Friday, July 16, 2021
NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI BORA WA YESU
Thursday, January 21, 2021
NAMNA HII HUPONYA NDOA MARA 100 ZAIDI.
Jambo hili likikosekana, mwanamke atachanganyikiwa, Mwanaume atakuwa wa lawama siku zote.
Nimetazama ndoa nyingi za mwanaume mvivu asiyejua majukumu yake.
Mwanamke akitazama kila kitu alichovaa ndani na nje, simu na vocha, na kila kitu alichonacho, kimetoka kwa mwanaume, Si tu, Atajivuna kwa marafiki, Lakini ATAKUHESHIMU na UTAMTAWARA.
MUNGU hakumpa Hawa Bustani, alimpa Adamu, Mungu hajawahi kumwambia Hawa ailime bustani, bali alimwambia Adamu, hata neno la kusema "matunda ya kila mti wa bustani waweza kula" MWA 2:16 hakumwambia Hawa, alimwambia Adamu.
Ina maana jukumu la kula na huduma, ni la Adamu kwenye familia, siyo Hawa. Ndiyo maana siku moja, siku moja tu, haikuhitaji nyingi, Adamu alipopumzika na kumuacha Hawa akajitafutie chakula, ndipo shetani anajitokeza, na ndipo anguko la familia ya kwanza linatokea, na madhara hadi sasa duniani tunayaona.
Nionyeshe familia ambayo, mwanamke anahusika kutafuta chakula, nitakuonyesha familia ambayo shetani amejenga nyumba karibu nao. Na ipo siku atawadondosha, as matter of time. GOD FORBID.
Hata uchumba ambao mwanamke ndiye chanzo cha pesa unahitaji mabadiliko.
Mwanaume asiyefanya kazi na kuhudumia mke wake na watoto, asitegemee kupata heshima na asiwe na tarajio la kumtawara mke wake. Biblia inasema...
Mithali 12 24
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
Ukiwa na bidii, bila hata kumwambia "niheshimu" bali akitazama wewe ndiyo chanzo cha kupendeza kwake, chanzo cha kula yake, chanzo cha kila kitu alichonacho. ATAKUHESHIMU automatic. Mwanamke anaheshimu sana chanzo cha heshima yake, shika sana hili neno.
Nikiwa nasoma chuo kikuu cha Dar es Salaam, nilikuwa nasoma huku nafanya biashara stendi ya Ubungo, asubuhi naamka naenda Kariakoo kufata bidhaa, ndipo naenda chuo. Jioni naenda kanisani kuonyesha sinema watu waokoke, nikirudi moja kwa moja maktaba kusoma, nilikuwa naomba mara nne hata zaidi kwa siku. Nilikuwa sina mkopo lakini kuna watu wenye mkopo niliwakopesha pesa.
Kwa neema ya Mungu sijawa pata Disco, Wala sijawa Carry, Wala sijawahi fanya SAP, Na bado msimu wa mvua nilirudi Morogoro kulima, maana nilikataa kula unga wa dukani kwenye maisha yangu, na mchumba wangu alitumia Smartphone ambayo mimi nilinunua na nilimuongezea pesa za kutosha katika biashara yake. Kwanini nilikataa kuwa mvivu.
Nakumbuka watu waliniita speed man, sababu nilikuwa natembea speed ni hatari.
Vijana wa kizazi hiki Mungu atusaidie tuache uvivu. Tuhudumie familia zetu. Bila kujali mke anafanya kazi gani, usihesabu pesa yake, hesabu majukumu yako.
Kama bado hujapata kazi inayoendana na elimu yako nikutie moyo, 2021 Inuka "Kabla hujapata unachotafuta kufanya, fanya kilicho mbele yako" (before you find what you finding to do, do what you find"
Suleman anasema Mhubiri 9 10
"Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.
Kabla hujafa kama masikini, angalau ionekane umejaribu kuushinda umaskini, maana hakuna aliyeandikiwa umasikini. Wewe ni mzao mteule, umeumbwa kwa mfano wake anaye miliki mbingu na nchi. You're Born A Winner, God can never birth a failure, even once.
