Friday, August 26, 2016

DISCOVER THE MEANING OF LIFE FROM BIBLICAL VIEW

LIFE GENERAL PRINCIPLE

2. DOING

this is second phase of life, is very important phase, while its important determined by how you spend the first phase, and how fast you're to work with opportunities that God provide according to your purpose.

Look Jesus First: After Jesus becoming what He was born to become  A Savior (the First Phase) then He immediately start doing.

He start to preach the gospel of the Kingdom in all towns, clean leapers, heal the deaf, make the blind to see, rise the dead, and cancel demons. Crucified and rise from the dead, and give salvation to all mankind.
In fact Jesus start doing, after he completely becoming what he was born to do.

Know who you are, then becoming what you discover you're, then immediately start doing what you become. Procrastination is tragedy.

"Know who you're, Become It, Immediately Do it"
~ Ev.Ulenje

Remember God will test you first to prove and to qualify you. He will never chose you because you qualify, but he will qualify you first or within the work.

3. LEGACY (After Life)

This is final phase of every human.

"Nothing is powerful than death"
Ev. Ulenje

When you die, everything die; despite the great plans and dream you have, the vision and great course, and career, but when death show up_everything die.

Fear of death cant stop death, only preparation for it and doing effective with life you have make death have no power. In fact the cure of all diseases and fear is death, when you die no diseases or fear can touch you. Only what you have done carry your name after you die, not your good clothes.

Its better to be victim of what you have done, than to be the king of what you procrastinate. At the end, the matter of all things is what you have done. Its better to live a short life of Glory than the long one of obscurity (anonymous)

After Jesus finished his work; Teach good news to the poor, set captivity free, open the blind, heal the broken heart, and preached the acceptable year of the Lord, He die on the cross, Resurrect, Announce the Great announce ever announced, that "It is Finished", he immediately went back to heaven, he didn't say Father no! I love the world. No because He knew the first and second phase is done, Now is time for legacy phase.

Note this: when He Go, His disciples immediately start preaching what he preach: the gospel of the kingdom.

Why? This is what He leave. He leave the generation who were Fisher of fish, he work hard with little sleep and uncomfortable rest to make them Fisher of man, and Kingdom Expansion Agents....the Question; what are you doing????

AFTER VISIBLE LIFE
What happen now?!: Jesus was not in visible world.....

Jesus finish His work, return to invisible world where He come from.... but look_his idea, perspectives, culture, thought and moral and life make him alive in visible world.

Think with me, sometimes you don't need to receive healing or answers for your prayers to feel the presence of Jesus in the world. In fact Jesus is not present in Visible world now, but you cant Ignore this Great eternal public figure in visible world_ we mention Him in books, Broadcastings, wearing clothes with His name, make Christmas trees and use His principles.

Act 11:26 is When Christian in Antioch who were consumed with Jesus Christ, and out of abundance of their heart their action, idea and their life perspective speak, people they called them Christian.

Act 24:5 Christian in Palestine after they consumed with Jesus, their action and idea of life speak, then people of Palestine they called then Nazarenes— to refer the nick name they called Jesus (Math 2:23)
These are few legacies am talking about.

You can do that too_You can live after you die_it's not ok to die in anonymity. Be ready to pay the price.

"The legacy need more commitment than people are willing to pay"

Get some of example of people who are still alive while they died: Paul, John, Peter, Luke, Timothy the Apostles, Martin Luther King Jr, John Wesley, T.R Osborn, Myles Monroe,  Oral Robert, Mother Teresa, Nelson Mandera, J.K Nyerere, Bishop Kurola etc.

Next part we gonna Focus How these Three phases work in our life and how to use them effective.
Thank you for reading....
Ev.Ulenje.
Director CWGM
GLORY TO GOD WHO IS SOURCE OF ALL TRUTH.

Thursday, August 25, 2016

DISCOVER THE MEANING OF LIFE Part 2

# GENERAL PRINCIPLE OF GOD CREATION: God plan, then create: Your birth is God planning; God first make a plan, then he form you exactly with power, talent and abilities to execute what he plan, then he plan the accurate time that is sufficient to accomplish what he plan.

He plan an accurate woman and man, and accurate event for you to meet and face (bad or good) and how you should be born. Then he allow birth according to what he plan. And what drive him is his plan. We call it Purpose of your born. What you're born to do. Plasm 90:10, 139:13-16, Job 31:15; 14:1-6.

• Don't say you have few days to accomplish your dream and what you're born to do.
Jesus had only 33.5 years to live in this visible world, Poul the apostle had only 60 years to live, but he accomplish his purpose to spread the gospel to the nations.

• Therefore: Life is time include  both experience, and what you do with it.

TO CROSS THE POINT
In this subject, we gonna lean How to Use our Time Effectively as God plan for us to Live.

A. LIFE IS PHASES
Life we live in, has phases. You can define many phases according to experience you encounter. But all are come together to these three phases: Becoming, Doing, And Legacy.

In can prove by using Jesus life in visible world and now in invisible world.
Jesus has effective, simple and meaning life.

JESUS LIFE
1. Becoming Someone (Kufanyika Fulani)
Jesus was born a king (Isaiah 7:14) whilst He use 30 years to become a king, He was born as Minister with all five  ministry yet He had to spend 30 Years to be trained For His earthly ministry, And 40 days to be tested.
He was first had to go to Egypt as it was written, He was able to live everywhere he could chose but he had been living in Nazareth, Why? As it was written, The Son will be called Nazarene.

