Wednesday, March 16, 2016

Part 6: MAANDALIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO....

MAANDALIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

Mithari 16:1
"Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;
Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.

Tumetoka mbali na leo tufike tamati, jitie nguvu kusoma maandalizi yote ni ya muhimu. Nakusihi usikose hata Part moja ya somo hili, bonyeza sehemu iliyoandikwa "home" na uanze na hili somo kuanzia Part 1 mpka 6. Hapo utakuwa umefanikiwa kupata semina hii yote. Tulioanza pamoja Mungu awabariki sana. Semina ijayo ni muhimu sana "TABIA NA UTUMISHI" usikose.
Tuendelee...

7. Je Upo Tayari Kumfanya Mwingine Awe na Furaha na Amani .

Karibu kila binaadamu amezaliwa na ubepari ndani yake, yaani ubinafsi. Popote hutazama anapata nini, hata yule atendae kwa wengine basi huwa na fikira kuwa Mungu atamlipa au kumbariki. Huwezi kufanya jambo pasipo kujitazama wewe.

Jambo ambalo mwanadamu yeyote analitafuta ni amani na furaha. Anataka chakula ili awe na furaha, anatafuta pesa ili awe na furaha. Nimewahi ona watu wenye pesa pasipo kuwa na amani kwenye ndoa yao, na watu masikini wenye amani na furaha kwenye ndoa yao.

Usisahau, jambo gumu kulitafuta kuliko yote hapa duniani ni amani. Ndiyo maana Biblia imesema "tafuteni..." Maana yake amani ni ya kuitafuta.

Ni vema ukajifunza nini huwafanya wanawake wawe na furaha na nini huwafanya wanaume wawe na furaha kabla ya kuingia kwenye ndoa. Ni vema ukajifunza kutafuta amani hata wakati ambapo umekosewa na kuchukizwa.

Mtu mmoja aliwa kunishangaa, baada ya kuona ananieleza jambo la kutisha ambalo watu wamenifanyia, lakini mimi nacheka. Alitegemea nitahuzunika na kuchukizwa sana. Kwanini Mungu amenisaidia kujua maana ya amani na kuitafuta hasa pale ambapo haipo au inataka kutoweka.

8. Je Unajua Kusamehe

Kwa haraka waweza kujibu "ndiyo" lakini fikiri wangapi si marafiki zako tena kwasababu tu umeshindwa kuwasamehe, au umesamehe makosa tu! Bado hujawasamehe wao, na ndiyo maana si marafiki zako kwa sasa.

Nisiwe na maneno mengi hapa, ila niseme tu, palipokuwa na wawili basi ndipo makosa huonekana, na kila mtu hujiona bora pale aonapo makosa ya mwenzie. Na kama watu wengi bado hawajakamilika, bado wana hisia zinazowashinda kuzikabiri kama hasira, chuki, wivu na mengine, kama kila mtu huwa anakosea. Ipo haja ya kuamini hata huyo unayesema ndiyo kwake basi ipo siku atakosea.

Basi nina uhakika upo umuhimu mkubwa wa kujifunza kusamehe hata makosa yasiyosameheka, hata pale mwenzio anaona hana haja ya kuomba msamaha. Naamini itakusaidia, lakini kama hujui kusamehe, kila kosa unataka useme, kila wakati unataka uonekane uko vema na mwengine amekosea basi vema ukaomba pooooo....kabla hujaanza uhusiano na mwenzio.

Unajua maana ya kutokusamehe ni kujisemea moyoni mwako hivi "yaani huyu mtu asiyekamilika, mdhambi ananitendea unyama mimi niliyekamilika, mtakatifu na nisiyekosea hata mara moja!!!!...." Hayo ndiyo maneno uyasemayo pindi unapokataa kusamehe. Jifunze kusema "nimekusamehe hata kama hujaombwa msamaha....ndipo useme ndiyo.

9. Je Una Tabia ya Ndoa

Naamini watu wengi hutazama umri wao na si tabia zao, na ndiyo maana wengi wameolewa na kuowa wakiwa bado.

Umri huletwa na miaka, tabia huletwa na mafunzo na fikra. Umri tunatazama miaka, tabia tunatazama matendo na fikra.

Nimeona ndoa za wengi walioowana wakiwa wadogo sana mpaka leo wanadumu na kuendelea nikiwatembelea huwa naona vicheko si vya uongo bali vya kweli. Na nimeona wapo walioowana wakiwa na umri mkubwa na ndoa zao hazijakaa salama hata vicheko vyao ni vya kudanganya wageni.

Siku ya leo maarifa yameongezeka, hatuna tena tatizo la maarifa bali tuna tatizo tu la kuwa na maarifa mengi. Nafikiri ni vema ukachambua na kutafuta maarifa ya KiMungu, wapo watumishi wengi waliofanikiwa kwenye ndoa Zao na wamejitahidi kuandika na kufundisha maarifa mengi ya ndoa. Kuwa msomaji, badiri ratiba ya matumizi ya smartphone yako, anza kusikiliza mafundisho ya Mungu, soma blog zao, soma vitabu vyao. Ili upate kujua maarifa hayo.

Maandalio ya moyo ni ya kwako, ila jawabu ni la Bwana. Usitazame umri na miamko ya mwili: tazama je una tabia za ndoa, je unaweza kuishi na mti mwingine na kuendana na tabia, udhaifu na utofauti wake. Usije ukawa unamsubiri Mungu, kumbe ni Mungu ambaye anakusubiri wewe.

Kila kitu kina tabia yake, na usipoifata hutofanikiwa. Kuna tabia za biashara, kuna tabia za kilimo, kuna tabia za wanasiasa, kuna tabia za wanafunzi, kuna tabia za wachungaji. Vivyo hivyo na ndoa, kuna tabia ndoa inahitaji uwe nazo.

Mfano; unajua kujari, unajua kusamehe, unajua kuchukuliana na watu, unajua thamani za watu pachoni pako, unajua kujitoa kwaajili ya mwingine, unajua kupika, unajua kusaidia, unajua kujitoa hata kama umechoka, unajua kuonesha utii hata kwa aliyekuudhi.

10. Je Umejiandaa kwa Matokea

Ndiyo yako ya kuingia kwenye ndoa ina matokeo na baada ya kusema ndiyo vitu vingi vinatarajiwa kutokea. Kwa haraka, tunatarajia watoto, kupungua kwa baadhi ya maamuzi yako binafsi, kupungua kwa uhuru wako, kuingiliwa maamuzi na mwingine, kuongozwa na mtu mwingine, kuongezeka kwa majukumu.

Ni vema ukajiandaa na matokeo hayo hata kabla ya kusema ndiyo. Haina maana ya kufikiri kuyakabiri yote kwa wakati mmoja bali ni kujiandaa nayo.

11. Je umejiandaa kukabiri Mabadiriko ya mtu.

Binaadamu siyo jiwe kwamba habadiriki.

Watu wanabadirika kiuchumi kushuka au kupanda, wanabadirika muonekano wa mwili na uzuri wao, mabadiriko ya nguvu, fikra na baadhi ya tabia, wanabadirika matendo, hata imani kuna wakati wanashuka na wakati wanapanda kiimani.

