Saturday, April 23, 2022

JUA UNDANI KUHUSU MAISHA YA MILELE

 *** MAISHA YA MILELE NA MWAMINI 


-( 1 Wathesalonike 4:13-18)

-Kwanini tunajifunza maisha ya milele? Ni muhimu sababu mtu ataweza ishi kwa kujizuia (mithali 29-18).

-Mtu anaejua Kuna maisha ya milele ataishi kwa umakini Sana

-MUNGU ametupa maisha ya sasa ili tujiandae na maisha ya milele


- MUNGU ametupa maisha ya sasa ni mchujo na kigezo kikubwa alichoweka ni utii Yani unae mtii ndie BWANA  wako

- Tamaa za shetani ni 

1)Tamaa ya mwili

2)Tamaa ya dunia

3)Kiburi Cha uzima


*Mwanadamu akifa anaenda wapi ??

- katika Agano la kale neno walilopata ni kuzimu (Zaburi 49-14) Yani walio haki na wasio haki wote wanaenda kuzimu ( Zaburi 88-3)

-YESU anakuja kutuonyesha kuwa kule kuzimu walitenganishwa walio haki na wasio haki ( Luka 16-19) YESU anatuletea neno peponi na jehanamu.


-Mtu asiyeokoka akifa anaelekea jehanamu ( Marko 9-45)

-Mwenye haki akifa anaelekea peponi( luka 23-43)

- peponi sio mbingu mpya peponi ni Mahali pa kufarijiwa

-Jehanamu sio Mahali pa mwisho kwa wasio haki Mahali pa mwisho ni kwenye ziwa la moto ( ufunuo 21-13)

- Walio haki wakifa wanaelekea peponi wakisubili pia hukumu kwa matendo ya mwili waliofanya baada ya kuokoka .

- peponi sio Mahali pa mwisho kwa waliokoka Bali ni mbingu mpya ama yerusalem mpya biblia inasema Mahali huko  ni pazuri hamn mfano Kuna Kuna dhahabu Safi Kama bilauri pia Kuna kuta nne ambazo marefu na mapana yake zimefanana kuta zimepambwa na madin Kama zumaridi  ,yakuti nk

- katika yerusalem mpya hutokumbuka maumivu 


* Nini maana ya kufa kwa mwamini ???

-Ni kuondoka toka mwili huu wa batili na kwenda kukaa na BWANA(2 Wakorinto5-6)

- Paulo alitamn kukaa na BWANA (wafilipi 1-21)

-Paulo anasema tuziweke kando zile dhambi zinazotuzuia( waebrania 12-1)


* Unaishi kwa ajili ya Nani???

- MUNGU anasema mbele yenu nimeweka uzima na mauti Ila chagueni uzima ( kumbukumbu la torati 30-19)

-(wafilipi 1-21)

-(warumi 6-21)


* Kiti Cha hukumu Cha KRISTO 

- Kwa walio haki

-wafu watafufuliwa kuungana na walio hai siku ile ya parapanda kuu ( 1wakorinto 15:50-53)

-(warumi 14-10)

-(2 wakorinto 5-10)

- sisi tuliokoka hatutahukumiwa pamoja na wasiokoka sisi tutahukumiwa maisha yetu baada ya kuokoka 

- Paulo anasema wengine kazi zao zitaungua Kama nyasi anasema wataokoka Ila kwa Moto 

 

* Vitu ambavyo tutatolea hesabu 

1)namna gani umeshiriki kuleta watu kwa KRISTO ( Daniel 12-3)

2) kwa habari ya ulimi 

3) kwa habari ya kushindwa dhambi( warumi 6:1-4)


-From pastor ulenje EM

Written by kayombo jr

Friday, July 16, 2021

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI BORA WA YESU

25/06/2021, PREACHED 27/06/2021 AT VICTORY EMPOWERMENT TEMPLE 

FANYIKA MWANAFUNZI

WEWE NI ZAIDI YA JINSI ULIVYO. UNAWEZA KUWA ZAIDI YA JINSI ULIVYO LEO.


Yesu aliwakuta wanafunzi wake wakiwa wavuvi, hata Galilaya walikuwa hawafahamiki, lakini walipofanyika wanafunzi, wakafika mpaka kwa Wayunani, mpaka Asia. 
Unaweza kufanyika zaidi ya jinsi ulivyo leo, kwa sababu unaweza kufanyika mwanafunzi. Kufanyika mwanafunzi wa Yesu ni daraja la kukuvusha daraja la maisha, ni ngazi ya kupanda ngazi nyingine ya maisha. Kama unawaza wapi pa kuanzia ili upae kimaisha, basi anzia na kufanyika mwanafunzi wa Kristo.

Kusudi la Kristo ni Kujipatia Watumishi.

Math 28:19, Yesu anasema, “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Yesu anaweka wazi, anataka wanafunzi. Na ukweli hajatutuma kukufundisha bali kukufanya mwanafunzi. Yesu amekuokoa ili uwe mwanafunzi.
Yesu anasema “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; MATH 11:29.

Ukisoma mstari wa juu yake ‘28’ anasema “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”. Kusumbuka iwe mwisho_ umekopa sana kufanikisha mipango, umeomba, umetafuta, umelia_ leo nenda kwa Yesu_ kanunue Biblia sema “nitajifunza kwa Mungu nami nipumzike, nipate raha”

Kwanini uwe mwanafunzi?

1. Sababu mwanafunzi pekee ndiye unaweza kumbadirisha. 
Anayekufundisha anakufanya uwe mtu fulani_ na hasa anakufanya yeye alivyo. 
Yesu hataki ujifunze kwa dunia, kwa sababu ukijifunza kwa dunia utakuwa kama dunia. Ila ukijifunza kwa Yesu utakuwa kama Yeye. Yesu anasema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake”. LUKA 6:40. 
Yesu anataka uwe kama yeye. Na dunia wanataka uwe kama wao_ lakini wote hao ni wageni hapa duniani, Yesu ni zamani kuliko wote_ wote wameikuta Biblia_ na ina shuhuda ya kufanikisha wengi_ ni bora leo ukachagua kuwa mwanafunzi wa Yesu. 
Unapofungua Biblia na kusoma, unafanyika neno, unafanyika kama Yesu.