Mwanaume ambaye mke wake ndiye anahudumia kila kitu, ni ngumu hata kumuuliza mke wako "unaenda wapi?" maana atakujibu "nisipotoka tutakula nini!, acha nitoke ile tule"
Ukiona ukiulizwa Ada ndiyo unaanza kuwa rohoni, jua kuna shida mahali.
Mwanume kuhudumia familia ni utukufu kwa Mungu, maana ndivyo alivyoumba, mmoja mfanyakazi mmoja msaidizi.
Nimalize kusema, Mithali 13 4
Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.
Ukiwa mvivu utatamani amani ya familia, utatamani uheshimiwe, lakini hutopata.
Na kuna wanaume ambao ni wachapakazi, wana pesa ila si wahudumiaji wa wake zao. Ndugu haijarishi kiwango cha pesa ulichonacho. Mwanamke anaheshimu sehemu ya chanzo chake cha heshimu. Mwanamke anapoishi na mwanaume asiyehudumia, hujiona ni bora kuishi na masikini.
Aliyekwambia kumpa zawadi mchumba wako dhambi nani, hata asipokumbuka sms zako, atakumbuka fadhila na utu wako.
Na mwanamke unayesoma ujumbe huu kumbuka...
Mke mwema... "Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato" MITH 31:11.
Mwanamke aliyejiweka kuwa mchumba au mke mwema ni, Biblia inasema hatakosa mapato. Hata kama hatofanya, lakini kama wewe ni mke mwema hutokosa mapato. Juhudi yako, ya kuhudumia familia yako, mume akiwa mbali, itaamsha akili yake, na atakuamini na hutokosa mapato.
Nionyeshe mwanamke mchapakazi na ni mwema kwa mumewe, huyo ndiye ambaye Mumewe atamwamini, na hatakosa mapato.
Ubarikiwe Sana.
Kwa Msaada wa Roho Limeandikwa na.
Pastor Ulenje EM.
0683-477827
2021 INAWEZEKANA.
Sunday, January 17, 2021
USIOGOPE, AMINI TU. MARKO 5:36.
Mathayo 19 26
Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.
Mungu anataka tufanikiwe,
Kumbukumbu la Torati 30 15
Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;
Mafanikio siyo karama, mafanikio ni uchaguzi. Mungu amekupa kuchagua kufanikiwa au kushindwa. Ila amekupa ushauri, chagua mafanikio.
INAWEZEKANA
1. Ni Kumwambia Mtu, Kuna Njia ya Kufanya ili Hilo Jambo Lifanikiwe.
Inawezekana alijaribu akashindwa kama Musa. Au wenda amejaribu mara nyingi sasa ameona haiwezekani. Au mbele yake anaona giza, hakuna kitu anaona anaweza fanya tena.
Sasa unamwambia INAWEZEKANA.
Katika kila jambo ambalo Mungu anaruhusu litokee kwenye maisha yako, kila mpango una njia ya kufanya. Kuna kitu hujajua tu bado ndiyo maana hujafanikiwa mpaka sasa.
Kuna mambo siyo kwamba hatuwezi ila kuna sehemu, kuna kanuni bado hatuijui.
Katika kila jambo linaloonekana haliwezekani, ni kweli kwamba kuna njia ya kulifanya liwezekane. Hata unayoyaona leo yamefanyika, mwanzo yalionekana hayawezekani. Mwaka 1904 wana sayansi walikutana Uingereza kuthibitisha kuwa hakuna kitu kinaweza tembea angani. Lakini Ndugu wawili watoto wa Wright maarufu kama Wright Brothers, waligomea maamuzi yale, wakasema inawezekana. Mwaka 1910 wakatembeza ndege kwa mara ya kwanza.
Siyo kwamba haiwezekani, Tatizo umekata tamaa, kutafuta nini unatakiwa ufanye. Bado ipo Njia.
Marko 5:
Mwanamke alitokwa na damu miaka mingi na kuteswa na madaktari wengi, lakini alipogundua njia ya uzima wake. Kuwa nikigusa pindo la Yesu nitapona, akapona. Usikate tamaa, bado kuna kitu unaweza fanya ukafanikiwa.
Si kwamba haiwezekani, ila hujapata mbinu ya Kufanya. Unajua kujua namna ya kufanya mambo kunaondoa miaka mingi ya mateso ba kutoa jasho.