Mabadiriko hayo yanapotokea: ni wakati wa kiangazi ambapo kila mtu anahitajika kuwa imara kuhakikisha boti haizami ndani ya maji.

Ni jambo linaweza kuoneka dogo, lakini kama usipoandaa ufahamu wako kujiandaa katika hili, kiangazi kijapo na kukukuta hauna chakura utakuwa kwenye shida.

12. Je una Uwezo na Upo tayari  Kujitoa

Upendo ni kujitoa, kwa hari na mari. Huwezi kusema unampenda mtu na haupo tayari kujitoa kwaajili yake, na kila mtu anatamani mtu anayejitoa kwaajili yake.

Kuna vitu huwezi kufanya pasipo kujitoa. Jiandae. Kuna wakati wa kuchukizwa: ni kujitoa kusamehe. Kuna wakati wa kuchoka na kutokuwa na kitu kabisa, kuna wakati wa kusaidia hata kama huna uwezo.

Kujitoa si kitu kidogo kinahitaji upendo wa dhati sana (deepest love) na kama huna upendo huu hutoweza.

Nina mengi ya kusema ila Roho Mtakatifu ndani yako atakufundisha mengi zaidi.

Kipimo kikubwa cha somo hili: Kumbuka nini kilikuachanisha na rafiki zako au wapenzi wako wa zamani, pia tazama ni nini ambacho hukipendi na kinakuchukiza kwa mke au mume wako, au mchumba wako. Utagundua uliacha nao urafiki au uchumba ni moja ya maandalizi haya hukuwa nayo, na hata sasa huridhiki kwasababu moja ya maandalizi huna.

Kuna KITABU kipo jikoni "BADO LIPO TUMAINI" utakapokiona dukani tafadhari nunua. Na zidi kuomba kwa habari ya watumishi.

Natamani kupata comment yako, phone call au whatsapp.
+255 718 721848
imaf2b@gmail.com

Monday, March 7, 2016

Part 5: MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MAANDARIZI MUHIMU KABLA YA KUSEMA NDIYO...

Bado Tunazidi kuchana Nyavu...
#SeminaKiganjaniMwako.

4.  Je upo Tayari Kubadirishwa, Kukosolewa, na Kuboreshwa

Moja ya hadithi niliyowahi kuisoma darasa la kwanza na  nisiyoisahau ni hadithi ya "Mti wa Mpapai uliogoma kwenda huku-na-huku kuufata upepo" upepo ulipozidi, mpapai ukaanguka.
Tunafahamu kuwa kila binaadamu ana udhaifu, ila Mungu ametupa uwezo wa kuwa wakamilifu: na hutumia watu wa karibu, matukio na majaribu katika maisha.
Naamini tunaingia kwenye ndoa si kushindana bali kukamilishana: ili kutimiza kusudi ambalo Mungu ameliweka katika maisha yetu.
1 Kor 11:11 "Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana"

Nikupe siri; Udhaifu wa mtu hugunduliwa na mtu mwingine hasa wa karibu yake sana" Dr Myles Munroe aliwahi toa mfano kusema "Ni vigumu kujua kuwa kiatu chako kinatoa harufu mpaka mtu mwingine akwambiye"

#Kama wote tupo kwenye safari ya kuelekea ukamilifu, na tunahitajiana ili kuwa wakamilifu, na tunafurahiana hasa pale tunapoonesha ukamilifu: basi kuwa tayari kuelimishwa, kupokea mafundisho mapya, fikra mpya, mipango mipya, na kuboreshwa baadhi ya tabia zako, ni MAANDARIZI YA MUHIMU SANA"

5. Je upo Tayari Kuacha Baadhi ya Vitu Unavyovithamini Kwaajili ya Mahusiano.

Idadi kubwa ya wachumba wameachana kutokana na kupishana na misimamo na mitazamo ambayo kila mmoja anathamini. Hata wanandoa wengi; mabishano yao makubwa mara nyingi, ni pale misimamo, mitazamo na fikra zinapogongana.
Misimamo; ni falsafa na mawazo ambayo mtu huamini kuwa ni sawa na yanapaswa kufatwa na wote ili kupata mafanikio.
#Kama hampo tayari kukaa chini na kujiandaa kupanga misimamo, mitazamo na falsafa ya pamoja na kuacha ya binafsi basi ni heri mkaomba pooooo! Kabla ya kusema ndiyo!! Na mkaendelea kukuza akiri zenu.

Maana mtakaposema ndiyo! Pasipo kuwa tayari kuacha baadhi ya misimamo ambayo inaweza kuwatenganisha, na kuunda misimamo ya pamoja; Itakuwa haina maana, sababu safari yenu itakuwa fupi.

6. Je Unaweza kulinda Maono yako; Huku Ukitimiza Kusudi la Pamoja.

Mwanzo 2:18;5:1
Hii ni mistari dhahiri inayoonesha kuwa Mungu ametuumba kutimiza kusudi moja pale tunapoungana na kuwa mtu mmoja; tofauti ni kwamba mmoja mjenzi, mwingine saidia.
Ila saidia asiyekuwa na maono, hafai, na mjenzi asiyekuwa na maono hafai kitu.
Saidia ni lazima maono yake yaendane na maono ya mjenzi, na kusaidia kusudi la pamoja kutimia.
Na mjenzi ni lazima maono yake yajulikane, yaendane na saidia wake; ili aweze kumsaidia.
Kusudi ni juu ya maono: Kusudi ni "Sababu ya wewe kuzaliwa" na maono ni "Kioo cha kutimiza kusudi lako na namna ya kufika kwenye kutimiza kusudi lako"

#Hivyo wote wawili muwe tayari kuunda maono yenu yaendane na safari ya kufika kwenye kusudi ambalo Mungu amewaumba kutimiza"
Haleluya!!!!

Sifa na Utukufu apewe Bwana
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu tunazidi kuenderea

Monday, February 29, 2016

Part 4: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO....

~ MAANDARIZI 15 KABLA YA KUSEMA NDIYO..."

Karibu sehemu ya nne ya somo letu...
Soma kila swali kwa umakini, kumbuka kujibu ndani ya moyo wako ukiwa peke yako.

Nianze kwa kusema: pindi unaposema ndiyo, kuna vitu vitabadirika kwenye maisha yako.

A. Ndiyo! yako hukuradhimu kubadiri tabia.
     Ili kuendana na furaha ya huyo umwambiaye ndiyo, kumbuka uwe tayari kuwa yeye anavyotaka. Na hivyo kuna vitu unafanya itakuradhimu vibadirike hata kama ulivipenda.

B. Kupungua kwa uhuru
     Kumbuka hutotakiwa kuendelea kuwa na uhuru kama uliokuwa nao, itakuradhimu umpe mwenzi wako sehemu ya uhuru.