     ✅ Yesu Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu” MATH 4:19. Yesu anataka akubadirishe kutoka mtu fulani uwe mtu mwingine, 
Kila aliyeamua kufanyika mwanafunzi_ baada ya mda fulani, watu wakasema “siyo yule tunayemjua” wengine kwa mshangao wanasema “ni wewe kweli, au mwingine”
  Paulo anasema “Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ROM 8:30. TENA Anasema “tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 KOR 3:18.
Usijipime leo, Hayo unayopitia ni milima na mabonde tu ya njiani_ fanyika mwanafunzi_ wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo. Kuna mtu Yesu anamtengeneza mwenye utukufu zaidi ya ulio nao leo. 

2. Sababu anataka akujulishe siri za ufalme.
Ukishasikia siri, maana yake kuna watu maalumu wanaostahili kujua. Yesu hakuja kumwambia kila mtu siri za ufalme wake, bali wanafunzi wake pekee. Yesu anawaambia wanafunzi wake “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa” MATH 13:11. 


3. Sababu anataka akutumie.
Yesu hajawahi kutumia mtu ambaye hajafanyika mwanafunzi. “watu wengi walimwamini…lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; YOH 2:23, 24. Kumwamini haina maana yeye amekuamini, na sifa ya kumuamini siyo kuwa mkamilifu, bali kuwa mwanafunzi. Pamoja na udhaifu alio nao Petro, lakini Yesu alimvumilia na akamuachia kanisa, kwanini_ wakati wengine wamekimbia, yeye akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, YOH 6:68.
Mungu sasa anataka kutumia watu wa kila sekta, wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, waimbaji ili kujipatia mavuno na kutangaza jina lake_ ili kuipa aibu dunia… wewe fanyika mwanafunzi. Naye atakutumia. 

Siyo Kila Mtu ni Mwanafunzi.

Kwenye biblia kuna makutano na wanafunzi. Kuhudhuria kanisani na kuokoka haina maana wewe ni mwanafunzi.
Unaweza ukahudhuria kanisani miaka 40 lakini usiwe mwanafunzi, kwasababu uwanafunzi siyo miaka uliyookoka, wala uliyohudhuria kanisani, uanafunzi ni maamuzi, siyo kuhudhuria. Wote ni mashahidi hasa kwa walimu ambao wanachapa sana, tulikuwa tunahudhuria darasani lakini tunasikia lakini hatusikilizi. 
Yesu anasema “Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. MATH 13:14, 15.
15. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Tunajuaje kuwa wewe ni mwanafunzi?

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI WA YESU.

Tuone sasa namna, unaweza kuwa mwanafunzi. Ni vigezo gani mwanafunzi anavyo.

1. Mwanafunzi Analiamini na Kulikubali Neno Lote.
Siyo nusu, siyo moja_ yote. 
Yesu siku zote alitumia maneno magumu ili kuchambua wanafunzi na makutano. Biblia inasema “wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena” wakakimbia wote, wakabaki wanafunzi tu. YOH 6:64-69. 
 Nao akawauliza “Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Petro akajibu akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, Nasi tumesadiki, tena tumejua wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu”. Mwanafunzi anaamini yote. Paulo anasema “…nikiyaamini yote…” MDO 24:14. 
Na huwezi sema umeamini mpaka umekubali ulichosikia, umekipokea na kukitendea kazi ulichosikia. 
Huwezi sema ni mwanafunzi mpaka umekubali, na kukishika kile mwalimu amesema. Na mwalimu wetu ni Yesu, na shule yake ni Biblia. Na anatumia watumishi wake kukueleza alichoandika. Paulo hajaandika Biblia, Mathayo hajaandika Biblia, mimi sijaandika Biblia_ wote waliandika yale Roho Mtakatifu amesema, nami nahubiri yale Biblia imesema. Nami natenda hayo hayo na naona matokeo, na Mungu amenituma nisema nawe, ili tuinuke pamoja.


2. Moyo wa unyenyekevu.
Pasipo moyo wa unyenyekevu huwezi kumfundisha mtu yeyote. 
Mtu mwenye kiburi anajua kila kitu, hata ambacho yeye mwenyewe anajua kuwa hajui. Lakini atalazimisha kwa maneno mengi kuwa anajua. 
Watu kama hao_ hawawezi kuwa wanafunzi. Sababu wanaenda kwa Mungu, huku wakiwa na ya kwao. 
Wanasema Mungu tufundishe, lakini kama ni kinyume na aliyosema mjomba, bwana vicoba, hatuwezi kukusikiliza.
Hakuna kazi ngumu kama kumfundisha mwanafunzi mwenye tution nyingi.
 
Yesu anasema “kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa” LUKA 14:11. Unafikiri kwanini Mungu anainua wanyenyekevu, kwa sababu mnyenyekevu ni kama mtoto anabebeka (Math) anafundishika,
Mungu anasema “…Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. ISAYA 48:17

Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko. MITH 16:18.

3. Mwanafunzi wa Yesu  Anakuwa.

Sifa ya mwanafunzi ni kukuwa. 
Kila mwalimu anapima mwanafunzi wake kwa kukuwa katika kile anamfundisha. 
Haijarishi umetokeo wapi kwenye wokovu, lakini kila siku inabidi ukue kila eneo_ kuomba, kusoma neno, kuhudhuria ibada, kufunga, kushuhudia.
Yesu anasema “Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini. MATH 13:23.

4. Mwanafunzi lazima awe ametubu.

Yesu anapoanza injili yake tu_ akasema nini ufanye ili uwe mwanafunzi wake.
Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. MATH 4:17

Kutubu siyo kuomba msamaha, ni zaidi ya hapo. Kutubu ni kubadiri unavyowaza, kubadiri mfumo wa maisha.

Yesu anaweka wazi, nimewakuta mna ufalme wa dunia hii, sasa geukeni acheni kuwaza na kufanya kama dunia, sasa muwaze na kufanya mambo kama ufalme wa mbinguni unavyotaka.