Kumb 2:1-3 Israeli walizunguka miaka mingi ndani ya jangwa wasiione njia. Siku moja Mungu akasema mlivyozunguka mlima huu vyatosha, geukeni upande wa kaskazini.
Israel wakakata tamaa, kuzunguka mda mrefu, siyo kwamba njia ya kufika haikuwepo, ila hawakuijua.
2021 Mungu anakwenda kukupa njia ya kufanya katika Jina la Yesu. Pokea.
Israel walipata neno la Mungu, neno likawaonyesha cha kufanya. Petro alifanya kazi ya kuchosha neno liliposhuka likampa cha kufanya, Mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12 alisikia habari za Yesu.
Kuna neno unalihitaji likupe cha kufanya...
A. Soma neno, Yoshua 1:8
B. Omba, Yoshua aliomba. Yoshua 7:6
C. Tafakari, kaa chini fikiri... Mda unaotumia kulia, ungekaa na kufikiri Neno La Mungu linasema nini kuhusu jambo lako na mpango wako, ungekuwa umeshapata njia.
D. Omba ushauri. MITH 13:10.
2. Unamwambia mtu Ambaye Anaona Jambo Au Mpango Hauwezekani.
Wakwanza anaona hakuna njia, huyu wa sasa anaona haliwezekani kabisa. Anaona ni jambo kubwa sana. Anaona ni mpango mkubwa kumzidi. Anaona Ha! Ngoja niwaze mengine, hii ni ndoto tu ya utotoni. Au watu wengi ameona hawajaweza na wengine wamemwambia haiwezekani.
Lakini naomba sikia....
Hakuna jambo haliwezekani kwa mtu aliyeokoka isipokuwa jambo lile ameliona yey mwenyewe kuwa haliwezekani.
Yesu anasema anabisha yupo mlangoni anabisha hodi mtu akifungua nitaingia ndani yake UFUN 3:20.
Aliyeingia ndani yako, Yeye anaweza yote. MATH 19:26 hilo kwa wanadamu haliwezekani ila kwa Mungu yote yanawezekana.
Yoh 14:10 Yesu anasema "bali ni Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake"
Kol 1:29 Paulo anasema "nikijitahidi kwa kadiri ya kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu.
Tangu ulipookoka Mungu anafanya kazi ndani yako.
Fil 2:13 Neno linasema "Ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, katika kulitimiza kusudi lake jema.
Mungu yupo ndani yako kufanya hilo jambo liwezekane, Mungu aliye ndani yako, kwake yote yanawezekana.
Math 17:20 anasema "
Mathayo 17 20
Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
Maana yake, Ukiona ugumu unaongezeka, badala ya kukata tamaa, wewe amini sana.
Kuona inawezekana ndiyo mwanzo wa kushinda mambo yanayoonekana hayawezekani.
__Yesu alimwambia Yairo (Marko 5:36) "Usiogope, Amini Tu"
Kumbe 2021 Mungu anaposema Yote Yanawezekana, anasema "Usiogope, wewe inua imani yako"
A. Kula chakuka cha imani_ Neno. RUM 10:17
B. Meng'enya hiko chakula_ Tafakari YOSH 1:8
C. Tendea kazi_ Tumia hilo neno. YAK 1:22
D. Usiyumbishwe_ EBR 10:34 usiyumbishwe kile umeamini unapoona ugumu unaongezeka au kwa maneno ya watu.... Yesu hana too late.
3. Unamwambia Mtu Anayeona Hana Uwezo Wa Kufanya.
Anajiona hana uwezo. Hana uwezo wa kifedha, elimu, ndugu, mtaji, upako.
Hakuna mlima mrefu kwa mwanadamu, mlima ni jinsi wewe unavyouona. Maana hata mlima mrefu kuliko yote duniani, watu wameupanda.
Mungu bado hajaumba mwanadamu ambaye hawezi kitu. Alipoumba akasema "ni chema sana" vingine vyote alipotazama akasema ni vema, lakini kwa mwanadamu akasema chema sana.
Mafanikio yana siri hii, Ukijiona huwezi hutoweza. Ila ukijiona unaweza utaweza. Simba siyo mnyama mwenye nguvu kuliko wanyama wote, siyo mnyama mrefu kuliko wanyama wote, wala siyo mnyama menene kuliko wote.... Ila yeye ndiye mfalme wa mwitu.
