uhusika wetu (simameni)
• waleta utumwa (wamisri)
• utumwa (kutofanya unayopenda)
• mafanikio ni vita (atawapigania)
• kusonga mbere hata kama umetoka utumwani/umefanikiwa
• no retreat no surrender/ hakuna kurudi nyuma wala kunyosha mikono juu ya kushindwa.
• maisha yanahitaji kukubari kwa imani ya wengine juu yako na juu ya unachokifanya,. Musa ilimradhimu kuwashawishi kwa maneno ya imani wana wa Israel ili tu wakubali jambo analotaka kulifanya.
• Watu ndiyo wa muhimu sana katika jambo lolote unalotaka kulifanya. Ishi na watu vizuri, sema nao vema, chukuliana nao vizuri, ishi nao kwa hekima, uhakikishe unapata wengi wa kukuunga mkono,
 “ni ngumu kukupenda wote, ila tu unawahitaji watu sahihi”.
• muache Mungu afanye sehemu yake, na usingoje afanye sehemu yako.
• usimuingilie Mungu sehemu yake na usingoje aingilie sehemu yako.
• Mungu akisema 'nenda' wewe nenda.
• ukianza safari usifikiri kurudi nyuma/ ukiaga kwenu usirudi.

Pia tunajifunza namna ya kutumia tatizo na kulifanya kuwa baraka na siyo tatizo;
Huwa napenda kuwaambia INAWEZEKANA... watu walipita kwenye sehemu ya mkwamo wa kusonga mbere kufanya jambo ambalo kwa mda huo li juu ya uwezo wao (impossible).
Rafiki yangu wa karibu nikiwa mtoto Mama mmoja, siwezi kumsahau, mume wake alipomuacha, na kumuachia mtoto mchanga na kwenda kuowa msichana mwingine, mda mwingi nilimuona na tabasamu na mwenye maneno ya kufariji na si mwenye uhitaji wa faraja, ukienda kumfarini utaishia kufarijiwa wewe, alikuwa ni mtu aliyeumba kichwa chake kuwa tayari kujifariji na kukabiri haiwezekani kuwa inawezekana, sasa yupo Kenya ana maisha mazuri.

Tunajifunza nini toka kwa Musa aliibadiri "haiwezekani kuwa inawezekana” ndani ya fikra yake na ya team yake yaani wana wa Israel, na imani iliyochipuka ikaungana na nguvu za Mungu na bahari ikagawanyika.

“Imani ndiyo njia pekee ya kutuunganisha na nguvu za Mungu”

1. Tambua tatizo mpaka hapo ulipo: Wamisri

2. Tambua kikwazo cha kufika unapotaka kufika: Bahari

3. Weka akiri zaidi kupata uhitaji, na uache kupoteza akiri kwenye tatizo, bali nini unataka; Musa alifikiri kuvuka ng'ambo si kurudi Misri.

4. Badiri fikra: ondoa hofu weka ujasiri

5. Tambua fikra za team yako na kuzishughulika: woga

6. Peleka akiri pa kupata usaidizi: Mungu

7. Tambua ushiriki wako, katika kuliondoa tatizo, ushiriki wa Mungu na wa timu yako: piga fimbo

8. Yakusanye matatizo yote na uyajue yote : Wamisri, Bahari, hofu yake na ya Waisrael, jangwa, hawana msaada.

9. Yatenge kwa utofauti wake na uyatatue kwa upekee wake: akaanza na Wana wa Israel kisha akaja Wamisri, akamalizia bahari, wakavuka.

10. Tengeneza mpango na mbinu nzuri ya kuyamaliza: Mungu akamtoa malaika aliyekuwa mbere yao na kumuweka nyuma, akaweza kiza kati ya Wamisri na mwanga kwa Israel ili kuwatenganisha.

11. Tembea katika imani huku ukimtazama Mungu; Musa alimwita Mungu na si mtu wa karibu, si Haruni wala Miriam, wala hakuanza kulia na kumueleza kila mtu.

12. Matatizo yasikufanye ukapunguza juhudi yako ya kusonga mbere: Musa hakupunguza munkari wa kwenda Kanaani, akaamnini Mungu atafanya lolote, saa yeyote.

