Wednesday, January 25, 2023

SOMO MAALUMU LA KUINULIWA NA MUNGU #04

 SOMO LA NNE

KUMKUMBUKA HULINDA AGANO LA KUINULIWA


Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo. Kumb 8:18 

Ndiyo! Utainuliwa lakini unahitaji zaidi ya kuinuliwa unahitaji kubaki katika kuinuliwa. Maana mara nyingi tumeshuhudia kwenye maisha yetu up and down sasa ukiendelea kupanda na kushuka hautafika popote. Bali ili ufike mbali ni lazima ukiwasha ndege yako kupaa ni moja kwa moja.

Neno la leo ni neno la kulihifadhi, sababu Mungu anaanza kukuinua kidogo kidogo sasa, hili neno litakusaidia kubaki kwenye sehemu ya kuinuliwa, kuzidishwa na kuongezwa daima.

KUMB 8:1_ Musa anawaambia Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo BWANA aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.

KANUNI #04 MUHIMU ILI KUBAKI KUINULIWA BILA KUSHUKA CHINI

#01. KUMBUKA MUNGU ALIPOKUTOA NA NAMNA ALIVYOKUINUA.

Mungu aliwapa amri  ya kumkumbuka ili wabaki kwenye kuongezwa, sababu alijua mwanadamu huwa anakumbuka akiwa hana, ila akipata anasahau; anasahau alipotoka, anasahau namna alivyofika alipo, na hasa anasahau aliyemuinua, hata akijitazama anaona ni kwa uwezo wake na ubora wake amefika pale.

KUMB 8:2, 12-14 ___Musa anawaambia Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa,

12 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;

13 na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau BWANA, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

Watu wengi wasipokuwa na kazi wanamtafuta Mungu, wakiwa hawana biashara, hawana mume, lakini wakipata basi wanatumia kazi, mume, biashara kama kisingizio kuwa hawawezi tena kuja kanisani kumtafuta Mungu. Wanasahau kuwa Mungu aliyewapa alijua kuwa huwezi firisika kama utampa muda. 

Hakuna mtu anaweza firisika kwa kumpa Mungu muda.


#02. MUNGU ANATUPELEKA JANGWANI KUTUFUNDISHA UNYENYEKEVU.

Shika hili Mungu anatuongozwa njia ya jangwani ili kutupeleka kwenye mafanikio, ili tujue kuwa Yeye ndiye mpaji wetu. Kuna watu jangwani wanafikiri ni wakati ambao hauna kitu cha kula wala kuvaa, hapana huyo siyo Mungu ni shetani kemea kwa Jina la YESU.

Mungu anatupeleka jangwani ili atuonyeshe kuwa yeye ni mpaji ___yaani anatuongoza sehemu ambayo tunakuwa hatuna uwezo wa kupata chakula wala mavazi kwa uwezo wetu alafu yeye anatupatia vyote hivyo na kuzidi bila hata juhudi zetu. Anafanya hivyo ili tujue kuwa yeye ndiye mpaji wetu.

KUMB 8:2, 3 Musa anawaambia Israel__

2 Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.

3 Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.

Israel walichukua miaka 40 kujifunza kuwa Mungu ni mpaji sababu walitaka sana kutumia nguvu zao. 

Kama utajifunza mwaka huu kuwa Mungu wako ndiye mpaji, na ya kuwa utakumbuka amri zake na kumkumbuka wakati wa kuongezeka, utakumbuka kuwa wakati upo jangwani ndiye alikulisha na halo ulipofika si kwa uwezo wako, basi atakuinua, Musa anasema alikujaribu ayajue ya moyoni mwako,

Kumbe kuna wakati Mungu anatupeleka sehemu ambapo tutakosa vitu, lakini atafanya tule tuvae ili ajue mioyo yetu kama itasema asante na kumtazama yeye peke yake bila kulalamika bali kuamini kuwa Yeye ndiye mpaji wetu. 


#03. TUNATAKIWA KUMKUMBUKA MUNGU SABABU YEYE NDIYE ATUPAYE NGUVU YA KUPATA UTAJIRI.

Nguvu ya kupata utajiri ni pamoja na ufahamu, nguvu, baraka, neema, kibali, na afya. Vyote hivi ni Mungu ndiye atupaye. Maana yake unatakiwa kumkumbuka sababu yeye ndiye atoaye hizo nguvu za kupata utajiri. 

KUMB 8:13, 14 __Musa anasema;

13 na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau BWANA, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

Musa anaongea kuhusu kutuongeza, kumbe kuna wakati Mungu ataanza kutuongeza. Neno linasema usimsahau BWANA Mungu wako. Kwanini, kwa sababu maongezeko huwa yanasababisha ulevi wa vitu, majigambo, na ubize __ mali ikiongezeka ina tabia ya kuchukua nafasi ya Mungu.

Kwanza lazima ujue Mungu hayupo kinyume na wewe kuwa tajiri ndiyo maana anatoa nguvu ya kupata utajiri, ila hataki mali ichukue sehemu yake; ndiyo maana anayemkumbuka wakati wa kuongezwa huwa anamuongeza zaidi.

Mungu sasa anakuongeza ndiyo maana ulichonacho leo hukuwa navyo jana, sasa kama utamkumbuka Mungu kwa maongezeko madogo basi atakuongeza sana na sana. 


#04. KUMKUMBUKA KUNAFANYA IMARA AGANO LA KUINULIWA.

KUMB 8:18 Musa Anaweka wazi __Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Anasema ili alifanye imara agano lake. Kumbe kumkumbuka ndiko kunaleta kufanywa imara agano la kuongezeka. 