Kwanini anapokutana nao, wao wanaogopa, ila yeye haogopi yoyote. Hata wale wenye nguvu zana. Tembo anaangusha mti, ila anakutana na simba analiwa, kwanini simba anaona "pamoja ni mnene wewe ni chakula"
Ukiona huwezi hutoweza, kwanini "siku ukisema naweza, basi utatafuta njia kwa kila hari, na utaweza"
Mwanamke mjamzito miezi 8, ilipotokea hatari aliruka ukuta. Aliambiwa rudia alishindwa. Kwanini, mwanzo alipoona hatari, kuna kitu kilisema ndani yake. UNAWEZA.
HESABU 13 MUSA anatuma wapelelezi, Wanarudi wanasema nchi ni nzuri, ila wanajiona hawana uwezo wa kuitamalaki. Wote wanafia jangwani.
Lakini Yoshua na Karebu wakasema "twaweza kushinda bila shaka HES 13:30.
Wengi wanapishana na mafanikio yao, uponyaji wao, majibu ya maombi yao, na kushindwa changamoto sababu wanaona haiwezekani. Inuka sema INAWEZEKANA.
Wanasema "Hakuna cha kufanya" No "Kipo cha Kufanya"
Wanasema "Hakuna Njia" No "Njia ipo"
Unajua kwanini wanaosema hatuwezi huwa hawawezi "Sababu huwa hawafanyi hiko kitu"
Wanajeshi wa Israel walipoona hawawezi kunshinda Goloathi hata kumfata hawakumfata... Lakini Daudi aliona anaweza, AKAMFATA.... Kwa Jiwe tu Down.
Unachokiogopa na kukiona ni kigumu.... Ni kidogo sana.
Tengeneza ufahamu kuwa Unaweza. Aliye ndani yako ni Mkuu Kuliko Chochote.
Mungu anatembea na watu wanaosema "Haijalishi Ugumu, Itafanyika"
_________________________
LAKINI KUMBUKA....
Neno linasema "bali kwa Mungu yote yawezekana"
Maana yake_ Lazima Mungu ahusike. Biblia ya Kingereza inasema "with God, All things are possible"
Mungu hawezi husika mpaka umeomba. Paulo alifanya mambo makubwa ambayo wengine walishindwa, siri yake anasema...
Filipi 4:13 "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu"
Mungu akikutia nguvu yote yatawezekana kwako.
Maombi, Maombi, Maombi.
Lazima 2021 Tuombe Zaidi ya Miaka Mingine, kama tunataka kufanya yaliyoshindikana yawezekane.
Unapoomba Unapata Vitu Viwili.
1. Uso wa Mungu_ Unakutana na uso wa Mungu kukupa njia ya kufanya, na nguvu zake.
2. Mkono wake_ wa kukusaidia unapokwama. Israel walikwama Misri na kufanywa watumwa lakini kwa Mkono wake aliwatoa.
3. Roho Mtakatifu_ kusafisha njia na kukufanya iwe unstoppable, uwe na ujasiri, uwe na imani, kukufanya ufanye mambo ambayo wanadamu wa kawaida hawawezi.
Unabii unapotoka unatoka kwa wote, lakini ni maamuzi ya mtu binafsi kufanya unabii utokee kwenye maisha yake. Hauji kuomba kumridhisha mchungaji, ila ni kwa ajili yako, ili upige hatua.
Leo unaona unaenda, ila kuna hatua ili upige ni lazima uombe leo. Kila mtu anakutana na hatua zisizowezekana, na ni hatua zisizowezekana zinawafanya watu wakuzidi kiuchumi na kiroho.
0718 721848
0683 477827
Pastor Ulenje EM
Tuesday, May 2, 2017
SHETENI HANA HARAKA
Monday, April 24, 2017
UBIZE NA MUEREKEO WA KANISA.