Why everything as it was written, the birth, the life, the death and even the resurrection: as it is written means: "HE SUPPOSE TO BECOME LIKE THIS"
Becoming means to develop your original identity that God pre-destined for you. Jesus identity was written, therefore despite the power He had to kill Herod, but He didn't Why, Because He suppose to become that identity.

In Luke 2, We see Jesus spent his 30 years not teaching but leaning and becoming, gaining favor from God and men. Here is the story; when he was Child about 12 years old, He go to Synagogue. The Bible never say, He teach, the Bible say, He ask question and listen. Why He want to become.
When John saw Jesus coming unto him, and saith, Behold the Lamb of God, which taketh away the sin of the world. John 1:29. Before that John identify himself as The One Crying In the Wilderness. John 1:23.
Why? Jesus become Lamb of God and John become One Crying in Wilderness.
And after the process of becoming, he Go to the wilderness to be tested, to be checked if he qualify. Angels come to worship Him, with joy because Jesus qualify to become as He was Born To become. Then He start Doing.

To be continued....
Thank you for reading...
Written by Ev. Ulenje
Director CWGM
GLORY BE TO GOD WHO PROVIDE ALL TRUTH

Monday, August 15, 2016

DISCOVER THE MEANING OF LIFE

MEANING OF LIFE
We should know the meaning of life, before going more deeper.
LIFE can be defined in term of How we live life and Time we live life, Biblical View (God Purpose)

A. How We Live
Life is experience, including what we face, what we do, what challenge us, what we wear and eat, how we feel about what we have and how we feel about our path, from birth to dearth, from unfortunate to fortune.

B. Time We Live
Life is time, time is life.
Your time is you life, and your life is your time.
Life is total of second you live in visible world. Eternal life has no time.
When God bless someone to live longer he give him more time. When God bless someone to have wonderful time, he give him wonderful life.

C. Biblical View
Bible include both How we Live and Time We live.

Bible define life total of time you live, how you start, how you live, what you do and how you finish the race.

I.e Bible compose what you encounter and how you respond, what you do, you intent in heart and the results of what you do, and How God view what you do and how He respond in your lifetime.

Life is time, filled with seasons and moment. Life is time filled with past, present and future.

Life is what you face, feel and do external and inside, and what you face and do in public and in private.

When we look someone life in funeral we always look the time he live, How he live, And What he do with that time.

TRUTH ABOUT TIME
• When God give us life, He give us the time with specific starting point, and the specific limit of that time that you cant exceed.
   - And God is looking how you use that time, and at the end Jesus shall never judge how long you live, but rather He will judge what you do with time and how you use that time.

• Even, at the funeral, people always discuss what you do and how you live, and how you care about them. Simply they judge someone ethics, moral, attitude, behavior.

• Something to Note: We Don't Have Two Life. We all have only One Life, Unless God Decide to bring you again as John The Baptist. To be raised again is not two life. Only Elijah experience second life as John Baptist. Because second life means to be physically born again.
To be born again is to be given A New Life in Spirit not Physically, that you will never leave this visible world, No!.

Means; Use your time well.

• To Go in Heaven or in hell, Is simply determined by How you spend and Do with Time.

• Note That: Despite, We all have different measures of time but we all have sufficient measure of Time according to what God want to be done through us in this Planet, for this and the coming generation. Hallelujah!

"You will never experience the meaning of life until you start living for God Glory, until you understand that you've been born for God"

"Never count that you give more, unless you give yourself "

Under the Strong Help of Holy Spirit.
Written by ULENJE
DIRECTOR CWGM

Monday, June 27, 2016

NGUVU NA MAMLAKA YA IMANI



NGUVU YA IMANI
                                                                                                                                                               
“hakuna kinachoshindikana kwa wale ambao bado wanaamini”
Mathayo 19:26
                                                                                               

Nguvu ni uwezo wa kitu kimoja kukifanya kitu kingine kufanya kitu pasipo kujali utayari wake. Imani ina nguvu ya kuamuru kitu chochote pasipo kujali wa hiko kitu. Imani ina nguvu ya kufanya chochote ambacho fikra za kibinaadamu hakiwezi kikawa kinawezekana, hata kama hiko kitu hakipo tayari. Yesu aliweza kufanya yote yaliyoshindikana na wanadamu, akayaamuru yatokee hata kama hayakutaka, hakuweza kufanya kitu pasipo imani. Je unataka kufanya makubwa zaidi ya aliyofanya Yesu, ni imani pekee inaweza kukufikisha huko. Nathubutu kusema kunena kwa lugha pasipo imani, hakuna litakalo tokea, kuomba kwa sauti au taratibu haisaidii, maana maneno ya kibinaadamu hayawezi kumfanya Yesu afanye lolote. Mungu ameipa nguvu imani tu pekee kuruhusu nguvu zake kutenda kazi.
“Ni Imani pekee ndiyo ina nguvu ya kuamuru kisichowezekana kiwezekane”
Nitoe mifano michache, Nguvu ya imani ndani ya Akida wa Kirumi (Luka 7:1-10), ijapokuwa hakuwa Myahudi wala hakuwa mtu wa dini ya aina yoyote ya Kiyahudi. Lakini imani yake ikaruhusu muuijiza juu yake. Mkumbuke yule mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12, nguvu ya imani ndani yake ikaruhusu muujiza wake (Marko 5:25-34). Jambo la kushangaza hapo ni kiwango cha nguvu ya imani ndani yao. Mkuu wa Sinagogi Yairo ndiye alikuwa wa kwanza kumfata Yesu kuwa mwanae anaumwa hawezi yu karibu na kufa (Marko 5:2124), lakini mwanamke ndiye alikuwa wakwanza kupokea muujiza kabla hata ya Yairo. Kwanini kiwango cha imani ndani yetu. Yairo alikuwa na imani mwanae atapona akiguswa na Yesu, mwanamke akaenda mbali zaidi, akaamini kuwa akigusa tu, hata kama Yesu hajatamka neno, hata kama hatojua basi atapona, kumbuka aliwaza kugusa pindo na ni kweli aligusa pindo, yaani aliamini hata Yesu asipojua, ili mradi akigusa pindo la vazi lake tu. Je una imani namna gani?
“kiwango cha imani ndani yako ndiyo kinaamua kiwango cha muujiza unataka kupokea”
Imani ni kitu kisichoonekana lakini kina uhai na kina nguvu, ambayo hata mwanadamu hana. Imani ina nguvu zaidi hata ya nguvu za Mmarekani, Barack Obama alipomuua Osama Bin Laden alifikiri amemaliza kazi, lakini huwezi kuishinda imani kwa mtutu au kumuua kiongozi, sasa tunashuhudia kutokea kwa vikundi vya kigaidi zaidi na Al-kaida bado ipo. Kusambaratisha vyama pinzani kwa kutumia polisi bado hakuwezi kuishinda imani ndani ya vijana dhidi ya chama pinzani. Wengine wanajiripua na mabomu sababu ya kusimamia wanachokiamini. Karibu kila vita duniani chanzo chake ni imani, kama siyo imani ya dini basi ni imani ya kisiasa. Imani ina nguvu hatari sana na isiyozuirika. Kama kitu unachopaswa kuwa nacho ili kufanya yote ambao unaona yapo juu ya uwezo wako basi kuwa na imani.