Others
5. Usiogope watu
Huwezi kuwa mwanafunzi kama unaogopa watu wanasema nini. Sababu siku zote Yesu anakwambia mambo ambayo watu hawataki, ni kinyume na wanavyojua, ni kinyume na wanavyotaka uishi. Kilichomponza Sauli ni kuogopa watu, akaacha kufanya Mungu alichomfundisha.
Yesu akasema 
6. Jikane mwenyewe_ luka 14:26
7. Beba msalaba wako_ luka 14:27

Hitimisho.
Omba unyenyekevu na maombi ya agano_ kuwa wanafunzi. Na weka agano kutenda nini neno linasema.

Ushauri au maombi.
0683 477 827 
0718 721848 

Thursday, January 21, 2021

NAMNA HII HUPONYA NDOA MARA 100 ZAIDI.


Jambo hili likikosekana, mwanamke atachanganyikiwa, Mwanaume atakuwa wa lawama siku zote.

Nimetazama ndoa nyingi za mwanaume mvivu asiyejua majukumu yake.

Mwanamke akitazama kila kitu alichovaa ndani na nje, simu na vocha, na kila kitu alichonacho, kimetoka kwa mwanaume, Si tu, Atajivuna kwa marafiki, Lakini ATAKUHESHIMU na UTAMTAWARA.

MUNGU hakumpa Hawa Bustani, alimpa Adamu, Mungu hajawahi kumwambia Hawa ailime bustani, bali alimwambia Adamu, hata neno la kusema "matunda ya kila mti wa bustani waweza kula" MWA 2:16 hakumwambia Hawa, alimwambia Adamu.

Ina maana jukumu la kula na huduma, ni la Adamu kwenye familia, siyo Hawa. Ndiyo maana siku moja, siku moja tu, haikuhitaji nyingi, Adamu alipopumzika na kumuacha Hawa akajitafutie chakula, ndipo shetani anajitokeza, na ndipo anguko la familia ya kwanza linatokea, na madhara hadi sasa duniani tunayaona.

Nionyeshe familia ambayo, mwanamke anahusika kutafuta chakula, nitakuonyesha familia ambayo shetani amejenga nyumba karibu nao. Na ipo siku atawadondosha, as matter of time. GOD FORBID.

Hata uchumba ambao mwanamke ndiye chanzo cha pesa unahitaji mabadiliko.

Mwanaume asiyefanya kazi na kuhudumia mke wake na watoto, asitegemee kupata heshima na asiwe na tarajio la kumtawara mke wake. Biblia inasema...

Mithali 12 24
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.

Ukiwa na bidii, bila hata kumwambia "niheshimu" bali akitazama wewe ndiyo chanzo cha kupendeza kwake, chanzo cha kula yake, chanzo cha kila kitu alichonacho. ATAKUHESHIMU automatic. Mwanamke anaheshimu sana chanzo cha heshima yake, shika sana hili neno.

Nikiwa nasoma chuo kikuu cha Dar es Salaam, nilikuwa nasoma huku nafanya biashara stendi ya Ubungo, asubuhi naamka naenda Kariakoo kufata bidhaa, ndipo naenda chuo. Jioni naenda kanisani kuonyesha sinema watu waokoke, nikirudi moja kwa moja maktaba kusoma, nilikuwa naomba mara nne hata zaidi kwa siku. Nilikuwa sina mkopo lakini kuna watu wenye mkopo niliwakopesha pesa.

Kwa neema ya Mungu sijawa pata Disco, Wala sijawa Carry, Wala sijawahi fanya SAP, Na bado msimu wa mvua nilirudi Morogoro kulima, maana nilikataa kula unga wa dukani kwenye maisha yangu, na mchumba wangu alitumia Smartphone ambayo mimi nilinunua na nilimuongezea pesa za kutosha katika biashara yake. Kwanini nilikataa kuwa mvivu.

Nakumbuka watu waliniita speed man, sababu nilikuwa natembea speed ni hatari.

Vijana wa kizazi hiki Mungu atusaidie tuache uvivu. Tuhudumie familia zetu. Bila kujali mke anafanya kazi gani, usihesabu pesa yake, hesabu majukumu yako.

Kama bado hujapata kazi inayoendana na elimu yako nikutie moyo, 2021 Inuka "Kabla hujapata unachotafuta kufanya, fanya kilicho mbele yako" (before you find what you finding to do, do what you find"

Suleman anasema Mhubiri 9 10
"Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.

Kabla hujafa kama masikini, angalau ionekane umejaribu kuushinda umaskini, maana hakuna aliyeandikiwa umasikini. Wewe ni mzao mteule, umeumbwa kwa mfano wake anaye miliki mbingu na nchi. You're Born A Winner, God can never birth a failure, even once.

Mwanaume ambaye mke wake ndiye anahudumia kila kitu, ni ngumu hata kumuuliza mke wako "unaenda wapi?" maana atakujibu "nisipotoka tutakula nini!, acha nitoke ile tule"

Ukiona ukiulizwa Ada ndiyo unaanza kuwa rohoni, jua kuna shida mahali.

Mwanume kuhudumia familia ni utukufu kwa Mungu, maana ndivyo alivyoumba, mmoja mfanyakazi mmoja msaidizi.

Nimalize kusema, Mithali 13 4
Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

Ukiwa mvivu utatamani amani ya familia, utatamani uheshimiwe, lakini hutopata.

Na kuna wanaume ambao ni wachapakazi, wana pesa ila si wahudumiaji wa wake zao. Ndugu haijarishi kiwango cha pesa ulichonacho. Mwanamke anaheshimu sehemu ya chanzo chake cha heshimu. Mwanamke anapoishi na mwanaume asiyehudumia, hujiona ni bora kuishi na masikini.

Aliyekwambia kumpa zawadi mchumba wako dhambi nani, hata asipokumbuka sms zako, atakumbuka fadhila na utu wako.

Na mwanamke unayesoma ujumbe huu kumbuka...

Mke mwema... "Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato" MITH 31:11.

Mwanamke aliyejiweka kuwa mchumba au mke mwema ni, Biblia inasema hatakosa mapato. Hata kama hatofanya, lakini kama wewe ni mke mwema hutokosa mapato. Juhudi yako, ya kuhudumia familia yako, mume akiwa mbali, itaamsha akili yake, na atakuamini na hutokosa mapato.