Kuongezwa ndiko kunaleta kuinuka. Ana maanisha anakuongeza sawa, lakini usiridhike, mkumbuke hapo atafanya imara zaidi hilo agano lake la kukuongeza. Maana yake ndipo utaendelea kuongezeka na kuongezeka.

Galatia 3:9 __ Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

Baraka ya Ibrahimu ni kuongezwa na kuzidishwa, lakini utaona Ibrahimu alishika agano, na kwa kushika kwake agano aliinuka siku zote bila kushuka chini.

2 Kor 9:8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Kumbe Mungu huwa anatujaza neema ili tukiwa na riziki tuzidi kuteda mema. Maana yake Mungu anakuongeza kidogo kwanza ili apime moyo wako, bidii yako ya kumkumbuka na kumuweka mbele inakupa kukuongeza siku hata siku.


Ubarikiwe Sana, Fanyia kazi haya uliyosoma hakika utaona Kubarikiwa Sana. 

MAOMBI

Eh! Mungu Baba nisaidie siku zote hata wakati nikiongezeka nisikusahau wewe, uniweke sehemu ya kuinuliwa na wewe siku zote. 

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827, pastorulenje@outlook.com 



Sunday, January 15, 2023

SIKIA SAUTI YA MUNGU, KUINULIWA NA BWANA NI FUMBO

 SOMO LA TATU LA KUINULIWA


SIKIA KWA BWANA, KUINULIWA NI FUMBO.


Mith 25:2, 

Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.

1 Sam 8:30

Daudi akauliza kwa BWANA, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote.


Nikupe Mifano Miwili, Uone Kuwa Kuinuliwa na Mungu ni fumbo...


1) HAUJUI SEHEMU YA KUINULIWA KWAKO.

Yusufu angeweza kudhania au yawezekana aliwahi kudhania kuwa atainuliwa kupitia Potifa, au yawezekana aliamini pale ameshainuliwa. Kwa sababu Potifa alikuwa akida wa Farao na mkuu wa askari, na kama aliweza kumfunga Yusuph kwenye gereza la mfalme maana yake alikuwa mtu mwenye cheo. 

Lakini Mungu anamuinua Yusufu kutokea gerezani na siyo kwa Potifa.

Usikate tamaa kwa sababu hujui mbinu ambayo Mungu anataka kuitumia ili akuinue, kwa sababu hujui sehemu gani Mungu anataka kukuinua, unaweza fikiri anakupeleka gerezani kumbe ndiyo anakupeleka sehemu ya kukuinua, unaweza fikiri anakupeleka chini kumbe anakupeleka sehemu ya kuinuliwa kwako.


2) KUNA WAKATI VITA NDIYO SEHEMU YA KUINUKA KWAKO.

1 Sam 15, 17, 27 (8-9), 30.

Ukisoma hiyo mistari utaona maadui ambao aliwaacha Sauli ndiyo Daudi anawapiga, Lakini kumbuka hawa ndiyo waliomshusha Suali, leo wanakuja kama Maadui. Daudi anauliza niwafute. Mungu anamwambia nenda. 

Daudi alipokewa na Sauli vizuri, akapendwa na Yonathani kama anavyopenda roho yake, lakini haikuwa sehemu ya kuinuka kwake, bali viliinuka vita, akachomewa nyumba, na wake zake wakatekwa. Kumbe Mungu alileta maadui zake, ambao Sauli aliwaacha ukiwapiga ni sehemu ya kuinuka kwako. 

Kupitia Amaleki Yoshua aliinuka na kujulikana kuwa anafaa, leo Daudi anainuka kupiga maadui ambao Sauli aliwaacha. 

Lakini yatufundisha Sehemu ambapo wengine wanaacha wewe muulize Bwana kwanza, yawezekana hizo changamoto zinazofanya wengi waache ni Adui za Bwana, Bwana anataka ushinde ili akupe kuinuliwa.

Walichoshindwa wao ndiyo sehemu ya kuinuka kwako (I am your replacement) ukishindwa kuomba mimi naomba, ukishindwa wachawi mimi naondoa, ukishindwa kufunga mimi nafunga, wakati unalala mimi naomba…

NINI CHA KUFANYA ILI KUCHUNGUZA SIRI YA KUINULIWA


I. FUNGUA MOYO WAKO KWA ROHO MTAKATIFU

1 KOR 2:9-10

9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

Kama kuinuliwa ni fumbo, na Roho ndiye pekee anaweza kukujulisha siri hiyo, kwa sababu yeye anayajua mafumbo ya Mungu.

Katika siku yako, tenga angalau asilimia 10 ya masaa yako 24 ukae na Roho Mtakatifu, Yeye atakujulisha siri ya kuinuliwa kwako.

Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani. MWA 41:16

Yusuph alisaidiwa na Roho Mtakatifu kumtafsiria Farao ndoto, na ndiyo ikawa point yako ya kuinuliwa.

Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake? MWA 41:38


II. TAZAMA ISHARA YA KUINULIWA

1 FAL 19:19, MWA 40:1-3

Mungu anapotaka akuinue, kwanza anatuma ishara, alipotaka kumuinua Musa, kwanza alimtumia ishara ya kijiti kikiwaka moto bila kuteketea.

Mungu alipotaka kumuinua Elisha, kwanza alimtumia ishara, Eliya akamfata na kumtupia vazi lake. Na Elisha alipoona akajua kabisa kuwa ni ishara ya kuchukua nafasi ya Eliya ya kuwa nabii wa kimataifa. Kwa sababu watumishi wa Mungu walipewa vazi maalumu na Mungu kama ishara ya nafasi zao.