13. Amini Fulsa, na jawabu inaweza kutokea saa yeyote na kwa namna yeyote: hawakufikiri kupasuka kwa bahari

14. Amini unaweza songa mbere zaidi: waliposikia wakapata moyo na nia, bahari ilipopasuka wakasonga mbere zaidi

15. Amini Mungu anaweza tokea mda wowote na kwa namna yeyote.

Alifanya kwa namna isiyoweza kufikilika kama angefanya vile, unaweza waza angeleta mtu alete maboti, au meri, au awauwe wa Wamisri kwa moto, hapana akawafanyia wasichofikiri.
Leo atafanya kwako. Kwa Jina la Yesu Kristo.

16. Weka suruhisho na siyo kukazana na ukubwa wa tatizo: Mungu alinishangaza hakuanza kuwakazia macho Wamisri, bali alikazia macho wao kusonga mbere, alikazia macho nini kinahitajika, na nini kifanyike wasonge mbele, hakutazama Wamisri.
Mungu akawapasulia njia, ndipo akawauwa Wamisri, kwa haraka utafikiri kwanini asingewauwa Wamisri, lakini alijua sasa akiwauwa, “enhee kwa wingi wao, wangepita wapi.
Leo hii Wamisri wanafananisha na utumwa wa pesa waliyokuwa nao wengi, na matatizo na changamoto nyingi ulizonazo.
Na kupasuka kuna maana ya usisimame ukaona umefika, bado hujammaliza adui, songa mbere, uhai wako, fulsa na nguvu ni kwamba bado unaweza songa mbere; shinda ugomvi wako na mafanikio uliyonayo ambayo yanakufanya usisonge mbere.

17: nini unahitaji kumaliza tatizo: Musa alihitaji fimbo ya kupiga maji yagawanyike. Na usiangalie mbali kwanza kupata kitu cha kumaliza tatizo, tazama kwanza nini unacho mkononi, nini unacho, kama ni kipawa, karama, au fedha kidogo, ndugu au rafiki wa karibu au watu sahihi. Tumia ulichonacho kwanza, na hivyo ulivyonavyo vitaleta unavyovihitaji kumaliza tatizo lako.
"Nyoka hatuanzi kummulika mbali, tunaanzia miguuni"

Tuendelee tena siku nyingine...
Karibu na ufurahie ufunuo wa siri za mbinguni kwa msaada wote wa Roho Mtakatifu.
Mungu awe nawe...

NAAMINI UMEBARIKIWA.
Bado tunaendelea
Fatana nami zaidi...

Saturday, October 17, 2015

BARAKA TANO ZA PETRO: JANA IMEKWISHA LEO NI SIKU MPYA, KESHO ITAKUWA NJEMA ZAIDI YA LEO.

BARAKA TANO ZA PETRO NA MAANA YA LEO, KESHO NA JANA.

UTANGULIZI
Jana Imekwisha, Leo ni Siku Mpya Kesho Yaweza kuwa Nzuri Zaidi ya Leo.
Huu ni mfulizo wa somo la muhimu sana kwa kila mtu, litakusaidia kutambua uko wapi na unaenda wapi, ni somo lililojaa kanuni za namna ya kuitumia leo yako kwa hekima na kuwa na Kesho nzuri. Somo litakupa kuelewa sehemu ya Mungu katika maisha yako na sehemu yako. Litaondoa maswali mengi kuhusu matumizi ya neema ya Mungu.
Mfululizo huu utamtazama Petro kwa kina: tabia zake, mitazamo yake, ucheshi wake, udhaifu na uimara wake na kutazama namna yote hayo alivyoweza kuyatumia hata kumfanya Yesu kwa neema akampa Baraka Tano na zote zikatimia. Na kutazama namna zinavyohusiana na maisha yetu ya leo na kujenga kesho yetu njema.

Nimetumia miaka mitatu sasa kuandaa somo hili. Na nitakayosema na wewe humu ni rasha rasha tu ya somo lenyewe ambalo lipo jikoni likioikwa zaidi kama kitabu.
Kwa msaada wa Roho mtakatifu mafunuo haya ya muhimu yameandikwa na kupewa uvuvio wa hari ya juu kubadiri maisha yako.
Fatana nami.

