Monday, December 21, 2015



SEMINA DEC 2015 -DAY 1

FUMBO LA MAISHA NA KUFIKIA HATIMA NJEMA

Yer 29:11
Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho"

Bwana anakuwazia mema, mawazo ya amani, kukupa tumaini siku yako ya mwisho: swali wewe je?

Maisha yana mwanzo, kati na mwisho. Wote hapa bado hatujafika mwisho, kuna wengine wapo katikati, na wengine wanakaribia mwisho.

Lakini lipo tumaini: hata kama unakaribia mwisho au upo katikati unaweza kuyafanya maisha yako yaanze mwanzo.

Yesu alikuja ili mwanadamu apate fulsa ya kuanza tena mwanzo maisha. Hata kama alichezea kete anaweza kuanza tena mchezo na akashinda.

Ibrahimu alikuwa mwisho, Mungu anakamuita na miaka 70 na kuanza na mwanzo. Musa anaitwa akiwa anafikiri yupo katikati ya maisha, Mungu anamuita kuanza mwanzo mpya wa maisha yake. Petro vivyo hivyo na Paulo anaitwa akiwa katikati ya maisha, anaitwa na kuanza tena mwanzo.

Somo hili ni la muhimu sana kwenye maisha yako, muhimu sana. Maana Roho anakwenda kutufundisha namna ya kuutumia mwanzo wa maisha yetu kutengeneza katikati na namna ya kutumia katikati ya maisha yetu ili kujenga mwisho mzuri ambao Bwana Mungu ametuandalia.

Mungu alipokupa nguvu ya maamuzi; basi alikupa nguvu ya kuamua hatima ya maisha yako. Mungu anapanga mwisho wako, ila kuufikia au kutoufikia hayo ni maamuzi yako. Mfano Sauli Mfalme na Sulemani na Joashi.

Mungu kukuwazia mwisho mzuri haina maana kwamba Mungu anashuka na kuja kuishi kwa niaba yako. Yeye anakupa marighafi na vitendea kazi na kuwa na wewe na kukusaidia.

Na utakapojitoa na kusimama ndani ya mstari wa kufikia mwisho aliokuandalia basi atahakikisha unaufikia, lakini utakapotoka nje ya mstari basi anakuacha na kumfikiria mtoto wako au mtu mwingine kuufikia mwisho huo. Na atajitahidi kukurudisha siku zote hatochoka, mpaka siku zako za kuishi zitakapoisha. Sababu yeye ni wa rehema huwarudi wale wamrudiao, hupenda watu wamrudie.

MWANZO.
Tuanze sasa...
• Maisha yamejawa na matukio tusiyo yatarajia. Kila siku yanatokea yale ambayo hatukuyapanga wala kutarajia yatokee.
• Maisha yamejawa na hasa huendeshwa na matokeo tusiyoyatarajia. Tunapofanya vitu na kupanga mipango huwa tunataajia mema na kujikuta tunapata tofauti.

• Maisha yamejawa na matukio ya kushangaza sana.
   Watu wanakuwa tofauti na walivyotajia au kutarajiwa kuwa:
   Waliopanga kuwa madaktari wanaishia kuwa wachungaji, waliopanga kuwa maaskofu wanaishia kuwa wachungaji au mashemasi, waliopanga kuwa wanasiasa au wafanyabiashara wanaishia kuwa wafanyakazi wa kawaida, bodaboda, wakulima au walimu, na wengine kuwa walevi wa pombe, sigara au bangi na madawa ya kulevya.
   Mwanafunzi anapanga kufika chuo kikuu na mzazi anajitahidi ili kutimiza ndoto za mwanae, matokeo yake anaishia kukuletea mtoto nyumbani au kushindwa mtihani na kuishia kidato cha nne au cha tano.
   Wazazi wanashangaa wale watoto waliowapenda sana na kutarajia kuwa ndiyo watawasaidia na kuwaona kuwa ndiyo watoto wema ndiyo wanakuja kuwa hawafai na wale waliokuwa hawafai ndiyo baadae wanakuja kuwa wamaana.
     Pastors and bishop become prisoners, politician come from high ranks to prison, beautiful girls become prostitute, those we call bad girl, poor, ignorant, they become our boss, ministers, chief secretary and C. E. O.
     Those we love in public, we hate after we see them in private.

MYSTERY OF LIFE
• Life become mystery when we wonder Why we still doing what we hate (we do, what we don't wanna to do), and what we desire to do, we don't do.
"What you desire to do you're not doing and many-times you're even not able to carry them out, and what you hate you don't have the ability to stop yourself from doing.

"In fact every one has its fault that neither fear nor law can stop from doing"

• Life become mystery when we try harder and more harder to stop ourself from doing some action, and we fail. We try to stop some attitude and behavior and we fail.
Sometime we cry, explain to people, pray and asking God mercy and grace and we wonder why we still do what we pray and ask to stop.

• We know something is evil, and we try to stop our mind and our body to execute them, A force come from our heart, a force that we don't know  even its name that our body and our mind succumb to do what we truly hate to do.
  And what we know is right and is what God want us to do, we force our mind and body to do, we wonder we are not.
  Eg. I desire to wake up early in the morning to pray I don't, I plan to pray in mid night I fail, I desire to fast and pray but I don't, I desire to be more powerful and spiritual in the kingdom of God, but I'm not. We desire to have good relationship with God and doing what he want, but we wonder we don't, everyday instead of saying yes I win, we ask for mercy.

• And the mystery of all, Many of us we are not what we desire and wish to become when we're youth.

• This is mystery to more than 90% of the world population: Many folks they don't even know themselves.
  We pretend to, but we don't.

* We try to know God but not ourselves,
   Whilst is difficult to know God if you don't know yourself      what Make me wonder is that, Even God, has a desire to see all of us, to know ourselves. That why, He never call somebody without tell him who he is. Before telling Abraham Go! He first tell him, I call you be father of the nations, Before telling Moses Go! He first tell him, Saviour of His people, Before tell Jeremiah, he first tell him why he make his birth.
# In fact, Your purpose is what carry your real identity"

"You wander and wander doing everything because you don't know yourself"

* when you know yourself, will make you to know that you cant live without God, and God Joy is your Joy and strength.
* Many folks die, only they know they're names but not themselves.
* And some they don't even bothering, that they do not know they are. Only they care, is to make living.
* Some people they try harder and harder to know who they are, finding they're purpose. But they become old and die, without achieving they're desire, Why? They finding from wrong source. God is only source, because is one who created you. (Recommend Book : Purpose Driven Life By Rick Warren and The Power of Purpose By Dr Myles Munroe)
* Many Elites, They only know they're positions and they're bosses and not them self. That why most of them they die with stress and Blood Pressure.

• Life has no experts: We're all facing challenges, problem, thing we cant handle, unexpected and unplanned events, and unexpected results. But Those Who have Faith in God are always safe.

• Everyone need better life, better world, better marriage and better family. And this make human an Utopia

• we all want more and plenty money, while some they lie, pretending that they don't need money, they lie, they need more, and they want more than you.

"Money is not everything, but is important to everything" Robert Kiyosaki

But seek ye first the Kingdom of God and His Righteousness and Other Thing (including money) shall be added to you"

• We live life but we don't know the meaning of it
This is what I know "we can have many definitions about life, but experience will tell you the truth" #Ev.Ulenje

Kesho tunaendelea
Umbali si shida waweza kuwa karibu nasi.
Ubarikiwe Sana kwa kusoma.
Naamini kuna kitu umepata, pita soma tena na tena.

+255 718 721 848
imaf2b@gmail.com

Wednesday, December 9, 2015

SEHEMU YA SITA: BARAKA TANO ZA PETRO NA KUJENGA KESHO KWA HEKIMA

Asante kwa kusoma sehemu ya tano, kama bado nakuomba katika Jina la Bwana Yesu tenga mda na usome sehemu ya tano, sasa tuendelee... ulenje.blogspot.com

B. KESHO

Baada ya kujifunza kuhusu jana sasa ni vema tukajua zaidi kuhusu kesho na kuona namna Petro alivyoweza kutumia leo yake kutengeneza kesho yake.

Petro siku zote alifanya jambo pasipo kutazama jana, hakutazama makosa, kati ya wanafuzi 12 Petro alikuwa ndiye mwanafunzi aliyekaripiwa na Yesu mara nyingi na kukosolewa mara nyingi lakini ndiye aliyetumiwa na kuwekwa karibu sana na Yesu, si hivyo tu, baada ya Yesu kuondoka Petro ndiye maanafunzi aliyeachwa kuwa kiongozi kati ya watume, ndiye aliyeambiwa waimarishe wenzio, ndiye aliyeambiwa kisha kondoo wangu, unaona pamoja na makosa yake yote lakini Mungu aliyakusanya yote na kuyafanya mema kwa kutimiza kusudi lake duniani.

"Unataka kumjua mtu asiyekosea, mtafute mtu asiyetumia fulsa"

Unataka kumjua mtu anayekosea na kuibuka mshindi, mtafute Petro, anayeona fulsa na kuitumia, wakamuita kiherehere, wakamuita mnafki, wakamuita charismatic, wakamuita msariti, lakini ndiye huwezi taja maendereo ya kanisa la kwanza na kuacha jina lake, hata Paulo anajua hilo, hata wewe unayesoma unajua hilo.

Uanataka kuwa mtu wa mafanikio, jaribu sana, ukikosea umia tena umia sana ili usirudie kosa hilo, jisamehe jisamehe tena jisamehe sana, kisha jaribu tena, ukikosea jaribu tena usiache kujaribu, hata ukifika mbinguni, jaribu kuimba kila wimbo jaribu kila wimbo mpaka uwekwe kiongozi wa kuimba kama cheo hiko kipo, lakini kubwa usiache kujaribu.

Najua ungetamani leo iwe ya pili kuelezwa, lakini hapana, siku zote ni za muhimu lakini kwa mafanikio ya mwanadamu LEO ni kuu na muhimu kuliko zote.

Kesho ni mda wa mbere ambao bado haujafikiwa na kuanza kutumika"
Katika mda uliyopewa na Mungu, kesho ni mda ambao bado hujaufikia.
Yesu akasema "Basi msiyasumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe" Math 6:34. Yesu hapa alikuwa akizungumzia siku ya kesho, ambayo ipo mikononi mwako, ambayo katika mda uliyopewa kuishi, kesho ya kwako.
Mtu aliyekufa hana kesho, mtu aliye bado mzima ndiye pekee mwenye kesho. Hivyo kesho ni yako, ukiwa hujaamka kesho, ujue siku zako ziliisha.
Siku ya mkesha wa mwaka mpya wa mwaka 2014 mchungaji wa kanisa la CLC alitoa hadithi ya ajari ya mtu aliyegongwa na gari aina ya Toyota iliyotokea mda wa mchana wa tarehe 31/12/2013, siku moja kabla ya mwaka mpya wa mwaka huo, kisha akasema "fikiri kama tukirudisha dakika moja nyuma, wewe unadhani yule mtu atakuwa anawaza nini kichwani mwake?" Akajibu mwenyewe akasema "lazima atakuwa anawaza mipango ya kufanya baadae". Sijatoa hii hadithi kukwambia usipange ya kesho, nimetoa hii hadithi kukuonesha kuwa, kesho ni yako kama ukiifikia, usipoifikia si yako,

Hivyo kati ya siku tatu: jana, kesho na leo. Tunayoimiliki ni leo tu pekee, si jana wala si kesho. Na usiumize kichwa kwa habari ya kesho, panga tu kwa habari ya kesho, umiza kichwa kwa habari ya leo. Tukizungumzia leo, utanielewa.

"Weka mipango ya kesho na kuwa na dhamira dhabiti ya kuitimiza ila Usiumize kichwa kwa habari ya kesho, Wala usiwaze kwa habari ya jana, umiza kichwa nini unapaswa kufanya na usichopaswa kufanya Leo, maana leo ndiyo siku pekee tunayoimiliki"

Ndugu mpendwa leo ndiyo yenye nguvu kubwa ya kubadiri maisha yako, si jana, wala si kesho.

UTAENDA JEHANAMU SI KWA ULIYOFANYA JANA SI KWA UNAYOPANGA KUFANYA KESHO, ni kwa unayofanya LEO"

Kesho ni siku ndani ya mda tuliyopewa na Mungu ambayo hatujaifikia bado, tukiifikia inaitwa leo, hakuna mtu anayeimiliki kesho. Kama hatujui kuwa tutakufa lini ndivyo hatujui kuwa tuna kesho. Hivyo kesho ni miliki yetu ila ni milki hewa. Inaweza tokea au isitokee.
Kifupi ni kwamba: Mungu amempa kila mtu kusudi yaani kazi ya kufanya na kumpa mda ambao anajua hiyo kazi itakuwa imeisha, kuna wakati anaweza kuongeza, pia mwandamu anaweza kwa kuounguza mwenyewe, hasa pale mwanadamu anapotumia nguvu yake ya maamuzi kufanya jambo ambalo linaweza changia kuondoa uhai wake, Daudi alilia (paraphrase) "Bwana nipe kuzijua siku za kuishi kwangu ili tujue namna ya kuenenda"