Nionyeshe mwanamke mchapakazi na ni mwema kwa mumewe, huyo ndiye ambaye Mumewe atamwamini, na hatakosa mapato.

Ubarikiwe Sana.
Kwa Msaada wa Roho Limeandikwa na.
Pastor Ulenje EM.
0683-477827
2021 INAWEZEKANA.


Sunday, January 17, 2021

USIOGOPE, AMINI TU. MARKO 5:36.

 Mathayo 19 26 

 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.



Mungu anataka tufanikiwe,


Kumbukumbu la Torati 30 15 

 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;



Mafanikio siyo karama, mafanikio ni uchaguzi. Mungu amekupa kuchagua kufanikiwa au kushindwa. Ila amekupa ushauri, chagua mafanikio.


INAWEZEKANA


1. Ni Kumwambia Mtu, Kuna Njia ya Kufanya ili Hilo Jambo Lifanikiwe.


Inawezekana alijaribu akashindwa kama Musa. Au wenda amejaribu mara nyingi sasa ameona haiwezekani. Au mbele yake anaona giza, hakuna kitu anaona anaweza fanya tena.


Sasa unamwambia INAWEZEKANA.


Katika kila jambo ambalo Mungu anaruhusu litokee kwenye maisha yako, kila mpango una njia ya kufanya. Kuna kitu hujajua tu bado ndiyo maana hujafanikiwa mpaka sasa.


Kuna mambo siyo kwamba hatuwezi ila kuna sehemu, kuna kanuni bado hatuijui.


Katika kila jambo linaloonekana haliwezekani, ni kweli kwamba kuna njia ya kulifanya liwezekane. Hata unayoyaona leo yamefanyika, mwanzo yalionekana hayawezekani.  Mwaka 1904 wana sayansi walikutana Uingereza kuthibitisha kuwa hakuna kitu kinaweza tembea angani. Lakini Ndugu wawili watoto wa Wright maarufu kama Wright Brothers, waligomea maamuzi yale, wakasema inawezekana. Mwaka 1910 wakatembeza ndege kwa mara ya kwanza.


Siyo kwamba haiwezekani, Tatizo umekata tamaa, kutafuta nini unatakiwa ufanye. Bado ipo Njia.


Marko 5:

Mwanamke alitokwa na damu miaka mingi na kuteswa na madaktari wengi, lakini alipogundua njia ya uzima wake. Kuwa nikigusa pindo la Yesu nitapona, akapona. Usikate tamaa, bado kuna kitu unaweza fanya ukafanikiwa.


Si kwamba haiwezekani, ila hujapata mbinu ya Kufanya. Unajua kujua namna ya kufanya mambo kunaondoa miaka mingi ya mateso ba kutoa jasho.


Kumb 2:1-3 Israeli walizunguka miaka mingi ndani ya jangwa wasiione njia. Siku moja Mungu akasema mlivyozunguka mlima huu vyatosha, geukeni upande wa kaskazini.


Israel wakakata tamaa, kuzunguka mda mrefu, siyo kwamba njia ya kufika haikuwepo, ila hawakuijua.


2021 Mungu anakwenda kukupa njia ya kufanya katika Jina la Yesu. Pokea.


Israel walipata neno la Mungu, neno likawaonyesha cha kufanya. Petro alifanya kazi ya kuchosha neno liliposhuka likampa cha kufanya, Mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12 alisikia habari za Yesu.


Kuna neno unalihitaji likupe cha kufanya...


A. Soma neno, Yoshua 1:8

B. Omba, Yoshua aliomba. Yoshua 7:6

C. Tafakari, kaa chini fikiri... Mda unaotumia kulia, ungekaa na kufikiri Neno La Mungu linasema nini kuhusu jambo lako na mpango wako, ungekuwa umeshapata njia.

D. Omba ushauri. MITH 13:10.


2. Unamwambia mtu Ambaye Anaona Jambo Au Mpango Hauwezekani.


Wakwanza anaona hakuna njia, huyu wa sasa anaona haliwezekani kabisa. Anaona ni jambo kubwa sana. Anaona ni mpango mkubwa kumzidi. Anaona Ha! Ngoja niwaze mengine, hii ni ndoto tu ya utotoni. Au watu wengi ameona hawajaweza na wengine wamemwambia haiwezekani.


Lakini naomba sikia....


Hakuna jambo haliwezekani kwa mtu aliyeokoka isipokuwa jambo lile ameliona yey mwenyewe kuwa haliwezekani.


Yesu anasema anabisha yupo mlangoni anabisha hodi mtu akifungua nitaingia ndani yake UFUN 3:20.


Aliyeingia ndani yako, Yeye anaweza yote. MATH 19:26 hilo kwa wanadamu haliwezekani ila kwa Mungu yote yanawezekana.


Yoh 14:10 Yesu anasema "bali ni Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake"


Kol 1:29 Paulo anasema "nikijitahidi kwa kadiri ya kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu. 


Tangu ulipookoka Mungu anafanya kazi ndani yako.


Fil 2:13 Neno linasema "Ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, katika kulitimiza kusudi lake jema.


Mungu yupo ndani yako kufanya hilo jambo liwezekane, Mungu aliye ndani yako, kwake yote yanawezekana.


Math 17:20 anasema "

Mathayo 17 20 

 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.


Maana yake, Ukiona ugumu unaongezeka, badala ya kukata tamaa, wewe amini sana.


Kuona inawezekana ndiyo mwanzo wa kushinda mambo yanayoonekana hayawezekani.


__Yesu alimwambia Yairo (Marko 5:36) "Usiogope, Amini Tu"


Kumbe 2021 Mungu anaposema Yote Yanawezekana, anasema "Usiogope, wewe inua imani yako"


A. Kula chakuka cha imani_ Neno. RUM 10:17

B. Meng'enya hiko chakula_ Tafakari YOSH 1:8

C. Tendea kazi_ Tumia hilo neno. YAK 1:22

D. Usiyumbishwe_ EBR 10:34 usiyumbishwe kile umeamini unapoona ugumu unaongezeka au kwa maneno ya watu.... Yesu hana too late.