Tuanzie hapa, Safari ya kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine kwa kutumia gari la abiria ni wakati mzuri sana. Ni fanani ya safari maisha, MAISHA YANAENDA KASI SANA, hata kuzidi uwezo wetu wa kuyamudu".
Jinsi gari linavyoenda mbere ndivyo barabara, nyasi za pembezoni mwa barabara na vyote vya nje ya gari utaona vikirudi nyuma, jinsi gari linavyoongeza kasi ndivyo vitu pia vinaongeza kasi ya kurudi nyuma. Pekee huwa napenda kutazama uzuri wa tendo hili, maana jinsi unavyosonga mbere ndivyo unavyokutana na nyasi zingine, miji mingine, barabara nyingine, na wote wanarudi nyuma kwa kasi. Nikiwa mtoto nilifikiri kuwa ni kweri vinarudi nyuma, ila shule na ukubwa ukachangia kujua kuwa kwenda mbele kwa gari ndiko husababisha vionekane kurudi nyuma, ila vyenyewe huwa tunaviacha palepale.

Maisha ni safari, maisha ni safari, maisha ni safari, huu ndiyo msemo niliousikia tangu miaka yangu ya utambuzi wa mema na mabaya. Leo naandika kitabu hiki nikiwa na ufahamu napata nguvu ya kuhoji na kuandika, kama maisha ni safari basi kuna gari la abiria tumepanda, na kama lipo basi lazima litakuwa na lina jina, na kama lipo kweri basi kuna barabara, kuna nyasi tunazoziacha nyuma kila siku, kuna miji na vijiji tunaviacha nyuma, kuna vituo tunaviacha nyuma, kuna watu wanashuka njiani nasi tunaendelea mbere, tunafika pia tunashuka wengine wanaendelea, kuna wakati tunafika hata mwisho wa safari.

Kama ni kweri; maisha ni safari, mda ndiyo kipimo cha safari yetu, kila mtu ana mda amewekewa kuishi, na kikomo cha mda wake ndiyo mwisho wa safari yake inayoitwa maisha, wapi tunaenda, tunaelekea kwenye mafanikio na kushindwa, tunaelekea kwenye furaha au huzuni, tunaelekea kwenye utajiri au umasikini, tunaelekea kwenye kuleta mabadiriko au kukubari mabadiriko, tunaelekea kwenye kuwa mfanyakazi au kuwa muajiri, tunaelekea kuwa muwekezaji au mteja, tunaelekea kuwa mtumwa au mtu huru, tunaelekea kufa unafahamika au hufaamiki, tunaeleka mbinguni au jehanamu.
Basi tulilopanda linaitwa ulimwengu;  ni tofauti na nchi au dunia, hivi ni sayari, lakini ulimwengu ni hari ya uathiri (influence), ni hari ya kitWu, mtu/watu kuwa na nguvu ya kufanya wengine kufanya kitu fulani kwa kupenda au kutopenda,
Hivyo tupo kwenye basi la kila mtu akitafuta nguvu ya kuwa na uwezo wa kuwafanya wengine wafanye anachotaka, ulimwengu umpe anachotaka, apate anachotaka, aishi anavyotaka, aende anapotaka, ale na kuvaa anavyotaka. Ukitazama kwa makini; utaona ni wachache ndani ya gari hili ulimwengu wamefanikiwa kufikia hapo, tunawaita matajiri/mabepari/wawekezaji/wajasiriamari, ila kundi kubwa; mabilioni na mabilioni ya watu bado wapo hawajafanikiwa; bado hawajafanikiwa kupata nguvu hizo, za kufanya unachotaka, kwenda unapotaka, kuwekeza unapotaka, kula unavyotaka, kusoma na kusomesha unapotaka, kufanya starehe unayotaka n.k.

Kumbuka hii ni sehemu ya kwanza wiki ijayo tunaendelea...