Friday, June 10, 2016

50 LESSONS FROM GOD CREATION

50 LESSONS FROM GOD's CREATION

Introduction

• Nothing exist from itself

• Everything that exist, starting from thought

• Everything path through faith before they becoming fact

• Everything in this planet has someone who first think, believe, plan, and develop a great commitment to create.

• Everything exist/created to solve some/specific problem(s)

• Everything can be used to help the creation of another-things

• The glory of a product is the glory of the creator: the glory of a product is when its solve problem, and make life comfortable.

• The glory of one who create a new and unique product, that is never existed, is higher than the one who create a copy, or improve the existed product.

• Great people discuss new thing, Normal people Copy and improve the existing product, Lazy people are just happy to enjoy what other create.

• Everything you see now, they are not there/here before, until somebody committed to create/produce.

• Everything you see was first impossible to average people, and possible to great people.

• What you think is impossible; Is not them that are impossible, is you that you're impossible to believe.

• When you pass by a large and very long lotion of about 30 floor; Even though you dont see/know the one who plan, design and built the building, but deep inside your conscious you believe that there is someone who design and built the building. And that is true.

• When you use the pen, a book, motorcycle, a car, an airplane, Television, radio, A road, anything you can mention; when you take a breath, deep inside your conscious, you believe there is someone somewhere built or produce that product.

• That is true: this is amazing, the one who create is human like you.

• The more amazing is this; You have the power to do that; EVERY HUMAN BEING CREATED WITH THE POWER, ENERGY AND ENOUGH SKILLS TO CREATE SOMETHING BEST WHICH CAN OUTLIVE HIS/HER LIFE.

• Do you want easy pass to become a millionaire, simple; create something new and unique. Its hard to stop Bill Gates to become billionaire. Because you cant run your company with cheap technology without using his product. You cant avoid Steve Job product If you want to use more quality and expensive computer product.

Never Miss Next Session
"PLACES WITH OPPORTUNITIES TO CREATE SOMETHING NEW!"

Under More Help from Holy Spirit
Written By;
#Ev.Ulenje
ChairPerson CWGM

Wednesday, March 16, 2016

Part 6: MAANDALIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO....

MAANDALIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

Mithari 16:1
"Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;
Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.

Tumetoka mbali na leo tufike tamati, jitie nguvu kusoma maandalizi yote ni ya muhimu. Nakusihi usikose hata Part moja ya somo hili, bonyeza sehemu iliyoandikwa "home" na uanze na hili somo kuanzia Part 1 mpka 6. Hapo utakuwa umefanikiwa kupata semina hii yote. Tulioanza pamoja Mungu awabariki sana. Semina ijayo ni muhimu sana "TABIA NA UTUMISHI" usikose.
Tuendelee...

7. Je Upo Tayari Kumfanya Mwingine Awe na Furaha na Amani .

Karibu kila binaadamu amezaliwa na ubepari ndani yake, yaani ubinafsi. Popote hutazama anapata nini, hata yule atendae kwa wengine basi huwa na fikira kuwa Mungu atamlipa au kumbariki. Huwezi kufanya jambo pasipo kujitazama wewe.

Jambo ambalo mwanadamu yeyote analitafuta ni amani na furaha. Anataka chakula ili awe na furaha, anatafuta pesa ili awe na furaha. Nimewahi ona watu wenye pesa pasipo kuwa na amani kwenye ndoa yao, na watu masikini wenye amani na furaha kwenye ndoa yao.

Usisahau, jambo gumu kulitafuta kuliko yote hapa duniani ni amani. Ndiyo maana Biblia imesema "tafuteni..." Maana yake amani ni ya kuitafuta.

Ni vema ukajifunza nini huwafanya wanawake wawe na furaha na nini huwafanya wanaume wawe na furaha kabla ya kuingia kwenye ndoa. Ni vema ukajifunza kutafuta amani hata wakati ambapo umekosewa na kuchukizwa.

