Monday, February 29, 2016

Part 4: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO....

~ MAANDARIZI 15 KABLA YA KUSEMA NDIYO..."

Karibu sehemu ya nne ya somo letu...
Soma kila swali kwa umakini, kumbuka kujibu ndani ya moyo wako ukiwa peke yako.

Nianze kwa kusema: pindi unaposema ndiyo, kuna vitu vitabadirika kwenye maisha yako.

A. Ndiyo! yako hukuradhimu kubadiri tabia.
     Ili kuendana na furaha ya huyo umwambiaye ndiyo, kumbuka uwe tayari kuwa yeye anavyotaka. Na hivyo kuna vitu unafanya itakuradhimu vibadirike hata kama ulivipenda.

B. Kupungua kwa uhuru
     Kumbuka hutotakiwa kuendelea kuwa na uhuru kama uliokuwa nao, itakuradhimu umpe mwenzi wako sehemu ya uhuru.

C. Misimamo inabadirika
     Kumbuka unayekutana naye ana misimamo, na ili mfurahi lazima uwe tayari kubadiri baadhi ya misimamo yako.
E. Marafiki wanabadirika
F. Matumizi ya simu yanabadirika
G. Mda wa kulala unabadirika

Neno "Nimekubali..." Ambalo mara nyingi hutamkwa na wanawake, ni dogo sana ila ndiyo chanzo cha mabadiriko ya maisha ya wengi. Na hii ndiyo siri, ni wale tu ambao wako tayari kuendana na mabadiriko yanayotokana na neno nimekubali hufaidi furaha ya Ndiyo yao.

"Wale tu ambao wako tayari kukubaliana na mabadiriko yatokanayo na Ndiyo yao, ndiyo hupata furaha ya mahusiano yao"

Tuanze sasa, leo tutajadiri maswali kadhaa na Part ijayo tutamalizia maswali mengine. Kumbuka ni maswali 15.

Sw 1. Je Unaweza Kuzikabiri Hisia Zako?

Mtu yeyote hata kama mlikuwa marafiki kaka na dada hapo mwanzo, mnapoingia kwenye uhusiano mvutano wa miili yenu unaumbika na hivyo kuwaletea hisia tofauti na hapo mwanzo.
Hivyo kabla ya kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi, ili kujizuia kutenda dhambi ya uasherati, lazima kwanza ujiulize kama una uwezo wa kukabiri macho yako na nguvu ya mwili wako kwa binti. Huna uwezo wa kukemea tamaa iondoke, bali una uwezo wa kuzuia kuyachokoza mapenzi.
Wengi husimama wakiwa single na hupotea pale wanapoanza mahusiano.

"Kabla ya kusema ndiyo, jiulize je una uwezo wa kutunza heshima yako mpaka Ndoa"

Turudi kwenye stori yetu kuhusu Angel: siku moja nikitoka kupata ibada yenye nguvu ya Casfeta- chuo kikuu cha UDSM, nakumbuka dada mmoja aliniambia "Ulenje sikuoni siku hizi kwenye ulimwengu wa roho". Nilishangaa lakini nikakumbuka Mungu amewahi kunionesha namna ninavyojiweka mbali naye. Usisahau wakati huo nilikuwa nahubiri madhabahu za ndani na majukwaani, naombea na watu wanapona.
Nakumbuka siku moja nikihubiri kanisa fulani, Mungu alijitukuza wakati wa maombezi, mpaka watu walianza kuitana mitaani na kuja kuombewa. Lakini nikirudi nyumbani Mungu ananionesha niko mbali naye.
Sikuwahi anzisha uhusiano na Angel, siku nilipogundua "bado sina uwezo,
Basi nilisubiri, mpaka namaliza chuo nikaendelea kusubiri, haikuwa dhambi, sikutaka kuwa mbali na Mungu"

Jifunze jambo hapo, ni kwa namna gani mpenzi wako anakuweka mbali na Mungu, kwa njia ya simu yako, au mnapokutana.
Kabla hujasema ndiyo kwa huyo umpendaye, Je una uwezo wa kuongoza hisia zako, na kuishi pasipo kumkosea Mungu. Najua baadhi watapinga, lakini wanaopenda roho zao, na kuwa tayari kukana nafsi zao kwaajili ya Bwana basi watapokea na kufanyia kazi ujumbe huu.