1. Kesho ni siku mbere ya leo
2. Kesho ni siku ambayo bado haijatumika
3. Kila mwanadamu ni mjinga kuhusu kesho
4. Na ujinga huleta woga na hofu kwa kila mwanadamu kuhusu kesho.
5. Woga na hofu huleta watu kuisumbukia sana kesho.
6. Kesho ni makisio tu si kitu halisi.
7. Masikini wanahofu na kuacha ije inavyotaka, matajiri wanapanga wanavyotaka ije
8. Masikini wanaamini kutofika kesho, matajiri wanatumai kufika kesho bila kujari umri wao
9. Masikini wanajadiri kesho, matajiri wanawekeza kupata faida kesho.
10. Mabepari wanawekeza kesho kwa hofu ya watoto wao, wenye hekima wanawekeza kwa kizazi kijacho
11. Maisha unayoishi leo, ndiyo yatakuwa kesho yako; maisha ya kesho, yatakupa unachompa wewe leo.
12. Hakuna unachofanya leo, usivune kesho, na kile unachopanda leo, ndicho utakachovuna kesho
13. Maamuzi yako ya leo, ndiyo matokeo ya kesho.
14. Kesho hujaifika, iache siku itoshe kwa maovu yake
15. Usiseme nitafanya kesho hata mara moja, fanya sasa. Toa mchango sasa, panga mipango sasa, tekeleza sasa, kuwa muaminifu sasa, tenda mema sasa, jenga ndoa nzuri sasa, saidia watu sasa. Kuna watu wanatamani waume na wake zao wafufuke ili waweze kusema "nimekusamehe mume wangu, au nimekusamehe mke" ila haiwezi kutokea. Samehe leo, mpende mume au mke leo, fanya malenzi ya Mungu leo.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU KESHO.
Tengeneza picha kwenye kichwa chako, wewe ndiyo Yusuph upo gerezani kwa kosa la kusingiziwa. Unapelekwa kufanya kazi za gerezani, unateswa na mijeredi, unakula chakula cha gerezani, miaka mitano inafika na huoni hata wa kuja kukuona au ndugu yako kujua kuwa mzima. Futa wazo kuwa unajua nini kiliendelea kwa Yusuph, fikiria haupo kwenye hadithi  na si hadithi, fikiria ni tukio la kweri kwako; hivi nini mawazo yatakuja kichwani mwako mfano; "nitatoka kweri?, nitatokaje?, itakuwaje wakiniuwa?, au nimkane Mungu wangu?, au nijifanye Mmisri?" Maswari mengi najua yalikuwa ndani ya Yusuph mpaka kufikia hatua ya kuwaambia wale wafanyakazi wa Farao waliopata fursa ya kutoka "msinisahau..." Kwanini alikuwa akitafuta njia ya kutoka, alikuwa hajui kesho yake. Ukweli wa hadithi ni kwamba anayeifahami hadithi anafahamu nini kinaendereana nini kitatokea, tofauti na yule asiyejua hadithi au yule ambaye anaipitia hadithi hiyo.
Yusuph alikuwa hajui nini kitatokea, wewe unajua nini kilimtokea, sasa kuielewa zaidi hadithi hii inatakiwa uivae hadithi hii ya Yusuph na iwe kama wewe, ndipo utajua kuwa mtu anayepitia hajui kesho.
Masikini kwao kesho ni kitendawili kisichokuwa na majibu. Kwao kesho siyo siku yao, ni siku ya wengine, kwao kesho kufika ni 0/100. Na hivyo hakuna anayewaza kesho. Anapopata pesa ya kula siku hiyo, anafurahi na kuona siku hiyo ni ya bahati sana, anafunga kazi na kupumzika. Anafungua pochi mda wa kula ukifika, akimaliza kula analala, akingoja kesho apate tena wapi ya kula. Maisha yote ni mkono na mdomo. Kwanini hawazi kwa habari ya kesho.
Matajiri hawawazi kwa habari ya kesho sana japo hofu yao kubwa kwa habari ya kesho, ni kushuka kiuchumi na kurudi kuwa kama jana yaani wanaogopa kurudi kuwa masikini. Hivyo kundi hili ni kundi lisilojiamini na lenye hofu kubwa sana, kuhusu kesho, utofauti wao na masikini, wao hawawazi kutofika, bali wao wanawaza itakuwaje wakifika wakiwa wameshuka chini kiuchumi na kurudi kama jana. Na hii huwafanya kuwa watu waoga sana wanapokuwa katika siku ya leo. Uzuri wao ni watu wa kupanga sana kwa habari ya kesho. Mabepari wao kesho ni siku ya muhimu sana na hivyo hutumia pesa, nguvu na tekinolojia  kupanga kwa habari ya kesho, mabepari huwaza faida, huwaza masikini atabaki vipi kuwa masikini, siku zote anafikiri na kubashiri kinachowesa kutokea kesho.

Mabepari huwa ni watu wa kufikiri sana, nini kitatokea kesho: uchumi kushuka au kupanda, pesa kushuka au kupanda, biashara kushuka au kupanda. Siku zote wanawaza hayo ili wajue namna ya kushindana na soko.

Wajamaa, wao na serikari tu; mara zote hutumia mda kusoma magazeti na kutazama television kuona nini serikari imepanga kufanya kesho, huwa makini kujua mipango ya serikari ya mda mfupi na muda mrefu na hufatiria kama inatimia. Watu hawa hupatikana hata nchi za kibepari pia.
"Watu wajamaa huwa wanawaza sana serikari imefanya nini kuliko hata wao wamefanya nini"

Watu wa ufalme wa Mungu wao huwa hawakondi wala kukosa furaja kwasababu ya kesho. Wao hutafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, kisha haki yao waliyonayo katika ufalme wa Mungu humfanya mfalme wao ambaye ni Mungu Baba kuwatengenezea fulsa. Soma vizuri kuwatengenezea fulsa, huwaandalia mazingira, huwapa kibari, huwapa hekima na maarifa zitakazowasaidia kufanikiwa. Kama ndege wa angani alivyokuwa hana shamba, hana ghara la kuifadhi chakula, wala hana duka ila Baba wa mbinguni humlisha.
Ukifanya uchunguzi wa ndege utagundua kuwa, yeye hutoka kiotani akiwa na matumaini kuna sehemu nitakuta chakula, nitakula na kupata chakula cha watoto wangu. Tazama maua ya kondoni, hayalimi wala hayavuni ila hata Sulemani na fahari yake hajapata kuvikwa kama maua hayo. Mauwa ili yaoate chakula, huwa yanaamini yakishusha mizizi yake na kuchanua maua yake wakati wa mchana yatapata chakuka na mwanga.

Jambo la msingi kuhusu ndege, anatoka kiotani kwenda kuchukua chakula alipowekewa na Baba wa mbinguni.

Maua huwa yanatoa mzizi na kuchanua ili yapate chakula na mwanga.

Nini cha kujifunza Yesu hakusema watu wa Ufalme wa Mungu wasifanye kazi au wasitoke mlangoni mwao na kutazama fulsa na kuzitumia, Kama Ndege anavyotoka kiotani na kwenda sehemu ambapo anaamini Mungu wake wa Mbinguni amemuandalia chakula, ndivyo nawe pia utoke mlangoni ukatazame fulsa pale ambapo Baba yake wa mbinguni amekuandalia.
Kama vile mauwa yanavyotoa miziz yake na majani yake yakiamini kwamba Baba wa Mbinguni amewaandalia maji na mwanga wa jua kwa chakula. Tafuta mtandao tafuta mawazo tafuta marafiki tafuta watu ukiamini kuwa Baba yako wa mbinguni kuna fulsa amekuandalia.

Jifunze katika mfano wa Yesu, kama Baba wa mbinguni anayalisha maua na ndege wa angani, itakuwaje wewe ambaye alikubali mpaka hata kufa kwaajili yako. Kuna fulsa nyingi amekuandalia toka mlangoni si kwa hofu, toka nje kwa imani, ukiamini kuna fulsa amekuandalia leo kufikia mafanikio yako.
Tuma tema barua ya maombi ya kazi, nenda tena kuomba kazi, fanya juhudi mpya maana Baba wa Mbinguni amekuandalia fulsa za kutosha.

Acha hofu na kesho, tafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na mengine hayo Yesu amekuandalia, wewe tazama fulsa na usonge mbele.

Mfano; Mungu atatoa watu kutoka mashariki na magharibi ya mbali kukuletea fulsa. Mamajusi toka mashariki ya mbali ni uthibitisho tosha kuwa Bwana atafanya hilo.

Watu wa ufalme wa Mungu huwa hawana tatizo, kwasababu wao, wameamini Baba yao wa mbinguni anawajua wao, na anashughukika kuwa mema. Hivyo kwao kesho siyo kitendawili, bali Mungu wao ndiyo tumaini kuu na kati ya watu wanaowaza na kutumaini kesho njema ni watu wa kundi hili.

FIKRA HASI KUHUSU KESHO.
watu wengi wanaoishi maisha ya kushindwa huwa wanaangukia kwenye makundi haya mawili.
1. Wale wanaosema "nani anayajua ya kesho" hivyo wanaishi kama wanakufa usiku na wanaona kufika kesho ni asilimia 0, wanaona kesho ni kama makisio tu, ni kama siku isiyofikika. Cha ajabu wanajikuta wamefika, hawana hata pesa ya kuanzia, au hata sehemu ya kuanzia, wanatafuta pesa ya kula, wanakula wanalala huku wakiwa na asilimia 0 za kuamka, wanajikuta wanaamka. Maisha yao huwa ni ya kujaa taabu, utumwa, manung'uniko, kukosa tumaini, kuhangaika, hawana malengo, hawana akiba, wanakula wanalala na kuamka.

Nimewahi kuwa na rafiki yangu nikiwa O-Level: baba yake alikuwa ni mtu mwenye pesa, na kuwafanya kuishi sehemu za watu wenye pesa maarufu kama Kilakala kwa watu wanaotoka Morogoro. Baada ya baba yake kustaafu, maisha yao yalibadirika na kuwa maisha ya shida sana kipesa, siku moja alikosa fedha ya nauli ya kurudi nyumbani kwao kutokea na shule, akanifata na kuniomba nauli, kwa kicheko nikamjibu "tatizo baba zenu wanakumbuka kujenga kwa pesa za kustaafu, nyumba ikiisha na pesa zimekwisha mnakuwa masikini" siku ile hakunielewa lakini akisha kuwa mkubwa atanielewa.

Watu wengi wanatumia pesa zao za mshahara zote, na kuacha kupanga ya kesho, wakiona watakufa kesho, wanashangaa hawafi.
• Watu hawa hutafuta pesa za leo bila kupanga kuhusu kesho yao.
• Huwa hawafanyi majukumu yao, wakiamini kesho itawafanyia majukumu yao.
• hawana mipango
• hawana maono wala ndoto
 • hawana uwekezaji wowote
• hawasaidii watu wengine

2. Kundi la pili ni wale wanaoitafutia kesho maisha na siyo wao wenyewe".
Watu hawa huangaika na kuhangaika wakaiitafutia kesho chakula, mavazi, heshima na utukufu. Kumbuka nimesema "wakiitafautia kesho" siyo "wakijitafutia".

Kundi hili ni watu wenye hofu, mashaka, kuhangaika, na wengi huwa wanatumia mpaka njia ambazo si harari, njia hatarishi, dhuruma, ufisadi na rushwa, ili kutengeneza kesho yao. Watu hawa huishia kuitafutia kesho yao, na kusahau kujitafutia wenyewe maisha. Kuitafutia kesho haki na kusahau kujitafutia wewe haki, si mafanikio ni utumwa.
Mr Msofe alijitahidi kutafuta pesa kwa hari nyingi, aliuza bangi, madawa ya kulevya, akajiunga na rushwa za kuizurumu serikari na dhuruma nyingi akiihofu kesho yake, pesa nyingi alizopata aliweka akiba akiogopa kuteseka kesho yake; akajenga majumba na makampuni, alipomaliza kufanya yote sasa aanze kula faida, akavamiwa na majambazi wenzie akapigwa risasi akafa" Kesho inafaidika yeye ameenda na maji.

Patric the great kijana maarufu, akaenda kwa mganga ili apate utajiri, baada ya kupata utajiri, akaowa na kupata mtoto, baada ya miaka mitano akaumwa akafa, mke akapokonywa mari na ndugu wakatapanya mari zikaisha.

Mzee James ili kupata utajiri akaradhimika kuhudhuria kanisani siku ya jumaapili pekee na siku zingine alikataa kufunga duka lake ili aende kanisani, alipopata utajiri wa kuanza kufanya biashara nje ya nchi, akapata ajari akafa, ndugu wakatapanya mari na mke wake akaishi maisha ya shida.
Mr Tomson alipopata pesa zake za ajira yake ya kusafisha ofisi za watu, kufagia na kuzoa taka taka. Pesa alizopata aliziifadhi chini ya kitanda chake, akisema kesho nitazitumia katika uzee wangu. Siku moja akapata ajari ya gari kabla ya uzee wake, akafa. Hakuwa na ndugu maeneo yale, wakatangaza kwenye vyombo vya habari ili wapate ndugu zake, hakuna aliyejitokeza. Serikari ikachukua jukumu la kumzika. Walipoifungua nyumba yake, wakakuta Dola zaidi ya milioni kumi na tano. Mr Tomson aliishi maisha ya kimasikini sana, kila mtu aliyesikia habari ya kukutwa kwa pesa zile na maisha ya Tomson kila mtu alihuzunika. Kwanini alitafuta maisha ya kesho akasahau kuyatafutia maisha yake.
• Watu wa kundi hili hutumia pesa nyingi kuweka akiba na si kuzalisha pesa zingine
• watu hawa hutumia mda mwingi kujenga ya kesho kuliko kujenga maisha yao, wakihofu kushuka kiuchumi zaidi kuliko kushuka kwa maisha yao, wakihofu vipi fulani akinipita
• watu kama hao ni waoga sana kwa habari ya kesho. Huwa hawana amani siku zote. Wanahofu sana kuwa wasipotafuta leo kesho watateseka sana.
• watu kama hawa, huishi kama masikini wakihifadhi na kutafuta ya kesho. Husema moyoni mwao heri nilale njaa leo, kesho nitashiba na kusaza.
Robert Kiyosaki amewahi sema "haina maana kuishi masikini na kufa tajiri"

Watu wengi wanaishi kama masikini wakisema wanahifadhi, wanajikuta wanaishi masikini nankufa tajiri wakiwaacha watoto na ndugu zao kama Fisi wakigombea mari zao. Unahitaji kujipanga.

"Jenga ufalme wa mbinguni ambapo mwivi wala kutu haviwezi kuharibu"

Kesho ni mda wa mbere ambao Mungu ameundaa kwaajili yako. Na ana mpango na wewe, anachotaka ni wewe kutafuta ufalme wake na haki yake, kisha mengine utazidishiwa. Kwa maana ndogo fanya nafasi yako na umuache Mungu afanye nafasi yake.

FIKRA SAHIHI KUHUSU KESHO

Usikose sehemu ya sita tukizungumzi fikra sahihi kuhusu kesho.
Asante kwa kusoma naamini Roho mtakatifu hajakuangusha, neno hili ni ya hai na linaponya soma vema hata mara mbili ili uelewa
Uliza swali aunacha comment na share ili unisaidie somo hili kufika na kwa wengine.
MUNGU AKUBARIKI
From Holy Spiri

Monday, December 7, 2015

KUFIKIA UKAMILIFU WA YESU KRISTO

KUFIKIA UKAMILIFU WA KRISTO


Utofauti wa Mungu na wanadamu katika kuona vitu,
1. Mwanadamu anaona mwanzo kisha mwisho, Mungu anaona mwisho kisha anarudi mwanzo na kupanga namna ya kufika mwisho

2. Mwanadamu anaona nje na kuweka hitimisho, Mungu anatazama ndani kwanza kisha anafanya cha ndani kuonekana nje.

3. Mwanadamu anatazama kitu, Mungu anatazama matokeo ya kitu

4. Mwanadamu anatazama mwisho wa kitu Mungu anatazama baada ya mwisho.

5. Siku zote Mwisho wa mwanadamu ndiyo mwanzo wa Mungu

6. Ana heri yule ajuaye mawazo ya Mungu kuliko yule ajuaye matendo, ishara na miujuza ya Mungu
I.e ana heri yule amjuaye Mungu kuliko yule anayejua matendo ya Mungu.