Mtu mmoja aliwa kunishangaa, baada ya kuona ananieleza jambo la kutisha ambalo watu wamenifanyia, lakini mimi nacheka. Alitegemea nitahuzunika na kuchukizwa sana. Kwanini Mungu amenisaidia kujua maana ya amani na kuitafuta hasa pale ambapo haipo au inataka kutoweka.

8. Je Unajua Kusamehe

Kwa haraka waweza kujibu "ndiyo" lakini fikiri wangapi si marafiki zako tena kwasababu tu umeshindwa kuwasamehe, au umesamehe makosa tu! Bado hujawasamehe wao, na ndiyo maana si marafiki zako kwa sasa.

Nisiwe na maneno mengi hapa, ila niseme tu, palipokuwa na wawili basi ndipo makosa huonekana, na kila mtu hujiona bora pale aonapo makosa ya mwenzie. Na kama watu wengi bado hawajakamilika, bado wana hisia zinazowashinda kuzikabiri kama hasira, chuki, wivu na mengine, kama kila mtu huwa anakosea. Ipo haja ya kuamini hata huyo unayesema ndiyo kwake basi ipo siku atakosea.

Basi nina uhakika upo umuhimu mkubwa wa kujifunza kusamehe hata makosa yasiyosameheka, hata pale mwenzio anaona hana haja ya kuomba msamaha. Naamini itakusaidia, lakini kama hujui kusamehe, kila kosa unataka useme, kila wakati unataka uonekane uko vema na mwengine amekosea basi vema ukaomba pooooo....kabla hujaanza uhusiano na mwenzio.

Unajua maana ya kutokusamehe ni kujisemea moyoni mwako hivi "yaani huyu mtu asiyekamilika, mdhambi ananitendea unyama mimi niliyekamilika, mtakatifu na nisiyekosea hata mara moja!!!!...." Hayo ndiyo maneno uyasemayo pindi unapokataa kusamehe. Jifunze kusema "nimekusamehe hata kama hujaombwa msamaha....ndipo useme ndiyo.

9. Je Una Tabia ya Ndoa

Naamini watu wengi hutazama umri wao na si tabia zao, na ndiyo maana wengi wameolewa na kuowa wakiwa bado.

Umri huletwa na miaka, tabia huletwa na mafunzo na fikra. Umri tunatazama miaka, tabia tunatazama matendo na fikra.

Nimeona ndoa za wengi walioowana wakiwa wadogo sana mpaka leo wanadumu na kuendelea nikiwatembelea huwa naona vicheko si vya uongo bali vya kweli. Na nimeona wapo walioowana wakiwa na umri mkubwa na ndoa zao hazijakaa salama hata vicheko vyao ni vya kudanganya wageni.

Siku ya leo maarifa yameongezeka, hatuna tena tatizo la maarifa bali tuna tatizo tu la kuwa na maarifa mengi. Nafikiri ni vema ukachambua na kutafuta maarifa ya KiMungu, wapo watumishi wengi waliofanikiwa kwenye ndoa Zao na wamejitahidi kuandika na kufundisha maarifa mengi ya ndoa. Kuwa msomaji, badiri ratiba ya matumizi ya smartphone yako, anza kusikiliza mafundisho ya Mungu, soma blog zao, soma vitabu vyao. Ili upate kujua maarifa hayo.

Maandalio ya moyo ni ya kwako, ila jawabu ni la Bwana. Usitazame umri na miamko ya mwili: tazama je una tabia za ndoa, je unaweza kuishi na mti mwingine na kuendana na tabia, udhaifu na utofauti wake. Usije ukawa unamsubiri Mungu, kumbe ni Mungu ambaye anakusubiri wewe.

Kila kitu kina tabia yake, na usipoifata hutofanikiwa. Kuna tabia za biashara, kuna tabia za kilimo, kuna tabia za wanasiasa, kuna tabia za wanafunzi, kuna tabia za wachungaji. Vivyo hivyo na ndoa, kuna tabia ndoa inahitaji uwe nazo.

Mfano; unajua kujari, unajua kusamehe, unajua kuchukuliana na watu, unajua thamani za watu pachoni pako, unajua kujitoa kwaajili ya mwingine, unajua kupika, unajua kusaidia, unajua kujitoa hata kama umechoka, unajua kuonesha utii hata kwa aliyekuudhi.

10. Je Umejiandaa kwa Matokea

Ndiyo yako ya kuingia kwenye ndoa ina matokeo na baada ya kusema ndiyo vitu vingi vinatarajiwa kutokea. Kwa haraka, tunatarajia watoto, kupungua kwa baadhi ya maamuzi yako binafsi, kupungua kwa uhuru wako, kuingiliwa maamuzi na mwingine, kuongozwa na mtu mwingine, kuongezeka kwa majukumu.

Ni vema ukajiandaa na matokeo hayo hata kabla ya kusema ndiyo. Haina maana ya kufikiri kuyakabiri yote kwa wakati mmoja bali ni kujiandaa nayo.

11. Je umejiandaa kukabiri Mabadiriko ya mtu.

Binaadamu siyo jiwe kwamba habadiriki.

Watu wanabadirika kiuchumi kushuka au kupanda, wanabadirika muonekano wa mwili na uzuri wao, mabadiriko ya nguvu, fikra na baadhi ya tabia, wanabadirika matendo, hata imani kuna wakati wanashuka na wakati wanapanda kiimani.

Mabadiriko hayo yanapotokea: ni wakati wa kiangazi ambapo kila mtu anahitajika kuwa imara kuhakikisha boti haizami ndani ya maji.

Ni jambo linaweza kuoneka dogo, lakini kama usipoandaa ufahamu wako kujiandaa katika hili, kiangazi kijapo na kukukuta hauna chakura utakuwa kwenye shida.