III. OMBA UNAJISIKIA AU HAUJISKII

YER 33:3

Hatuombi kwa sababu tunajisikia, bali unajisikia aua haujisikii inatakiwa kuomba. Yesu hajasema mtakapojisikia kuomba, bali alisema ombeni.

Biblia inasema

Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

Utakapoamua kumuita Mungu na kumuita zaidi, Mungu atakuonyesha makubwa na magumu usiyoyajua. Usiyoyajua ni sehemu ya fumbo la kuinuliwa kwako. Huwezi kuonyeshwa makubwa na Mungu alafu ukaishi maisha ya chini.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827 

pastorulenje@outlook.com 


Nifatirie zaidi katika mitandao ya kijamii kama...

Pastor Ulenje 


JITIE NGUVU KATIKA BWANA ILI KUINULIWA NA BWANA

 SOMO LA PILI LA KUINULIWA NA MUNGU


JITIE NGUVU KATIKA BWANA, INUKA


1 SAMWELI 30:1-8

Kujitia nguvu katika Bwana ni kukumbuka ya kwamba yupo Mungu ambaye naweza nikamtegemea, yupo Mungu ambaye nikimtafuta atanipigania na kunipa ushindi.


KWANINI UJITIE NGUVU KATIKA BWANA?


1. KWASABABU BWANA AMETUHIFADHI HAI.

Wakati wa changamoto zote, unachokihitaji hasa ni kuwa hai, kwa sababu ukiwa hai unaweza kugeuza yote uliyokutana nayo kuwa ushuhuda. Kwa sababu majaribu hayawezi kukuharibu kama bado una uhai wa kuendelea kujaribu. 

Pamoja na yote tuliyokutana nayo, ila Bwana alihakikisha yanatuliza, yanatuumiza, yanatuvunja moyo ila hayatuuwi. Siyo kwamba hayakuwa na nguvu ya kutuuwa, ila kwa sababu Bwana alikuwa upande wetu kuhakikisha tunaishi, ili siku moja tuje kusema Farasi na mpanda Farasi aliwatupa baharini. 1 Sam 27:8,9.

Pamoja na yote Daudi aliyokutana nayo, Bwana alihakikisha Suali hamuuwi, alihakikisha Wafilisti hamuuwi, alihakikisha Waamaleki hamuuwi_ kwanini kwa sababu Bwana alitaka kuyageuza yote aliyopitia kuwa kitabu cha SIFA CHENYE SURA nyingi kuliko zote kwenye Biblia 150. 

Biblia inasema Mhubiri 9:4 Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);

Maadamu Una Uhai, Bado Lipo Tumaini, Inuka Jitie Nguvu Katika Bwana.


2. KWA SABABU MACHOZI TULIYOLIA HAYAJATUTOA TULIPO TEKWA.

Daudi na wenzie mianne wakainua sauti zao na kulia, siyo tu walilia, bali waliinua sauti zao na kulia mpaka walipokuwa hawana nguvu za kulia tena; lakini majibu hayakutokea. Wakaanza kumlaumu Daudi lakini lawama hazikuwasaidia.

Mungu ameweka machozi ili kutujulisha kwamba kuna jambo la uchungu, ila siyo njia ya kututoa kwenye uchungu. Mungu ameweka machozi ili watu wajue kuwa upo matekani, ila siyo ya kukutoa kwenye mateka. Kama umeamua kulia ni bora ulie kuinuka kwa mkono wa Bwana ili siyo ulie kuonyesha namna unapitia. Adui amekuteka ili ulie, unapolia unampa sifa kuona amekuweza. Daudi akainuka, akajitia nguvu katika Bwana, ndipo ukombozi wao ukapatikana. 


Kama machozi hayajakupa matokeo, Leo inuka Jitie Nguvu katika Bwana, Mungu wako Anakusubiri umalize kulia na kulalamika ili Akusaidie. 

Wakati Daudi na wenzie wanalia, Mungu alikuwa akiwatazama, ila Daudi alipojitia nguvu, Mungu akainua mkono wake na kuwainua na hapo ukawa mwanzo wa Daudi kuwa Mfalme na wenzie kuwa majemedari wa jeshi na wakuu wa Israel ambao hapo kwanza walimfata Daudi sababu walikuwa na njaa na madeni.


3. KWA SABABU BWANA AMEHAKIKISHA TUNABAKIWA NA NAIVERA.

Wakati adui anateka vyote kuhani tulibakiwa naye, na naivera nayo ikabaki. Naivera lilikuwa ni vazi la kikuhani, ambalo kuhani alivaa anapojihudhurisha kwa Bwana, na ni vazi lilibeba majina ya makabila ya wana wa Israel. 

Adui ameiba vyote, ila damu ya Yesu bado tunayo, ambayo haishindwi kwa dhambi zetu, haishindwi kwa nguvu za adui, haishindwi kwa nguvu ya pesa, adui ataiba vyote ili naivera bado tunayo, vazi la damu ya Yesu bado tunalo ambalo kwa hilo tunasogea mbele za Mungu wetu na kupokea nguvu mpya ya kumshinda adui aliyetushinda.

Ebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

Maadamu bado una vazi la damu ya Yesu, Acha kubaki chini, Jitie nguvu katika BWANA 2023, inuka.