7. Kila anayetaka kuwa hodari wa imani kwanza lazima ajue mawazo ya Mungu na Mungu mwenyewe

8. Imani huonekana tu mahari ambapo hapana majibu
Kama sehemu ina majibu hapo siyo imani

9. Imani ni kuamini kitu ambacho hujawai kuona kutokea.
Mfano wa Martha

10. Kufikia ukamilifu wa Kristo ni kufikia kwenye imani ya Kristo

11. Imani ni kufika wakati wa ulichosoma kwenye neno na kuhubiliwa unakuta ni tofauti kwenye maisha halisi

12. Mungu hufanya na huruhusu kila kitu kwa kusudi lake.

13. Mungu unayemtumikia hayupo kukuepusha usipate matatizo, mjaribu, kushindwa, udhaifu, na majaribu bali yupo ili akupitishe katika hayo kwaajili ya utukufu wake.

14. Unapombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.

Usiogope unapopitia hayo, maana ni Mungu wako amekupitisha.
Kama ukitaka kuwa na Mungu anayekuepusha na majaribu basi 80% ya Biblia ilipaswa tuitoe, maana asilimia zaidi ya asilimia 80 ya Biblia ni hadithi za watu waliopitia mateso na majaribu, kuanzia mwanzo mpaka ufunuo
Na kipimo cha wewe kuwekwa kwenye Biblia ni kupitishwa kwenye majaribu, mateso na udhaifu
Ibrahimu hazai
Mussa hajuo kuongea
Yakobo mwongo, mwizi
Esau mwoga wa njaa
Gideoni mwoga
Samson mdhaifu kwa wanawake
.......................

Yoh 16:33

Mara nyingi ndani ya ibada na makongamano mengi ya watu waliookoka tumekuwa tukifundishwa imani ya matendo ya Mungu
Yeye atafanya njia
Yeye atakuwa nawe
Yeye atakutetea
Ataponya nyumba yako
Hakuna uchawi wala uganga nyumba ya Israel
Atakuwa nawe daima
N.k

Lakini wengi tumeshangaa kuona tulichoamini na tunachokiona ni tofauti
Tulichosoma kwenye Biblia na kinachotokea kwenye maisha halisi ni tofauti
Tulichohubiliwa na tunachokiona ni tofauti

Unafika wakati
Familia uliyoamini inafunikwa na Mungu; mke anasumbua, mume anasumbua, mtoto anakuletea mimba
Ulivyoamini kuwa hatutakopa tutakopesha, unakuta ni tofauti, una madeni na mengine yanaongezeka

Uliamini hakuna uchawi juu ya Israel wala magonjwa ya kutisha, unashangaa anatoka kuumwa mume anakuja mtoto, usiku vita vya kichawi haviishi

Uliamini kutawara si kutawalia, unajikuta unatawaliwa na kuhama chini ya utawara wa bosi huyu na bosi huyu.

Uliamini kwa mikutano na kushuhudia na kulitangaza Jina la Yesu watu watajaa maelfu kwa maelfu kanisani unakuta katika maisha halisi hata mtoto haokoki na hata mtoto wako pia hajaokoka.

Leo tunaongelea imani ambayo unafika wakati hata neno uliloliamini halitokei
Mungu aliyemwamini humuoni
Mahubiri uliyoamini hayatokei

Maombi unaomba tena kwa kufanya kwa kujidhiki na kushirikisha na wengine lakini ndiyo kwanza mambo yanaongezeka kuwa magumu na majibu kutoonekana

Unaomba kwa ushahidi wa vifungu, lakini hakuna majibu

Imani wakati ambapo nini unaamini ni tofauti na unachoona katika maisha halisi.
..............................


Yesu anapowaaga wanafunzi wake,
Anaamua kuweka hitimisho/conclusion ya maisha yake yote toka anazaliwa mpaka anaenda kuteswa mpaka anapaa mbinguni, kwa kutumia sentensi moja tu

"Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu"

Luka 2:52 anamtambulisha Yesu tofauti na yeye anavyosema
Si kwamba alikosea Luka anamtambulisha Yesu wakati ana miaka 1-30

Luka anasema "naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu"

Katika umri wa miaka 1-30 Yesu akafurahia maisha yale, akaona ulimwengu huu mwema sana.

Hivyo ndivyo kwa wengi wetu, tulipozaliwa, wakati wa utoto tuliitazama dunia katika uwema sana, ukiamka asubuhi baba ameshaacha pesa ya kula shule nyumbani
Kitu kikiisha unasema tu mama au baba analeta
Ukaishi pasipo kujua ulimwengu halisi aliouongelea Yesu kwenye Yohana 16:33

Tambua kuna kuwa
1. NJE YA ULIMWENGU
2. Na kuwa NDANI YA ULIMWENGU

Wakati ule ulikuwa nje ya ulimwengu, wala ulikuwa hujui kinachowapata wazazi wako ndani ya ulimwengu

Wazazi Wakija sebureni wanacheka, unaona yes ngoja nikue kumbe maisha ni furaha, ukiongezeka umri unafurahi sana maana unatamani kufikia ukubwa kama wao ili ujitegemee.

Unapanda darasa na kumaliza shule unafurahi sana, unaolewa na kupata kazi unafurahi

Sasa mchezo unaanza unapotoka nje ya ulimwengu na kuingia ndani yake, na kukuta maisha ya ndani ya ulimwengu ni tofauti na ulivyokuwa unafikiri ukiwa mtoto kwa wazazi (nje ya ulimwengu)

Ulikuwa unasikia maisha magumu, sasa una yaishi hayo maisha.
Ulihadisiwa kuna kupitia majaribu sasa unapitia
Ulihadisiwa sana kwa habari za matatizo ya ndoa ya fulani na fulani na kuna wakati ukawaona wazembe sasa unapitia
Ukamuona mtu anafukuzwa kazi, ukasema mzembe, sasa unapitia

Ukamuona mtu hana kazi yuko nyumbani sasa unapitia

Ulikuwa ukiona tu baba anamfukuza mpangaji ukaona mpangaji mzembe anakunyimia fedha ya shule, leo ndiyo unaishi maisha ya kushindwa kulipa kodi

Hooooo
Unachanganyikiwa
Na kusema waoooh! This is the world

Yesu alipopitia maisha ya kukubaliwa, akawa akifurahi na kucheka na mama yake, na kuuliza je mkate si bora kuliko neno litokalo kwa Bwana?
Anakutana na Wakuu wa hekelu na kujadiri nao neno la Mungu akiwauliza maswali na wakimsifu sana.
Anafurahi kujenge meza na vitu na makochi akiwa seremara

Anafika miaka 30 na kuingia ndani ya ulimwenguni.

Anaona wao this is a world my mumy live?

Anaona walimu alioshiriki nao neno la Mungu hekaluni ndiyo hao hao anafika hekaluni wanamkataa

Watu walioona akiponya na kuwafanyia ishara na miujiza mbele yao ndiyo hao wanasema asurubiwe

Akaona waaooo! Kumbe nje ya ulimwengu ni tofauti na ndani ya ulimwengu.

Rafiki zako wa utotoni uliohisi watakutetea ndiyo hao watakusaidia mahakamani ndiyo hao wanasema afungwe, watu uliowahi hata kuwasaidia walipokuwa na shida leo kwako wanasema afungwe, watu walioona wema wako, leo wanasema mwongo mwizi huyo.

watu uliofikiri watakuwa ndiyo washirika wa kwanza kwenye kanisa ulilolianzisha, ndiyo hao wanakuwa wa kwanza kusema hukuitwa

Watu uliotegemea kukusaidia kutoka kimaisha leo wanasema hatuwezi, hata hawataki kuwa karibu na wewe.

Yesu anaona wanafunzi wake waliompenda sana na kumuita rabi, mfalme, na Mungu akawatambulisha ni mwanangu mpendwa, na kuwa naye mpaka kwenye dhiki na kuwafanyia miujiza baharini
Ndiyo hao hao wengine wanamsaliti, na wengine wanakimbia hawataki hata kuona anavyosurubiwa

Wanafunzi wengine waliomfata zaidi ya 15000 na kula mikate na samaki wa miujiza, hao ndiyo wa kwanza kupiga kerere msurubishe

Hii inatisha

Yesu anashangaa Baba yake yaani MUNGU BABA ambaye alipata kibari kwake na hata mara kadhaa akasema kuwa "Huyu Ni Mwanangu Mpendwa Msikilizeni Yeye" ambaye Yeye huwa tunategemea huonekana wakati wa mateso, hasa wakati ambapo tumechoka hatuna jibu, Yeye huleta jibu, huyo naye anafika katika hatima ya mwisho ya angalau kupata tumaini kwake au hata neno la kufariji, huyo naye anamuacha, Yesu akaseme "Eloi Eloi Lama Sabaktani"

"Ukifika wakati wa kukomazwa kiroho na Mungu, kuna wakati anakaa kimya ili kukufundisha imani ya kumtumaini na kumpenda Yeye na si vitu akupavyo"

Yesu anafika msalabani, hakuna tumaini tena ni kifo tu kinamngoja, anatazama kulia na kushoto haoni msaada zaidi ya mama yake tu analia, anaona kama hawa wameniacha sawa, anaamua kumtazama Baba yake juu

My God!!!!!!
Anaona afadhari hata ya hawa ambao wamejificha lakini angalau wanamuangalia, anamuona Baba yake amegeuza shingo hataki hata kumuangalia

Na kumbuka Yoh 16:31-32

Huyo ndiye Baba ambaye alijidai kwa wanafunzi wake na kuamini wakimuacha wao, Yeye  atakuwa naye

Huu ndiyo wakati wa kuonesha imani

Yesu anafikiwa Na wamama wanampa maji huku wakilia, Yesu anawatazama,

Tazama sasa baada ya Yeye kujionea huruma anawaonea huruma wao
WHY? Anatazama ikiwa Yeye Mungu na mwana wa Mungu na dunia imemuonesha dhiki namna ile, itakuwaje kwa mti mkavu. Twende pamoja usichukuzwe.

Yesu anawaambia msinililie mimi, mimi ndiyo naelekea mwisho na nikitoka mwisho naelekea upande wa pili wa ushindi na kuitwa mfalme wa wafalme
Jililieni ninyi na watoto wenu, ikiwa dunia wamenitenda mimi mti mbichi itakuwaje kwenu

Kwa maana nyingine Yesu anawaambia ndiyo mmenifata lakini kuna wakati mtaona mlichosikia na kuamini viko tofauti, mtaona dhiki, umasikini, uadui na kukataliwa

Yesu akiwa msalabani kwa machozi anaita Eloi Eloi Lama sabaktani, Mungu wangu mbona umeniacha

Yesu anafika wakati haoni jibu, anapanga kete na kupanga, weka mawazo na kuweka, panga na kupangua
Omba na machozi ya damu
Anatazama msaada wa wanafunzi wake haoni jibu, wote wamelala
Kuna wakati miimili ya kukusaidi watalala, watakuacha peke yako
Anarudi kuomba Mungu haji,

Luka 22:43-44 anasema akiwa katika dhiki, malaika akaja kumtia nguvu
Lakini baada ya uchungu kupotea, ndiyo kwanza unaongezeka baada ya machozi ya maji sasa machozi ya damu, anaomba na kuomba Baba amuepushie kikombe kile inashindikana, panga na kupangua

Alafu ebu fikiri, Yesu alikuwa anaomba kikombe kimuepuke, badala ya Mungu Baba kuepusha kikombe, eti anamtuma malaika aje kumtia nguvu. Lile halikuwa jibu Yesu aliloenda kuomba mwanzo, alitaka kikombe kimuepuke, malaika anakuja kumtia nguvu.

"Kuna wakati Mungu atataka upite jangwana ili akufundishe kitu, wakati huo hutohitaji kutoka, utahitaji kutiwa moyo, lengo ni umalize somo"

Yesu akasema "ikiwa ni mapenzi yako" wakati huo utahitaji kutiwa moyo na mapenzi ya Mungu lazima kutimia"

Je umewahi pitia jaribu, unaomba na kuomba Mungu alifanyie hata wepesi, unafika hata kufunga tatu mpaka nne kavu lakini wapi bora ungekula tu....
Ita na watu wanakusaidia kufunga, wanakushauri lakini wapi ndiyo kwanza linazidi come on... Machozi ya maji yanabadirika sasa unaamia kilio cha kwikwi moyo wako umekata tamaa

Unapanga kete hazipangiki, unapanga hazipangingi, shauriwa na kushauliwa kama wanakuchelewesha tu
Ita mke, marafiki, wachungaji hakuna msaada.

Hapo ndipo imani ninayoongelea hapa inatumika

Wakati ambapo Biblia inasema nitafanya mlango wa kutokea alafu ndiyo unaona hata dirisha dogo ulilokuwa unatazamia kupenya hapo nalo limefunga
Haleluya

Yesu alipoona hii ngoma nzito
Akaamua anyoshe mikono juu
Akasema kwa imani "Ee Baba ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu bali ni mapenzi yako yatendeka"

Nenda hapa utanielewa

Yoh 11:4
Yesu analetewa habari ya Lazaro kutoka kwa maumbu yake yaani Mariamu na Martha, Yesu anajibu tofauti na matarajio ya mwanadamu awaye yeyote duniani

Anawaambia "naye Yesu aliposikia, alisema Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwaajili ya utukufu wa Mungu, ili mwana wa Mungu atukuzwe"

Kumbuka Yesu ni mponyaji na Lazaro ni rafiki yake, na Lazaro anakujua kuwa Yesu ni mponyaji hivyo tu kujua kuwa ana taarifa ni faraja tosha.

lakini haendi

Cha kufurahisha hakuna aliyehoji, wala Martha hakuwatuma tena watu, wala hakuja mwenyewe
Lazaro rafiki yake Yesu aliyekuwa akishuudia Yesu akifufua wafu na kuponya viwete na kwa moyo wote akaamini

Leo Yesu anataka kumfundisha kumjua si kuona miujiza
Lazaro anaita msaada, lakini hauji mpaka anafika mwisho, anakufa

Najua umewahi kufika wakati, umemuita Bwana na kuona yu kimya hata unaoomba nao ukafika wakati ukawaambia Mungu amekaa kimya, pamoja na shutuma bado Mzee wa siku anakaa kimya
Nyumba unafukizwa, watoto wanarudi nyumbani, fedha ya kula tu ni tatizo, ada je
Unaomba sana, leo unazika huyu, kesho mwanao wa kike anakuletea mimba, na mtaa mzima wanajua ni mlokole na unajisifu kuhusu wokovu wa wanao
Yesu amekaa kimya

Nazungumzia imani ambayo hata wakati unaona mwisho wa mambo yote yenyewe bado inaamini, wewe siyo wa kwanza, kufika wakati kuchoka

Martha anafika wakati amechoka, Anamtazama Yesu, Yesu hatokei, anajipa moyo
Mwisho anaona ndugu yake hawezi kabisa na mwili unaacha roho, ohooo hapo ndipo anachoka na kuona sasa imekwisha

Najua umewahi fika wakati huo, wakati ambao unaamini na umesoma kwenye Biblia ndiyo wakati wa Bwana kutokea
Unaona ndiyo kwanza hata maombi hayana uwepo wake, ni makavu kama hujaokoka
Unajiona labda una dhambi, unaanza kutubu, yote pia ni kama unasema hewani
Hiyo ndiyo imani ninayoiongelea hapa

Lazaro amekufa, Martha anawaza Yesu atakuja kumfufua, mpaka wanazika haji
Come on, je bado unayo imani? Unapofika nyakati hizi.