12. Je una Uwezo na Upo tayari  Kujitoa

Upendo ni kujitoa, kwa hari na mari. Huwezi kusema unampenda mtu na haupo tayari kujitoa kwaajili yake, na kila mtu anatamani mtu anayejitoa kwaajili yake.

Kuna vitu huwezi kufanya pasipo kujitoa. Jiandae. Kuna wakati wa kuchukizwa: ni kujitoa kusamehe. Kuna wakati wa kuchoka na kutokuwa na kitu kabisa, kuna wakati wa kusaidia hata kama huna uwezo.

Kujitoa si kitu kidogo kinahitaji upendo wa dhati sana (deepest love) na kama huna upendo huu hutoweza.

Nina mengi ya kusema ila Roho Mtakatifu ndani yako atakufundisha mengi zaidi.

Kipimo kikubwa cha somo hili: Kumbuka nini kilikuachanisha na rafiki zako au wapenzi wako wa zamani, pia tazama ni nini ambacho hukipendi na kinakuchukiza kwa mke au mume wako, au mchumba wako. Utagundua uliacha nao urafiki au uchumba ni moja ya maandalizi haya hukuwa nayo, na hata sasa huridhiki kwasababu moja ya maandalizi huna.

Kuna KITABU kipo jikoni "BADO LIPO TUMAINI" utakapokiona dukani tafadhari nunua. Na zidi kuomba kwa habari ya watumishi.

Natamani kupata comment yako, phone call au whatsapp.
+255 718 721848
imaf2b@gmail.com

Monday, March 7, 2016

Part 5: MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

Bado Tunazidi kuchana Nyavu...
#SeminaKiganjaniMwako.

4.  Je upo Tayari Kubadirishwa, Kukosolewa, na Kuboreshwa

Moja ya hadithi niliyowahi kuisoma darasa la kwanza na  nisiyoisahau ni hadithi ya "Mti wa Mpapai uliogoma kwenda huku-na-huku kuufata upepo" upepo ulipozidi, mpapai ukaanguka.
Tunafahamu kuwa kila binaadamu ana udhaifu, ila Mungu ametupa uwezo wa kuwa wakamilifu: na hutumia watu wa karibu, matukio na majaribu katika maisha.
Naamini tunaingia kwenye ndoa si kushindana bali kukamilishana: ili kutimiza kusudi ambalo Mungu ameliweka katika maisha yetu.
1 Kor 11:11 "Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana"

Nikupe siri; Udhaifu wa mtu hugunduliwa na mtu mwingine hasa wa karibu yake sana" Dr Myles Munroe aliwahi toa mfano kusema "Ni vigumu kujua kuwa kiatu chako kinatoa harufu mpaka mtu mwingine akwambiye"

#Kama wote tupo kwenye safari ya kuelekea ukamilifu, na tunahitajiana ili kuwa wakamilifu, na tunafurahiana hasa pale tunapoonesha ukamilifu: basi kuwa tayari kuelimishwa, kupokea mafundisho mapya, fikra mpya, mipango mipya, na kuboreshwa baadhi ya tabia zako, ni MAANDARIZI YA MUHIMU SANA"

5. Je upo Tayari Kuacha Baadhi ya Vitu Unavyovithamini Kwaajili ya Mahusiano.

Idadi kubwa ya wachumba wameachana kutokana na kupishana na misimamo na mitazamo ambayo kila mmoja anathamini. Hata wanandoa wengi; mabishano yao makubwa mara nyingi, ni pale misimamo, mitazamo na fikra zinapogongana.
Misimamo; ni falsafa na mawazo ambayo mtu huamini kuwa ni sawa na yanapaswa kufatwa na wote ili kupata mafanikio.
#Kama hampo tayari kukaa chini na kujiandaa kupanga misimamo, mitazamo na falsafa ya pamoja na kuacha ya binafsi basi ni heri mkaomba pooooo! Kabla ya kusema ndiyo!! Na mkaendelea kukuza akiri zenu.

Maana mtakaposema ndiyo! Pasipo kuwa tayari kuacha baadhi ya misimamo ambayo inaweza kuwatenganisha, na kuunda misimamo ya pamoja; Itakuwa haina maana, sababu safari yenu itakuwa fupi.

6. Je Unaweza kulinda Maono yako; Huku Ukitimiza Kusudi la Pamoja.

Mwanzo 2:18;5:1
Hii ni mistari dhahiri inayoonesha kuwa Mungu ametuumba kutimiza kusudi moja pale tunapoungana na kuwa mtu mmoja; tofauti ni kwamba mmoja mjenzi, mwingine saidia.
Ila saidia asiyekuwa na maono, hafai, na mjenzi asiyekuwa na maono hafai kitu.
Saidia ni lazima maono yake yaendane na maono ya mjenzi, na kusaidia kusudi la pamoja kutimia.
Na mjenzi ni lazima maono yake yajulikane, yaendane na saidia wake; ili aweze kumsaidia.
Kusudi ni juu ya maono: Kusudi ni "Sababu ya wewe kuzaliwa" na maono ni "Kioo cha kutimiza kusudi lako na namna ya kufika kwenye kutimiza kusudi lako"

#Hivyo wote wawili muwe tayari kuunda maono yenu yaendane na safari ya kufika kwenye kusudi ambalo Mungu amewaumba kutimiza"
Haleluya!!!!

Sifa na Utukufu apewe Bwana
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu tunazidi kuenderea

Monday, February 29, 2016

Part 4: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO....