C. Misimamo inabadirika
     Kumbuka unayekutana naye ana misimamo, na ili mfurahi lazima uwe tayari kubadiri baadhi ya misimamo yako.
E. Marafiki wanabadirika
F. Matumizi ya simu yanabadirika
G. Mda wa kulala unabadirika

Neno "Nimekubali..." Ambalo mara nyingi hutamkwa na wanawake, ni dogo sana ila ndiyo chanzo cha mabadiriko ya maisha ya wengi. Na hii ndiyo siri, ni wale tu ambao wako tayari kuendana na mabadiriko yanayotokana na neno nimekubali hufaidi furaha ya Ndiyo yao.

"Wale tu ambao wako tayari kukubaliana na mabadiriko yatokanayo na Ndiyo yao, ndiyo hupata furaha ya mahusiano yao"

Tuanze sasa, leo tutajadiri maswali kadhaa na Part ijayo tutamalizia maswali mengine. Kumbuka ni maswali 15.

Sw 1. Je Unaweza Kuzikabiri Hisia Zako?

Mtu yeyote hata kama mlikuwa marafiki kaka na dada hapo mwanzo, mnapoingia kwenye uhusiano mvutano wa miili yenu unaumbika na hivyo kuwaletea hisia tofauti na hapo mwanzo.
Hivyo kabla ya kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi, ili kujizuia kutenda dhambi ya uasherati, lazima kwanza ujiulize kama una uwezo wa kukabiri macho yako na nguvu ya mwili wako kwa binti. Huna uwezo wa kukemea tamaa iondoke, bali una uwezo wa kuzuia kuyachokoza mapenzi.
Wengi husimama wakiwa single na hupotea pale wanapoanza mahusiano.

"Kabla ya kusema ndiyo, jiulize je una uwezo wa kutunza heshima yako mpaka Ndoa"

Turudi kwenye stori yetu kuhusu Angel: siku moja nikitoka kupata ibada yenye nguvu ya Casfeta- chuo kikuu cha UDSM, nakumbuka dada mmoja aliniambia "Ulenje sikuoni siku hizi kwenye ulimwengu wa roho". Nilishangaa lakini nikakumbuka Mungu amewahi kunionesha namna ninavyojiweka mbali naye. Usisahau wakati huo nilikuwa nahubiri madhabahu za ndani na majukwaani, naombea na watu wanapona.
Nakumbuka siku moja nikihubiri kanisa fulani, Mungu alijitukuza wakati wa maombezi, mpaka watu walianza kuitana mitaani na kuja kuombewa. Lakini nikirudi nyumbani Mungu ananionesha niko mbali naye.
Sikuwahi anzisha uhusiano na Angel, siku nilipogundua "bado sina uwezo,
Basi nilisubiri, mpaka namaliza chuo nikaendelea kusubiri, haikuwa dhambi, sikutaka kuwa mbali na Mungu"

Jifunze jambo hapo, ni kwa namna gani mpenzi wako anakuweka mbali na Mungu, kwa njia ya simu yako, au mnapokutana.
Kabla hujasema ndiyo kwa huyo umpendaye, Je una uwezo wa kuongoza hisia zako, na kuishi pasipo kumkosea Mungu. Najua baadhi watapinga, lakini wanaopenda roho zao, na kuwa tayari kukana nafsi zao kwaajili ya Bwana basi watapokea na kufanyia kazi ujumbe huu.

Sw 2. Je Unajua Unaenda Kufanya Nini?

Nilimuuliza binti fulani swali kama hilo, akajibu nitafua, nitaosha vyombo, na kumpikia chakula kizuri kila siku.

"Watu wawili hawawezi kwenda pamoja, kama wasipopatana"

Sina mengi ya kusema katika hili, soma mwanzo 2:20 Biblia inasema "lakini hakuona wa kufanana naye"

Hivyo Mungu uheshimu wa kufanana naye, japo Mungu alizungumzia wasichana wote, maana hakutoa ulinganifu wa msichana na msichana, bali ni msichana na wanyama, na kuona kiumbe msichana ndiye anafaa; ila alionesha jambo la msingi "kuwa anaheshimu sana mfanano"

Kila msichana ni mzuri, ila ni vema wa kufanana na wewe.

Swali letu ni "Je unajua unaenda kufanya nini?. Ni swali dogo, ila kufanana siyo shida, shida huyo unayefanana naye anajua anaenda kufanya nini mtakapokuwa pamoja"

Unashangaa, unapokaa chini na wachumba au wanandoa, na kuwaeleza tatizo ni "mnafanana ila hamfanyi mnayopaswa kufanya" wanacheka, na wengi husema "kwanini mtumishi: sikujua hayo hapo mwanzo?, mwingine aliniambia "tatizo ni kutokujua mtumishi"

"Kanuni ni ndogo, ukijua na kufanya unachopaswa kufanya uhusiano utaenda, usipojua cha kufanya na Ukafanya usichotakiwa kufanya uhusiano hautaenda"
Ev. Ulenje

Nakusihi katika Jina lake Bwana Yesu, tumia mda kusikiliza mafundisho ya watumishi wanaoaminika, soma neno la Mungu, Biblia imejaa stori za kila aina ya ndoa, soma vitabu vya waandishi wa kiroho wanaoaminika, sikiliza watumishi.
Kubwa kabisa muombe Bwana akufundishe njia zake. Na utambua nini unahitajika kufanya wakati wa ndoa, kisha kuwa na amani ya kusema ndiyo, achana na mambo ya umri na miemuko ya mwili, Mungu anatazama uwezo wa ndani na Ndoa pia inategemea sana uwezo wako wa ndani, si miemuko
Ya mwili wako, au umri wako.

"Mungu huwaepusha baadhi ya wasichana kukutana na waume zao, kwasababu ya kuwaepusha wanaume hao na maumivu" Dr Myles Munroe

Kuolewa si umri, umaarufu, karama, huduma au msisimko wa mwili ni uwezo wa ndani.

Fikiria hili, hata kwa wanaume pia.

SW 3. Je Unajua Kutambua

1 Wakorintho 13:9-12
Soma kwa makini mstari huo, ila naomba niandike sehemu muhimu.
Biblia inasema "Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;....nilipokuwa mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga...wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu, wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana"

Hakuna siri kubwa katika kuwa na ndoa nzuri kama "kuwa na uwezo wa kufahamu yaliyojificha nyuma ya neno "nakupenda" unalolisikia.

Natamani kuishia hapa; ila ngoja niendelee: wengi wanalia kwenye mahusiano si kwamba hawakuambiwa "nakupenda" na wapenzi wao, bali walishindwa kutambua nini kipo nyuma ya neno "nakupenda" walilolisikia.

Watu wawili wanasema "nakupenda" je una uwezo wa kutambua "nakupenda ipi ni ya kweli na imetoka kwa Mungu" na ipi ni ya kibinaadamu.

Mwanaume una uwezo wa kufahamu "ndiyo" unayoipokea na nini kipo nyuma yake: je ni Mungu au shetani, je ni hatima nzuri au mbaya. Na kwa wasichana pia, je unatambua nyuma ya hiyo nakupenda; je ni Mungu, Shetani, Hatima nzuri au mbaya.

Kama huna uwezo huo, basi ni bora ukaacha kujenga nyumba, Yesu anasema usije ukajenga msingi, ukashindwa kumalizia na wenzio wakakucheka. Ni bora ukaomba poooo....mapema kabla ya huyo mwanaume au mwanamke hajaja.