"Maisha yanaenda kasi, zaidi hata ya uwezo wetu wa kuyamudu"

Kama gari ni ulimwengu, nyasi, na vingine ambavyo huwa tunaviona vikipita na kurudi nyuma kwa kasi ni nini?. Shetani na dunia haijawahi kuwa na jipya, siku zote ni yale yale, dhambi iliyomwangusha huyu, kesho inamwangusha yule, baada ya miaka kadhaa inamwangusha mwingine, jaribu na changamoto iliyomkumba huyu ndiyo hiyo kesho humkumba yule; nimekuwa mshauri wa watu wa rika tofauti kwa miaka kadhaa sasa, sijawahi sikia tatizo ambalo ni jipya, yote yanafanana, tofauti ni mtu na aina ya watu waliyopatwa basi. Nyasi na miji tunaipita huwa havitembei viko pale pale, gari la mbere na gari la nyuma watazikuta palepale na kuzipita, ukipita jana, leo na kesho utazikuta pale pale, hata zikikatwa, miji na vijiji vitabaki, katika safari hii kila mtu atapitia changamoto, majaribu, vikwazo, na makosa kadhaa. Na yote huwa yanafanana.
Cha ajabu, kwanini watu wanashindwa, yaani aliloshindwa huyu kesho yule naye anashindwa; watu hawataki taarifa na kujifunza.

Mfululizo wa somo hili la BARAKA TANO ZA PETRO ni kukusaidia kujua kanuni za kuwa salama katika safari, kujua kuitumia leo yako vema na namna ya kuandaa na kutumaini kesho yako, na pia kukusaidia kufika salama mahari unapotaka ufike katika safari ya maisha uliyoianza, na  kuwa moja ya kundi dogo lenye nguvu ya kuongoza na kuathiri ulimwengu uende wanapotaka, kufanya zaidi, kushinda adui yako mkubwa ambaye ni mafanikio yako ya sasa, kuishi maisha ya mafanikio na amani ya furaha, kuondokana na utumwa wa pesa.
Daniel aliishi nchi ya utumwa lakini aliifanya Babel iende yeye anakokutaka, akainuliwa na kuwa sehemu ya juu ya maliwali wote wa Babeli na juu ya Uliwali wote wa Babeli. Leo ni zamu yako, tumechoka kuishi kama watumwa katika nchi zetu wenyewe. Tumechoka kuishia katikati ya mafanikio yetu wakati Mungu ametuumba kufanya zaidi ya tuliyofanya.

PETRO MWANAFUNZI WA KIPEKEE
Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi, muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.
Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvu samaki na si kukaa na familia.
2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.
3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.
4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumwomo Kristo japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.
5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanasungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapi hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuw hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa. Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.
6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20
7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 12. Siku zote alitazama maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari.
8. Petro aliwaza chanya siku ziku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwa ona, akaamini akaenda, alipoambiwa wokovu kwa mataifa, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ni ya jana, sasa si wakati uliyopita.
9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.
10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.
11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa sa leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15


SEHEMU YA TATU
MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, Mr. Maneno akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana, akanitazama "unajua nilikuwa na akiri sana zaidi hata yako dogo", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Mr Maneno hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.

Monday, March 3, 2014

WAMNGOJAO BWANA TUTAPAA KAMA TAI (Isaya 40:26-31)


Isaya 40:25-31(31)
Tai ni ndege wa tofauti na ndege wengine kabisa.