Martha anakata tamaa, wanamzika Lazaro
Martha amekwisha, tatizo sasa ni basi
Yesu ndipo anatokea
Martha anamwambia Bwana umechelewa kuja mtoto ameshafukuzwa shule,

mke wako ndiyo amepinda tayari asikii wala haambiliki, amesharudi kwao tayari, hata kitanda kila mtu na chake
Anaumwa kabaki mifupa
Biashara na fremu tumesharudisha
Chumba na vyombo tulitoa nje hukuja, sasa na kuuza tumeuza vyote tumerudi kwa wazazi kuomba hifadhi, kama ni aibu tumeshaipata
Wakati alisema atatufichia aibu, ni masikini tayari, na huduma nimeshaacha, chuo nimesha Disco, sina ada; Yesu ndiyo unakuja, umeshachelewa.

Je umewahi pita wakati Yesu anakuja kujibu maombi yako too late (ameshachelewa) na ulivyotarajia.

Yesu anamwambia

"Sikukwambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu".

Naongelea imani ambayo, bado unaamini wakati uliyosoma kwenye Biblia ni tofauti na unavyoona kwenye maisha halisi

Yesu alikuwa anataka Martha asiishie kumpima Yesu kwa vilema na viwete na wafu waliokufa asubuhi mchana anawafufua, alitaka asimpime katika ufufuo wa wafu pekee katika siku ya mwisho, kuna kiwango cha imani alitaka kumpeleka.

Jiulize Kiwango gani Mungu anataka kukupeleka?

Ipo level ambayo unamwamini Mungu, mruhusu Mungu akuonesha anaweza fanya zaidi ya hapo ulipo, zaidi ya aliyowahi kukufanyia, muache akuoneshe anaweza zaidi ya ulivyoona zaidi ya ulivyoamini.

Alitaka ajue Utukufu wa Mungu ni mkuu sana pale ambapo hakuna majibu, pale ambapo akiri za mwanadamu haziwezi endelea mbele tena. Anachoka

"Lolote linafanyika kwako ni kwa utukufu wa Mungu, ambao huonekana baada ya kufika mwisho"

Lazaro anateseka, Martha analia, kumbe Mungu anajua mwisho wa jambo kabla hata ya mwanzo na ameweka kwa utukufu wake.

Yesu anapotazama, mateso na machozi yale anakumbuka kuwa Baba yake huwa anatenda mwisho wa akili za wanadamu.

"Unapombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.

Yesu ananyosha mikono juu
Na kusema ikiwa ni mapenzi yako na yatendeke

Na hii ndiyo imani
Wakati ambao huna majibu ya mambo unayopitia,

kama kweli una imani na Mungu na si kanisa, si mchungaji
Unaona marafiki, washirika, ndugu na wote wamesimama kushoto wanakutaza na hawana msaada kwako wowote huo ndiyo wakati wa kuonesha imani yako
Wakati wa Kuacha Mapenzi ya Mungu na yatendeke

Biblia inasema katika
Ebrania 12:1-3

"Yesu kwajili ya furaha aliyowekewa mbele aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu"

Hivyo tunapoongelea ukamilifu wa Kristo tunaongelea pale mtu anapofika wakati hayatazami mateso yake, hatazami kushindwa, hatazami kukataliwa, bali anatazama furaha iliyoko mbele yake, furaha iliyo ndani ya jaribu hilo

Hivyo imani ni kutazama ya mbele na kuyafumbia macho ya sasa hata kama Mbele imefunikwa na kiza kinene, haionekani, inaona ulipo ndiyo mwisho
Uko tayari hata kufa hivyo hivyo ulivyo

"Imani ni kupika hatua pale ambapo huoni mwisho wa ngazi" Martin Luther King Jr

Na ukayafumbia macho na kutazama mbele, kwa kutokuitazama aibu ya sasa, hiyo ndiyo imani na ndiyo iliyokamilifu katika Kristo

1. Naongelea wakati ambao Yakobo amechoka, na Mbingu zinafunuka na kugundua kumbe pale alipo kuna Mungu
Wakati ambao katika hari ya kushindikana kabisa, na kuona Mungu amekuacha, unakuja kugundua kumbe Mungu yupo hapo ulipo

2. Wakati ambapo imani yako inagoma kuamini, na inakuradhimu kuanza kushindana na imani yako
1 Timothy 6:12
Imani yako inagoma kuamini, lakini wewe unashindana nayo na kuishinda mpaka inaamini

3. Wakati wa kutazama mwisho na kuona furaha uliyowekewa mbele kisha kurudi mwanzo na kuona unatokaje ulipo

4. Ni wakati wa kuwa na subira na saburi na kusubiri kuyaona mapenzi ya Baba wa Mbinguni
Huu ndiyo ukamilifu wa Kristo

Waooooo

Mungu alibariki neno lake
Kristo neema yako iwe nawe
Roho mtakatifu awe ushirika nawe unaposoma ujumbe huu
Mungu uwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja nami katika kuandaa ujumbe huu, kuufundisha makanisa kadhaa na leo kuuandika kwako.


From the Holy Spirit
Written by Ev. Ulenje Mwaipungu.

Saturday, December 5, 2015

SEHEMU YA TANO: BARAKA TANO ZA PETRO FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA

FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA

Unaweza kubadiri jana yako na ukawa tajiri wa kesho.
Fanya hivi

"Tendo unachopaswa kutenda, usitende usichopaswa kutenda"

FIKRA NNE TOFAUTI KUHUSU JANA

A. Kundi la Watu ambao Huamini wanaweza kufuta makosa ya jana kwa kufanya zaidi leo.
Jim Rohn anakutana na binti akiuza maandazi ya aina tofauti, binti anamuonesha tabasamu zuri na kutangaza maandazi yake, Jim anapenda sana tabasamu la yule binti, na kwasababu alikuwa ni mpenzi sana wa maandazi ya aina ile, na tabasamu la binti akajikuta anavutiwa kununua.

“Huwezi kufanya usichoweza kufanya, kama hukujiandaa kufanya, wenye maandarizi bora ndiyo pekee wanaweza kufanya kwa ubora”

Jim akauliza bei, binti akamjibu kwa dharau akijua ni kiasi kidogo sana cha pesa "yapo maandazi ya rangi tofauti, na yote nayauza Dola $2 pekee”
Jim pia akakubaliana na binti pia kuwa ni kiasi kidogo sana, lakini kilichomkwamisha, akajitazama mfukoni hana kiasi hiko kidogo. Ndiyo ni kiasi kidogo ila ndiyo hana, Jim akafikiri "ni mtu mzima, ana familia, ana mtoto, anaishi Amerika, kwa aibu akalazimika kumdanganya, ili tu afiche aibu, akajibu kwa ujasiri wa kutengeneza "Nina maandazi mengi tu nimenunua, yanatosha kwa familia yangu"

“Tatizo laweza kuendelea kuwa tatizo, kama halitashughulikiwa kama tatizo”

Ficha tatizo ila si kwa wote, maana unahitaji Mungu, Fikra chanya, Maono, Ndoto, Kuona mbali na Watu ili ufanikiwe”

Binti alipotazama ujasiri wa Jim akaamini, akaondoka.
Lakini baada ya binti kuondoka, Jim anaingia ndani na ghafla akiri zinamjia, na kufikiri “Siwezi kuendelea kuishi namna hii”

Tukio moja likabadirisha maisha ya Jim Rohn, Jim Rohn akanyanyuka siku na kuwa milionea, mwalimu mhamasishi (Motivation Speaker), akazunguka karibu dunia yote akifundisha namna ya kufanikiwa na kuongeza ubora wao, Kila mtu alipenda kusikia japo neno lake moja, na katika maisha yake alipenda kusema"

"Usitamani iwe rahisi, tamani uwe bora”

Haikuwa rahisi, ila aliponyanyuka siku hiyo akaongeza ubora wa fahamu zake kuhusu kesho yake, na kusema SIWEZI KUENDELEA KUISHI MAISHA HAYA.
Maisha yake yakabadirika.

“Namna unavyoiona kesho, Ndivyo utakavyokuwa”

SWALI: nini kinakutia hasira leo, ni tukio gani linakupa hasira leo, ni dharau ipo inakupa hasira, nani kakunyima kazi, nani kakufukuza kazi, nani kakuibia, nani amezina mafanikio yako. Jibu lipo...

"Kisasi kizuri ni kuwa na mafanikio makubwa"

TAARIFA MUHIMU
Dunia imejaa matajiri ambao ni masikini wa jana. Na KESHO dunia itajaa matajiri ambao ni masikini wa leo" kama hauamini, Omba uhai, utaona. Lakini nakuombea uje kuwa wewe.

Nikupe siri kabla ya kusonga mbele: Kutafuta mafanikio ni kazi ngumu, ila kuwa masikini ni kazi ngumu zaidi"

Dunia imejawa na watu wenye furaha ya maisha, ndoa, kazi, wamejawa na maisha wanayopenda kuyaishi, lakini jana walikuwa wanaishi katika maisha wasiyoweza hata kuyahadithia. Yamejawa na aibu na matukio ya huzuni.
Pamoja na shuhuda za watu hawa ambao walikuwa masikini jana leo ni matajiri lakini nashangaa  bado bilioni ya watu duniani wanaishi maisha yao ya jana na kuiabudu leo hata kukata tamaa na kesho yao.

Jibu ni dogo... Kwanini unakata tamaa, kwani una hofu kama utafika, kwanini unaanza na kuanguka, unainuka na kuanguka...

JE WAJUA
1. Historia nyingi za watu waliofanikiwa zipo kwenye vitabu, na namna walivyofanikiwa, Cha ajabu matajiri ndiyo wanaosoma vitabu na vipeperushi, masikini hawasomi, na wengine wamebakia vile vile, walivyo jana ndivyo walivyo leo, kwanini?

2. Fikra za masikini kuwa jana yao ni matokeo ya mambo waliyofanyiwa na wengine, matokeo ya jinsi walivyo; "sina akiri, mimi ni kilema, mimi ni kipofu, mimi ni yatima, nilikosea kuowa, nilikosea kuchagua elimu hii, nilikosea kuchagua mtu wa kufanya naye biashara, serikari ilikuwa mbovu". Kundi hili huwa halikosi sababu.
Watalaumu serikari, wazazi walikuwa masikini, sina elimu, walimu walikuwa hawafundishi, wazazi hawakunipa mtaji, ndugu hawakunijari, uchaguzi haukuwa huru na haki, barabara mbovu.

Na hii huwafanya kutofikiri nini wanaweza kufanya leo.

3. Matajiri na watu waliofanikiwa hutumia semina na makongamano kufundisha masikini namna walivyofanikiwa. Cha ajabu hawaendi, ni matajiri tu ndiyo huenda.
"Unaweza kuifanya kesho yako kuwa njema, kama utaamua kuitumia leo yako vema.
Petro alitumia kila fulsa ya kuongea aliyoipata kutengeneza kesho yake njema.
Jibu la swali ni rahisi
Tajiri ana kuwa tajiri na masikini masikini, kwasababu tajiri ameamua kuwa tajiri na kujenga tabia ya kuwa tajiri.
Kutumia mda vizuri, kujifunza mbinu za kufanikiwa, kuona leo kama siku iliyipita na jana kama historia.
Wanatumia mda wao vema, wako smart.

B. Kundi la Watu ambao bado wanaishi Jana Yao.
Kundi la pili ni...
Kuna watu wengine wapo kwenye kundi lapili, wao wapo  dunia ya leo lakini bado wanaishi dunia ya jana. Bila kujari kipato ulicho nacho, hata kama ni tajiri ila kama bado unawaza yaliyotokea jana na kukufanya kuona leo huwezi fanya kitu basi bado unaishi jana, una fikra za masikini.
Kundi la watu wachache na waliofanikiwa, wanaoitwa matajiri,

"Hivi unadhani naweza kuwa mtakatifu? Huyu ni kijana anayejiuliza. Watu wengi bado wanaishi kwenye makosa waliyofanya jana, bado wanaishi kwa  kukumbuka waliyofanyiwa jana. Bado wanakumbuka yaliyotokea jana.
Na fikra hii huzaa maisha ya tabu, wanashindwa kufanya kitu chochote,  wanashindwa kutafuta fulsa, na hata zinapotokea wanashindwa kuzitumia, kwanini, bado wanawaza jana.
Asingeniibia fedha ningekuwa tajiri, haya ni mawazo ya kijana wa miaka 24-30, "mimi ni kijana mwema, nasari, natoa zaka, nasaidia masikini, nafanya kazi kwa bidii, lakini ni masikini. Muulize kwanini? Anajibu: "ndugu zangu hawanisaidii, baba yangu alikuwa masikini.
Haya yote ni mawazo ya jana. Badirika.
Acha kuwaza sababu toka nje, mafanikio yako ni kazi yako.

"Usisubiri wengine, fanya nafasi yako, na muache Mungu afanye nafasi yake"

Siku moja nimewahi kukutana na tajiri mmoja Mr. Mwacha nikapata fulsa ya kumshirikisha habari ya kumaliza chuo,  "mzee natafuta kazi ila kazi nyingi mshahara wake upo chini kweli" alinitazama, akacheka na kunijibu kwa ujasiri, neno lililobadirisha fikra yangu, akasema "hata ndege ili iruke lazima ianzie nyuma". Nikacheka ila nikaweka akirini. Baadae nikagundua, tajiri huwa anawaza jana alikuwa anarudi nyuma ili apae juu zaidi, huwa wao hawakati tamaa hata kama leo hana hata dola centi 25, bado anawaza kufanikiwa.

“Kufanikiwa ni kiwango unachoweza kwenda juu pale unapodondoka chini”

Masikini anawaza jana alirudi nyuma kwasababu yeye ni masikini, watu wanamuonea, jinsi alivyo: utaifa wake, rangi yake, ni kilema, ni Mwafrika mweusi, baba ni masikini.

C. Watu wengine Wao wanatazama tu serikari imefanya nini,
hawa ni watu wa takwimu na makabrasha, na mabingwa wa kusoma taarifa na si kanuni. Macho yao ni serikari ilifanya nini mpaka tupo hapa na haya yanatupata.