Ninayo mengi ya kusema katika hili, ila Roho mtakatifu akufundishe zaidi. Wengi wanalia. Wamejikuta wameng'ang'ania sehemu ambayo wenye uwezo wa kutambua walimwambia hapana, yeye akalazimisha "ndiyo" sasa analia.

Je una uwezo wa kutambua..."nakupenda unayoisikia" au "Ndiyo" unayoisikia. Maana tunafahamu kwa sehemu, na wakati wa utoto tunafahamu kama watoto, kama bado una babaika kujibu "je ni Mungu au ni hisia zangu" ni heri ukaomba poooooo!!!! Mapema, na "ukajifunza kuongeza uwezo wako wa KiMungu wa ndani" wa Utambuzi wa utu uzima"

Nitaendelea maandalizi ya nne siku tati Zijazo....
Usikose....

Kwa msaada wa Roho Mtakatifu somo limeandikwa na
Ulenje Mwaipungu

Sunday, February 21, 2016

Part 3: MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA NDIYO...

MISINGI IKIHARIBIKA...

Tuchokoze jambo hili la msingi kisha Part 4 tuanze kujadiri "mambo ya msingi ya kufanya maandarizi" kabla ya kusema Ndiyo!

"Huwezi chora ramani ya nyumba, baada ya kujenga msingi

Zaburi 11:3
Mfalme Daudi yeye anauliza
        "Kama misingi ikiharibika,
          Mwenye haki atafanya nini?

Huwezi jenga ghorofa la ngazi 30 kwa kujenga msingi wenye uwezo wa kubeba ghorofa la ngazi tano. Utachekwa tu.

Daudi anasema "mwenye haki atafanya nini" hajasema mwenye dhambi.

Si peke yako, hata wengi hujiuliza "nafunga sana, namtumikia Mungu kwa moyo wote, natoa zaka na dhabihu, ni mchungaji, ni askofu, ni mshirika mwaminifu sana, nampenda mke wangu, ni mwaminifu wa ndoa yangu, ila mbona ndoa yangu inasumbua?

Daudi anasema mwenye haki atafanya nini? Unafanya yote yanayokufanya uwe mwenye haki, ila ndoa haijakaa vema. Haleluya, nasema haleluya!. Hapa lazima kuna jambo la ziada la ambalo Daudi analifahamu.

Maandarizi kabla ya kusema ndiyo, maandarizi kabla ya kuingia kwenye ndoa, ni wakati wa muhimu sana kuliko hata ndoa yenyewe.

Maana msingi wa nyumba ni muhimu sana kuliko hata nyumba yenyewe.

Kuna wengine husema hayo mengine hujijua huko huko, kwani nani kazaliwa anajua, jibu ni fupi tu, unapotaka kujenga ghorofa la ngazi 30, na umeshajenga msingi wa ghorofa ya ngazi 10,  huwezi kubadirisha ramani wakati wa kujenga  ngazi ya 9, na kusema nataka ghorofa ya ngazi 30 na si ngazi 10. Wote watakushangaa, la sivyo itakulazimu ubomoe ngazi ulizojenga zote, kisha ubomoe msingi wote na ndipo uuweke msingi na upya kwa jinsi unavyotaka kubadiri, ambapo gharama yake ni kubwa sana kuliko hata ungekuwa makini mwakati wa kujenga msingi.

Huwezi kubadiri ramani ya nyumba  katikati ya ujenzi. Hivyo nathubutu kusema ni vema kutazama tunaujenga vipi msingi wa ndoa tunayotaka kuingia, hata kabla ya ndoa yenyewe.

KUMB:
        "Kama misingi ikiharibika,
           Mwenye haki atafanya nini

Usikose sehemu ya Nne, kumbuka ndiyo kiini cha somo. TUTAJADIRI maandarizi ya kufanya moja baada ya lingine.
Asante kwa kusoma.

Utukufu kwa Bwana Mungu na Mwanaye Yesu Kristo

Monday, February 15, 2016

Part 2. MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA "NDIYO..."

Nianzie hapa...

" huwezi kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Nazungumzia maandarizi kabla ya kusema "Ndiyo"

Yesu  anasema "maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumaliza?"

Na hii na ndiyo sababu ya ndoa nyingi kusumbua. Wengi tunaowa kwa miemko na kutazama umri, na si uwezo wetu wa ndani, na kutazama "kama una uwezo?" Ndoa si kuishi pamoja, kuna zaidi ya maana nyingi ya neno "kuishi pamoja".
Yesu analeta kesi mezani, anasema "Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, wakisema mtu huyu, alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza"

Siku hiyo niliishiwa nguvu, haikuwa na maana ya ugonjwa kuingia moyoni mwangu, "ilikuwa ni ishara ya kuwa sikuwa na nguvu za kujenga mnara unaitwa ndoa". Na haikuwa kesi ya umri, ilikuwa kesi ya uwezo wangu wa ndani wa kuwa na uhusiano wa uchumba. Kabla hujasema ndiyo, usiulize kama unampenda au kama anakupenda, ni swali dhaifu sana, usiulize umri wako ni swali dhaifu sana, kaa chumbank peke yako, jifanyie ukaguzi binafsi, ukiwa na Mungu wako, ikiwezekana muulize Mungu anayekujua zaidi, je una uwezo?. Kama huna kabla ya kusema "Ndiyo" chukua mda kuzingatia moyoni mwako, na ujenge uwezo kwanza. Alafu unajua nini cha ajabu, kuwa na uwezo haichukui mda, siku moja mpaka mbili kwa uwezo wa ndani, siku kadhaa kwa uwezo wa nje.
Twende pamoja...

Yesu ananifurahisha hapa anaposema "Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

Hii ni siri kubwa katika maisha "mazingira siku zote si rafiki" ndoa siku zote hutaka kuwapeleka ninyi chini, mgombane na mchukiane, dunia na matukio ya kimaisha siku zote si rafiki. Hivyo "kabla ya kusema Ndiyo, swali la msingi, je unaweza kupambana na mazingira ya ndoa na changamoto zake" usiogope, hakuna mtaaramu wa maisha, wote tunatembea kwenye neema ya Mungu, wote tuna matatizo yetu tusiyotaka kuyasema yote, ila swali, kwanini wengine wanapotea kwenye matatizo, ambayo wengine wanasimama? Tofauti ni ule uwezo wa ndani.

Wote wana changamoto fulani za ndoa, hata kama wana miaka 25-50 ya ndoa, wana vitu hawawezi kusema, ila katika hayo waliyopitia wakashinda, kuna wengine walianguka. Unaanza kunielewa, nini shida; Ni uwezo wa ndani ya mtu wa kukabiri changamoto na kuzishinda.

Yesu anamaliza kusema "na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali"

Waooo!!! Kama ukiona huwezi kumtii mwanaume kama vile unavyomtii Kristo na kumfanya awe kichwa kwako kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa, basi omba pooo! Mwanaume akali mbali"

 kama ukiona "huwezi kuvumilia makosa na udhaifu wa mwanamke/msichana, hata pale anapoweza kukuumiza sana kama vile Kristo anavyolivumilia kanisa, na kukubari kufa ili alisafishe, basi omba pooo mwanamke akali mbali" waoooo!!!! Incredible.