Sw 2. Je Unajua Unaenda Kufanya Nini?

Nilimuuliza binti fulani swali kama hilo, akajibu nitafua, nitaosha vyombo, na kumpikia chakula kizuri kila siku.

"Watu wawili hawawezi kwenda pamoja, kama wasipopatana"

Sina mengi ya kusema katika hili, soma mwanzo 2:20 Biblia inasema "lakini hakuona wa kufanana naye"

Hivyo Mungu uheshimu wa kufanana naye, japo Mungu alizungumzia wasichana wote, maana hakutoa ulinganifu wa msichana na msichana, bali ni msichana na wanyama, na kuona kiumbe msichana ndiye anafaa; ila alionesha jambo la msingi "kuwa anaheshimu sana mfanano"

Kila msichana ni mzuri, ila ni vema wa kufanana na wewe.

Swali letu ni "Je unajua unaenda kufanya nini?. Ni swali dogo, ila kufanana siyo shida, shida huyo unayefanana naye anajua anaenda kufanya nini mtakapokuwa pamoja"

Unashangaa, unapokaa chini na wachumba au wanandoa, na kuwaeleza tatizo ni "mnafanana ila hamfanyi mnayopaswa kufanya" wanacheka, na wengi husema "kwanini mtumishi: sikujua hayo hapo mwanzo?, mwingine aliniambia "tatizo ni kutokujua mtumishi"

"Kanuni ni ndogo, ukijua na kufanya unachopaswa kufanya uhusiano utaenda, usipojua cha kufanya na Ukafanya usichotakiwa kufanya uhusiano hautaenda"
Ev. Ulenje

Nakusihi katika Jina lake Bwana Yesu, tumia mda kusikiliza mafundisho ya watumishi wanaoaminika, soma neno la Mungu, Biblia imejaa stori za kila aina ya ndoa, soma vitabu vya waandishi wa kiroho wanaoaminika, sikiliza watumishi.
Kubwa kabisa muombe Bwana akufundishe njia zake. Na utambua nini unahitajika kufanya wakati wa ndoa, kisha kuwa na amani ya kusema ndiyo, achana na mambo ya umri na miemuko ya mwili, Mungu anatazama uwezo wa ndani na Ndoa pia inategemea sana uwezo wako wa ndani, si miemuko
Ya mwili wako, au umri wako.

"Mungu huwaepusha baadhi ya wasichana kukutana na waume zao, kwasababu ya kuwaepusha wanaume hao na maumivu" Dr Myles Munroe

Kuolewa si umri, umaarufu, karama, huduma au msisimko wa mwili ni uwezo wa ndani.

Fikiria hili, hata kwa wanaume pia.

SW 3. Je Unajua Kutambua

1 Wakorintho 13:9-12
Soma kwa makini mstari huo, ila naomba niandike sehemu muhimu.
Biblia inasema "Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;....nilipokuwa mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga...wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu, wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana"

Hakuna siri kubwa katika kuwa na ndoa nzuri kama "kuwa na uwezo wa kufahamu yaliyojificha nyuma ya neno "nakupenda" unalolisikia.

Natamani kuishia hapa; ila ngoja niendelee: wengi wanalia kwenye mahusiano si kwamba hawakuambiwa "nakupenda" na wapenzi wao, bali walishindwa kutambua nini kipo nyuma ya neno "nakupenda" walilolisikia.

Watu wawili wanasema "nakupenda" je una uwezo wa kutambua "nakupenda ipi ni ya kweli na imetoka kwa Mungu" na ipi ni ya kibinaadamu.

Mwanaume una uwezo wa kufahamu "ndiyo" unayoipokea na nini kipo nyuma yake: je ni Mungu au shetani, je ni hatima nzuri au mbaya. Na kwa wasichana pia, je unatambua nyuma ya hiyo nakupenda; je ni Mungu, Shetani, Hatima nzuri au mbaya.