"Taarifa haiwezi kukuweka huru, kweli itakuweka huru"

Watu hawa Macho yao hutazama serikari ilitenda nini siyo wao walitenda nini. Petro hakuitwa Zelot kama Simoni, yeye hakutaka kupambana na Warumi, alihangaika kuongeza uwezo wake wa kuvua samaki, kuvua watu, kuhubiri injili, kufanya miujiza na mafanikio yakamfata. Haa walipopambana naye, hakupambana, alilinda tu Jina la Bwana.
Acha mambo ya kuifanya serikari mzazi; kutegemea ikurishe na kukupa maisha bora, kuwa mzazi wako binafsi na mhusika mkuu wa mafanikio yako.

"Hukumbukwa wale wanaotoa msaada kwa dunia, husahaulika wale wanaosaidiwa na dunia"

Martin Luther, Martin Luther King Jr, John Bunyan, Dr Living Stone, Abraham Lincolin, Mother Teresa, Albert Einstein, Musa, Yohana Mabatizaji, Paulo na Mkuu wa wote wa rohoni na wenye mwili Yesu Kristo:

Walipojitoa kuisaidia dunia hawakusahaulika. Acha kumlaumu mtu kushindwa kwako, angalia umekosea wapi, hata kama wamekutenda nini, bado unaweza kutumia hayo kwa mafanikio yako.

D. Kundi la Wafikiri Chanya.
Petro alifikiri chanya kila siku: akasema Bwana tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kingine cha Eliya na kingine cha Musa. Aliamini kuna kitu kitabadirika. Amini ukioata siku moja kukaa na Bwana kama Sulemani mambo yatabadirika.
Watu wa kundi hili ni watu watakaofanikiwa, kundi hili huwa wana amani na ni wakomboa mda saa zote, husahau waliyotenda jana na kutazama fulsa ya leo, na hutenda wakitazama nini wanapaswa kutenda leo.
Ni wachapa kazi wasiyopumzika, maana kwao jana hutosha kwa maovu yake, na faida zake, hata kama alifanya mambo makubwa ya kuushangaza ulimwengu, yeye anasahau na kutazama anayopaswa kuyatenda leo.
Hata kama jana alishindwa, yeye huamini leo ni SIKU MPYA NA FULSA MPYA. Wanatoka nje ya milango ya nyumba au geto zao na kwenda kutafuta fulsa, wanazitumia na kufanikiwa, hata kama watashindwa tena. Huendelea kuzitafuta fulsa zingine. Yaani wao hawakomi kutafuta na kuzitumia wanapozipata.

Mstari wa maisha: jana imeshapita, leo ni siku mpya na fulsa mpya, kesho yaweza kuwa nzuri zaidi ya jana.

FIKRA NZURI KUHUSU JANA
Nini kinatupa utofauti kuhusu jana, Tabia ndiyo inatupa utofauti wa fikra kuhusu jana. Fikra sahihi ni kufikiri:
1. Jifunze kutoka jana yako.
• Wapi ulikosea; usifanye tena
• Nini ulifanya kikakupa hasara: usifanye tena
• nini ulishindwa: ongeza uwezo na ufanye

“Usitamani ingekuwa rahisi, tamani uwe na uwezo" Jim Rohn.

2. Kubali ukweli
Kubali kuwa ulikosea, usipinge kila kitu, na ubadirike.

3. Usiruhusu jana kukuadhibu, itumie kwa faida yako.
Kwanini una huzunika, kwanini unasikitika, achana na hayo. Usiruhusu ikuadhibi, tumia mapito hayo kwa kufanya zaidi, hiyo ndiyo bora zaidi.

"Ana heri anaejari mwisho wake kuliko anayesumbuka na mwanzo wa shida”

4. Usihamishe uhusika wako kwa yeyote
Usiwaze kama ingekuwa hivi ningekuwa, waza kama ungekuwa hivi ingekuwa hivi. Usiseme baba angekuwa tajiri, ningekuwa tajiri, sema ningekuwa nina mipango na kusimamia mipango yangu ningekuwa tajiri. Petro hakusema Yesu bahari ni chafu hatujapata kitu, alisema Tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitazisha nyavu.

5. Ongeza uwezo
Petro aliposema kwa neno lako nitashusha nyavu, alimaanisha kukubali uwezo wake wa ndani ulikuwa mdogo, na kukubali kuwa uwezo wa Yesu ulikuwa mkubwa, hivyo kwa neno lake anashusha nyavu.
Ni mara ngapi katika jana yako umefanya kazi ya kuchosha pasipo matokeo chanya, kwanini ulishindwa, UWEZO WAKO WA NDANI ULIKUWA MDOGO.
Soma vitabu, sikiliza mafundisho, hudhuria semina, jifunze  kwa waliofanikiwa na kwa walioshindwa, ongeza uwezo wako wa ndani, kaaa karibu na waliofanikiwa, omba msaada kwako, kwa nguvu zao utafanikiwa.
Kumbuka Yesu alimwambia nini Petro "nitakufanya kuwa mvuvi wa watu"
Yesu hakutaka kumwambia Petro tatizo ni serikari ya Rumi, tatizo ni upepo au uwepo wa Mafarisayo na Masadukayo, akamwambia tatizo ni wewe, tatizo ni uwezo wako wa ndani, Yesu akatumia miaka mitatu kumfundisha Petro na kuongeza uwezo wake wa ndani, na akawa mtume kiongozi. Siku nilipoiona nyumba ya Petro kwenye dokomentari kuhusu maisha yake nilishangaa.

"Usitamani jana ingekuwa rahisi, tamani ungekuwa bora" Jim Rohn.

Leo nimemtumia sana Jim Rohn kwasababu natamani ujifunze kwake, mtu aliyeweza kupatwa na hasira na maisha yake ya jana, na kuweka ahadi ya kuibadirisha.

Tutaenderea...

Unafikiri ufanye nini kasahihisha jana yako
"Tenda unachotakiwa kutenda, Usitende usichotakiwa kutenda"

Somo lijalo tutaangalia hasa maana ya kesho na namna watu wanavyoitazama kesho. Na mwisho tutaangalia kuhusu leo, ambayo ndiyo lengo hasa la somo hili.

Tutajifunza Kanuni nyingi za msingi za namna ya kutumia leo.

Asante kwa kusoma, Mungu akubariki kwa mda wako.
Naamini ROHO MTAKATIFU AMEKUSAIDIA KWA SEHEMU.

Friday, November 20, 2015

SEHEMU YA NNE: BARAKA TANO ZA PETRO (KANUNI ZA KUTUMIA LEO YAKO)

MAISHA NI NINI

Hili ni zaidi ya swali, kila mtu anayeweza kupata mda wa kufikiri maisha yake (experience) atapata kusema kuhusu maisha.
Maisha ni neno gumu kujua.

“Unaweza kuwa na maana nyingi kuhusu maisha, ila mapito yatakwambia ukweli”

Hii ni sehemu ya nne ya somo letu, leo tutaangalia sana kuhusu maana ya leo, leo ni nini, pia tutaangalia fikra tofauti za watu na namna inavyoathiri kutumia leo yao.


Maisha ni mda, ni mda uliopimwa au usiopimwa, maisha hupimwa na mda. Na kama ni mda usiyoweza kuhesabika hayo ni maisha ya milele, na kama ni mda unaohesabika basi hiyo ni miaka ya kuishi.

Huwezi taja miaka ya Mungu, ila unaweza taja miaka yako, huwezi taja miaka ya mtu anayeishi milele.

Mda wa kuhesabu miaka ni ule unaokuwepo hapa duniani pekee, ukishaondoka na kufa basi sasa unaelekea kwenye maisha ya umilele, huwezi huko tena kuhesabu miaka. Maisha ya hapa duniani ya yanahesabika na kila mtu kapewa kwa kipimo maalumu

“Maisha ya hapa duniani ni mtihani wa kuona uwezo wetu wa kuishi milele”

Jinsi unavyotumia mda wako duniani, utavuna baada ya kufa” Hakimu wa Haki Yesu hatoangalia umeishi miaka mingapi, ataangalia umeishi vipi.

"Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe" Ayubu anazungumzia maisha ya mwanadamu kuwa siku zake zimeamriwa yaani zina kikomo na kikomo kimeshapangwa/kimeamriwa na tayari na kipo mikononi mwake.  "mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu, naye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa, hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe" Ayubu 14:1-2,5.

Nimetamani ujue kuwa siku zetu za kuishi hapa duniani zimepimwa, na zimeamriwa, zina mwanzo na zina mwisho.

Mwandishi wa Zaburi anamuomba Mungu "basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie hekima" Zaburi 90:12, alianza kusema "Bwana, unijulishe mwisho wangu, na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; nijue jinsi nilivyo dhaifu" Zaburi 39:4.

Hii yote yatuonesha maisha ya hapa duniani ni mda na kama mda una kipimo basi maisha yako yana kipimo na ipo siku yatafika mwisho,

Swali unaendaje na wakati huo uliopimwa, na unataka uwe umefanya nini ndani ya masaa hayo.

Nakuthibitishia kuwa wakati wako ukifika mwisho utaondoka tu hapa duniani
Usiwe kama Mfalme Hezekia, wakati wake ulipofika Mungu akamfata na kumwambia “atengeneze mambo ya nyumba yake, lakini Hezekia akatafsiri tofauti, Mungu hakuwa anamlaani bali anamtaarifu kiwa katika ugonjwa huo bado itakufa. Lakini alipoomba sana, Mungu ni msikivu akamsikia. Lakini kwa kuongeza siku hizo chache, Kwanza siku Hezekia akakosea, Biblia inasema baada ya kupona, hakumpa Mungu utukufu, akawaonesha wageni milki yote ya nyumba ya Israel, Sasa hezekia aliyeomba kuongezewa mda, unajua nini kilitokea tena, Hezekia akautumia ule mda kumzaa mtoto Manase, Manase akawa mfalme mbaya kuliko wafalme wote waliopita na waliyokuja katika israel.

Tumia mda wako vizuri...

“Nioneshe sababu nyingi za kushindwa maisha, mimi nitakuonesha moja, ni kughairisha.

Acha kughairi ghairi, kila siku nitafanya nitafanya. Sulemani anauliza E mvivu utaamka lini?
Anza kufanya leo jambo unaliona bado. Kuna wakati utafika hutoweza kufanya.

Usitumie mda wako mwingi kutaka kumpendeza kila mtu. Usitumie mda wako kujaribu kufanya kila kitu, jitambue wewe ni nani, umezaliwa kufanya nini na nini unapata hamasa kubwa unapofanya, pesa zitakufata mbele.
Kumbuka hadithi ya Martha na Mariamu. Martha akaanza kuhangaika hangaika akitaka kumpikia Kristo na kufanya kila jambo, Martha akatulia miguuni pa Yesu akimsikiliza; akaacha mengi na kushughulika na moja tu: Ufalme wa Mungu.

“Nioneshe sababu bilioni za mwanadamu kutotimiza kusudi lake, nitakuonesha moja tu, kujaribu kutaka kufanya kila kitu”

Tumia nusu ya miaka yako hapa duniani kufanyika mtu halisi uliyezaliwa kuwa, na tumia mda wako wa mwisho kufanya ulichozaliwa kuwa.

Andrew Carnegie baada ya kufa, walipoenda kwenye nyumba yake, wakapata karatasi ndogo. Mr Carnegie aliandika akiwa na miaka 20 “Nitatumia mda wangu wa mwanzo kuwa milionea, nitatumia nusu ya pili kugawa zote”.
Mr Carnegie alikusanya Dola za kimarekanj zaidi ya milioni 450 na anapokufa akawa amegawa zote.
Inaleta raha.

Usipoteze mda muhimu katika mambo yasiyo muhimu. Heshimu mda wako, watu wengi wanaotazama TV sana huwa hawaji kuonekana kwenye TV, wakoonekana si kwa mema.

Jim Rohn amewahi kumuuliza mtu, gharama ya TV, yule mtu akajibu $12 akamwambia hapana, gharama ya TV ni $12,000 kwa mwaka. Kwanini, watu wengi wanahesabau gharama ya kununua TV na siyo ya kutazama TV. Rafiki yangu kila kitu unachokipa mda, usisahau unakipa sehemu ya maisha yako. Maana mda ni maisha.

Twende pamoja, heshimu mda wako,  kwa maana ndogo kuheshimu dakika moja ni kuheshimu sehemu ya maisha yako.

Maisha yamegawanyika katika Jana, Leo na Kesho.

Lazima tuiheshimu jana, najua umefundishwa kutotazama jana. Lakini kutazama jana ni vema: tazama jana kwa namba ulizoongeza kwenye akaunti yako, thamani yako iliyoongezeka kwa Mungu na kwa jamii, tazama umefanya nini mpaka sasa, narudia tazama umefanya nini mpaka sasa?.

Kuna kanuni inasema utavuna ulichopanda. Kutazama jana inakusaidia kujua uliponda nini jana na ulipandaje na ulikuzaje; na maana ulivyo leo ni mavuno ya ulichopanda jana.

Tazama jana na ugeuze yote yaliyotokea kwako na yote uliyokosea na kupatia na kuyageuza kuwa falsafa na mbinu mpya ya mafanikio.

Yaliyotokea jana na uliyokosea jana yanaweza kufanywa na kuwa mbinu ya mafanikio ya leo. Unataka uthibitisho: jaribu.

Leo ni siku ya baraka: hakuna zawadi nzuri kama leo.

“Mtu anauliza, Je naweza kubarika, jibu rahisi; Ndiyo unaweza,
Anauliza lini sasa jibu rahisi siku utakayoamua kubadirika

Yaweza kuwa kesho; No! Mwambiye siku yoyote inayoitwa Leo.

Kesho ni ajabu; inaweza kuwa njema, inaleta tumaini, inaleta furaha.
Kwanini ukate tamaa wakati huijui kesho.

Tufatane pamoja ili tujue maana ya siku zote tatu: Jana, Leo na Kesho.

A. JANA
Jana ni sehemu ya mda ambao mtu ameutumia ndani ya kipimo cha maisha yake.
Jana ni marighafi au nguvu isiyoweza kurudi wala kuzalishwa tena. Jana ni sehemu ndogo sana ya mda uliyopewa na Mungu kuishi na kutimiza kusudi lake hapa duniani.
Wanafunzi wa chuo kikuu kimoja  cha hapa Tanzania, walijikuta kwenye wakati wa kununua moja ya vinywaji maarufu na vya gharama duniani kwa gharama ya kutupa, kwa bei ya hasara, kwanini zile bidhaa zilikuwa zinaelekea kuisha mda wake wa kuishi (expire date), baada ya mwezi mmoja zingekuwa zimeshaharibika. Jinsi bidhaa inavyokaa dukani ndivyo inavyozidi kutumia mda wake wa kuharibika na kutumika.