4. JITIE NGUVU KATIKA BWANA KWA SABABU UKIFUATA UTAYAPATA. 

Daudi alipoacha kulia na kujitia nguvu katika Bwana, ndipo Bwana anamwambia, Inuka_ Ukiwafuata utawapata na utawapokonya yote waliyoiba, yote waliyochukua. Kumbe tunayofikiri hayawezi kuisha, yanaweza kuisha, yale tunasema hatuwezi kupita, tunaweza kupita, yale tunawaza hayawezi kutuachia, yanaweza kutuachia; 

Lakini kama tutainua imani, na kujitia nguvu katika Bwana, basi tutavipata. Kwa nini, kwa sababu Bwana ameshaondoa nguvu zilizo juu yao.

Yoshua na Kalebu wakawaambia makutano; Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope. Hesabu 14:9.

Unayoyaogopa yameondolewa nguvu zake, unayosema yanakutesa, yanakuliza, ni magumu, huwezi kutoka; yameondolewa nguvu zake_ tatizo siyo yenyewe tena, tatizo ni wewe hutaki kuinuka na kuyafuatia. Ukiyafuatia utayapata_ Ukiinuka na kupigana utashinda.

Kumbe tunavyohofu hatuwezi kuvipata, hatuvipati kwa sababu tunahofu ya kutokuvipata, kumbe kesho tunayohofu itakuwa mbaya, siyo kwamba ilitakiwa kuwa mbaya, inakuwa mbaya ni kwa sababu hatujaifuta tumeacha siku zote itufate sisi, YESU anasema 

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Math 6:34.

Kesho imewekwa ijisumbukie yenyewe, wewe ifuate kwa imani, maovu ya leo yasikukatishe tamaa maana siku inatosha kwa maovu yake.

Bado Lipo Tumaini, Kama utajitia nguvu katika Bwana, Utawapata Hakika


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

pastorulenje@outlook.com 

Nifatirie kupitia mitandao ya Kijamii 

Tiktok, Facebook, Youtube na Instagram kwa Jina la Pastor Ulenje.



MAANA YA KUINULIWA NA MUNGU

SOMO LA KWANZA LA KUINULIWA NA MUNGU.

MAANA YA KUINULIWA

 1. MTU ALIKUWA CHINI UNAMSIMAMISHA 

Mtu ambaye yupo chini  ni yule ambaye ni daraja la mwisho mbele ya wengine, katika uchumi, maisha yake, uzima wake au historia yake, au familia aliyotoka, Mungu anampeleka kiwango cha juu, anampa historia, anampa heshima na daraja la juu. 

Mfano mzuri ni Daudi alitoka kuchunga kondoo, akafika kuwa na jeshi la watu minne, akafika kuwa mfalme wa Yuda, akafika kuwa mfalme wa Israel, akakuwa kuwa baba wa mfalme wa wafalme na Mungu akamwambia jina lake litabaki milele katika Uflme wa Israel. 

Lakini Bwana alipomuita, aliinuka na kumpiga Goliathi, na BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Zaburi 78:70-71.


2. MTU ALIKUWA CHINI SANA UNAMSIMAMISHA. 

Kuna watu wako chini sana kiwango ambacho hata aliye chini anamuona yuko chini, kiwango ambacho hata wewe mwenyewe unajikatia tamaa, hata Mungu akitaka kukuinua unamcheka kuwa hutoweza kuniinua kwa kiwango hiki cha chini, kisha Mungu anakuja anakuinua. 

Mungu anawasimamisha. Mfano mzuri ni Musa, kwa sababu alikuwa kiwango cha chini sana kiwango cha kwenda kufanya kazi kwa baba mkwe, mwanaume kufanya kazi kwa baba mkwe, ni kiwango ambacho hata masikini atakuona upo chini na atakudhalau, 

Ndiyo maana Mungu alipokuja kumuinua alikataa hata Mungu, ikamlazimu Mungu atumie ishara nyingi kumthibitishia lakini bado hakuamini, ila alipoinuka na kwenda Mungu aliposema, BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Kutoka 3:14-15


3. MTU AMEDONDOKA UNAMSIMAMISHA. 

Mtu ambaye alikuwa amesimama, kila kitu kinaenda vema, na kila mtu anampa heshima na amekuwa mtu mkuu, kisha katika njia ya maisha anadondoka, watu wanamkatia tamaa, kisha Bwana anakuja anamuinua na kuwa na uwezo wake wa zamani.

Mfano mzuri ni Samsoni, alikuwa mtu mkuu katika nchi yake, ameuwa simba, kauwa majeshi ya wafilisti na nchi yake ikampa heshima kama mwamuzi wao, lakini akadondoka mpaka kuwa kiwango cha chini mpaka kuwa kipofu, ila alipoinuka na kuomba toba mbele za Mungu, BWANA AKAMUINUA.

Soma ___Waamuzi 16:28-29


3. WEWE MWENYEWE KUINUKA HUWEZI 

Kuna mtu yuko chini kiwango ambacho hawezi kuinuka pale anapopewa nafasi ya kuinuka, kwa sababu imefika ameshajihesabia kuwa yeye ni wa chini na wengine ni wa juu. 

Mfano ni yule mtu aliyekuwa kiwete toka tumboni, hajawahi kusimama kwenye maisha yake, alafu leo Petro anamwambia simama, naamini hakuamini_ mpaka Petro akaamua kumsaidia kuinuka, naamini kwako ambae unaona huwezi inuka, inuka kwa maneno haya na BWANA ATAKUINUA kwa sababu naamini amenituma kwa ujumbe huu uinuke.

Soma ____Mdo 3:1-8


4. MTU ALIYEKATA TAMAA KUINUKA ALAFU ANASIMAMISHWA. 

Kuna mtu amejaribu mara nyingi, mara nyingi na mara nyingi tena na tena kusimama na akashindwa, alafu Bwana anakuja kumuinua.