Kama huna uwezo huo, basi ni bora ukaacha kujenga nyumba, Yesu anasema usije ukajenga msingi, ukashindwa kumalizia na wenzio wakakucheka. Ni bora ukaomba poooo....mapema kabla ya huyo mwanaume au mwanamke hajaja.

Ninayo mengi ya kusema katika hili, ila Roho mtakatifu akufundishe zaidi. Wengi wanalia. Wamejikuta wameng'ang'ania sehemu ambayo wenye uwezo wa kutambua walimwambia hapana, yeye akalazimisha "ndiyo" sasa analia.

Je una uwezo wa kutambua..."nakupenda unayoisikia" au "Ndiyo" unayoisikia. Maana tunafahamu kwa sehemu, na wakati wa utoto tunafahamu kama watoto, kama bado una babaika kujibu "je ni Mungu au ni hisia zangu" ni heri ukaomba poooooo!!!! Mapema, na "ukajifunza kuongeza uwezo wako wa KiMungu wa ndani" wa Utambuzi wa utu uzima"

Nitaendelea maandalizi ya nne siku tati Zijazo....
Usikose....

Kwa msaada wa Roho Mtakatifu somo limeandikwa na
Ulenje Mwaipungu

Sunday, February 21, 2016

Part 3: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MISINGI IKIHARIBIKA...

Tuchokoze jambo hili la msingi kisha Part 4 tuanze kujadiri "mambo ya msingi ya kufanya maandarizi" kabla ya kusema Ndiyo!

"Huwezi chora ramani ya nyumba, baada ya kujenga msingi

Zaburi 11:3
Mfalme Daudi yeye anauliza
        "Kama misingi ikiharibika,
          Mwenye haki atafanya nini?

Huwezi jenga ghorofa la ngazi 30 kwa kujenga msingi wenye uwezo wa kubeba ghorofa la ngazi tano. Utachekwa tu.

Daudi anasema "mwenye haki atafanya nini" hajasema mwenye dhambi.

Si peke yako, hata wengi hujiuliza "nafunga sana, namtumikia Mungu kwa moyo wote, natoa zaka na dhabihu, ni mchungaji, ni askofu, ni mshirika mwaminifu sana, nampenda mke wangu, ni mwaminifu wa ndoa yangu, ila mbona ndoa yangu inasumbua?

Daudi anasema mwenye haki atafanya nini? Unafanya yote yanayokufanya uwe mwenye haki, ila ndoa haijakaa vema. Haleluya, nasema haleluya!. Hapa lazima kuna jambo la ziada la ambalo Daudi analifahamu.

Maandarizi kabla ya kusema ndiyo, maandarizi kabla ya kuingia kwenye ndoa, ni wakati wa muhimu sana kuliko hata ndoa yenyewe.

Maana msingi wa nyumba ni muhimu sana kuliko hata nyumba yenyewe.

Kuna wengine husema hayo mengine hujijua huko huko, kwani nani kazaliwa anajua, jibu ni fupi tu, unapotaka kujenga ghorofa la ngazi 30, na umeshajenga msingi wa ghorofa ya ngazi 10,  huwezi kubadirisha ramani wakati wa kujenga  ngazi ya 9, na kusema nataka ghorofa ya ngazi 30 na si ngazi 10. Wote watakushangaa, la sivyo itakulazimu ubomoe ngazi ulizojenga zote, kisha ubomoe msingi wote na ndipo uuweke msingi na upya kwa jinsi unavyotaka kubadiri, ambapo gharama yake ni kubwa sana kuliko hata ungekuwa makini mwakati wa kujenga msingi.

Huwezi kubadiri ramani ya nyumba  katikati ya ujenzi. Hivyo nathubutu kusema ni vema kutazama tunaujenga vipi msingi wa ndoa tunayotaka kuingia, hata kabla ya ndoa yenyewe.