Kama huyawezi haya aliyoandika mtume Paulo waefeso 5:22-25
Omba pooooo mapema kabla ya mke au mume hajaja kwenye maisha yako.

Ngoja tumalize kabisa Yesu aliyosema kwenye hii luka 14.
"Basi kadharika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu". Kama haupo tayari kuacha aina ya maisha unayoishi, mitizamo yako na misimamo yako, marafiki zako wa kike na wakiume na mengine ambayo unayeanza naye uhusiano hataki, au yanaweza kusababisha kutoenderea na upendo wake kwako, basi omba pooo! Akali mbali, usiwe mke wake, au mume wake.

Yesu anamalizia "Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee?, haifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia. Na asikie. Waoooo! Ndoa ni kitu chema sana, ila kama kikiharibika itiwe nini hata ikolee, semina na semina zinafanyika, masomo na masomo yanaandikwa ila bado ndoa ni tatizo, kwanini? Hakuna maandarizi.

Swali "je unaweza kutumia kitu vizuri kama hujui namna ya kukitumia"

Tuendelee kuchana nyavu, sehu ya tatu ipo njiani

Mungu alibariki neno lake.
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu Limeandikwa na Ev. Ulenje
0718721848.
imaf2b@gmail.com

Friday, February 12, 2016

MAANDARIZI KABLA YA KUSEMA "NDIYO..." Part 1

PREPARATION BEFORE YOU SAY I DO

Mwaka 2013, nimewahi kumpenda msichana fulani jina naliweka nyuma ya pazia, ila namwita Angel. Maisha yangu ya kutumia mda mwingi kumtafuta Mungu na kutafakari matendo yake, yalinipa kuwa na maisha ya tofauti na mtazamo tofauti kuhusu wasichana na hata ndoa. Nilikuwa wazi hata kusema siamini katika ndoa, siamini kuwa naweza kupenda au hata kuowa. Nilivutiwa sana na maisha ya Mtume Paulo na hata sasa navutiwa sana na maisha yake, hivyo niliwaza nije kuisha pasipo kuowa kama yeye.

Hivyo niliishi namna hiyo mpaka nafika chuo mwaka wa tatu, bado sikuwa nikiamini kuhusu kuowa au kuhusu kupenda. Tabasamu la Angel likanifanya kubadiri muelekeo wa maisha yangu. Nikajikuta kubadiri hata laini ya simu toka tigo na kutumia Airtel sababu tu ya kupata mawasiliano yake. Kwakuwa sikujua kukabiri maisha yale mapya niliyoyaanza, ilichukua mda kumwambia Angel tuanze uhusiano unaoitwa uchumba.

Ili ilichukua miezi mingi sana kuvumilia ile hari, wapendwa kupenda huku ukiogopa kusema kwa unayempenda ni mateso, na kumchukia mtu unayeogopa kumwambia unamchukui ni kifo cha moyo unaoishi. Kila nilipomuona huyu Angel nilisahau hata kuwa niliwahi weka malengo ya kutoowa.
Siku moja uvumilivu ukanishinda, ilikuwa ni siku ya jumaapili. Uzuri Angel tulikuwa tukisali kwenye Fellowship moja ya Casfeta hapo chuoni. Siku hiyo nikaweka moyoni mwangu, kuwa lazima nimwambiye Angel, nini nawaza juu yake. Nikaamka kitandani na kuchukua simu yangu, na kutafuta jina lake, nini kilitokea...

Ninapobonyeza batani ya simu kubonyeza nitume sms, nikasikia sauti ikiniuliza swali gumu na jepesi sana, ambalo kupitia swali hilo ndipo tunapata somo la leo
Nikaulizwa "Are you capable?" Yaani "Je una uwezo?". Nguvu zikaniisha mwilini, nikakosa hata uwezo wa kusimama kwa miguu yangu, nikaanguka kitandani, ubongo ukasimama kuwaza, na hata leo simuwazi tena huyo msichana, upendo ule wa muemko ukaishia pale, hadithi ya maisha yangu ikaanza tena. Kuna jambo natamani kukufundisha hapo.
Mungu aliniuliza "Je una uwezo?". Lilikuwa ni swali la msingi sana. Nilitumia mda wa miezi mingi sana hata kuelewa kuwa kuna somo Mungu alitamani vijana na hata wanandoa waelewe.

"Kufunga ndoa pasipo maandarizi ya ndani (tabia, fikra, mitazamo na akiri) ndiyo mwanzo wa kuvunjika ndoa hata kabla haijafungwa

Friday, January 15, 2016

BADO LIPO TUMAINI #2021 INAWEZEKANA.


BADO LIPO TUMAINI

#2021INAWEZEKANA.

2021 MWAKA WA KUFANIKIWA KWA CHOCHOTE MTU ATAKACHOANZISHA.

Mwaka wa kupanda na Kuvuna

Huu ni mwaka wa mtu ambaye hajakata tamaa ya kuanzisha jambo jipya au kuendeleza anachofanya.
Makanisa yanayokwenda kufanya Injili Bwana anakwenda kuleta mavuna mengi zaidi.

Mtu anatakayeinuka na kufanya tena atavuna mavuno mengi

Mhubiri 3:1
Kwa kila jambo kuna majira yake
Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

Mara nyingi huwa tunajiuliza kwanini tunafanya mambo kwa juhudi na akili zote huku tukimtegemea Mungu lakini hatuoni matokeo makubwa.

Leo Roho Mtakatifu atufundishe kwa habari ya mpanzi.

Mathayo 13:3-9
3. Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda.
4. Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila;
5. nyingine zikaanguka penye miamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara zikaota, kwa udongo kukosa kina;
6. na jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka.
7. Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga;
8. nyingine zikaanguka penye udongo mzuri, zikazaa, moja mia, moja sitini, moja thelathini.
9. Mwenye masikio na asikie.

Hii ni ajabu,
Mpanzi alipopanda mara ya kwanza kwa bahati mbaya zikaanguka penye miiba, si kwamba aliangusha penye miba: hapana Yesu anasema zilianguka, kwa maana nzuri mpanzi alikusudia zianguke penye udongo mzuri lakini zikaanguka penye miiba zenyewe.

Ndiyo nimepanga sikukurupuka kufanya mambo lakini hayajafanikiwa. Yeshua anasema mwizi akaja akaiba.

Mkulima hakukata tamaa, si kwamba hakuumia, Yesu hakutaka stori iwe ndefu, ila mkulima aliumia tena sana. Lakini mwaka 2021 tujifunze toka kwake, hakukata tamaa, akainuka na kupanda tena.

Alipopanda tena Yesu anasema zikaanguka penye miamba, mbegu hizi pia si kwamba aliziangusha makusudi, hapana, alipanga mipango, alitumia akili na utaaramu wote lakini ni kawaida unapotupa mbegu zingine zinaanguka tofauti na matarajio.