Bila kupinga tunaishi dunia ya watu bize sana,
asubuhi baba kazini, akifika ni bize, hata mama anayebaki nyumbani pia ni bize_ ameshika kupiga deki, kuosha vyombo, mtoto n.k.
wafanyabiashara na wajasiliamari ni bize...
sasa kuja kwa simu za Smartphone na vipindi vizuri vya TV na siasa kuchukua sehemu kubwa ya maisha; basi ubize umeongezeka_ asubuhi lazima uguse Facebook, na kundi la whatsapp limesema nini, bado hujafika kutazama picha nzuri instagram, na sentensi fupi twitter...
unaporudi jioni, mama ni kupika, baba taarifa ya habari, huku anacheza na simu mkononi akicheka na marafiki fb, na whatsapp...
TUMEKUWA BIZE SANA...
MPAKA TUNASAHAU....kuomba, Kusoma neno, kutafakari sheria na hukumu za Mungu, na namna ya kutenda kazi ndani ya ufalme...
Dada mmoja (jina nahifadhi) nilipomwambia kuna wakati sipokea simu, sijibu sms, wala whatsapp hata kama sms ni nzuri_ Alisema nalinga, LAKINI: Naijua faida ya kutenga masaa ya simu, whatsapp, insta na fb.
***Sasa Siku ya Jumapili si siku ya BWANA TENA, bali ndiyo siku ya KUPUMZIKA...
Hata kanisani tunaomba ibada iishe mapema, ili tukale na kupumzika na familia nyumbani, na kuna rafiki ndiyo siku ya kuja kukusalimu.
huwezi kukataa "NI MAMBO MENGI LEO YANACHUKUA MDA WETU MWINGI, ambao, TUNGETUMIA KUTAFAKARI, KUPANGA NA KUMJUA MUNGU ZAIDI.
- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa ni mda wamaombi?
- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa wa kusoma neno
- Ni kipi kimeiba mda wako wa kutafakari
- Ni kipi kimechukua shahuku yako ya kushuhudia
- Ni kipi kimechukua pesa yako ya sadaka na kuchangia injili_ ni vocha au bando...
***Unafikiri ni hekima kusoma neno Dk 30 na kukaa mtandao Saa 1.30 na zaidi....Kuomba lisaa 1, na kukaa mtandaoni usiku Masaa 2. IS NOT FAIR, kweli IS NOT FAIR....
NAAMINI
Ukitazama nyuma kabla huna smartphone kuna vitu ulikuwa hufanyi sasa unafanya
kuna udhaifu ulikuwa huna, sasa unao
kuna dhambi inakutesa na ilikuwa haikutesi
kuna mda unamwibia Mungu...
Tunapokuwa Bize tuangalie TUSIMSAHAU Mungu wetu,
tuangalie TUSITENDE dhambi
YESU aliposema "Upendo wa wengi utapoa, alimaanisha alichosema, na alimaanisha kama alivyosema.
Ujumbe kwa wote_ We must Refocus_
#ChurchBACKtoFocus.
Written by
Ev. Ulenje
Director CWGM
Inspire by the Holy Spirit.
fungua ulenje.blogspot.com kwa masomo zaidi.
Sunday, April 23, 2017
Kanuni Moja MUHIMU, Kumtafuta Mungu Nyakati Hizi.
Kanuni MUHIMU, Mimi naona ni muhimu sana, kwa kila mtu kuijua na kuiweka moyoni, na kuifanyia kazi.
Nianze na kusema, Mungu alisema kwa wana wa Israel "Mtanitafuta na 'kuniona', mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote" Ye
maana ya "kumtafuta kwa moyo wote" ukiipata, ndiyo mwanzo wa kuanza kumtafuta Mungu kama Mungu anavyotaka, na utakuwa ndiyo mwanzo wa kumpata.
NI KAMA HIVI...
Kijana mmoja akamfata mzee tajiri na kumwambia "nataka kuwa tajiri kama wewe", Yule tajiri akamwambia tuonane kesho saa nne asubuhi ufukweni mwa bahari.
kijana akashangaa " kuna uhusiano gani kati ya kutaka utajiri na kwenda ufukweni"
Tajiri akamsisitiza "unataka utajiri, kesho saa nne asubuhi njoo Ufukweni"
Kesho kijana akafika ufukwe wa bahari akiwa amevaa suti amependeza saa nne asubuhi, Tajiri akamwambia "anza kupiga hatua kuingia ndani ya bahari". Kijana akaanza kupiga hatua, maji yakafika magotini, Maji yakafika mabegani, yakafika mdomoni, tajiri anazidi kumwambia aende. Maji yalipofika puani, anashindwa kuhema, kijana akatoka haraka majini, akasema "huyu mzee ana kichaa". Mzee akamfata kwa haraka na kumshika kichwa na kumzamisha kichwa ndani ya maji_ Kijana akaanza kuhangaika ajitoe,
maana alikuwa anashindwa kuhema. Tajiri akaendelea kumkandamiza ndani ya maji. kwa mda baada ya kijana kuhangaika sana, akamtoa. Kisha akamuuliza "Je! Unapokuwa ndani ya maji, nini hasa unataka?"