KUMB:
        "Kama misingi ikiharibika,
           Mwenye haki atafanya nini

Usikose sehemu ya Nne, kumbuka ndiyo kiini cha somo. TUTAJADIRI maandarizi ya kufanya moja baada ya lingine.
Asante kwa kusoma.

Utukufu kwa Bwana Mungu na Mwanaye Yesu Kristo

Monday, February 15, 2016

Part 2. MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA "NDIYO..."

Nianzie hapa...

" huwezi kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Nazungumzia maandarizi kabla ya kusema "Ndiyo"

Yesu  anasema "maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumaliza?"

Na hii na ndiyo sababu ya ndoa nyingi kusumbua. Wengi tunaowa kwa miemko na kutazama umri, na si uwezo wetu wa ndani, na kutazama "kama una uwezo?" Ndoa si kuishi pamoja, kuna zaidi ya maana nyingi ya neno "kuishi pamoja".
Yesu analeta kesi mezani, anasema "Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, wakisema mtu huyu, alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza"

Siku hiyo niliishiwa nguvu, haikuwa na maana ya ugonjwa kuingia moyoni mwangu, "ilikuwa ni ishara ya kuwa sikuwa na nguvu za kujenga mnara unaitwa ndoa". Na haikuwa kesi ya umri, ilikuwa kesi ya uwezo wangu wa ndani wa kuwa na uhusiano wa uchumba. Kabla hujasema ndiyo, usiulize kama unampenda au kama anakupenda, ni swali dhaifu sana, usiulize umri wako ni swali dhaifu sana, kaa chumbank peke yako, jifanyie ukaguzi binafsi, ukiwa na Mungu wako, ikiwezekana muulize Mungu anayekujua zaidi, je una uwezo?. Kama huna kabla ya kusema "Ndiyo" chukua mda kuzingatia moyoni mwako, na ujenge uwezo kwanza. Alafu unajua nini cha ajabu, kuwa na uwezo haichukui mda, siku moja mpaka mbili kwa uwezo wa ndani, siku kadhaa kwa uwezo wa nje.
Twende pamoja...

Yesu ananifurahisha hapa anaposema "Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

Hii ni siri kubwa katika maisha "mazingira siku zote si rafiki" ndoa siku zote hutaka kuwapeleka ninyi chini, mgombane na mchukiane, dunia na matukio ya kimaisha siku zote si rafiki. Hivyo "kabla ya kusema Ndiyo, swali la msingi, je unaweza kupambana na mazingira ya ndoa na changamoto zake" usiogope, hakuna mtaaramu wa maisha, wote tunatembea kwenye neema ya Mungu, wote tuna matatizo yetu tusiyotaka kuyasema yote, ila swali, kwanini wengine wanapotea kwenye matatizo, ambayo wengine wanasimama? Tofauti ni ule uwezo wa ndani.

Wote wana changamoto fulani za ndoa, hata kama wana miaka 25-50 ya ndoa, wana vitu hawawezi kusema, ila katika hayo waliyopitia wakashinda, kuna wengine walianguka. Unaanza kunielewa, nini shida; Ni uwezo wa ndani ya mtu wa kukabiri changamoto na kuzishinda.

Yesu anamaliza kusema "na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali"

Waooo!!! Kama ukiona huwezi kumtii mwanaume kama vile unavyomtii Kristo na kumfanya awe kichwa kwako kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa, basi omba pooo! Mwanaume akali mbali"

 kama ukiona "huwezi kuvumilia makosa na udhaifu wa mwanamke/msichana, hata pale anapoweza kukuumiza sana kama vile Kristo anavyolivumilia kanisa, na kukubari kufa ili alisafishe, basi omba pooo mwanamke akali mbali" waoooo!!!! Incredible.

Kama huyawezi haya aliyoandika mtume Paulo waefeso 5:22-25
Omba pooooo mapema kabla ya mke au mume hajaja kwenye maisha yako.