Jinsi binaadamu anavyotumia masaa 12 ya siku na kuingia masaa 12 ya siku nyingine ndivyo anavyozidi kuupunguza ule mda aliyowekewa au kuamriwa tayari na Mungu kama muandishi wa Zaburi alivyothibitisha, na ndivyo kweli.
Hivyo kama ulipewa siku 1000, 000 za kuishi hapa duniani, jana ulipoitumia sasa una 999,999, bila ubishi.

MAMBO YA MSINGI KUHUSU JANA
1. Huwezi kuigusa tena jana
2. Huwezi kufanya chochote ndani ya jana
3. Huwezi kusahihisha ulichofanya jana
5. Una nafasi ya kurekebisha matokeo ya uliyofanya jana pekee na si kufuta ulichofanya.
6. Jana ni historia, si hatima ya maisha yako.
7. Wakati wa msiba wako hawatakumbuka ulichotaka kufanya jana watakumbuka ulichofanya pekee.
8. Ulivyo leo ni matokeo ya uliyofanya jana
9. Kukumbuka na kuhuzunika ya jana ni kupoteza wakati, hekima ni kutazama nini unacho na unaweza fanya leo.
10. Jana inapaswa kutumika kama elimu tu ya leo, ulikosea wapi, ulikoseaje, na namna ya kurekebisha
11. Waliyokufanyia jana; unaweza kuyarekebisha leo
12. Leo ina nguvu zaidi ya jana.
13. Huwezi kuipata tena jana. Imepita

INAWEZEKANA...
Ndugu mpendwa inawezekana jana ulikuwa ni masikini sana, au hata leo, inawezeka jana umetenda dhambi, ninaposema jana nasema kwa wakati uliyopita iwe ni robo saa iliyopita au miaka kumi au hamsini iliyopita au sekunde moja iliyopita, inawezekana umekuwa mtumwa wa pesa, au inawezekana umekuwa ni yatima wazazi wamekufa, au una maisha hayo kwasababu ni mjane hivyo upo hivyo kwasabau ya uliyotebdewa jana, inawezeka upo hivyo kwasababu ya waliyokufanyia jana.
Inawezekana kampuni yako imeshuka kutoka na waliyokufanyia watu jana, washirika wa kampuni yako wamekusaliti, umepata hasara, umefanya uzembe fulani. Au namna yeyote ile.
Na sasa kuna maisha unayoishi, au kuna hari kampuni yako inapitia, lakini hiyo ni jana, tuzungumzie leo, itakusaidia kutoka maisha ya chini kuelekea maisha ya juu zaidi.

Usitazame jana, maadamu umeamka. Jifunze tu kanuni za kutumia leo yako vema.

Jifunze kanuni kuhusu leo.

Jana imepita achana nayo, jifunze tu ulikiseaje kupanda mbegu zako, au ulipanda mbegu gani. Panda mbegu njema sasa na uitunze na kuilinda mpaka iote na linda mazao mpaka uvune.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU JANA


Karibu tena Siku sehemu inayofata, tutaona fikra tofauti kuhusu jana na kuenderea na somo letu.

Asante kwa kusoma
Mungu akubariki.
Ev.Ulenje.

Tuesday, November 17, 2015

SEHEMU YA TATU: BARAKA TANO ZA PETRO

SEHEMU YA TATU
BARAKA TANO ZA PETRO

JINSI PETRO ALIVYOTUMIA LEO.

Leo tuangalie kiundani kuhusu Petro na uhusika wake katika maisha ya Yesu akiwa duniani. Na pia tuone namna Petro alivyoweza kutumia leo yake aliyopewa na Mungu kwa neema. Na tuone namna alipotoka na namna alivyoweza kubadiri maisha yake na namna alivyoweza kuendana na baraka alizopewa hata zikaweza kutimia.

UHUSIKA WA PETRO

Petro alikuwa Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi na muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.

Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvua samaki na si kukaa na familia.

2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.

3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.

4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumuokoa Kristo asiteswe na Wayahudi na kufa japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.

5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanazungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuwa hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.

6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20

7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 11 waliobaki. Siku zote alitazama “maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari”.

8. Petro aliwaza chanya siku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwahi ona kitendo hiko toka azaliwe, akaamini akaenda, alipoambiwa habari za wokovu kwa mataifa katika maono, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ya jana, na kuwaza positive.

9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.

10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.

11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
“Tunashinda woga kwa kufanya tunachokiogopa kufanya”
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
“Unataka uijue siku ya kuanza kufanikiwa KiMungu, ni siku utakayoanza kufikiri kwa habari ya wengine”

5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
Akimaanisha “mwanaume shujaa ni yule mwenye uwezo wa kusimama peke yake”

7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa za leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15

Zote hizi tutaziangalia kiundani na kuzichambua kiurahisi zaidi ili kila mtu afahamu.
Namna alivyozipata na namna zilivyomfikia na namna zilivyotimia kwake.
Ila kwanza tuangalie maana ya jana, leo na kesho kiundani na kimafunuo zaidi.


MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, rafiki yangu mmoja akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika na hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana,
Akanitazama kwa makini na kuniambia "unajua Ulenje nilikuwa na akiri zaidi hata yako", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Yule rafiki hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.

MDA NI NINI...
Mda una maana nyingi ila huwezi kupinga hii.
Kifupi Mda ni maisha
Mda ni maisha yenye mwanzo na mwisho.
Mda si wa milele kama maisha ya milele, maisha ya milele hayana mda, huwezi kuyapima, yenyewe ni ya milele, yapo na yanaendelea kuwepo.
Unapotamka mda unazungumzia kipimo chenye mwanzo na mwisho. Unapotamka maisha niliyokaa shule, unatamka mda uliyokaa shule, ukihesabu kuna kipimo. Unapotamka nina miaka sabini unatamka mda uliyokaa duniani ni miaka sabini. Hivyo mda ni maisha, yana kipimo, yana mwisho.
Yesu anasema "imetupasa kufanya kazi zake yeye aliyenipeleka (nani?, Mungu) maadamu ni mchana; usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi"

"Yesu alipokuja alipewa mda wa kukaa ulimwenguni, na ilimradhimu kukimbizana nao: kwanini mda una kipimo”.
Ukipewa kazi ya kufanya kwa siku moja, maana yake yake ni masaa 12.
Moja ya huzuni ambayo huwa naisikia kwa wazee na watu wazima wenye miaka juu ya 50 wengi kila ninapopata mda wa kukaa nao, huwa wanasema "tulitamani kufanya mengi sana, tulipokuwa vijana kama ninyi, ila mambo yakawa mengi tukashindwa". Kwanini mda umeisha, kwa wao kufanya hayo, walipewa mda wakajisahau wakadhani wana umilele. Ila lipo tumaini toka kwenye kitabu hiki, kuwa hata kama una miaka 80 bado inawezekana.
Bado kwako unayesoma kitabu hiki, una miaka 20, 30, 35,  40, 45, 50, 55, 60, 65, 70, au yeyote ndani ya hiyo; jua kuna wakati utafika hayo unayoyafikiri hutoweza kuyafanya, na yataishia kwenye fikra zako tu.

MAISHA NI NINI...



Fatana nami tutenderea...
UBARIKIWE KWA KUSOMA.
By EV.ULENJE MWAIPUNGU

Tuesday, October 20, 2015

SEHEMU YA PILI: BARAKA TANO ZA PETRO NA KANUNI KUMI ZA KUFIKIA MAFANIKIO YAKO.

Tunaendelea
Kwanza naomba amini maneno haya;

"Maadamu yu hai...
1. Unaweza songa mbere zaidi
2. Unaweza toka hapo ulipo
3. Unaweza kuwa mtu huru
4. Unaweza kuwa mtu uliyefikiri kuwa
5. Unaweza kuishi maisha ya mafanikio unayotaka kuishi
6. Unaweza kuacha historia nzuri katika ulimwengu huu
7. Unaweza kubadirika
8. Unaweza kubadiri tatizo lako kuwa neema
9. Unaweza kubadiri historia mbaya kuwa nzuri
10. Unaweza kuinua maono yako na kuyaanza tena na kuyatimiza.
11. Bado unaweza kuwa jasiri tena
12. Unaweza kuwa mtakatifu tena na mwenye haki
13. Unaweza kuwa mtumishi tena
14. Unaweza kufanya uliyowaza kuyafanya.

Bado unaweza....
Na "LEO" ndiyo siku pekee unayoweza kufanya maamuzi ya kufanya haya. Jana haikuwa siku sahihi, kesho haigusiki, na hatujui.


JANA IMEISHA, LEO NI SIKU MPYA,  KESHO YAWEZA NZURI ZAIDI YA LEO
Tangazo hili naomba liingie ndani yako. Soma mfululizo huu kwa umakini, soma kanuni kumi kwa umakini, baada ya kusoma vitabu vingi vya watu waliofanikiwa, na kuona, na kusikia wengi waliofanikiwa, kupitia Biblia na kusoma watu waliofanikiwa, na maisha yangu binafsi; nimekuja kugundua kanuni hufanya kazi kwa yeyote pasipo kujali kabila lake, dini yake, taifa lake, rangi yake, umri wake, nchi anayotoka, elimu yake, na wote waliofanikiwa waliishi maisha ya kushindwa kwanza, ila walipoamua kufata kanuni maisha yao yalibadirika, na nilichogundua hawakutumia miaka au miezi, walitumia siku moja kama dhahabu inayotoka kwa Mungu kwa neema, inaitwa leo.
Kanuni zikiheshimiwa huleta mafanikio, zikivunjwa huleta kushindwa, uamuzi ni wako, kazi ya karama ya mwandishi ni kupokea toka kwa Roho Mtakatifu na kuandika kwa utiifu wote bila kupunguza, kazi ya msomaji ni kusoma, kuamini na kutendea kazi.
Mimi naanza kufanya jukumu langu.

Wote tunakubali tunaishi kwenye dunia inayokubari mabadiriko, dunia inabadirishwa na wachache, dunia yenye wengi wanaoshangaa na kuhadithia mafanikio ya wengine, wachache ndiyo wamiliki wa mali za dunia, wengi ni watumishi na wateja wa hawa wachache, nani kazaliwa na kitu, hapana; wao wamevipata wapi? Hapa hapa duniani, na sisi twaweza kuvipata wapi? Hapa hapa duniani
Nianze kusema wote tumeumbwa ili tuwe wamiliki
Jambo la kwanza alilolifanya Mungu alipomuumba Adamu ni kumpa umiliki, akamwambia "ukataware" kutawara ni umiliki, huwezi kutawara vitu ambavyo havipo chini yako, soma mwanzo 9:2 Baada ya wanadamu kukosea na Mungu kuwaangamiza kwa Ghalika, Mungu anafanya agano jipya na Nuhu na neno la kwanza ni kummilikisha vitu vyote duniani, Mungu amekupa umiliki, lakini ni kumiliki kwa niaba yake, Yeye bado atabaki Bwana yaani Adon kwa Kiebrania, yaani mmiliki kwa kiswahili, Yeye yupo juu ya vyote, ila amempa mwanadamu ataware kwa niaba yake
Swali kwanini humiliki, kwanini umekuwa mteja na mfanyakazi wa hili kundi dogo la mabepari,
Ipo kanuni ya kuondoka ulipo na kurudi namna ya Mungu alivyokuumba.

Wana wa Israel walifurahi kwenda Misri wakati nchi yao ilipokumbwa na njaa yaani Kanaani, Yusuph akawapokea, Mungu alikuwa ameshaagana na Ibrahimu kuwa atakipeleka kizazi chake Misri na kuwa watumwa kwa miaka 400 kisha atawaokoa na kuwarudisha kwenye nchi aliyomwahidi Ibrahimu.
Wana wa Israel moja ya vitu ambavyo hawawezi kusahau ni kuwa watumwa ndani ya Misri kwa mda wa zaidi ya miaka 400.

Mtumwa ni mtu ambaye hufanya kitu pasipo kutaka/ pasipo kuwa na matakwa yake. Mtumwa huenda asipotaka, hufanya kazi asiyotaka, hula chakula asichotaka, hulala mda asiyotaka, hupumzika mda asiyotaka, huishi maisha asiyotaka, hulala mahari asipotaka, huvaa nguo asizotaka; kuwa mtumwa ni heri ya kutozaliwa.

Wana wa Israel najua walifika wakati wakasema ni heri tusingezaliwa.
Mtu asiyekuwa katika kundi la wamiliki wa mali na uchumi wa dunia hii; yawezekana ukawa mmoja wa hao, atakula chakula asichokitaka, atavaa nguo asizozitaka, atafanya kazi mpaka mda asiyoutaka, atafanya kazi asiyoitaka, atalala mahari asipopataka, atanunua vitu asivyovitaka, atalala mahari asipopataka, ataishi maisha asiyoyataka, huu ni utumwa, wengine katika sayari hii wamekuwa ni mtumwa wa kiwango kidogo cha pesa walichonacho; "Pesa ndiyo jawabubla mambo yote"

Mara ngapi umeingia kwenye mtihani wa shule au chuo, umejiandaa kwa kusoma, kila kifaa unacho, peni, rula, na umevaa nguo za kupendeza: unaingia ndani ya chumba cha mtihani, unakaa vizuri kwenye kiti, unafunua karatasi ya mtihani, na kukuta kichwani una asilimia 30 ya yale yaliyoulizwa, kati ya maswali 20 unayajua maswali saba tu, ina maana asilimia 70 ya mtihani hujui. Wewe unadhani majibu hayapo ya maswali hayo, ukitaka kujua majibu yapo, tazama wa kulia kwako utamuona anajibu mtihani kwa tabasamu akionesha kuyajua yote;
"si kwamba pesa kama haijibu mambo yote unayoyahitaji kwamba imepoteza uwezo wake wa kujibu, ila ni kwamba unazo chache, umekusanya chache, umezipata chache.
Kushindwa kujibu maswali yote hakuna maana kichwa chako hakina uwezo wa kujibu; ila hayo saba ndiyo ambayo uliyasoma na kuyaweka kichwani, kichwa hakiwezi kujibu zaidi ya uliyoyaweka ndani yake wakati unajisomea, ukilazimisha utakosa tu.
Ndivyo pesa ilivyo; siyo kwamba haiwezi kujibu mambo yote unayotaka; tatizo ni kwamba hizo ndizo ulizotafuta, hizo ndizo ulizopata, hizo ndizo ulizonazo.
Kama wenzio wananunua vitu vya gharama ya Laki tano, ndizo walizokusanya, wewe nguo ya 3000 ndiyo uliyokusanya, na huwezi zidi hapo. Kanuni ndani ya kitabu hiki zinataka kuondoka na utumwa huu wa na kuwa mmiliki na uwe na pesa zenye jawabu la mambo yote.
Mungu amenipa kanuni hizi ili tu utoke ulipo na uwe na kesho yenye furaha na ushuhuda.