Kijana akajibu "nataka kuhema"
Tajiri akamjibu "Hadi utakapofika wakati wa kutaka utajiri kama unavyotaka kuhema, hapo utakuwa tajiri"
NINI MAANA YAKE...
Tuhamishe hii hadithi kwetu watu wenye fikra tofauti na ulimwengu, sisi tumeagizwa kutafuta kwanza ufalme wa Mungu na mengine tutazidishiwa.
neno hili liki-ingia moyoni mwako, KUMTAKA MUNGU KAMA UNAVYOTAKA PUMZI"
kati ya kitu muhimu sana kwetu ni pumzi, na tunahakikisha hatuipotezi_ na ndiyo HITAJI NAMBA MOJA KWETU.
Unapokuwa ndani ya maji, huwezi kutazama simu, TV, mama, Wala kumsikiliza mjomba, wala mume, au mke ila ni moja tu KUPATA KUHEMA..
Sidhani kama utakumbuka kula, au kuchati, kama unataka unatafuta pumzi, bali unachohitaji ni PUMZI TU.
UKIFIKA kumtaka Mungu namna hiyo_ Kuacha vyote na kushughurika na kumtaka kama unavyohitaji pumzi...
UTAKUWA UMEFIKA KUMTAKA KWA MOYO WOTE.
KANUNI YA PILI: Sema KANUNI namba 1 hata mara saba zaidi, asubuhi na jioni, mpaka uone inajisema yenyewe moyoni, hapo itakuwa imechukua maisha yako yote.
Sema nami
NIKIMTAKA MUNGU SANA KAMA NINAVYOTAKA KUHEMA NITAMPATA ZAIDI.
Ukifika kumtafuta Mungu, na kuona huwezi ishi pasipo Yeye, ukarudia kusema hata ikafika moyoni, itachukua moyo wako wote.
Jina la Bwana Libarikiwe
Contact: 0718721848
Sunday, November 27, 2016
UNAONAJE?
Utofauti wa Mungu na wanadamu katika kuona vitu,
1. Mwanadamu anaona mwanzo kisha mwisho, Mungu anaona mwisho kisha anarudi mwanzo na kupanga namna ya kufika mwisho
2. Mwanadamu anaona nje na kuweka hitimisho, Mungu anatazama ndani kwanza kisha anafanya cha ndani kuonekana nje.
3. Mwanadamu anatazama pito/jaribu, Mungu anatazama matokeo ya pito.
4. Mwanadamu anatazama mwisho wa kitu Mungu anatazama baada ya mwisho.
5. Siku zote Mwisho wa mwanadamu ndiyo mwanzo wa Mungu
6. Ana heri yule ajuaye mawazo ya Mungu kuliko yule ajuaye matendo ya Mungu, ishara na miujuza ya Mungu
I.e ana heri yule amjuaye Mungu kuliko yule anayejua matendo ya Mungu.
7. Kila anayetaka kuwa hodari wa imani kwanza lazima ajue mawazo ya Mungu na Mungu mwenyewe
8. Imani huonekana tu mahari ambapo hapana majibu
Kama sehemu ina majibu hapo siyo imani
9. Imani ni kuamini kitu ambacho hujawai kuona kutokea.
Mfano wa Martha, kuamini mtu wa siku nne kufufuka, hajawahi ona, lakini Yesu alipomwambia Yeye ndiyo huo ufunguo aliamini.
10. Kufikia ukamilifu wa Kristo ni kufikia kwenye imani ya Kristo
11. Imani ni kufika wakati wa ulichosoma kwenye neno na kuhubiliwa unakuta ni tofauti kwenye maisha halisi unayopitia, na ukazidi kuamini, ukiamini kuwa aliyeahidi ni mwaminifu.