Mfano ni aliyekuwa hawezi katika birika la kwenye mlango wa kondoo, birika la Bethzatha, amejaribu kuinuka kwa miaka 38 ni miaka mingi sana, malaika anapokuja anajaribu kuinuka ajitupe kwenye birika hawezi, mpaka watu wamemkatia tamaa naye akajikatia tamaa kwa sababu amejaribu mara kwa mara, lakini Yesu anamwambi simama, jitwike godoro lako uende. Aliposimama, BWANA AKAMUINUA.

Soma ____Yoh 5:1-8


5. MAANA YAKE NI KUWA CHINI SIYO MWISHO WA MAISHA. 

Kama Mungu alimuinua Daudi aliyekatiwa tamaa na baba yake, kama Mungu alimuinua Musa aliyejikatia tamaa yeye mwenyewe, Samsoni ambaye taifa lilimkatia tamaa, mtu ambaye hata kuinuka mwenyewe hakuweza, mtu dhaifa kiwango cha kujaribu kuinuka miaka 38 asiweze, Sarah aliyekaa bila mtoto miaka 85 mpaka alipoambiwa utazaa akacheka__ LIPO TUMAINI KWAKO LA KUINUKA.

Lakini pia mwambie mtu yeyote “Usinikatie tamaa tafadhali, BWANA ANAWEZA KUNIINUA. Lakini pia na wewe jiambie “Usijikatie tamaa tafadhali, BWANA ANAWEZA KUNIINUA. Waambie watu wasikuandika MWISHO, Wala wewe Usijiandika MWISHO… Maadamu unaishi BWANA ANAKUINUA. 


KANUNI ZA MSINGI KUINULIWA 2023

1. Mkumbuke BWANA MUNGU wako. 
     Mh 12:1, Kumb 8:18 

2. Kuwa na imani ya KUINUKA. 
    Math 9:6-7 

Mimi ni Pastor Ulenje 
+255 683 477827 
pastorulenje@outlook.com 

Follow me kupitia 
Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama Pastor Ulenje. 

Wednesday, January 11, 2023

 DHANA HALISI ZA MAFANIKIO

(PRECEPTS TO SUCCEED)

The Original Concepts for Personal Success


Dhana ni wa wazo kuhusu jambo fulani.

Natamani tuone wazo halisi kuhusu Mafanikio. 

Na wazo halisi kuhusu mafanikio tunalipata kwa Mungu. Wazo halisi ni la muhimu sana sababu ndilo linakupa mafanikio halisi.

Mafanikio unaweza kuyapata kwa namna yoyote, na watu wakahisi umefanikiwa na kumbe ni mafanikio feki, tutakuja kuona ufupi wa furaha ya maisha yako na mwisho wako.

Mwaka huu mpya natamani twende kwenye mafanikio halisi, mafanikio ambayo yanatokana na baraka ya Bwana, ambayo haichanganyikani na majuto ndani yake. Binafsi leo naweka agano la kuzifata.

Kwanza naomba ijurikane sisi wana wa Mungu, ni watoto wa Mungu ni mawakili wa ufalme wa Mungu, hivyo tupo duniani kumuwakilisha Mungu, tupo duniani kuwavuta watu wa duniani waje kwenye ufalme wetu. 

Na njia kuu ya kufanya hivyo, ni kutumia kanuni zetu za mafanikio kw usahihi na bidii ili watu wa ulimwengu huu wakiona, watamani kufata kanuni zetu na kuingia kwenye ufalme wetu. Lakini kama tutafanikiwa kwa njia zao, basi hatutakuwa na sababu yoyote ya kuwavuta wao kwetu.


Tunapomaliza mwaka 2022 kuingia mwaka 2023 dalili zimeonekana wazi kwa Tanzania na dunia kuwa uchumi unazidi kushuka, hata Oxford Economics yenye jopo la wachumi 300 wamefanyia utafiti nchi zaidi ya 200 na kuona uchumi unashuka toka pato la 3% mpaka 1.3%. kwa namna hii tunahitaji kanuni za Mungu ili kuwa salama


Jiandae kutembea na kanuni za Mungu ambazo hazitashindwa.


1.   MFANO WA MUNGU 

   ðŸ‘‰ ILI KUTAWARA

Biblia inasema katika 

Mwa 1:26 na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyaa, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho chini ya nchi 

na Sura ya 27 inaweka wazi kuwa Mungu akaumba mtu kwa mfano wake. 

Mungu alimpa mwanadamu cha kwanza ni mfano wake na sura yake, ndipo akasema wakatawale. 

Kutawala ndiyo siraha ya kwanza mwanadamu kufanikiwa, kama ukitawala katika huduma umefanikiwa, ukitawala katika biashara umefanikiwa, ukitawala kazini umefanikiwa. Kwa sababu ili ufanikiwe lazima watu wakujie, na ukitawala maana yake watu wanakujia kupokea bidhaa yako au huduma yako, hapo umefanikiwa


Lakini ili upate utawala wa kweli, sifa ya kwanza ni lazima ufanane na Mungu. Kufanana na Mungu ni katika nia ya ndani, katika nia ya matendo yake, na namna ya kuishi binafsi na watu wengine. Na hasa aliongelea utu wa ndani.

Paulo anasema katika 

Efeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Tuliumbwa katika Kristo, sababu kule kuumbwa kwa kwanza kwa lile kosa la adui kulitufanya kuharibika. Siyo muonekano wa nje, bali ndani. Na anaonyesha kuna matendo Mungu aliyaweka tangu awali, ambayo sababu ya anguko mwanadamu akawa hawezi tena kuyafanya.