Mbegu hizi zikampa matumaini mkulima, Yesu anasema zikaota, zikamfariji mkulima, tofauti na zile za mwanzo, lakini zikakosa mizizi hazikudumu zikafa.

Mkulima aliumia sana, kama wewe unavyoumia unapoona kuna vitu vinaanza kufanikiwa lakini vinakwamia njiani.

Tujifunze kwa mkulima 2021 hii, mkulima hakukata tamaa, akainuka na kupanda tena, alipopanda safari hii kukawa na afadhari, akapanda, safari zikaanguka penye miiba, Yesu anasema Math 13:22
Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai.

Yesu hasemi mbegu zilikufa, lakini anasema halizai. Mbegu imekuwa lakini miiba inausonga mti hata usizae.

Ni mengi tunayo tunayafanya katika mwili na katika ufalme wa Mungu. Si kwamba yamekufa ila yapo na hatuoni yakizaa.
Kuna mengi tunayo kama ni kazi, huduma au biashara. Yapo tu lakini hayazai. Hayatoi faida tunayoitarajia.

2021 tujifunze kwa mkulima, yeye hakukata tamaa, alitambua siri moja, kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

Tuelewe jambo moja watu wa Mungu.
Majira ndiyo husema tufanye nini, na siyo tufanye nini husababisha majira fulani kutokea.

Mfano: kupanda mahindi hakuleti mvua, ila mvua husababisha tupande mahindi. Hivyo ili mahindi yaote ni lazima tusubiri mvua.

Vivyo hivyo, majira yanabadirika kila wakati yakizunguka ndani ya mwaka. Na kila majira yanatueleza nini cha kufanya.

Kipindi cha kiangazi ni kibaya sana, ni kipindi cha majaribu kila mbegu huangukia penye miiba, si kipindi cha kukaa ni kipindi cha kupita tu. Ila ni lazima mtu kupita ili ajifunze utii na kumjua Mungu.

Kipindi cha vuli hiki ni kibaya zaidi, majani yanapukutika, kila kitu kinaondoka, marafiki, tumaini, wakati mwingine hata amani na kibari, kila kitu kinaondoka. Musa amewahi pita huku, Yesu amewahi pita huku, hata wanafunzi wake walimkimbia, Paulo aliwahi pita huku, hata Watu wa Yerusalemu wakasema anafundisha Injili tofauti na ya Kristo, akaomba mara tatu udhaifu umtoke ikashindikana.
Hiki si kipindi cha kukaa, ni cha kupita tu.

Mkulima alijua haya, adui atakuja atachukua tu mbegu, maana ni majira ya vuli.

Masika, hiki ni kipindi cha neema, huleta tumaini jipya, imani na upendo mpya, kila mtu hutamani kukaa hapa. Kila upandacho kinaota. Na hii na ndiyo 2021.

Mkulima akaenda shambani akapanda, Yesu anasema ikazaa moja 100, zingine 60 na zingine 30. Hii ni njema sana Haleluya.

Mwaka huu ni wa kuanzisha vilivyoshindikana huko nyuma, ni mwaka wa kupanda upya tena. Kama ni biashara panda (anzisha), hata kama ilisimama, ilikufa, haizai, anzisha tena, kama huduma ilisimama anza tena, kama ni mikutano fanya ya kutosha. Kama ni kuowa na kuolewa anza mchakato tena, maana ni mwaka wa Bwana kuotesha vyote vilivyopandwa. Na havitachelewa.

MUHIMU
Huu ni wakati wa kumtumainia Bwana kuutafuta ufalme wake kuliko miaka yote. Kwa maana baraka nyingi zitawakuta hao.

Zaburi 37:5, Math 6:33, Isaya 40:31

Yesu hapendezwi na wenye hofu na mashaka, anapendezwa na wenye moyo wa imani, wanaokesha usiku na mchana wakitafuta ufalme wake na haki yake.

Yesu anasema mfano wa ndege wa angani ambao hawavuni, wala hawapandi, wala hawana ghara lakini Baba wa mbinguni huwalisha, je ninyi si zaidi ya hao.

Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo, hayafanyi kazi, wala hayasokoti, Yesu akaendelea kusema hata Sulemani na fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama moja wapo ya hayo, Yesu akamalizia kusema Ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo na kesho hutupwa karibuni, je hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wenye imani haba. Mathayo 6:26-33

Kuna mambo ya kujifunza hapo, Yesu anasema "tafuteni kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa"

Unapoenda kununua maharage, nyongeza ambayo unazidishiwa huwa hatuilipii, hapo tunakubaliana.

 Kitu cha kuzidishiwa huwa hakiitaji nguvu wala malipo. Unapewa bure.

Ila kuzidishiwa, ina maana kwamba kuna kitu ulikuwa umekifanyia kazi au umekigharamia. Na sasa mpaji anapokuja, anakupa ulichogharamia na ndipo kinafata kitu kinaitwa kuzidishiwa.

Ila kwanza umenunua, umetafuta, umepata cha kupewa kwanza.

Ila kama huna unachostahili kupokea (hujanunua kitu) , maana yake cha kuzidishiwa hapo hamna tena.

Hivyo ili ustahili kupata cha kuzidishiwa kwanza inatakiwa upate kitu kwanza (yaani utafute kitu fulani kwanza).
Ambacho ni kipi? Ni ufalme wa Mbinguni. Tafuta, toa gharama, kwa nguvu mpaka uuteke ufalme wa Mungu. Sasa ukishaiteka huo, ndipo muuzaji (mpaji) anakuja 2021 kuja kukuzidishia.

Mwaka 2021 hakikisha unang'ang'ania ufalme wa mbinguni kwa nguvu mpaka unauteka, na kama umeshauteka basi shikiria usiuchie mpaka upate ahadi zako ambazo ni kuzidishiwa, kufanikiwa katika kila jambo unalokwenda kulifanya.

Sasa, elewa mfano wa ndege, Yesu hapendi watu wenye hofu na waliokata tamaa ya kupanda. Tazama ndege anapoamka asubuhi, anakuwa ana imani kuwa Baba wa mbinguni ameandaa pumba sehemu nitaenda kula.

Wewe anzisha biashara, anzisha mradi, anza huduma, anza mpango wa ndoa, anza chochote, kisha wateja, washirika, mchumba, au support hilo wewe amini tu, nyanyuka Bwana ameshaandaa. Hiyo siyo kazi yako.
ANGALIZO: ndege hakuwahi tengeneza pumba. Wengi wanaziba nafasi ya Mungu kwa kutumia mpaka njia zisizo harali kulazimisha kutengeneza pumba, acha nafasi ya Mungu.

Mfano wa maua: Maua hayana shida, yenyewe yanafanya kazi moja tu, hayaondoki kwenye udongo: usiondoke kwa Mungu. Kisha yanatoa mizizi yake, yakiamini Mungu ameandaa maji sehemu nitakwenda kuyanyonya.

Ebu fikiri Sulemani pamoja na utajiri wake wote, aliweza kupata chochote alichokitaka, chochote ambacho moyo wake ulikitamani, lakini bado Yesu anasema maua yamevikwa zaidi ya Sulemani, lazima Yesu kuna kitu anajua sisi hatujui.