3. Unamwambia Mtu Anayeona Hana Uwezo Wa Kufanya.


Anajiona hana uwezo. Hana uwezo wa kifedha, elimu, ndugu, mtaji, upako.


Hakuna mlima mrefu kwa mwanadamu, mlima ni jinsi wewe unavyouona. Maana hata mlima mrefu kuliko yote duniani, watu wameupanda.


Mungu bado hajaumba mwanadamu ambaye hawezi kitu. Alipoumba akasema "ni chema sana" vingine vyote alipotazama akasema ni vema, lakini kwa mwanadamu akasema chema sana.


Mafanikio yana siri hii, Ukijiona huwezi hutoweza. Ila ukijiona unaweza utaweza. Simba siyo mnyama mwenye nguvu kuliko wanyama wote, siyo mnyama mrefu kuliko wanyama wote, wala siyo mnyama menene kuliko wote.... Ila yeye ndiye mfalme wa mwitu.


Kwanini anapokutana nao, wao wanaogopa, ila yeye haogopi yoyote. Hata wale wenye nguvu zana. Tembo anaangusha mti, ila anakutana na simba analiwa, kwanini simba anaona "pamoja ni mnene wewe ni chakula"


Ukiona huwezi hutoweza, kwanini "siku ukisema naweza, basi utatafuta njia kwa kila hari, na utaweza"


Mwanamke mjamzito miezi 8, ilipotokea hatari aliruka ukuta. Aliambiwa rudia alishindwa. Kwanini, mwanzo alipoona hatari, kuna kitu kilisema ndani yake. UNAWEZA.


HESABU 13 MUSA anatuma wapelelezi, Wanarudi wanasema nchi ni nzuri, ila wanajiona hawana uwezo wa kuitamalaki. Wote wanafia jangwani.


Lakini Yoshua na Karebu wakasema "twaweza kushinda bila shaka HES 13:30.


Wengi wanapishana na mafanikio yao, uponyaji wao, majibu ya maombi yao, na kushindwa changamoto sababu wanaona haiwezekani. Inuka sema INAWEZEKANA.


Wanasema "Hakuna cha kufanya" No "Kipo cha Kufanya"


Wanasema "Hakuna Njia" No "Njia ipo" 


Unajua kwanini wanaosema hatuwezi huwa hawawezi "Sababu huwa hawafanyi hiko kitu"


Wanajeshi wa Israel walipoona hawawezi kunshinda Goloathi hata kumfata hawakumfata... Lakini Daudi aliona anaweza, AKAMFATA.... Kwa Jiwe tu Down.


Unachokiogopa na kukiona ni kigumu.... Ni kidogo sana.


Tengeneza ufahamu kuwa Unaweza. Aliye ndani yako ni Mkuu Kuliko Chochote. 


Mungu anatembea na watu wanaosema "Haijalishi Ugumu, Itafanyika"


_________________________



LAKINI KUMBUKA....


Neno linasema "bali kwa Mungu yote yawezekana" 


Maana yake_ Lazima Mungu ahusike. Biblia ya Kingereza inasema "with God, All things are possible"


Mungu hawezi husika mpaka umeomba. Paulo alifanya mambo makubwa ambayo wengine walishindwa, siri yake anasema...


Filipi 4:13 "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu"


Mungu akikutia nguvu yote yatawezekana kwako.


Maombi, Maombi, Maombi.


Lazima 2021 Tuombe Zaidi ya Miaka Mingine, kama tunataka kufanya yaliyoshindikana yawezekane.


Unapoomba  Unapata Vitu Viwili.


1. Uso wa Mungu_ Unakutana na uso wa Mungu kukupa njia ya kufanya, na nguvu zake.

2. Mkono wake_ wa kukusaidia unapokwama. Israel walikwama Misri na kufanywa watumwa lakini kwa Mkono wake aliwatoa.

3. Roho Mtakatifu_ kusafisha njia na kukufanya iwe unstoppable, uwe na ujasiri, uwe na imani, kukufanya ufanye mambo ambayo wanadamu wa kawaida hawawezi.


Unabii unapotoka unatoka kwa wote, lakini ni maamuzi ya mtu binafsi kufanya unabii utokee kwenye maisha yake. Hauji kuomba kumridhisha mchungaji, ila ni kwa ajili yako, ili upige hatua.


Leo unaona unaenda, ila kuna hatua ili upige ni lazima uombe leo. Kila mtu anakutana na hatua zisizowezekana, na ni hatua zisizowezekana zinawafanya watu wakuzidi kiuchumi na kiroho.


0718 721848

0683 477827

Pastor Ulenje EM



Tuesday, May 2, 2017

SHETENI HANA HARAKA

SHETENI HANA HARAKA

Soma ni muhimu....
Mara nyingi watu husumbuliwa na baadhi ya tabia, au kuwa nazo kwa kujua au kutojua_ hasa ni Kiburi, Uvivu, Tamaa ya mwili, tamaa ya macho, Kupenda pesa, maneno mengi, na matumizi mabaya ya fedha... na kushinda katika kila jambo...na kushinda kupanda kiroho. 

Mara nyingi tunashughurika sana na kumurika Miguuni, tunasahau kuwa adui wa miguuni huanzia mbali, kabla ya kufika miguuni. Ukweli ni kwamba mengi yanayotusumbua leo ni matunda tu ya magugu ambayo ibilisi aliyapanda wakati tulipolala, na wakati anapanda ukweli, hakuwa na haraka_ alijua mbegu itaota, kama mwenye shamba asipoamka mapema.
Ulipokuwa unafanya baadhi ya vitu na ukiona ni kawaida, na wakati mwingine mama, ndugu, au rafiki walinyamaza kimya, au wewe mwenyewe uliona kuwa ni kawaida tu, ila leo mti umeota, matunda yanaonekana_ ndipo unashituka. 

siandiki kumsifu shetani, naandika ili kufichua mbinu kubwa ambayo shetani hutumia dhidi ya watumishi na wakristo wengi...hasa kutufanya tusifike mbali.