SIFA ZA TAI
1.      tai anatembea na tai wenzie
na sio ndege wengine yeyote; sio mwewe wala kunguru
Ø  watu wapenda mafanikio wanatembea na wapenda mafanikio
Ø  watakatifu na watakatifu.
2.      tai anapaa umbari mrefu zaidi ya ndege wengine.
Ø  Mungu ni lazima atupe nguvu za kufanikiwa zaidi ya wengine
Ø  Mafanikio kazini zaidi ya wengine
Ø  Biashara mafanikio na wateja wengi zaidi
Ø  Tenda nyingi zaidi
Ø  Max nyingi zaidi kwa wanafunzi
3.      Tai anatazama umbari mrefu zaidi (kilometa 5 mbere)
na akikiona kitoweo au kitu hukivuta na kuonekana karibu na kukifata mpaka akipate, hata kama vikitokea vizuizi huwa hajari na hupambana mpaka akipate.
Ø  Hata majaribu yajapo 2014 hatutojari bali tunatazama ahadi za Jehova mpaka tutakapozifikia
Ø  Hata kama wakitokea watu kupinga, kazi au mume lakini tunatazama ahadi za Bwana mpaka tuzipate
Ø  Majaribu yajapo tunafumba macho na kuzivuta ahadi za Bwana na kuzitazama hizo tu.
Ø  Lolote na hilo (piga uwa) kupaa kama tai lazima.
4.      Tai hali mizoga bali anakula chakula halisi (kipaya/flesh)
Ø  Tunatafuta taarifa mpya na sio za zamani.
Ø  Hatutotumia vitu vya kale; kuazima au kupewa bali 2014 ni mwaka mpya na mafanikio mapya.
Ø  Sisi sio watu wa kazi za kale
Ø  Sisi sio watu wa asiri tena; ugonjwa na mikosi ya babu ni ya babu sisi tunaanza upya.
5.      Tai anatumia kimbunga au upepo mkali kupumzisha mbawa na kupaa juu zaidi.(upepo mkali unaoambatana na radi, mvua, na ngulumo kali).
Wakati ndege wengine wanajificha kwenye miti na vichaka kuogopa
Ø  Wakati wengine wanalalamika matatizo na shida wewe unatumia majaribu na shida hizo kupaa zaidi angani.
Ø  Tumngojeao Bwana tunatumia dhiki, uchi na adha kupaa juu zaidi kimafanikio.
6.      Tai wanapotaka kukutana (kujenga ndoa).
·         Mwanaume humfata mwanamke juu, mwanamke agunduapo hushuka chini na kuchukua gome au ganda la mti na kupaa nalo juu.
·         Akifika juu analiachia lianguke chini; mwanaume analiata kwa kasi, na jinsi linavyoongeza kasi naye anaongeza kasi; akilipata anarudi nalo juu na kumpa mwanamke.
·         Mwanamke anapaa tena juu zaidi na kuliachia tena; na mwanaume kulifata kama mwanzo na kulirudisha kwa mwanamke
·         Na mwanamke hupaa tena juu
·         Kitendo hiko hufanyika zaidi ya saa moja
·         Mpaka pale mwanamke atakapoona umbari wa kwenda juu unatosha na baada ya kuona mwanaume amefauru mchezo ndipo anakubari.
Ø  Kabla mtu hujakubari urafiki au ukaribu naye mpime kwanza
Ø  Sisi ni wa thamani (tumngojeao Bwana)
Ø  Sisi sio watu wa kawaida
Ø  Sio watu wa chipsi na keki au soda
Ø  Hatupatikani kirahisi
Ø  Ni bidhaa hadimu
Ø  Thamani yetu ni kubwa makazini; wanatuhitaji na wakibaki wao tu mambo yote yanaharibika.
Ø  Dunia yatuhitaji; ndio maana tukiondoka tu na dunia ndio mwisho wa mchezo wake.
Ø  2014 ni kutafutwa kama lulu
7.      Wanashirikiana kwenye uzazi
·         Tai jike anapotaka kuzaa; jike na dume wanashirikiana kutafuta eneo la juu la ncha ya mlima ambapo mnyama na adui hawezi kufika.
·         Mwanaume anaenda kutafuta miba na kuweka sehemu hiyo na kushuka tena chini kuleta magome ya mti kujenga kiota juu ya ile miba
·         Na kushuka tena chini na kuchukua miba na kuweka juu ya yale magome; anashuka tena na kuchukua nyasi na kufunika ile miba
·         Kisha anashuka tena na kuchukua ngozi kufunika zile nyasi
·         Baada ya kumaliza kujenga kibanda anarudi tena chini kuchukua miba mingi zaidi na kufunika kile kiota; kuzuia maadui.
Ø  Mwanaume na wanawake lazima tushirikiane katika kujenga familia; familia tujenge pamoja.