Lakini nini maua yanafanya, moja hayatoki kwenye udongo: usitoke kwa Mungu tafadhari, mbili yanatoa mizizi.

2021 ni mwaka ambao Bwana amendaa masika ya ajabu sana, toa mizizi yako.

Anzisha biashara tena, panda tena. Fanya chochote, anza kilimo au mifugo,chochote, na Bwana anakwenda kutoa maji.

ANGALIZO: Maua huwa hayapeleki mizizi mahari pasipo na maji.

Muombe sana Mungu akuongoze wapi upeleke mizizi.

Usiwe mkuyu, unaolazimisha kupata maji wakati wa kiangazi na kulazimika kuwa na mizizi mirefu sana, ili kupata maji yalipo.

Kufanikiwa kwa njia ndefu sana kunachosha sana, omba Mungu masika ije, ujue maji yalipo, haraka uchomoe mizizi na uanze kuvuna zabibu Katika Jina la Yesu.

Kumbuka kujifunza kwa mpanzi, kwa ndege wa angani na kwa ua.

Kwa msaada wa Roho Mtakatifu somo hili limeandikwa na Kuhubiriwa Tarehe 31/12/2020 saa 4:42 - 5:26 Usiku.
Na
Pastor Ulenje EM.
Na kutumwa kama somo maalumu kwako. 


NA IKAWE KWAKO KATIKA MEMA SOMO HILI KWA JINA LA YESU. 

0683 477827
0718 721848


Thursday, December 31, 2015

2016 BWANA ANAKUWAZIA MEMA, WEWE JE?

WEKA ALAMA, JENGA JINA JEMA KATIKA UFALME WA MUNGU.

2016 ndiyo hii,
Mengi twaweza kuyafikiri kuyafanya, katika mwaka ujao.
Jambo la kufikiri, mwaka unapoisha, utakuwa umefanya jambo watu watazame au utakuwa unatazama watu waliyofanya.

Maana kuna watu hupokea mwaka kwa kufurahi kuongeza umri na wengine hutazama nini wamefanya.

Mfano: mtu mmoja alienda kwenye duka wanalouza ubongo. Muuzaji akamwambia kuna aina nne za ubongo. Akaanza kumuonesha aina:
Akamuonesha aina ya kwanza, ni bongo waliyofanikiwa kugundua Satelite, ndege, na magari, akamuonesha aina ya pili, ni wale waliyofanikiwa kugundua radio, simu, na television, akamuonesha aina ya tatu waliyofanikiwa kugundua kutengeneza majumba ya kufahari, madaraja na hoteri za kisasa, akamuonesha ubongo aina ya nne, ambao wao hawajafanikiwa kugundua chochote, wao hata kujenga vyoo vy ikulu huwaita watu toka nje kuwajengea
Mnunuzi akauliza bei, na kuambiwa bongo za kwanza mpaka namba tatu ni bei rahisi sana, ila ubongo wa mwisho ni aghari sana huwezi kununua, mnunuzi akashangaa inawezekanaje ubongo ambao hawajafanya chochote kuwa aghari zaidi ya bongo waliyofanya vitu vikubwa.
Akamwambia huu ubongo una uwezo mkubwa ndani yake, ambao bado haujatumika.

Mwanzo wa somo:
Dr Myles Munroe aliwahi sema, mari na utajiri haupo kwenye migodi, wala haupo kwenye visima vya mafuta.
Bali utajiri upo karibu na nyumba yako, utajiri upo kwenye makaburi.
Mungu akiyatazama makaburi anahuzunika, maana anaona nyimbo ambazo hazitoweza kuimbwa tena, anaona mahubiri hayatoweza kuhubiriwa tena, anaona vitabu havitaweza kuandikwa tena, anaona sadaka zilizo bank hazitoweza jenga makanisa tena, anaona vipawa havitaweza kutumika tena, anaona karama hazitaweza kutumiwa tena.
Hamu ya Mungu ni kuona kila mtu aliyemuumba na kumuokoa anafanya kazi aliyomuumba kuifanya.
Na ufahari wa Mungu ni pale mtu aliyemuumba na kumuokoa anafanya kazi aliyomuumba kuifanya.
Fahari ya Toyota inapofanya kazi kwa mtengeneza toyota, na toyota inakuwa na jina jema inapofanya kazi iliyoumbiwa kuifanya.
Vivyo hivyo na fahari ya simu inapofanya kazi, ni kwa mtengeneza simu, na simu hujenga jina jema pale inapofanya kazi iliyotengenezwa kuifanya.
Fahari ya Mungu ni pale bidhaa aliyoitengeneza inafanya kazi, aliyoiumba kufanya. Na jina jema hutengenezwa na mtu pale anapofanya kazi aliyoumbiwa kuifanya.

Mithari 22:1
Mhubiri 7:1
Sulemani anasema ni heri siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.
Watu wanaogopa hasa siku ya kufa. Na siku ya kuzaliwa huwa ni siku ya sherehe kwa kila mtu, watu hufurahi na kufanya na sherehe, lakini Suremani anasema hiyo siku si heri. Siku ya msiba watu wanalia na kuomboleza, Sulemani anasema hiyo siku ndiyo heri. Hapa kuna kitu Sulemani anajua sisi hatujui.
Paulo alipofika wakati wa kufa kwake, akasema vita nimevipiga mwendo nimeumaliza na imani nimeilinda, anasema mwendo ameumaliza. Hakuogopa kufa kwasababu alijua mwendo ameumaliza: kazi ameimaliza.
Yesu hakuogopa kufa, hata akasema imekwisha, kwanini hakuogopa kufa, sababu alijua kazi yake ameimaliza.
Ukiona kazi umeimaliza, kufa inakuwa ni sawa na kuingia ndani ya chumba, unahamia sehemu nyingine.

Kitu cha kwanza kwa mtoto kukishika ni jina lake, hata kama atakuwa hajui kuona au kuongea, hata kutambaa, mama atamrazimisha alijue jina lake, kwa kumuita kila wakati.
Hata akifika shule, ni ufahari kwa walimu na wazazi wanapoona mtoto wao anajua kuandika jina lake. Hii inanipa kukua kuwa jina lina umuhimu sana.
Nilipokuwa utotoni nilidhani maana ya jina ni herufi, kama I. M. A. N. U. E. L na kujua kuwa ni kutoka na jina lilipotokea mfano Mungu pamoja nasi kwa jina la Imanuel, ila baada ya kusoma vitabu, Biblia, kusikiliza mahubiri na maisha binafsi nikaja kugundua maana ya jina ni zaidi ya nilivyofikiri.
Kuna watu wenye majina mazuri kama John, Jane, Petro, Happy, Precious, Michael, wanakosa kazi na watu wenye majina kama Mwantumu, Mboneghe, Nailejileji, wanapata kazi.
Nikagundua maana ya jina inatokana na alama uliyoweka.

Kwanini watu wanapenda majina kama Mathayo, Petro, Yohana, Daudi, Sarah, prisca, Rahabu, au Mary.