"Shetani hana haraka..." Ni neno lilibadiri muerekeo mkubwa wa maisha na matendo yangu. Mama yangu katika huduma (Mama Nyagawa) aliniambia, akinisisitiza kuwa **sasa sina kiburi ila napaswa kuwa makini, maana shetani hana haraka, hupanda kiburi leo, akitegemea kesho atavuna

nafikiri alimaanisha kama nilivyoelewa "kuwa napaswa kulinda adui asipande mbegu" ndipo nikakumbuka Yesu alivyosema "lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake" 

Napenda kutazama na kucheza, (mpira wa kikapu),  moja ya wachezaji wa NBA ninaowapenda sana ni Stephen Curry,  naamini ni mchezaji bora hajawahi tokea tangu wakati wa Michael Jordan. 
Siku moja Stephen Curry alifunga gori katikati ya wachezaji na wazuiaji waliobobea na hata kupewa tuzo kama Briant, lakini mchambuzi alipovuta picha kwa karibu akaona Curry amefunga lile gori akiwa amefumba macho, kila mtu alishangaa, kweli kudumbukiza kile kitundu cha kikapu ukiwa umefumba macho!!
Lakini_ Siku ya jana yake, Curry alifanya mazoezi kudumbukiza mpira kwenye kikapu, upande ule aliyotumia kufunga gori mara 77. Fikiri sasa!!
"Stephen Curry alitumia kumbukumbu ya misuri, hakuhitaji macho"

Unapofanya jambo mara kwa mara, mara kwa mara_ kwa kujua au kutokujua,  baadae inaingia kwenye mifupa_ na ikishaingia kwenye mifupa, TABU ndipo huanza. Mtu hujaribu kuacha na kubadirika, akipata matokeo madogo. wazungu huita "Addiction" na wengine hufanya wasijue_ kuwa wanakosea, hata kujihesabia haki, hata wakisikia injili,  mchana watafanya lile lile.
"Mambo mengi ambayo mtu hufanya katika nusu ya pili ya maisha yake, ni yale aliyopanda katika nusu yake ya kwanza"

BADO LIPO TUMAINI
Kama ilivyo jino kwa jino, jicho kwa jicho, Yesu amesema "Kesheni basi... 
Paulo amesema "msimpe ibilisi nafasi" Efeso 4:7
Hakikisha ni nini kinapandwa kwako...
JIBU NI MOJA: Muwahi shetani_ tuwe wajanja kama nyoka na wapole kama ua...Anza kupanda tabia unazotaka

ANZA KUPANDA TABIA UNAZOTAKA
Andika chini VIPI UNATAKA KUWA, Andika kwa peni, na anza Siku hiyo hiyo kufanya mazoezi ya hizo tabia...itachukua mda lakini nakwambia tena ndani ya siku 360 utanipa matokeo...ukifanya hivyo kwa mwaka itakuwa ni tabia yako.

"utapata shida mwanzo, ukifanya na kufanya na kufanya... ila baadae itaingia mifupani... na ikiingia mifupani tu, wewe ni mshindi...

Amka asubuhi saa 10...kuomba
Anza kuomba zaidi ya saa moja kabla ya kulala
Anza kusoma neno saa zaidi ya moja kila siku
Anza kuwa mfadhiri
anza kuhubiri injili kwa mmoja mmoja
anza kutoa sadaka, zaka na shukrani n.k

Anza kuwa unavyoitaka leo_ kama AMIRA inavyoenea taratibu ndani ya ngano na kuiteka ngano yote, ndivyo tabia njema itateka mwili wako wote.
NINI UNATAKA KUWA
Andika chini tabia nzuri zote unazotaka kuwa nazo, Anza leo kuzifanya, itakuaa shida, utaona kushindwa...ila songa mbele "unaposhindwa, usilie kuacha safari, lia kuendelea"

SIKIA NENO MUHIMU
"Haupo una-po-taka KUWA sababu haupo una-vyo-taka KUWA"
Anza kujenga unavyotaka kuwa leo_ Ili baadae uwe unapovyotaka na unapotaka kuwa.
Shetani anapanda tabia kwa siri, sababu anajua wengi hupotea wanapofika juu na kukosa tabia za kuwatunza wabaki juu...
Usikose somo lijalo
Kwa msaada wa Roho mtakatifu 

Ev.Ulenje 
Director CWGM. 
Contact: 0718721848 , imaf2b@gmail.com . 


Monday, April 24, 2017

UBIZE NA MUEREKEO WA KANISA.

BUSY AND WORK...

Bila kupinga tunaishi dunia ya watu bize sana,
asubuhi baba kazini, akifika ni bize, hata mama anayebaki nyumbani pia ni bize_ ameshika kupiga deki, kuosha vyombo, mtoto n.k.

wafanyabiashara na wajasiliamari ni bize...

sasa kuja kwa simu za Smartphone na vipindi vizuri vya TV na siasa kuchukua sehemu kubwa ya maisha; basi ubize umeongezeka_ asubuhi lazima uguse Facebook, na kundi la whatsapp limesema nini, bado hujafika kutazama picha nzuri instagram,  na sentensi fupi twitter...

unaporudi jioni, mama ni kupika,  baba taarifa ya habari, huku anacheza na simu mkononi akicheka na marafiki fb, na whatsapp...

TUMEKUWA BIZE SANA...

MPAKA TUNASAHAU....kuomba, Kusoma neno, kutafakari sheria na hukumu za Mungu, na namna ya kutenda kazi ndani ya ufalme...

Dada mmoja (jina nahifadhi)  nilipomwambia kuna wakati sipokea simu, sijibu sms, wala whatsapp hata kama sms ni nzuri_ Alisema nalinga, LAKINI: Naijua faida ya kutenga masaa ya simu, whatsapp, insta na fb.

***Sasa Siku ya Jumapili si siku ya BWANA TENA, bali ndiyo siku ya KUPUMZIKA...

Hata kanisani tunaomba ibada iishe mapema, ili tukale na kupumzika na familia nyumbani, na kuna rafiki ndiyo siku ya kuja kukusalimu.

huwezi kukataa "NI MAMBO MENGI LEO YANACHUKUA MDA WETU MWINGI, ambao, TUNGETUMIA KUTAFAKARI, KUPANGA NA KUMJUA MUNGU ZAIDI.

- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa ni mda wamaombi?
- Ni kipi kimechukua mda wako uliokuwa wa kusoma neno
- Ni kipi kimeiba mda wako wa kutafakari
- Ni kipi kimechukua shahuku yako ya kushuhudia

- Ni kipi kimechukua pesa yako ya sadaka na kuchangia injili_ ni vocha au bando...

***Unafikiri ni hekima kusoma neno Dk 30 na kukaa mtandao Saa 1.30 na zaidi....Kuomba lisaa 1, na kukaa mtandaoni usiku Masaa 2. IS NOT FAIR, kweli IS NOT FAIR....

NAAMINI
Ukitazama nyuma kabla huna smartphone kuna vitu ulikuwa hufanyi sasa unafanya
kuna udhaifu ulikuwa huna, sasa unao
kuna dhambi inakutesa na ilikuwa haikutesi
kuna mda unamwibia Mungu...

Tunapokuwa Bize tuangalie TUSIMSAHAU Mungu wetu,
tuangalie TUSITENDE dhambi

YESU aliposema "Upendo wa wengi utapoa, alimaanisha alichosema, na alimaanisha kama alivyosema.

Ujumbe kwa wote_ We must Refocus_
#ChurchBACKtoFocus.

Written by
Ev. Ulenje
Director CWGM

Inspire by the Holy Spirit.
fungua ulenje.blogspot.com kwa masomo zaidi.

Sunday, April 23, 2017

Kanuni Moja MUHIMU, Kumtafuta Mungu Nyakati Hizi.

KUMTAFUTA MUNGU KATIKA NYAKATI HIZI

Kanuni MUHIMU,  Mimi naona ni muhimu sana, kwa kila mtu kuijua na kuiweka moyoni, na kuifanyia kazi.

Nianze na kusema, Mungu alisema kwa wana wa Israel "Mtanitafuta na 'kuniona', mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote" Ye

maana ya "kumtafuta kwa moyo wote" ukiipata, ndiyo mwanzo wa kuanza kumtafuta Mungu kama Mungu anavyotaka, na utakuwa ndiyo mwanzo wa kumpata.

NI KAMA HIVI...
Kijana mmoja akamfata mzee tajiri na kumwambia "nataka kuwa tajiri kama wewe", Yule tajiri akamwambia tuonane kesho saa nne asubuhi ufukweni mwa bahari.
kijana akashangaa " kuna uhusiano gani kati ya kutaka utajiri na kwenda ufukweni"
Tajiri akamsisitiza "unataka utajiri, kesho saa nne asubuhi njoo Ufukweni"
Kesho kijana akafika ufukwe wa bahari akiwa amevaa suti amependeza saa nne asubuhi, Tajiri akamwambia "anza kupiga hatua kuingia ndani ya bahari". Kijana akaanza kupiga hatua, maji yakafika magotini, Maji yakafika mabegani, yakafika mdomoni, tajiri anazidi kumwambia aende. Maji yalipofika puani, anashindwa kuhema, kijana akatoka haraka majini,  akasema "huyu mzee ana kichaa". Mzee akamfata kwa haraka na kumshika kichwa na kumzamisha kichwa ndani ya maji_ Kijana akaanza kuhangaika ajitoe,

maana alikuwa anashindwa kuhema. Tajiri akaendelea kumkandamiza ndani ya maji. kwa mda baada ya kijana kuhangaika sana, akamtoa. Kisha akamuuliza "Je! Unapokuwa ndani ya maji, nini hasa unataka?"
Kijana akajibu "nataka kuhema"
Tajiri akamjibu "Hadi utakapofika wakati wa kutaka utajiri kama unavyotaka kuhema, hapo utakuwa tajiri"

NINI MAANA YAKE...
Tuhamishe hii hadithi kwetu watu wenye fikra tofauti na ulimwengu,  sisi tumeagizwa kutafuta kwanza ufalme wa Mungu na mengine tutazidishiwa.

neno hili liki-ingia moyoni mwako,  KUMTAKA MUNGU KAMA UNAVYOTAKA PUMZI"

kati ya kitu muhimu sana kwetu ni pumzi, na tunahakikisha hatuipotezi_ na ndiyo HITAJI NAMBA MOJA KWETU.
Unapokuwa ndani ya maji, huwezi kutazama simu, TV, mama, Wala kumsikiliza mjomba, wala mume, au mke ila ni moja tu KUPATA KUHEMA..
Sidhani kama utakumbuka kula, au kuchati, kama unataka unatafuta pumzi, bali unachohitaji ni PUMZI TU.
UKIFIKA kumtaka Mungu namna hiyo_ Kuacha vyote na kushughurika na kumtaka kama unavyohitaji pumzi...
UTAKUWA UMEFIKA KUMTAKA KWA MOYO WOTE.

KANUNI YA PILI: Sema KANUNI namba 1 hata mara saba zaidi, asubuhi na jioni, mpaka uone inajisema yenyewe moyoni, hapo itakuwa imechukua maisha yako yote.
Sema nami
NIKIMTAKA MUNGU SANA KAMA NINAVYOTAKA KUHEMA NITAMPATA ZAIDI.
Ukifika kumtafuta Mungu, na kuona huwezi ishi pasipo Yeye, ukarudia kusema hata ikafika moyoni, itachukua moyo wako wote.
Jina la Bwana Libarikiwe

Contact: 0718721848

Sunday, November 27, 2016

UNAONAJE?

KUFIKIA UKAMILIFU WA KRISTO


Utofauti wa Mungu na wanadamu katika kuona vitu,
1. Mwanadamu anaona mwanzo kisha mwisho, Mungu anaona mwisho kisha anarudi mwanzo na kupanga namna ya kufika mwisho

2. Mwanadamu anaona nje na kuweka hitimisho, Mungu anatazama ndani kwanza kisha anafanya cha ndani kuonekana nje.

3. Mwanadamu anatazama pito/jaribu, Mungu anatazama matokeo ya pito.

4. Mwanadamu anatazama mwisho wa kitu Mungu anatazama baada ya mwisho.

5. Siku zote Mwisho wa mwanadamu ndiyo mwanzo wa Mungu

6. Ana heri yule ajuaye mawazo ya Mungu kuliko yule ajuaye matendo ya Mungu, ishara na miujuza ya Mungu
I.e ana heri yule amjuaye Mungu kuliko yule anayejua matendo ya Mungu.