Yesu anasema zamani haikuwa hivi, ila sababu ya ugumu wa mioyo yenu.

Ukisoma 

Efeso 4:24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. 

Ukisoma tena Kolosai 3:10 Paulo anasema mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

Kama tunataka kufanikiwa katika uchumi, dhana ya kwanza kabisa ni kuwa watawara, kutawala katika mauzo ya biashara zetu, kutawala kazini, kutawala katika huduma. 

Mwa 17:1-5 Mungu anamwambia Ibrahimu, Mimi ni Mungu mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. Abramu akanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi.  

Mungu alipomwambia awe mkamilifu alimaanisha awe afanane na yeye, awe tofauti na wanadamu. Na Ibrahim alipoanguka kifudifudi ishara kukubali, Mungu akwambia sasa nitafanya agano la kukupa kutawara.

Na Yesu anatuamuru tuwe tofauti na watu wengine katika Math 5:48 ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu


2.   PUMZI YA UHAI.

  👉 HAPO UTAWEZA FANYA CHOCHOTE.


Biblia inasema 

Mwa 2:7 Bwana akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Neno la msingi hapo ni mwanadamu akawa nafsi hai. Maana yake ile pumzi ya uhai ndiyo ikamfanya kuwa nafsi hai. Mtu asiye hai hawezi kufanya chochote. Adamu alipokufa kiroho ndipo mahangaiko ya mwanadamu yalianza. 

Lakini inaonyesha uhai wa mwanadamu unatoka kwa Mungu, mwanadamu hawezi chochote pasipo Mungu, mwanadamu pasipo Mungu kinachofata ni mahangaiko tu. 

Utaona mwanadamu alipopewa pumzi ya uhai akawa nafsi hai ndipo Bwana anampa kazi sasa ya kufanya. Kazi ni jukumu la kukuletea pesa, kukuletea mafanikio lakini huwezi fanya kazi pasipo ile pumzi ya uhai, mwisho wake ni mahangaiko,  

Kinachofanya wengi wasipate mafanikio ni kwa sababu wanahangaika na kazi, wanaacha walichopewa ili kufanikisha kazi. Na wengine wanapata mafanikio feki ambayo mwisho wake ni mauti.

Ibrahimu baada ya kutembea sana kuendea nchi ambayo Bwana atamuaonyesha. Mwanzo 12:7 Bwana anamwambia uzao wako nitawapa nchi hii. Kabla hata ya kuanza kuilima wala kujenga hema, akamjengea Madhabahu BWANA aliyemtokea, mstari wa 8 unasema ...akaliitia jina la BWANA.

Hii ilimaanisha Ibrahimu alijua, sawa Mungu amenipa sehemu ila lazima nimtake Yeye kwanza ambaye ndiye pumzi ya uhai ili nifanikiwe katika hii nchi...

Yesu amekaa miaka 30 bila kuanza kazi aliyoijia mpaka aliposhukiwa na Roho mtakatifu Luka 3:22-23. Neno la Bwana linamjia Zakaria kwa Zerubabeli Zekaria 4:6 kusema Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.

Wakati kanuni za dunia zimeshindwa, na umezijaribu sana, 2023 kaa chini na Roho Mtakatifu kwanza muulize nini nifanye, pili mshirikishe katika kila unalofanya. Ufanye 2023 siyo mwaka wa kujaribu bali wa kufanya. Baada ya Israel kuzunguka miaka 40 mlima Seiri, sauti ya Bwana ikamjia Musa peteni njia hii (Kumb 2:1-3). 

Weka mkazo sana katika kumtaka Bwana 2023 zaidi ya miaka yote, taka sana ufalme wake na haki yake, yale ambayo wengine wanayasumbukia hawayapati au wanatumia njia ya udhalimu kuyapata, wewe Mungu atakupa kibali na kukuweka katika nafasi ya kuyapata.


3.   BARAKA ZA BWANA.

 ðŸ‘‰ ILI UONGEZEKE


Baada tu ya mwanadamu kuwa nafsi hai, Mungu akambariki. 

Mwanzo 1:28 Biblia inasema Mungu akawabarikiwa, Mungu akawaambia Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini,na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Nikwambie tu wazi unahitaji baraka za Bwana kuliko unavyoweza ukafikiri. 

Watu wengi wanapenda kuongezeka, wanapenda kuzaa vitu, kuanzisha biashara, kampuni na wanataka waende dunia nzima pasipo baraka za Bwana. 

Baraka ni uwezesho wa Mungu ndani ya mtu wa kufanikiwa. Baraka ni kibali cha Mungu, ni neema.

Mtu aliyebarikiwa, ile baraka inampa kufanikiwa katika kila analogusa. Haina maana hatokutana na changamoto, ila ile baraka inampa ulinzi na kushinda.

Biblia inaweka wazi mtu aliyebarikiwa atakuwa tajiri, Mith 10:22 inasema Baraka ya Bwana hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo. 

Katika agano jipya 

Efeso 1:3, 4, Paulo anasema Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo. Kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo

Hilo neno kama na neno ili tuwe linaunganisha kuonyesha Kumbe kuwa mtakatifu, kuwa mtu usie na hatia mbele zake inaambatana kabisa na baraka zetu kutenda kazi, ndiyo maana hata Adamu utakatifu ndiyo ulilinda baraka yake.  