~ MAANDARIZI 15 KABLA YA KUSEMA NDIYO..."

Karibu sehemu ya nne ya somo letu...
Soma kila swali kwa umakini, kumbuka kujibu ndani ya moyo wako ukiwa peke yako.

Nianze kwa kusema: pindi unaposema ndiyo, kuna vitu vitabadirika kwenye maisha yako.

A. Ndiyo! yako hukuradhimu kubadiri tabia.
     Ili kuendana na furaha ya huyo umwambiaye ndiyo, kumbuka uwe tayari kuwa yeye anavyotaka. Na hivyo kuna vitu unafanya itakuradhimu vibadirike hata kama ulivipenda.

B. Kupungua kwa uhuru
     Kumbuka hutotakiwa kuendelea kuwa na uhuru kama uliokuwa nao, itakuradhimu umpe mwenzi wako sehemu ya uhuru.

C. Misimamo inabadirika
     Kumbuka unayekutana naye ana misimamo, na ili mfurahi lazima uwe tayari kubadiri baadhi ya misimamo yako.
E. Marafiki wanabadirika
F. Matumizi ya simu yanabadirika
G. Mda wa kulala unabadirika

Neno "Nimekubali..." Ambalo mara nyingi hutamkwa na wanawake, ni dogo sana ila ndiyo chanzo cha mabadiriko ya maisha ya wengi. Na hii ndiyo siri, ni wale tu ambao wako tayari kuendana na mabadiriko yanayotokana na neno nimekubali hufaidi furaha ya Ndiyo yao.

"Wale tu ambao wako tayari kukubaliana na mabadiriko yatokanayo na Ndiyo yao, ndiyo hupata furaha ya mahusiano yao"

Tuanze sasa, leo tutajadiri maswali kadhaa na Part ijayo tutamalizia maswali mengine. Kumbuka ni maswali 15.

Sw 1. Je Unaweza Kuzikabiri Hisia Zako?

Mtu yeyote hata kama mlikuwa marafiki kaka na dada hapo mwanzo, mnapoingia kwenye uhusiano mvutano wa miili yenu unaumbika na hivyo kuwaletea hisia tofauti na hapo mwanzo.
Hivyo kabla ya kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi, ili kujizuia kutenda dhambi ya uasherati, lazima kwanza ujiulize kama una uwezo wa kukabiri macho yako na nguvu ya mwili wako kwa binti. Huna uwezo wa kukemea tamaa iondoke, bali una uwezo wa kuzuia kuyachokoza mapenzi.
Wengi husimama wakiwa single na hupotea pale wanapoanza mahusiano.

"Kabla ya kusema ndiyo, jiulize je una uwezo wa kutunza heshima yako mpaka Ndoa"

Turudi kwenye stori yetu kuhusu Angel: siku moja nikitoka kupata ibada yenye nguvu ya Casfeta- chuo kikuu cha UDSM, nakumbuka dada mmoja aliniambia "Ulenje sikuoni siku hizi kwenye ulimwengu wa roho". Nilishangaa lakini nikakumbuka Mungu amewahi kunionesha namna ninavyojiweka mbali naye. Usisahau wakati huo nilikuwa nahubiri madhabahu za ndani na majukwaani, naombea na watu wanapona.
Nakumbuka siku moja nikihubiri kanisa fulani, Mungu alijitukuza wakati wa maombezi, mpaka watu walianza kuitana mitaani na kuja kuombewa. Lakini nikirudi nyumbani Mungu ananionesha niko mbali naye.
Sikuwahi anzisha uhusiano na Angel, siku nilipogundua "bado sina uwezo,
Basi nilisubiri, mpaka namaliza chuo nikaendelea kusubiri, haikuwa dhambi, sikutaka kuwa mbali na Mungu"

Jifunze jambo hapo, ni kwa namna gani mpenzi wako anakuweka mbali na Mungu, kwa njia ya simu yako, au mnapokutana.
Kabla hujasema ndiyo kwa huyo umpendaye, Je una uwezo wa kuongoza hisia zako, na kuishi pasipo kumkosea Mungu. Najua baadhi watapinga, lakini wanaopenda roho zao, na kuwa tayari kukana nafsi zao kwaajili ya Bwana basi watapokea na kufanyia kazi ujumbe huu.

Sw 2. Je Unajua Unaenda Kufanya Nini?

Nilimuuliza binti fulani swali kama hilo, akajibu nitafua, nitaosha vyombo, na kumpikia chakula kizuri kila siku.

"Watu wawili hawawezi kwenda pamoja, kama wasipopatana"

Sina mengi ya kusema katika hili, soma mwanzo 2:20 Biblia inasema "lakini hakuona wa kufanana naye"

Hivyo Mungu uheshimu wa kufanana naye, japo Mungu alizungumzia wasichana wote, maana hakutoa ulinganifu wa msichana na msichana, bali ni msichana na wanyama, na kuona kiumbe msichana ndiye anafaa; ila alionesha jambo la msingi "kuwa anaheshimu sana mfanano"

Kila msichana ni mzuri, ila ni vema wa kufanana na wewe.