7. Kila anayetaka kuwa hodari wa imani kwanza lazima ajue mawazo ya Mungu na Mungu mwenyewe

8. Imani huonekana tu mahari ambapo hapana majibu
Kama sehemu ina majibu hapo siyo imani

9. Imani ni kuamini kitu ambacho hujawai kuona kutokea.
Mfano wa Martha, kuamini mtu wa siku nne kufufuka, hajawahi ona, lakini Yesu alipomwambia Yeye ndiyo huo ufunguo aliamini.

10. Kufikia ukamilifu wa Kristo ni kufikia kwenye imani ya Kristo

11. Imani ni kufika wakati wa ulichosoma kwenye neno na kuhubiliwa unakuta ni tofauti kwenye maisha halisi unayopitia, na ukazidi kuamini, ukiamini kuwa aliyeahidi ni mwaminifu.

12. Mungu hufanya na huruhusu kila kitu kwa kusudi lake.

13. Mungu unayemtumikia kuna wakati hayupo kukuepusha usipate matatizo, mjaribu, kushindwa, udhaifu, na majaribu bali yupo ili akupitishe katika hayo kwaajili ya utukufu wake.

14. Unapaombiwa utukufu wa Mungu huonekana mwisho, si mwisho wa Mwanadamu, ni mwisho alioupanga Mungu, ambapo ni baada ya mwisho wa mwanadamu.

Usiogope unapopitia hayo, maana ni Mungu wako amekupitisha.
Kama ukitaka kuwa na Mungu anayekuepusha na majaribu basi 80% ya Biblia ilipaswa tuitoe, maana asilimia zaidi ya asilimia 80 ya Biblia ni hadithi za watu waliopitia mateso na majaribu, kuanzia mwanzo mpaka ufunuo
Na kipimo cha wewe kuwekwa kwenye Biblia ni kupitishwa kwenye majaribu, mateso na udhaifu
Written by
Ev. Ulenje

Wednesday, October 5, 2016

SIRI YA KUFIKIA MAFANIKIO HARAKA

SIRI YA KUFIKIA MAFANIKIO HARAKA.

Mungu hawezi kukupa kazi, au mafanikio makubwa na kukukabidhi mapenzi yake kwasababu bado unawaza kidunia (Misri).
Kama unataka kufanikiwa haraka  _pambana na fikra yako,

Jitahidi kufanana na Yesu unavyofikiri na kuamua (ondoka Misri). Jinsi unavyobaki kidunia basi Mungu anakuchukua katika safari ndefu. Anajua huwezi kukabiri vita vya Kanaani, bado unajiona panzi

Itazame dunia kama Yesu anavyoitazama "Utakuwa namna unavyotazama"

Watu waliozaliwa ndani ya wokovu. Shika sana imani ya wazazi wako. Vizazi vilipozidi na walipokaa sana Kanaani wakasahau agano ambalo Mungu alifanya na baba zao, wakaanza kuabudu miungu mingine.

Mungu aliwauwa kwasababu hawakutaka kufikiri kama Yeye Mungu anavyofikiri. Kuna namna nyingi za kumshusha utukufu Mungu, ila zote huanzia kwenye fikra. neno la Mungu. Mungu alitamani wawatazame majitu kama Yeye anavyowatazama.

Yesu ametuokoa kutoka ulimwenguni, kazi sasa kuishi  ulimwenguni kama watu wa mbinguni. Kanaani ni mbinguni: hapa katikati wale ambao bado wanawaza kama Misri tutawaacha jangwani.

Wewe hukuwa mtenda dhambi ulizaliwa mwenye dhambi, Yesu alituokoa na utumwa huo.

Umeandikwa na Ulenje
Asante Roho Mtakatifu.

Monday, September 19, 2016

THE MEANING OF LIFE: OUR LIFE Part 3

OUR LIFE

Our life is filled with three phases: becoming, Doing, and Legacy. You cant jump from one stage to another.
In fact what you do now, tell us what you chose to become or unintentional chose to become.
Nothing you do is accident. That you didn't plant in your heart one day.

1. BECOMING
For smart people, this is a phase of becoming themselves , or what you chose anyhow.
For insecure person, this is a stage of trying to be somebody, (he see they are great, or he is impressed by them). And for brainwashed people, this is their stage of becoming like American, or English people.
And majority of them, they become anybody: trying to copy anybody, moving from someone to another one,  today they copy Reinhard Bonke, tomorrow they copy Don Moen, Next day they copy Women of Faith, Hillsong, they copy Populat singers and popular preacher, instead of being themselves. And their dressing style, they don't even care what are they type, they try to copy J Zee, tomorrow they copy Diamond, Next day Jennifer Lopez, Rose Muhando.

2. DOING

General Principle "You will sow what you reap, you reap what you sow"

After you become what you chose to become, or what you try harder to become then you start doing (intentionally or unintentionally)
After you become a woman or man of prayer then it become your habit and simple to pray, After you become woman and man of faith then you believe everything are possible and big things, after you become a preacher and evangelist then you preach, after you become a giver the you give, after you become son of God then you walk like God.
We will see how someone becoming, I know you have desire to become someone, while you're not, and may be you try harder and harder and you fail. But through this message Holy Spirit is going to help you, and you will find is very simple to cancel what you wont to Be, and start becoming what you want to become.

In another side, you were trying to smoke and now you become a smoker, you tried to commit fornication and now you become a fornicator, you take slide many thing and now you become a procrastinator, lazy and poor.

What you're now, is what you sow.

Wise people, they are so curious to know, are they becoming what they're born to do, if is not, they change direction, and  start becoming what they're born to do.

Wise example is Abraham, Moses, Peter, Poul and Luke. Who changed direction to become what they had been to become. I'm happy with Luke who turn from a doctor and a trader into a kingdom writer of the gospel and act of apostles.

To be continued
For more
0718 721848