Ø  Kanisa lazima tubebane: muujiza wa mtu upo mikononi mwetu
Ø  Nyumba zetu, familia zetu, maisha yetu ni lazima yalindwe na Damu ya Yesu.
Ø  Wako makini kufanya mambo yao nasi lazima tufanye mambo kwa umakini.
Ø  Baba anafanya jukumu kama kichwa na mama anakaa pembeni na kutia moyo
8.      Wakati wa kufundisha watoto.
·         Mama yao anawatoa kwenye kiota sababu ya uwoga wanarudi tena
·         Hivyo mama yao anatoa ngozi na kubakiza miba- hivyo wanaporudi tena ndani wanakutana na miba wanachomwa na kutokwa na damu
·         Wanashangaa baba na mama yao aliyewapenda sana leo amewageuka na kuwaumiza.
·         Na baadae mama yao anawasukuma pembeni ya ncha ya mlima na kuanza kuruka kwa hofu.
·         Kabla hawajaanguka chini baba yao anatokea na kuwabeba wasianguke na kuwarudisha mlimani
·         Kitendo hiko kinaendelea mpaka wahakikishe wote wanajua kuruka sawa sawa.
Ø  Wanapopatwa na mshangao wa mateso hayo- hapo hapo wanapata maarifa na mbinu mpya za kimaisha na kuishi
Ø  Mungu anakuwekea miba (shida, dhika, uchi na adha na mateso na majaribu) kwa mema; ili upate mafunzo na kukufanya uwe bora zaidi ya sasa.
Ø  Wakati mwingine anafanya kama amekuacha kumbe yupo pembeni akikutazama na kabla hujaanguka anakuja kukubeba
Ø  Tumngojao Bwana mwaka huu ni lazima tubebwe na Jehova katika Jina la YESU.
Ø  Na atakujaribu kwa kila hatua mpaka ufuzu mafunzo yote na kuitwa mkakamavu: ukifuzu level moja anakupeleka level nyingine mpaka uwe umekomaa ndipo anakuacha.
Ø  Tunapaswa kujifunza kutoka kwenye matatizo na sio kuraumu
Ø  Kawaida watu wanaopata mateso, magumu na matatizo magumu na mengi ndio ambao wanatoka na maarifa, hekima na uzoefu zaidi. MFANO DAUDI NA SULEMANI
9.      Tai anaishi miaka mingi zaidi
·         Anaishi miaka 70
·         Lakini kufika miaka hii, anapaswa kufanya uamuzi mgumu katika maisha yake.
·         Akifika miaka 40;
o   Mdomo wake unachoka/unazeeka na kushindwa tena kuchukua mawindo(ukari na uregu wa mdomo unapinda)
o   Kutokana na uzee na uzito wa mabawa, manyoya yanarundikana kifuani na kumfanya kushindwa kuruka.
·         Anabakiwa na maamuzi mawili tu
o   Kufa
o   Au kupitia mateso na maumivu ya siku 150 (miezi 5)
·         Kitendo hiko kitamtaka tai apande juu ya ncha ya mlima kwenye kiota chake na kujipiga kwenye mawe mpaka ncha ya mdomo wake ivunjike yote.
·         Na kukaa akisubiri mpaka ncha ya mdomo iote yote.
·         Baada ya hapo analazimika kutoa manyoya yake yote ya uzeeni mpka abaki pasipo hata na nyoya
·         Baada ya miezi 5 anapata manyoya mapya na kuishi tena miaka 30.
Ø  Anaonesha kwamba wamngojeao Bwana kumbe kumbe tuchakaapo kuna kuzaliwa upya na kufanya upya tena na kuishi miaka mingine zaidi tukiwa na nguvu mpya.
Ø  Ni lazima tukubari kubadirika hata kama mengine yanaumiza; kwenye ufalme wa Mungu
Ø  Kujitoa kwenye matatizo ya kale ni lazima tukubari kupoteza faida za sasa (vya thamani vya sasa) kwaajiri ya baadae
Ø  Tunapaswa kutoa mambo yote ambayo hayana umuhimu kwetu kwa sasa ili kufanyika upya; kwaajiri ya kesho yetu
Ø  Lazima tukubari mateso, majaribu na shida kwaajiri ya baadae
Ø  Wakati fulani twapaswa kutoa tamaduni zetu, tabia, na mazoea fulani ili kuweka tabia na ufahamu mpya
Ø  2014 Bwana anakwenda kurenew maisha yetu na kutupa mapya yenye raha zaidi.
Ø  Maombolezo 3:22
Ø  Ayubu 17:9


THANKS ALMIGHTY GOD, Please my Dear God go and teach your people yourself; but I give all my body to use me as a tools, For Your Glory. In Jesus Name... Amen