Ngoja tumalize kabisa Yesu aliyosema kwenye hii luka 14.
"Basi kadharika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu". Kama haupo tayari kuacha aina ya maisha unayoishi, mitizamo yako na misimamo yako, marafiki zako wa kike na wakiume na mengine ambayo unayeanza naye uhusiano hataki, au yanaweza kusababisha kutoenderea na upendo wake kwako, basi omba pooo! Akali mbali, usiwe mke wake, au mume wake.

Yesu anamalizia "Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee?, haifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia. Na asikie. Waoooo! Ndoa ni kitu chema sana, ila kama kikiharibika itiwe nini hata ikolee, semina na semina zinafanyika, masomo na masomo yanaandikwa ila bado ndoa ni tatizo, kwanini? Hakuna maandarizi.

Swali "je unaweza kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Tuendelee kuchana nyavu, sehu ya tatu ipo njiani

Mungu alibariki neno lake.
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu Limeandikwa na Ev. Ulenje
0718721848.
imaf2b@gmail.com

Friday, February 12, 2016

MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA "NDIYO..." Part 1

PREPARATION BEFORE YOU SAY I DO

Mwaka 2013, nimewahi kumpenda msichana fulani jina naliweka nyuma ya pazia, ila namwita Angel. Maisha yangu ya kutumia mda mwingi kumtafuta Mungu na kutafakari matendo yake, yalinipa kuwa na maisha ya tofauti na mtazamo tofauti kuhusu wasichana na hata ndoa. Nilikuwa wazi hata kusema siamini katika ndoa, siamini kuwa naweza kupenda au hata kuowa. Nilivutiwa sana na maisha ya Mtume Paulo na hata sasa navutiwa sana na maisha yake, hivyo niliwaza nije kuisha pasipo kuowa kama yeye.

Hivyo niliishi namna hiyo mpaka nafika chuo mwaka wa tatu, bado sikuwa nikiamini kuhusu kuowa au kuhusu kupenda. Tabasamu la Angel likanifanya kubadiri muelekeo wa maisha yangu. Nikajikuta kubadiri hata laini ya simu toka tigo na kutumia Airtel sababu tu ya kupata mawasiliano yake. Kwakuwa sikujua kukabiri maisha yale mapya niliyoyaanza, ilichukua mda kumwambia Angel tuanze uhusiano unaoitwa uchumba.

Ili ilichukua miezi mingi sana kuvumilia ile hari, wapendwa kupenda huku ukiogopa kusema kwa unayempenda ni mateso, na kumchukia mtu unayeogopa kumwambia unamchukui ni kifo cha moyo unaoishi. Kila nilipomuona huyu Angel nilisahau hata kuwa niliwahi weka malengo ya kutoowa.
Siku moja uvumilivu ukanishinda, ilikuwa ni siku ya jumaapili. Uzuri Angel tulikuwa tukisali kwenye Fellowship moja ya Casfeta hapo chuoni. Siku hiyo nikaweka moyoni mwangu, kuwa lazima nimwambiye Angel, nini nawaza juu yake. Nikaamka kitandani na kuchukua simu yangu, na kutafuta jina lake, nini kilitokea...

Ninapobonyeza batani ya simu kubonyeza nitume sms, nikasikia sauti ikiniuliza swali gumu na jepesi sana, ambalo kupitia swali hilo ndipo tunapata somo la leo
Nikaulizwa "Are you capable?" Yaani "Je una uwezo?". Nguvu zikaniisha mwilini, nikakosa hata uwezo wa kusimama kwa miguu yangu, nikaanguka kitandani, ubongo ukasimama kuwaza, na hata leo simuwazi tena huyo msichana, upendo ule wa muemko ukaishia pale, hadithi ya maisha yangu ikaanza tena. Kuna jambo natamani kukufundisha hapo.
Mungu aliniuliza "Je una uwezo?". Lilikuwa ni swali la msingi sana. Nilitumia mda wa miezi mingi sana hata kuelewa kuwa kuna somo Mungu alitamani vijana na hata wanandoa waelewe.

"Kufunga ndoa pasipo maandarizi ya ndani (tabia, fikra, mitazamo na akiri) ndiyo mwanzo wa kuvunjika ndoa hata kabla haijafungwa