Swali letu ni "Je unajua unaenda kufanya nini?. Ni swali dogo, ila kufanana siyo shida, shida huyo unayefanana naye anajua anaenda kufanya nini mtakapokuwa pamoja"

Unashangaa, unapokaa chini na wachumba au wanandoa, na kuwaeleza tatizo ni "mnafanana ila hamfanyi mnayopaswa kufanya" wanacheka, na wengi husema "kwanini mtumishi: sikujua hayo hapo mwanzo?, mwingine aliniambia "tatizo ni kutokujua mtumishi"

"Kanuni ni ndogo, ukijua na kufanya unachopaswa kufanya uhusiano utaenda, usipojua cha kufanya na Ukafanya usichotakiwa kufanya uhusiano hautaenda"
Ev. Ulenje

Nakusihi katika Jina lake Bwana Yesu, tumia mda kusikiliza mafundisho ya watumishi wanaoaminika, soma neno la Mungu, Biblia imejaa stori za kila aina ya ndoa, soma vitabu vya waandishi wa kiroho wanaoaminika, sikiliza watumishi.
Kubwa kabisa muombe Bwana akufundishe njia zake. Na utambua nini unahitajika kufanya wakati wa ndoa, kisha kuwa na amani ya kusema ndiyo, achana na mambo ya umri na miemuko ya mwili, Mungu anatazama uwezo wa ndani na Ndoa pia inategemea sana uwezo wako wa ndani, si miemuko
Ya mwili wako, au umri wako.

"Mungu huwaepusha baadhi ya wasichana kukutana na waume zao, kwasababu ya kuwaepusha wanaume hao na maumivu" Dr Myles Munroe

Kuolewa si umri, umaarufu, karama, huduma au msisimko wa mwili ni uwezo wa ndani.

Fikiria hili, hata kwa wanaume pia.

SW 3. Je Unajua Kutambua

1 Wakorintho 13:9-12
Soma kwa makini mstari huo, ila naomba niandike sehemu muhimu.
Biblia inasema "Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;....nilipokuwa mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga...wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu, wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana"

Hakuna siri kubwa katika kuwa na ndoa nzuri kama "kuwa na uwezo wa kufahamu yaliyojificha nyuma ya neno "nakupenda" unalolisikia.

Natamani kuishia hapa; ila ngoja niendelee: wengi wanalia kwenye mahusiano si kwamba hawakuambiwa "nakupenda" na wapenzi wao, bali walishindwa kutambua nini kipo nyuma ya neno "nakupenda" walilolisikia.

Watu wawili wanasema "nakupenda" je una uwezo wa kutambua "nakupenda ipi ni ya kweli na imetoka kwa Mungu" na ipi ni ya kibinaadamu.

Mwanaume una uwezo wa kufahamu "ndiyo" unayoipokea na nini kipo nyuma yake: je ni Mungu au shetani, je ni hatima nzuri au mbaya. Na kwa wasichana pia, je unatambua nyuma ya hiyo nakupenda; je ni Mungu, Shetani, Hatima nzuri au mbaya.

Kama huna uwezo huo, basi ni bora ukaacha kujenga nyumba, Yesu anasema usije ukajenga msingi, ukashindwa kumalizia na wenzio wakakucheka. Ni bora ukaomba poooo....mapema kabla ya huyo mwanaume au mwanamke hajaja.

Ninayo mengi ya kusema katika hili, ila Roho mtakatifu akufundishe zaidi. Wengi wanalia. Wamejikuta wameng'ang'ania sehemu ambayo wenye uwezo wa kutambua walimwambia hapana, yeye akalazimisha "ndiyo" sasa analia.

Je una uwezo wa kutambua..."nakupenda unayoisikia" au "Ndiyo" unayoisikia. Maana tunafahamu kwa sehemu, na wakati wa utoto tunafahamu kama watoto, kama bado una babaika kujibu "je ni Mungu au ni hisia zangu" ni heri ukaomba poooooo!!!! Mapema, na "ukajifunza kuongeza uwezo wako wa KiMungu wa ndani" wa Utambuzi wa utu uzima"

Nitaendelea maandalizi ya nne siku tati Zijazo....
Usikose....

Kwa msaada wa Roho Mtakatifu somo limeandikwa na
Ulenje Mwaipungu

Sunday, February 21, 2016

Part 3: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MISINGI IKIHARIBIKA...

Tuchokoze jambo hili la msingi kisha Part 4 tuanze kujadiri "mambo ya msingi ya kufanya maandarizi" kabla ya kusema Ndiyo!

"Huwezi chora ramani ya nyumba, baada ya kujenga msingi

Zaburi 11:3
Mfalme Daudi yeye anauliza
        "Kama misingi ikiharibika,
          Mwenye haki atafanya nini?

Huwezi jenga ghorofa la ngazi 30 kwa kujenga msingi wenye uwezo wa kubeba ghorofa la ngazi tano. Utachekwa tu.

Daudi anasema "mwenye haki atafanya nini" hajasema mwenye dhambi.

Si peke yako, hata wengi hujiuliza "nafunga sana, namtumikia Mungu kwa moyo wote, natoa zaka na dhabihu, ni mchungaji, ni askofu, ni mshirika mwaminifu sana, nampenda mke wangu, ni mwaminifu wa ndoa yangu, ila mbona ndoa yangu inasumbua?

Daudi anasema mwenye haki atafanya nini? Unafanya yote yanayokufanya uwe mwenye haki, ila ndoa haijakaa vema. Haleluya, nasema haleluya!. Hapa lazima kuna jambo la ziada la ambalo Daudi analifahamu.

Maandarizi kabla ya kusema ndiyo, maandarizi kabla ya kuingia kwenye ndoa, ni wakati wa muhimu sana kuliko hata ndoa yenyewe.

Maana msingi wa nyumba ni muhimu sana kuliko hata nyumba yenyewe.