Ndiyo maana utaona baada ya Bwana kumaliza kumuumba mtu, na kumpatia baraka zote akampa Discipline. Adabu, akamwambia utaishi ndani ya bustani lakini kwa mipaka, kula miti yote lakini miti fulani usile. 

2023 jiandae kuishi kwa mipaka, ishi maisha ukifanya unayopaswa kufanya, achana na yale ambayo yanakuondoa kwenye reli, kwa maana yaliyofanya mpaka sasa una struggle ni kutoishi kwa mipaka.

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827 

FOLLOW ME KWA; 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram 

Kama Pastor Ulenje.


 



MAANA YA KUJITIA NGUVU KATIKA BWANA, INUKA

JITIE NGUVU KATIKA BWANA, INUKA.


1 SAMWELI 30:1-8

Kujitia nguvu katika Bwana ni kukumbuka ya kwamba yupo Mungu ambaye naweza nikamtegemea, yupo Mungu ambaye nikimtafuta atanipigania na kunipa ushindi.


KWANINI NIJITIE NGUVU KATIKA BWANA.


1.     KWASABABU BWANA AMETUHIFADHI HAI

Wakati wa changamoto zote, unachokihitaji hasa ni kuwa hai, kwa sababu ukiwa hai unaweza kugeuza yote uliyokutana nayo kuwa ushuhuda. Kwa sababu majaribu hayawezi kukuharibu kama bado una uhai wa kuendelea kujaribu. Pamoja na yote tuliyokutana nayo, ila Bwana alihakikisha yanatuliza, yanatuumiza, yanatuvunja moyo ila hayatuuwi. Siyo kwamba hayakuwa na nguvu ya kutuuwa, ila kwa sababu Bwana alikuwa upande wetu kuhakikisha tunaishi, ili siku moja tuje kusema Farasi na mpanda Farasi aliwatupa baharini. 1 Sam 27:8,9.

Pamoja na yote Daudi aliyokutana nayo, Bwana alihakikisha Suali hamuuwi, alihakikisha Wafilisti hamuuwi, alihakikisha Waamaleki hamuuwi_ kwanini kwa sababu Bwana alitaka kuyageuza yote aliyopitia kuwa kitabu cha SIFA CHENYE SURA nyingi kuliko zote kwenye Biblia 150. 

Biblia inasema Mhubiri 9:4 Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);


Maadamu Una Uhai, Bado Lipo Tumaini, Inuka Jitie Nguvu Katika Bwana.


2.     KWA SABABU MACHOZI TULIYOLIA HAYAJATUTOA TULIPO TEKWA.

Daudi na wenzie minne wakainua sauti zao na kulia, siyo tu walilia, bali waliinua sauti zao na kulia mpaka walipokuwa hawana nguvu za kulia tena; lakini majibu hayakutokea. Wakaanza kumlaumu Daudi lakini lawama hazikuwasaidia.

Mungu ameweka machozi ili kutujulisha kwamba kuna jambo la uchungu, ila siyo njia ya kututoa kwenye uchungu. Mungu ameweka machozi ili watu wajue kuwa upo matekani, ila siyo ya kukutoa kwenye mateka. Kama umeamua kulia ni bora ulie kuinuka kwa mkono wa Bwana ili siyo ulie kuonyesha namna unapitia. Adui amekuteka ili ulie, unapolia unampa sifa kuona amekuweza. Daudi akainuka, akajitia nguvu katika Bwana, ndipo ukombozi wao ukapatikana. 

Kama machozi hayajakupa matokeo, Leo inuka Jitie Nguvu katika Bwana, Mungu wako Anakusubiri umalize kulia na kulalamika ili Akusaidie. Wakati Daudi na wenzie wanalia, Mungu alikuwa akiwatazama, ila Daudi alipojitia nguvu, Mungu akainua mkono wake na kuwainua na hapo ukawa mwanzo wa Daudi kuwa Mfalme na wenzie kuwa majemedari wa jeshi na wakuu wa Israel ambao hapo kwanza walimfata Daudi sababu walikuwa na njaa na madeni.


3.     KWA SABABU BWANA AMEHAKIKISHA TUNABAKIWA NA NAIVERA.

Wakati adui anateka vyote kuhani tulibakiwa naye, na naivera nayo ikabaki. Naivera lilikuwa ni vazi la kikuhani, ambalo kuhani alivaa anapojihudhurisha kwa Bwana, na ni vazi lilibeba majina ya makabila ya wana wa Israel. 

Adui ameiba vyote, ila damu ya Yesu bado tunayo, ambayo haishindwi kwa dhambi zetu, haishindwi kwa nguvu za adui, haishindwi kwa nguvu ya pesa, adui ataiba vyote ili naivera bado tunayo, vazi la damu ya Yesu bado tunalo ambalo kwa hilo tunasogea mbele za Mungu wetu na kupokea nguvu mpya ya kumshinda adui aliyetushinda.

Ebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.


Maadamu bado una vazi la damu ya Yesu, Acha kubaki chini, Jitie nguvu katika BWANA 2023, inuka.


4.     UKIFUATA UTAYAPATA. 

Daudi alipoacha kulia na kujitia nguvu katika Bwana, ndipo Bwana anamwambia, Inuka_ Ukiwafuata utawapata na utawapokonya yote waliyoiba, yote waliyochukua. Kumbe tunayofikiri hayawezi kuisha, yanaweza kuisha, yale tunasema hatuwezi kupita, tunaweza kupita, yale tunawaza hayawezi kutuachia, yanaweza kutuachia; Lakini kama tutainua imani, na kujitia nguvu katika Bwana, basi tutavipata. Kwa nini, kwa sababu Bwana ameshaondoa nguvu zilizo juu yao.