Mbali na hapo kuna watu ni watumwa wa hari zao za maisha, waweza kuwa tajiri lakini ni mtumwa wa ndoa, furaha, amani na huishi unavyotaka kuishi, huoni faida ya pesa yako katika maisha yako ya kawaida. Kanuni hizi zitagusa huko pia.
Na mfululizo huu ni maalumu kwa kila mtu, kama ni tajiri, mjasiliamari, muwejezaji, na yeyote, kama unayo leo, kitabu hiki kitakupa mwanga wa kufanya zaidi; kama unaishi bado waweza kufanya zaidi, soma mfululizo huu ili tumshinde adui wa kufanya zaidi ambaye ni mafanikio yako uliyonayo.

PART ONE
sehemu hii hasa tutaangalia msingi wa somo letu, maana ya siku tatu (leo, jana na kesho), pia tutaangalia watu tofauti jinsi walivyotumia leo yao, na tutazama makundi muhimu, hasa wale ambao leo yao, imesababishwa na historia, matukio au sababu fulani kama kukisa elimu, yatima, mjane, kilema, n.k

SEHEHEMU YA KWANZA
MSINGI WA NENO

KANUNI: kanuni ni imani na sheria ambazo mtu huziamini na kuzisimamia na kuzifanya mwongozo wa maisha yake.
Kanuni ni za asiri si za kubuni, kanuni zimefanikiwa kufanya kazi kila mahari kwasababu ni za asiri. Mwanadamu ameumbiwa, kuzifata si hiyari ni lazima, kanuni hazina jaji, usipofata zinakuhukumu zenyewe, hapa hapa duniani.
Yesu alisema, Mimi sitowahukumu ila maneno yangu ndiyo  yatakayowahukumu"
Nimewahi kuwa na rafiki yangu miaka ya 2005 mpaka 2008, alikuwa ni mtu anayefanya vizuri sana toka tukiwa shule ya msingi, tulipofika sekondari alifanya vema toka kidato cha kwanza mpaka cha pili na alikuwa mbere yangu kimasomo, nilishangaa kidato cha tatu akaanza kuwa nyuma yangu, nilipochunguza alikuwa amejenga mahusiano ya kimapenzi na binti fulani ambaye kwa pale shule alikuwa ana historia ya kutembea na wavulana wengi, nikamfata na kujaribu kumshauri lakini alinijibu kuwa "acha ushamba dogo" nilipomng'ang'aniza akanijibu kwa kebehi "niache, kwani haya si maisha yangu" nikamuacha ila siku ile ile nakumbuka hata mama yangu nilimshirikisha kuwa "rafiki yangu unayemjua amebadirika na sijui kama atafauru".

Ilikuwa ni rahisi kujua kuwa hawezi kufauru kidato cha nne hata kama si nabii, kwanini alienda kinyume na kanuni. Kanuni haziitaji hakimu wala jaji, bali zenyewe ni za asiri, unapovunja zinakuvunja.
Mfano usinywe sumu, usizini, usilewe, usinywe sumu, usiwe mvivu, hizi ni moja ya sheria za asiri, unapovunja haihitaji hakimu, zinakuvunja hapo hapo.
Kumbuka Yesu kasema, ni heri msingesikia, lakini sasa mmesikia hukumu i juu yenu.
Unapovunja kanuni, unatupa ruhusa ya kujua mwisho wako wa majuto, unapojitoa na kufata kanuni, unatupa furaha ya kujua mwisho wako mzuri.
Msingi wa kitabu hiki si kukupa mawazo, ila nataka upate kanuni.
Sihofu umesoma vitabu vingapi na ukabaki kama ulivyo, mimi najali kuwa, kwa kusoma mfululizo huu hutabaki kama ulivyo.
Na kwa waliofanikiwa naamini utafanya vizuri zaidi maadamu bado unayo leo.

Tuanze na mdano wa Mpakwa mafuta wa Bwana Mungu, kuwatoa Israel toka utumwani Misri kwenda Kanaani.
Anatoka kutoka maisha ya anasa ndani ya ikulu ya Farao mpaka kuwa masihi wa Bwana. Na kuandika vitabu vitano muhimu kwenye Biblia, Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na KumbuKumbu la Torati.

KUTOKA14:13-14
"Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. 14. Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

Maneno ya msingi ya kuyakumbuka kila unaposoma mfululizo wa somo hili ni:
• msiogope simameni tu
• mkaone wokovu
• Bwana atakaowafanyia
• Wamisri mliowaona leo
• hamtawaona Wamisri tena milele
• mtanyamaza kimya

Toka hapa tunapata maneno ya msingi;
Mafanikio hutokana na...
• uhusika wa Mungu (atawapigania)
• uhusika wetu (simameni)
• waleta utumwa (wamisri)
• utumwa (kutofanya unayopenda)
• mafanikio ni vita (atawapigania)
• kusonga mbere hata kama umetoka utumwani/umefanikiwa
• no retreat no surrender/ hakuna kurudi nyuma wala kunyosha mikono juu ya kushindwa.
• maisha yanahitaji kukubari kwa imani ya wengine juu yako na juu ya unachokifanya,. Musa ilimradhimu kuwashawishi kwa maneno ya imani wana wa Israel ili tu wakubali jambo analotaka kulifanya.
• Watu ndiyo wa muhimu sana katika jambo lolote unalotaka kulifanya. Ishi na watu vizuri, sema nao vema, chukuliana nao vizuri, ishi nao kwa hekima, uhakikishe unapata wengi wa kukuunga mkono,
 “ni ngumu kukupenda wote, ila tu unawahitaji watu sahihi”.
• muache Mungu afanye sehemu yake, na usingoje afanye sehemu yako.
• usimuingilie Mungu sehemu yake na usingoje aingilie sehemu yako.
• Mungu akisema 'nenda' wewe nenda.
• ukianza safari usifikiri kurudi nyuma/ ukiaga kwenu usirudi.

Pia tunajifunza namna ya kutumia tatizo na kulifanya kuwa baraka na siyo tatizo;
Huwa napenda kuwaambia INAWEZEKANA... watu walipita kwenye sehemu ya mkwamo wa kusonga mbere kufanya jambo ambalo kwa mda huo li juu ya uwezo wao (impossible).
Rafiki yangu wa karibu nikiwa mtoto Mama mmoja, siwezi kumsahau, mume wake alipomuacha, na kumuachia mtoto mchanga na kwenda kuowa msichana mwingine, mda mwingi nilimuona na tabasamu na mwenye maneno ya kufariji na si mwenye uhitaji wa faraja, ukienda kumfarini utaishia kufarijiwa wewe, alikuwa ni mtu aliyeumba kichwa chake kuwa tayari kujifariji na kukabiri haiwezekani kuwa inawezekana, sasa yupo Kenya ana maisha mazuri.

Tunajifunza nini toka kwa Musa aliibadiri "haiwezekani kuwa inawezekana” ndani ya fikra yake na ya team yake yaani wana wa Israel, na imani iliyochipuka ikaungana na nguvu za Mungu na bahari ikagawanyika.

“Imani ndiyo njia pekee ya kutuunganisha na nguvu za Mungu”

1. Tambua tatizo mpaka hapo ulipo: Wamisri

2. Tambua kikwazo cha kufika unapotaka kufika: Bahari

3. Weka akiri zaidi kupata uhitaji, na uache kupoteza akiri kwenye tatizo, bali nini unataka; Musa alifikiri kuvuka ng'ambo si kurudi Misri.

4. Badiri fikra: ondoa hofu weka ujasiri

5. Tambua fikra za team yako na kuzishughulika: woga

6. Peleka akiri pa kupata usaidizi: Mungu

7. Tambua ushiriki wako, katika kuliondoa tatizo, ushiriki wa Mungu na wa timu yako: piga fimbo

8. Yakusanye matatizo yote na uyajue yote : Wamisri, Bahari, hofu yake na ya Waisrael, jangwa, hawana msaada.

9. Yatenge kwa utofauti wake na uyatatue kwa upekee wake: akaanza na Wana wa Israel kisha akaja Wamisri, akamalizia bahari, wakavuka.

10. Tengeneza mpango na mbinu nzuri ya kuyamaliza: Mungu akamtoa malaika aliyekuwa mbere yao na kumuweka nyuma, akaweza kiza kati ya Wamisri na mwanga kwa Israel ili kuwatenganisha.

11. Tembea katika imani huku ukimtazama Mungu; Musa alimwita Mungu na si mtu wa karibu, si Haruni wala Miriam, wala hakuanza kulia na kumueleza kila mtu.

12. Matatizo yasikufanye ukapunguza juhudi yako ya kusonga mbere: Musa hakupunguza munkari wa kwenda Kanaani, akaamnini Mungu atafanya lolote, saa yeyote.

13. Amini Fulsa, na jawabu inaweza kutokea saa yeyote na kwa namna yeyote: hawakufikiri kupasuka kwa bahari

14. Amini unaweza songa mbere zaidi: waliposikia wakapata moyo na nia, bahari ilipopasuka wakasonga mbere zaidi

15. Amini Mungu anaweza tokea mda wowote na kwa namna yeyote.

Alifanya kwa namna isiyoweza kufikilika kama angefanya vile, unaweza waza angeleta mtu alete maboti, au meri, au awauwe wa Wamisri kwa moto, hapana akawafanyia wasichofikiri.
Leo atafanya kwako. Kwa Jina la Yesu Kristo.

16. Weka suruhisho na siyo kukazana na ukubwa wa tatizo: Mungu alinishangaza hakuanza kuwakazia macho Wamisri, bali alikazia macho wao kusonga mbere, alikazia macho nini kinahitajika, na nini kifanyike wasonge mbele, hakutazama Wamisri.
Mungu akawapasulia njia, ndipo akawauwa Wamisri, kwa haraka utafikiri kwanini asingewauwa Wamisri, lakini alijua sasa akiwauwa, “enhee kwa wingi wao, wangepita wapi.
Leo hii Wamisri wanafananisha na utumwa wa pesa waliyokuwa nao wengi, na matatizo na changamoto nyingi ulizonazo.
Na kupasuka kuna maana ya usisimame ukaona umefika, bado hujammaliza adui, songa mbere, uhai wako, fulsa na nguvu ni kwamba bado unaweza songa mbere; shinda ugomvi wako na mafanikio uliyonayo ambayo yanakufanya usisonge mbere.

17: nini unahitaji kumaliza tatizo: Musa alihitaji fimbo ya kupiga maji yagawanyike. Na usiangalie mbali kwanza kupata kitu cha kumaliza tatizo, tazama kwanza nini unacho mkononi, nini unacho, kama ni kipawa, karama, au fedha kidogo, ndugu au rafiki wa karibu au watu sahihi. Tumia ulichonacho kwanza, na hivyo ulivyonavyo vitaleta unavyovihitaji kumaliza tatizo lako.
"Nyoka hatuanzi kummulika mbali, tunaanzia miguuni"

Tuendelee tena siku nyingine...
Karibu na ufurahie ufunuo wa siri za mbinguni kwa msaada wote wa Roho Mtakatifu.
Mungu awe nawe...

NAAMINI UMEBARIKIWA.
Bado tunaendelea
Fatana nami zaidi...

Saturday, October 17, 2015

BARAKA TANO ZA PETRO: JANA IMEKWISHA LEO NI SIKU MPYA, KESHO ITAKUWA NJEMA ZAIDI YA LEO.

BARAKA TANO ZA PETRO NA MAANA YA LEO, KESHO NA JANA.

UTANGULIZI
Jana Imekwisha, Leo ni Siku Mpya Kesho Yaweza kuwa Nzuri Zaidi ya Leo.
Huu ni mfulizo wa somo la muhimu sana kwa kila mtu, litakusaidia kutambua uko wapi na unaenda wapi, ni somo lililojaa kanuni za namna ya kuitumia leo yako kwa hekima na kuwa na Kesho nzuri. Somo litakupa kuelewa sehemu ya Mungu katika maisha yako na sehemu yako. Litaondoa maswali mengi kuhusu matumizi ya neema ya Mungu.
Mfululizo huu utamtazama Petro kwa kina: tabia zake, mitazamo yake, ucheshi wake, udhaifu na uimara wake na kutazama namna yote hayo alivyoweza kuyatumia hata kumfanya Yesu kwa neema akampa Baraka Tano na zote zikatimia. Na kutazama namna zinavyohusiana na maisha yetu ya leo na kujenga kesho yetu njema.

Nimetumia miaka mitatu sasa kuandaa somo hili. Na nitakayosema na wewe humu ni rasha rasha tu ya somo lenyewe ambalo lipo jikoni likioikwa zaidi kama kitabu.
Kwa msaada wa Roho mtakatifu mafunuo haya ya muhimu yameandikwa na kupewa uvuvio wa hari ya juu kubadiri maisha yako.
Fatana nami.

Tuanzie hapa, Safari ya kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine kwa kutumia gari la abiria ni wakati mzuri sana. Ni fanani ya safari maisha, MAISHA YANAENDA KASI SANA, hata kuzidi uwezo wetu wa kuyamudu".
Jinsi gari linavyoenda mbere ndivyo barabara, nyasi za pembezoni mwa barabara na vyote vya nje ya gari utaona vikirudi nyuma, jinsi gari linavyoongeza kasi ndivyo vitu pia vinaongeza kasi ya kurudi nyuma. Pekee huwa napenda kutazama uzuri wa tendo hili, maana jinsi unavyosonga mbere ndivyo unavyokutana na nyasi zingine, miji mingine, barabara nyingine, na wote wanarudi nyuma kwa kasi. Nikiwa mtoto nilifikiri kuwa ni kweri vinarudi nyuma, ila shule na ukubwa ukachangia kujua kuwa kwenda mbele kwa gari ndiko husababisha vionekane kurudi nyuma, ila vyenyewe huwa tunaviacha palepale.

Maisha ni safari, maisha ni safari, maisha ni safari, huu ndiyo msemo niliousikia tangu miaka yangu ya utambuzi wa mema na mabaya. Leo naandika kitabu hiki nikiwa na ufahamu napata nguvu ya kuhoji na kuandika, kama maisha ni safari basi kuna gari la abiria tumepanda, na kama lipo basi lazima litakuwa na lina jina, na kama lipo kweri basi kuna barabara, kuna nyasi tunazoziacha nyuma kila siku, kuna miji na vijiji tunaviacha nyuma, kuna vituo tunaviacha nyuma, kuna watu wanashuka njiani nasi tunaendelea mbere, tunafika pia tunashuka wengine wanaendelea, kuna wakati tunafika hata mwisho wa safari.