Kuna wengine husema hayo mengine hujijua huko huko, kwani nani kazaliwa anajua, jibu ni fupi tu, unapotaka kujenga ghorofa la ngazi 30, na umeshajenga msingi wa ghorofa ya ngazi 10,  huwezi kubadirisha ramani wakati wa kujenga  ngazi ya 9, na kusema nataka ghorofa ya ngazi 30 na si ngazi 10. Wote watakushangaa, la sivyo itakulazimu ubomoe ngazi ulizojenga zote, kisha ubomoe msingi wote na ndipo uuweke msingi na upya kwa jinsi unavyotaka kubadiri, ambapo gharama yake ni kubwa sana kuliko hata ungekuwa makini mwakati wa kujenga msingi.

Huwezi kubadiri ramani ya nyumba  katikati ya ujenzi. Hivyo nathubutu kusema ni vema kutazama tunaujenga vipi msingi wa ndoa tunayotaka kuingia, hata kabla ya ndoa yenyewe.

KUMB:
        "Kama misingi ikiharibika,
           Mwenye haki atafanya nini

Usikose sehemu ya Nne, kumbuka ndiyo kiini cha somo. TUTAJADIRI maandarizi ya kufanya moja baada ya lingine.
Asante kwa kusoma.

Utukufu kwa Bwana Mungu na Mwanaye Yesu Kristo

Monday, February 15, 2016

Part 2. MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA "NDIYO..."

Nianzie hapa...

" huwezi kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Nazungumzia maandarizi kabla ya kusema "Ndiyo"

Yesu  anasema "maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumaliza?"

Na hii na ndiyo sababu ya ndoa nyingi kusumbua. Wengi tunaowa kwa miemko na kutazama umri, na si uwezo wetu wa ndani, na kutazama "kama una uwezo?" Ndoa si kuishi pamoja, kuna zaidi ya maana nyingi ya neno "kuishi pamoja".
Yesu analeta kesi mezani, anasema "Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, wakisema mtu huyu, alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza"

Siku hiyo niliishiwa nguvu, haikuwa na maana ya ugonjwa kuingia moyoni mwangu, "ilikuwa ni ishara ya kuwa sikuwa na nguvu za kujenga mnara unaitwa ndoa". Na haikuwa kesi ya umri, ilikuwa kesi ya uwezo wangu wa ndani wa kuwa na uhusiano wa uchumba. Kabla hujasema ndiyo, usiulize kama unampenda au kama anakupenda, ni swali dhaifu sana, usiulize umri wako ni swali dhaifu sana, kaa chumbank peke yako, jifanyie ukaguzi binafsi, ukiwa na Mungu wako, ikiwezekana muulize Mungu anayekujua zaidi, je una uwezo?. Kama huna kabla ya kusema "Ndiyo" chukua mda kuzingatia moyoni mwako, na ujenge uwezo kwanza. Alafu unajua nini cha ajabu, kuwa na uwezo haichukui mda, siku moja mpaka mbili kwa uwezo wa ndani, siku kadhaa kwa uwezo wa nje.
Twende pamoja...

Yesu ananifurahisha hapa anaposema "Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

Hii ni siri kubwa katika maisha "mazingira siku zote si rafiki" ndoa siku zote hutaka kuwapeleka ninyi chini, mgombane na mchukiane, dunia na matukio ya kimaisha siku zote si rafiki. Hivyo "kabla ya kusema Ndiyo, swali la msingi, je unaweza kupambana na mazingira ya ndoa na changamoto zake" usiogope, hakuna mtaaramu wa maisha, wote tunatembea kwenye neema ya Mungu, wote tuna matatizo yetu tusiyotaka kuyasema yote, ila swali, kwanini wengine wanapotea kwenye matatizo, ambayo wengine wanasimama? Tofauti ni ule uwezo wa ndani.

Wote wana changamoto fulani za ndoa, hata kama wana miaka 25-50 ya ndoa, wana vitu hawawezi kusema, ila katika hayo waliyopitia wakashinda, kuna wengine walianguka. Unaanza kunielewa, nini shida; Ni uwezo wa ndani ya mtu wa kukabiri changamoto na kuzishinda.

Yesu anamaliza kusema "na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali"

Waooo!!! Kama ukiona huwezi kumtii mwanaume kama vile unavyomtii Kristo na kumfanya awe kichwa kwako kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa, basi omba pooo! Mwanaume akali mbali"

 kama ukiona "huwezi kuvumilia makosa na udhaifu wa mwanamke/msichana, hata pale anapoweza kukuumiza sana kama vile Kristo anavyolivumilia kanisa, na kukubari kufa ili alisafishe, basi omba pooo mwanamke akali mbali" waoooo!!!! Incredible.

Kama huyawezi haya aliyoandika mtume Paulo waefeso 5:22-25
Omba pooooo mapema kabla ya mke au mume hajaja kwenye maisha yako.

Ngoja tumalize kabisa Yesu aliyosema kwenye hii luka 14.
"Basi kadharika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu". Kama haupo tayari kuacha aina ya maisha unayoishi, mitizamo yako na misimamo yako, marafiki zako wa kike na wakiume na mengine ambayo unayeanza naye uhusiano hataki, au yanaweza kusababisha kutoenderea na upendo wake kwako, basi omba pooo! Akali mbali, usiwe mke wake, au mume wake.

Yesu anamalizia "Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee?, haifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia. Na asikie. Waoooo! Ndoa ni kitu chema sana, ila kama kikiharibika itiwe nini hata ikolee, semina na semina zinafanyika, masomo na masomo yanaandikwa ila bado ndoa ni tatizo, kwanini? Hakuna maandarizi.

Swali "je unaweza kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Tuendelee kuchana nyavu, sehu ya tatu ipo njiani

Mungu alibariki neno lake.
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu Limeandikwa na Ev. Ulenje
0718721848.
imaf2b@gmail.com