Yoshua na Kalebu wakawaambia makutano; Hesabu 14:9. Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope. 

Unayoyaogopa yameondolewa nguvu zake, unayosema yanakutesa, yanakuliza, ni magumu, huwezi kutoka; yameondolewa nguvu zake_ tatizo siyo yenyewe tena, tatizo ni wewe hutaki kuinuka na kuyafuatia. Ukiyafuatia utayapata_ Ukiinuka na kupigana utashinda.

Kumbe tunavyohofu hatuwezi kuvipata, hatuvipati kwa sababu tunahofu ya kutokuvipata, kumbe kesho tunayohofu itakuwa mbaya, siyo kwamba ilitakiwa kuwa mbaya, inakuwa mbaya ni kwa sababu hatujaifuta tumeacha siku zote itufate sisi, YESU anasema 

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Math 6:34.

Kesho imewekwa ijisumbukie yenyewe, wewe ifuate kwa imani, maovu ya leo yasikukatishe tamaa maana siku inatosha kwa maovu yake.


Bado Lipo Tumaini, Kama utajitia nguvu katika Bwana, Utawapata Hakika.


Mimi ni Pastor Ulenje 

 +255 683 477827 

FOLLOW ME 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama 

PASTOR ULENJE


Tuesday, January 10, 2023

UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU

 UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU


1.    Roho ndiye analishuhudia neno ndani yetu.


Yoh 15:26 Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia

1 Yoh 5:7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli

Tena kuhusu kuokoka Yoh 3:5 Yesu anasema Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, maana yake siyo neno peke yake, Roho lazima awepo ili neno kumuokoa mtu.


2.    Roho ndiye analisema neno la Mungu midomoni mwetu.


Yesu anasema Marko 13;11 msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni; kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu

Kwenye Mathayo 10:20 anasema kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu

Siri ya kufikia hapa ni kujaa Roho Mtakatifu, Biblia inasema kwenye Mdo 4:8 Petro akijaa Roho Mtakatifu, alipoongea wazee wakashangaa mbona hawa watu hawajasoma wametoa wapi ujasiri huu.


3.    Roho ndiye anayekupa uwezo wa kuisikia sauti ya Mungu.


Ufu 1:10 Yohana anasema Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu

Ukisoma Eze 2:2 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami. 

Kumbe muda wote alikuwa hamsikii Yeye aliyesema naye.

Ukisoma Efeso 3:1-6

1 Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;

2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.

5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo 


4.    Roho ndiye anayetupa kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.


Ukisoma 1 Kor 2:9-12 

9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Kumbe yapo ambayo Mungu amekuandalia lakini kuyapata ni lazima Roho apate kukufunulia, la sivyo utaendelea kuteseka ikiwa uliyokirimiwa yapo.

Na siri kubwa ili Roho akufunulie ni kuwa mtu wa Rohoni, anasema katika mstari wa mwanadamu wa tabia ya asili yaani tabia ya mwilini hayapokei mambo ya Roho wa Mungu, kwake ataona ni upuuzi, kwanini kwa sababu yanatambulikana kwa jinsi ya Rohoni.


5.    Roho ndiye anatusaidia kulishika Neno


Eze 36:27 anasema Nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu,nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. 

Ni baada ya Mungu kuona mwanadamu ameshindwa kuenenda katika sheria zake wala kushika hukumu zake wala kuzitenda, ndipo akaweka roho yake ndani yako.

Ukisoma Warumi 7:23-25 Paulo anaonyesha wazi akipambana kuushinda mwili, lakini jibu anasema ni Roho mtakatifu ndiye anaweza kumuweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.


6.    Roho ndiye analithibitisha neno linapofika wakati wake.


Kila ahadi ya Mungu inapofika wakati wa kutimia unaona Roho anatokea kwenye tukio. Kuzaliwa kwa Yesu unaona mariamu anashika ujauzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Luka 1:35.

Ukisoma Mdo 13:2 Paulo anaitwa kuwa mtume wa mataifa, lakini anakaa miaka 11 Antiokia bila kufanya wito mpaka Roho anashuka na kusema sasa ndiyo wakati Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi niliyowaitia.

Siri kubwa waliingia kufunga na kumsifu Mungu, waliingia rohoni, kama wasingeingia rohoni wakati ungewapita. Acha kujichelewesha kwa kupenda sana kuwa ubize, tenga muda wa kuwa rohoni huu ndiyo wakati wa kupiga hatua uliyoisubiri.


7.    Roho ndiye anathibitisha Neno kwa Ishara na Nguvu.


Watu walipoona Yesu anafanya ishara nyingi wakasema akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote... Math 8:16, 

Lakini Yeye anakuja anasema kwenye Sura ya 12 hiyo Math 12:28 Lakini nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu. Kumbe wao waliona neno lake pekee, kumbe neno lake lilichanganyika na Roho Mtakatifu.

Mdo 13:9 Inasema Sauli, ambaye ndiye Paulo akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho yule mchawi akamwambia angalia mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu. Ikawa, kwanini kwa sababu neno lake lilichanganyika na nguvu za Roho.

Ndipo anasema kwenye 1 Thes 1:5 Injili haikuwafikia katika maneno tu, bali katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu.

Kama unataka neno lako liwe na nguvu unapotamka katika maombi, siri ni Roho Mtakatifu, Unataka Neno litokee kwenye maisha yako, Roho ndiye anafanya neno litokee kwako pale unapolitenda.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

Follow me 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama Pastor Ulenje... hakika Utabarikiwa