Kama ni kweri; maisha ni safari, mda ndiyo kipimo cha safari yetu, kila mtu ana mda amewekewa kuishi, na kikomo cha mda wake ndiyo mwisho wa safari yake inayoitwa maisha, wapi tunaenda, tunaelekea kwenye mafanikio na kushindwa, tunaelekea kwenye furaha au huzuni, tunaelekea kwenye utajiri au umasikini, tunaelekea kwenye kuleta mabadiriko au kukubari mabadiriko, tunaelekea kwenye kuwa mfanyakazi au kuwa muajiri, tunaelekea kuwa muwekezaji au mteja, tunaelekea kuwa mtumwa au mtu huru, tunaelekea kufa unafahamika au hufaamiki, tunaeleka mbinguni au jehanamu.
Basi tulilopanda linaitwa ulimwengu;  ni tofauti na nchi au dunia, hivi ni sayari, lakini ulimwengu ni hari ya uathiri (influence), ni hari ya kitWu, mtu/watu kuwa na nguvu ya kufanya wengine kufanya kitu fulani kwa kupenda au kutopenda,
Hivyo tupo kwenye basi la kila mtu akitafuta nguvu ya kuwa na uwezo wa kuwafanya wengine wafanye anachotaka, ulimwengu umpe anachotaka, apate anachotaka, aishi anavyotaka, aende anapotaka, ale na kuvaa anavyotaka. Ukitazama kwa makini; utaona ni wachache ndani ya gari hili ulimwengu wamefanikiwa kufikia hapo, tunawaita matajiri/mabepari/wawekezaji/wajasiriamari, ila kundi kubwa; mabilioni na mabilioni ya watu bado wapo hawajafanikiwa; bado hawajafanikiwa kupata nguvu hizo, za kufanya unachotaka, kwenda unapotaka, kuwekeza unapotaka, kula unavyotaka, kusoma na kusomesha unapotaka, kufanya starehe unayotaka n.k.

Kumbuka hii ni sehemu ya kwanza wiki ijayo tunaendelea...

"Maisha yanaenda kasi, zaidi hata ya uwezo wetu wa kuyamudu"

Kama gari ni ulimwengu, nyasi, na vingine ambavyo huwa tunaviona vikipita na kurudi nyuma kwa kasi ni nini?. Shetani na dunia haijawahi kuwa na jipya, siku zote ni yale yale, dhambi iliyomwangusha huyu, kesho inamwangusha yule, baada ya miaka kadhaa inamwangusha mwingine, jaribu na changamoto iliyomkumba huyu ndiyo hiyo kesho humkumba yule; nimekuwa mshauri wa watu wa rika tofauti kwa miaka kadhaa sasa, sijawahi sikia tatizo ambalo ni jipya, yote yanafanana, tofauti ni mtu na aina ya watu waliyopatwa basi. Nyasi na miji tunaipita huwa havitembei viko pale pale, gari la mbere na gari la nyuma watazikuta palepale na kuzipita, ukipita jana, leo na kesho utazikuta pale pale, hata zikikatwa, miji na vijiji vitabaki, katika safari hii kila mtu atapitia changamoto, majaribu, vikwazo, na makosa kadhaa. Na yote huwa yanafanana.
Cha ajabu, kwanini watu wanashindwa, yaani aliloshindwa huyu kesho yule naye anashindwa; watu hawataki taarifa na kujifunza.

Mfululizo wa somo hili la BARAKA TANO ZA PETRO ni kukusaidia kujua kanuni za kuwa salama katika safari, kujua kuitumia leo yako vema na namna ya kuandaa na kutumaini kesho yako, na pia kukusaidia kufika salama mahari unapotaka ufike katika safari ya maisha uliyoianza, na  kuwa moja ya kundi dogo lenye nguvu ya kuongoza na kuathiri ulimwengu uende wanapotaka, kufanya zaidi, kushinda adui yako mkubwa ambaye ni mafanikio yako ya sasa, kuishi maisha ya mafanikio na amani ya furaha, kuondokana na utumwa wa pesa.
Daniel aliishi nchi ya utumwa lakini aliifanya Babel iende yeye anakokutaka, akainuliwa na kuwa sehemu ya juu ya maliwali wote wa Babeli na juu ya Uliwali wote wa Babeli. Leo ni zamu yako, tumechoka kuishi kama watumwa katika nchi zetu wenyewe. Tumechoka kuishia katikati ya mafanikio yetu wakati Mungu ametuumba kufanya zaidi ya tuliyofanya.

PETRO MWANAFUNZI WA KIPEKEE
Ni mwanafunzi machachari na mchangamfu, nahisi alikuwa ni mtu muongeaji, mtu wa kucheka na tabasanu mda wote, mwenye siasa kidogo, mcheshi, muoga, mwenye silka kubwa ya uongozi, kiherehere, na mtu ambaye hutochoka kukaa naye, ila utachoka tu kumsikiliza maana anaonekana alikuwa ni bingwa wa kuongea.
Petro katika maisha yake anakuja kupewa baraka tano na Bwana Yesu, ila kuzifikia, kuna kazi ilimbidi afanye, alipitia maisha ya kupatia na kukosea.
Petro hakuwa mwanafunzi aliyekuwa namba moja kwa ukaribu na Kristo lakini alifanikiwa katika kupata baraka nyingi ukisoma vitabu vya injili. Hivyo anatupa fulsa sisi ya kumchambua na kutusaidia kujua tunawezaje kujifunza toka kwake.

MAMBO YA MSINGI KUJUA KUHUSA PETRO
1. Petro alikuwa ni mvuvi, masikini, mwenye dhambi, alikuwa chini ya ukoloni wa Kirumi, na maisha yake aliyatumia kuvu samaki na si kukaa na familia.
2. Petro alikuwa alikuwa ni mtu wa kutochoka kujaribu: mda mwingi alisema linalotoka moyoni kujibu maswali ya Yesu na kuchangia mada za Yesu, kuna wakati akapatia na kuna wakati alikosea, lakini hakuchoka kujaribu tena na tena hata alipozuiwa, hakuacha.
3. Alikuwa muoga, ila aliyejitahidi kuushinda uoga wake, hata wakati aliposhindwa alijaribu tena; aliogopa kusema kuwa yeye ni wa Yesu, kuogopa kupigwa kama Yesu, lakini Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo walipoleta taarifa ya kufufuka kwa Yesu, mitume wengine wakaona ni upuuzi yeye hakusita kuwa wakwanza kwenda kuona bila kujari kuwa alikuwa anaenda kwa mtu aliyemkana, siku waliposhukiwa na Roho Mtakatifu akawa wakwanza kusema kati ya wanafunzi 120 waliyobaki, siku zote alipambana na hofu yake, aibu, na woga wake.
4. Alikuwa tayari kufa kwaajili ya wengine, alikuwa tayari kufa ili tu injili iwafikie na wengine. Alikuwa tayari kupambana ili kumwomo Kristo japo haikuwa sahihi kufanya hivyo. Alikuwa tayari kufika mpaka lango la behewa ya kuhani mkuu kuona Yesu anafanywa nini na makuhani.
5. Petro alikuwa ni mwenye njaa na kiu ya haki: alipoona Eliya na. Musa wanasungumza na Yesu akaona hapa ndipo pa kukaa, akamwambia Yesu "...Bwana Mkubwa, ni vizuri sisi kuwapi hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa na kimoja cha Eliya" hali hajui asemalo. Japo alikuw hajui asemalo lakini alionesha kiu na ufalme wa. Mungu, kiu na kukaa penye dirisha la mbinguni. Na kwa hapo Yesu akambariki.
Petro aliacha vyote na kumfata Yesu, hata alipofanywa kuwa kiongozi wa makanisa yote hapo Uyahudi bado alizidi kuifanya kazi ya Mungu na kuutafuta ufalme wake.
6. Alisimamia anachokiamini kwa gharama yeyote; hata walipomshawishi kuwa aache kulihubiri Jina la Yesu, bado alisimama pamoja na Yohana na kuwaambia "...ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe, maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia. Mdo 4:19-20
7. Alikuwa mtu wa kutazama leo; Petro hata wakati alipokosea, alichukua kuwa hilo ni kosa la jana, akawa analisahihisha na kusonga mbele, kiukweli Petro alikuwa ni mtu wa kukosea sana, ila alikuwa ni mtu mwenye kutumia sana fulsa. Petro alipoambiwa na Yesu "rudi nyuma ewe shetani" Yoh 18:10, ndiye huyo huyo anakuja kumwambia nipo "tayari kwenda na wewe gerezani" Luka 22:33, Yesu anamwambia utanikana mara tatu, Petro hakusita kwenda naye kwenye maombi, aliposinzia na kuamshwa mara kadhaa, hakusita kunyanyua upanga na kumkata sikio la kuume mtumwa mmoja wapo wa kuhani mkuu, Yesu anamsahihisha, hakukosa kwenda naye mpaka malangoni mwa behewa ya kuhani mkuu, na huko alipomsaliti, pia hakusita kuomba msamaha, na kuwa mwanafunzi wa kwanza kufika kaburini kuhakiki kufufuka kwa Yesu na kuonana na Yesu kati ya wale mitume 12. Siku zote alitazama maadamu ni hai, naweza kusahihisha na nikafanya kitu chema, kikafuta baya la jana na kunifanya kuwa mtu wa muhimu, mafanikio na mwenye kibari.
8. Petro aliwaza chanya siku ziku zote; siku zote alipoona fulsa imetokea, akaishinda hasi na kuweka chanya, alipoona Yesu amesema, ikawa ni fulsa, akaamini inawezekana, alipoambiwa kavue samaki wa kwanza atatoa pesa, japo hakuwa ona, akaamini akaenda, alipoambiwa wokovu kwa mataifa, Wayahudi wengine ilichukua miaka na miaka, lakini yeye aliamini saa hiyo hiyo alipoambiwa na Mungu, aliwaza chanya siku zote, hakutamani kubakiwa na hasi, aliiweka hasi ni ya jana, sasa si wakati uliyopita.
9. Petro aliamini anapohusika Mungu yote yanawezekana: Petro alipoambiwa shusha nyavu, hakuuliza mara mbiri "...kwa neno lako nitashusha nyavu" akashusha, alipoambiwa kavue samaki utapata pesa, haraka akaenda, Roho Mtakatifu alipowashukia, saa hiyo hiyo akaanza kuzungumza kwa ujasiri watu watubu, alipomuona kirema akiomba omba, hakutaka kuambiwa sasa unaweza kuponya, akafanya muujiza.
10. Alikuwa na roho kubwa ya uongozi. Petro alikuwa na roho ya kuongoza, najua kuwa kila mtu ana silka ya uongozi ila Petro alikuwa na roho ya uongozi, hii roho kila mtu huzaliwa nayo, ila ni jukumu la mtu binafsi kuifanya hii roho ichipuke na kufanya kazi. Petro alitamani kila kitu awe kiongozi, kila kitu afanye yeye, kila kitu kiwe sawa, kila kitu kiende inavyohitajika. Na hivyo Yesu akamfanya kuwa kiongozi. Kiongozi ni yule mtu ambaye yuko tayari kujitolea katika mambo yote, na hapa ndipo sehemu kubwa pekee inayomuwezesha mtu kuichipua roho ya uongozi.
11. Petro alikuwa mtu wa mahesabu na mfanya kwa faida. Wakati wote waliponyamaza kuhusu kumfata Yesu, Petro hakukaa kimya akaona aulize. "...tazama tumeacha vyote tukakufata; tutapata nini basi?" Petro hakutaka kufanya kitu kwa kujitoa kisichokuwa na matokeo ya maganikio yanayoitwa faida mbere.

NINI TUNAJIFUNZA...
1. Unaweza toka chini kabisa mpaka kuwa juu kabisa.
2. Usichoke kujaribu uonapo fulsa
3. Kila binaadamu anazaliwa na woga, shinda woga wako.
4. Kubari kufa kwaajili ya wengine, kuiponya nafsi yako ni kuwa tayari kuiuwa nafsi yako kwaajiri ya Kristo na watu wengine
5. Alitafuta kwanza ufalme wa Mungu, na mengine akazidishiwa; alifanya sehemu yake na kumuacha Mungu afanye sehemu yake.
6. Kama unachokimini kiko sawa, simama ulipo, usiyumbe wala kuyimbishwa. "The strongest man is a one who stand alone" Karl Max
7. Usisumbue mda wako kutazama jana, tazama fulsa sa leo, usitazame kushindwa au mafanikio yako ya jana, tazama fulsa za leo na uzitumie kwa nguvu ile ile iliyoko ndani yako, bila kuregea.
8. Hata wakati inahitajika uwaze hasi, au wengine wanawaza hasi, wewe waza chanya. Shinda mawazo hasi.
9. Amini wakati na mahari anapohusika Mungu yote yanawezekana.
10. Chipusha roho ya uongozi kwa kujitolea. Unapowapa watu vitu wanavyohitaji watakupa wewe zaidi ya unavyoviitaji.
11. Kuwa mtu wa mahesabu, hesabu hasara na faida. Unapotoa vyote kuanzisha biashara utapata nini basi, unapotumika usitumike kiuvivu, jitume ukijua faida yako ni kubwa toka kwa Yesu, umempa mtu mda wako kuonana naye, utapata nini basi, umeenda sehemu utapata nini basi. Chochote unachofanya lazima utazame utapata nini basi.

BARAKA TANO ZA PETRO
ngoja tuziorodheshe baraka hizo tano na ukurasa wa mbere tutaona namna alivyofanya kwa sehemu yake kwa uaminifu pasipo kuingilia nafasi ya Mungu, pasipo kumngoja Mungu aje afanye sehemu yake na Mungu akafanya sehemu yake kwa uaminifu na hivyo akafika alipoahidiwa na kutamani kufika.
1. Mvuvi wa watu—Luka 5:10B
2. Mwamba wa kanisa—Math 16:18
3. Mmiliki wa funguo za ufalme wa mbinguni—Math 16:19
4. Muimarishi wa wengine—Luka 22:32
5. Mlisha kondoo—Yoh 21:15


SEHEMU YA TATU
MAANA YA JANA, KESHO NA LEO

Mwaka wa 2009 nikiwa natoka shule ya sekondari ya Kigurunyembe nikiwa na marafiki zangu kadhaa, Mr. Maneno akanyanyua kinywa na kutamka kwa huzuni iliyochanganyika hasira na majuto kwa mbali, akasema "kama isingekuwa yule msichana nisingekuwa nimeferi" tukacheka sana, akanitazama "unajua nilikuwa na akiri sana zaidi hata yako dogo", nikamjibu kwa kebeghi "ndiyo basi tena, neno ningelijua huja mwisho wa safari" alikasirika na kujaribu kunipiga ila hakuweza. Wakati huo mimi tulikuwa tukisubiri kuchaguliwa kwenda elimu ya kidato cha tano, sasa kati ya wanne tulikuwa tukitembea wakati ule ni mimi pekee niliyekuwa na matokeo ya kufauru. Mr Maneno hakuwa anajuta kuferi, ila alikuwa anajuta alichofanya wakati aliokuwa amepewa kusoma akautumia kufurahi na kula anasa na msichana.