12. Mungu hufanya na huruhusu kila kitu kwa kusudi lake.
13. Mungu unayemtumikia kuna wakati hayupo kukuepusha usipate matatizo, mjaribu, kushindwa, udhaifu, na majaribu bali yupo ili akupitishe katika hayo kwaajili ya utukufu wake.
14. Unapaombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.
Usiogope unapopitia hayo, maana ni Mungu wako amekupitisha.
Kama ukitaka kuwa na Mungu anayekuepusha na majaribu basi 80% ya Biblia ilipaswa tuitoe, maana asilimia zaidi ya asilimia 80 ya Biblia ni hadithi za watu waliopitia mateso na majaribu, kuanzia mwanzo mpaka ufunuo
Na kipimo cha wewe kuwekwa kwenye Biblia ni kupitishwa kwenye majaribu, mateso na udhaifu
Written by
Ev. Ulenje
Wednesday, October 5, 2016
SIRI YA KUFIKIA MAFANIKIO HARAKA
Mungu hawezi kukupa kazi, au mafanikio makubwa na kukukabidhi mapenzi yake kwasababu bado unawaza kidunia (Misri).
Kama unataka kufanikiwa haraka _pambana na fikra yako,
Jitahidi kufanana na Yesu unavyofikiri na kuamua (ondoka Misri). Jinsi unavyobaki kidunia basi Mungu anakuchukua katika safari ndefu. Anajua huwezi kukabiri vita vya Kanaani, bado unajiona panzi
Itazame dunia kama Yesu anavyoitazama "Utakuwa namna unavyotazama"
Watu waliozaliwa ndani ya wokovu. Shika sana imani ya wazazi wako. Vizazi vilipozidi na walipokaa sana Kanaani wakasahau agano ambalo Mungu alifanya na baba zao, wakaanza kuabudu miungu mingine.
Mungu aliwauwa kwasababu hawakutaka kufikiri kama Yeye Mungu anavyofikiri. Kuna namna nyingi za kumshusha utukufu Mungu, ila zote huanzia kwenye fikra. neno la Mungu. Mungu alitamani wawatazame majitu kama Yeye anavyowatazama.
Yesu ametuokoa kutoka ulimwenguni, kazi sasa kuishi ulimwenguni kama watu wa mbinguni. Kanaani ni mbinguni: hapa katikati wale ambao bado wanawaza kama Misri tutawaacha jangwani.
Wewe hukuwa mtenda dhambi ulizaliwa mwenye dhambi, Yesu alituokoa na utumwa huo.
Monday, September 19, 2016
THE MEANING OF LIFE: OUR LIFE Part 3
Our life is filled with three phases: becoming, Doing, and Legacy. You cant jump from one stage to another.
In fact what you do now, tell us what you chose to become or unintentional chose to become.
Nothing you do is accident. That you didn't plant in your heart one day.
1. BECOMING
For smart people, this is a phase of becoming themselves , or what you chose anyhow.
For insecure person, this is a stage of trying to be somebody, (he see they are great, or he is impressed by them). And for brainwashed people, this is their stage of becoming like American, or English people.
And majority of them, they become anybody: trying to copy anybody, moving from someone to another one, today they copy Reinhard Bonke, tomorrow they copy Don Moen, Next day they copy Women of Faith, Hillsong, they copy Populat singers and popular preacher, instead of being themselves. And their dressing style, they don't even care what are they type, they try to copy J Zee, tomorrow they copy Diamond, Next day Jennifer Lopez, Rose Muhando.
2. DOING
General Principle "You will sow what you reap, you reap what you sow"
After you become what you chose to become, or what you try harder to become then you start doing (intentionally or unintentionally)
After you become a woman or man of prayer then it become your habit and simple to pray, After you become woman and man of faith then you believe everything are possible and big things, after you become a preacher and evangelist then you preach, after you become a giver the you give, after you become son of God then you walk like God.
We will see how someone becoming, I know you have desire to become someone, while you're not, and may be you try harder and harder and you fail. But through this message Holy Spirit is going to help you, and you will find is very simple to cancel what you wont to Be, and start becoming what you want to become.
In another side, you were trying to smoke and now you become a smoker, you tried to commit fornication and now you become a fornicator, you take slide many thing and now you become a procrastinator, lazy and poor.
What you're now, is what you sow.
Wise people, they are so curious to know, are they becoming what they're born to do, if is not, they change direction, and start becoming what they're born to do.
Wise example is Abraham, Moses, Peter, Poul and Luke. Who changed direction to become what they had been to become. I'm happy with Luke who turn from a doctor and a trader into a kingdom writer of the gospel and act of apostles.
To be continued
For more
0718 721848
Friday, August 26, 2016
DISCOVER THE MEANING OF LIFE FROM BIBLICAL VIEW
2. DOING
this is second phase of life, is very important phase, while its important determined by how you spend the first phase, and how fast you're to work with opportunities that God provide according to your purpose.
Look Jesus First: After Jesus becoming what He was born to become A Savior (the First Phase) then He immediately start doing.
He start to preach the gospel of the Kingdom in all towns, clean leapers, heal the deaf, make the blind to see, rise the dead, and cancel demons. Crucified and rise from the dead, and give salvation to all mankind.
In fact Jesus start doing, after he completely becoming what he was born to do.
Know who you are, then becoming what you discover you're, then immediately start doing what you become. Procrastination is tragedy.
"Know who you're, Become It, Immediately Do it"
~ Ev.Ulenje
Remember God will test you first to prove and to qualify you. He will never chose you because you qualify, but he will qualify you first or within the work.
3. LEGACY (After Life)
This is final phase of every human.
"Nothing is powerful than death"
Ev. Ulenje
When you die, everything die; despite the great plans and dream you have, the vision and great course, and career, but when death show up_everything die.
Fear of death cant stop death, only preparation for it and doing effective with life you have make death have no power. In fact the cure of all diseases and fear is death, when you die no diseases or fear can touch you. Only what you have done carry your name after you die, not your good clothes.
Its better to be victim of what you have done, than to be the king of what you procrastinate. At the end, the matter of all things is what you have done. Its better to live a short life of Glory than the long one of obscurity (anonymous)
After Jesus finished his work; Teach good news to the poor, set captivity free, open the blind, heal the broken heart, and preached the acceptable year of the Lord, He die on the cross, Resurrect, Announce the Great announce ever announced, that "It is Finished", he immediately went back to heaven, he didn't say Father no! I love the world. No because He knew the first and second phase is done, Now is time for legacy phase.
Note this: when He Go, His disciples immediately start preaching what he preach: the gospel of the kingdom.
Why? This is what He leave. He leave the generation who were Fisher of fish, he work hard with little sleep and uncomfortable rest to make them Fisher of man, and Kingdom Expansion Agents....the Question; what are you doing????
AFTER VISIBLE LIFE
What happen now?!: Jesus was not in visible world.....
Jesus finish His work, return to invisible world where He come from.... but look_his idea, perspectives, culture, thought and moral and life make him alive in visible world.
Think with me, sometimes you don't need to receive healing or answers for your prayers to feel the presence of Jesus in the world. In fact Jesus is not present in Visible world now, but you cant Ignore this Great eternal public figure in visible world_ we mention Him in books, Broadcastings, wearing clothes with His name, make Christmas trees and use His principles.
Act 11:26 is When Christian in Antioch who were consumed with Jesus Christ, and out of abundance of their heart their action, idea and their life perspective speak, people they called them Christian.
Act 24:5 Christian in Palestine after they consumed with Jesus, their action and idea of life speak, then people of Palestine they called then Nazarenes— to refer the nick name they called Jesus (Math 2:23)
These are few legacies am talking about.
You can do that too_You can live after you die_it's not ok to die in anonymity. Be ready to pay the price.
"The legacy need more commitment than people are willing to pay"
Get some of example of people who are still alive while they died: Paul, John, Peter, Luke, Timothy the Apostles, Martin Luther King Jr, John Wesley, T.R Osborn, Myles Monroe, Oral Robert, Mother Teresa, Nelson Mandera, J.K Nyerere, Bishop Kurola etc.
Next part we gonna Focus How these Three phases work in our life and how to use them effective.
Thank you for reading....
Ev.Ulenje.
Director CWGM
GLORY TO GOD WHO IS SOURCE OF ALL TRUTH.