Kwanini wasiwape watoto wao majina kama Goliath, Ahabu, Yezebeli, Nebukadreza, Pilato, Herode, Iddi Amini, Senokarebu au Mabutu
Kutokana na alama waliyoweka.

Mtu aliyeweza kufanikiwa kutumia kiasi kikubwa cha ubongo kuliko wanadamu wote Albert Eastern aliwahi sema "Jaribu kuwa siyo mtu wa mafanikio, bali mtu wa thamani...maisha yanayo ishi kwa ajili ya wengine ndiyo maisha ya thamani"

Matendo na utumishi wa mtu ndiyo hujenga alama, na alama inajenga jina.
Kwahiyo; alama ya mtu inajengwa kutokana na matendo aliyofanya na utumishi aliyotumika.

Mfano Luka 7:1-5.
Akida Mrumi, aliyepatwa na tatizo la mtumwa wake kuumwa. Alipowatuma wazee kwenda kumuomba Yesu amponye mtumwa wake, wale wazee wakamwambia Yesu, "amestahili mtu huyu kutendewa jambo hili, maana analipenda taifa letu, ametujengea na hekalu".

NAMNA YA KUWEKA ALAMA, ILI KUJENGA JINA JEMA KATIKA UFALME WA MUNGU.
Ziko njia nyingi, ila leo tuongelee utumishi.
1. Tambua maono ya kanisa, na ujiunganishe nayo.
Maono ni kuona mbere kwa hekima. Nini kanisa au mchungaji anatamani kufika, au anatamani kanisa lifike. Kuna maono ya mda mfupi na ya mda mrefu, jiunganishe nayo kuhakikisha yanatimia.
Usipotambua maono ya kanisa utajitafutia mambo yako mwenyewe, utatumika, na kuishia kufanya mambo yanayoonekana hayana maana.

2. Tambua wewe ni nani, Kwanini uko hapo, na Unaweza kufanya nini.
Usipojua wewe ni nani utajitumia vibaya. Utafanya yasiyo yako.
Usipojua kwanini uko hapo; utapoteza mda na usifanye ulichopaswa kufanya, na hautofurahia maisha ya kuwa hapo.
Usipojua unaweza kufanya nini; utajaribu kufanya kila kitu, na kujikuta mpaka siku yako yako ya kufa, bado hujafanya chochote.

3. Kuwa chanzo cha mabadiriko:
Kuna watu kanisani ni waanzisha mabadiriko, na wengine washangaa mabadiriko.
Wanaoshangaa mabadiriko hawatengenezi jina, wanaosababisha mabadiriko, huweka alama na kujenga jina jema.

4. Kuwa sababu ya suruhisho la matatizo kanisani.
Kuna watu kanisani husababisha matatizo, hujenga jina baya na wengine ni suruhisho la matatizo; hujenga jina jema.
Kumbuka kushindwa kutoa suruhisho na wewe unakuwa tatizo.
Kama tatizo ni keyboard kanisani na washirika hawawi suruhisho la kupatikana na wao wanakuwa tatizo. Wataitwa washirika wasiyotoa michango. Wanakuwa tatizo kwa mchungaji, akijiuliza awafanyaje ili watoe.

5. Jitoe sadaka: kuwa wa kujitolea
Wakisema tunahitaji mtu, usiwe mtu wa kurudi nyuma, songa mbele, wanaosonga mbele hujenga majina mema, wanaorudi nyuma hawajengi majina.
Filipi 1:23.

6. Ishi kwa ajili ya wengine: Jitoe kwa ajili ya wengine.
Fanya kuona wengine wananufaika
2 Timotheo 2:10
Kuwa sababu ya wengine kufurahia ibada.

7. Usisubiri fanya (Just Do It)
Kampuni ya Nike mwaka wa 1988 January ilikuwa na utajiri wa dola milioni 177 lakini kwa kuanzisha neno la Just Do It ikawafanya mwenzi December kuwa na utajiri wa dola bilioni 9.2 sawa na tilioni 18.4 za kitanzania.
Kuna siri ndani ya neno; fanya usisubiri.
Wale wanaoona kitu na kufanya bila kusubiri wengine watafanya hujenga majina mema, ila wale wanaosema fulani atafanya hujenga majina mabaya.

8. Tafuta sehemu sahihi na ujenge jina hapo.
Kama ni kusafisha kanisa, kutoa, kufuta viti, kumtumza mchungaji, kutembelea watu, injili au kufundisha.

9. Kuwa mtu wa maono
Mtu wa maono ni mtu anayewafanya wengine kuona. Wakati wengine wanasema haiwezekani, yeye husema hebu tujaribu hivi, inawezekana.

10. Jenga tabia njema
Tabia ni wewe halisi, ni wewe nje ya ibada, nje ya madhabahu. Unafanya nini unapokuwa peke yako, unafanya nini ukifanikiwa au tukikupa cheo.
Tabia ina nguvu kuliko kipawa chako, kuliko karama au huduma.

11. Kuwa mtu wa kusadiki.
Mtu anayesadiki ni mtu anayeamini kitu kinawezekana na kushikiria kitu mpaka kinafanikiwa. Ni mtu anayeweza kuhangaikia maono ya kanisa zaidi hata ya mchungaji.

12. Tengeneza uhusiano mzuri na wengine
Tuwe furaha kwa watu wengine katika utendaji kazi.
Kuna baadhi ya kazi na maono ya kanisa huonekana ni magumu, si kwamba ni maono au kazi ngumu bali kuna tu fulani yupo.

13. Kuwa mtendaji kazi na si mfanyakazi.
Kuna mtumishi na anayetumika
Mtumishi yeye utumishi na utenda kazi upo moyoni.
Mtumishi anapotumika hufanya kwa moyo, na ni mtii hata kama mchungaji hayupo, hata kama hajatumwa, hata kama hakuna ujira, hakuna sifa alizopewa, hatazami aliyoyafanya, bali hutazama nini anapaswa kufanya.
Mfanyakazi: yeye kazi haipo moyoni, hufanya ili apate sifa, ujira au zawadi, hukwazika asiposifiwa, hukwazika akifanya peke yake, hukwazika akitoka kufanya kazi moja na kuambiwa afanye nyingine, hukwazika akikwazwa kazini, hupenda kuonekana afanyapo, si mti kiongozi asipokuwepo.

FAIDA ZA KUWEKA JINA JEMA.
1. Jina jema ni zaidi ya pesa na mali nyingi.
Maana pesa na mali huwa na kikomo, lakini jina jema hufungua milango na fulsa zaidi.

2. Jina jema hufungua mlango na kukupa kibari.
Kibari ni mlango uliyofunguka na kupitisha baraka.
Kibari huwavuta watu wa thamani kwako, kibari huvuta mafanikio na kuongeza thamani yako.
Mfano Yusuph na Daudi walipata kibari.

3. Hukupa ulinzi
Jina jema linakulinda, kila mtu atakuwa ni shahidi yako, kila mtu atapenda usishindwe na kanisa litahangaika unaposhindwa. Utakuwa kidonda kwa mchungaji, atakuita mwanae.

4. Hutakufa hakika.
Mtu mwenye jina jema kama Paulo hawezi kufa, huwezi kuhubiri injili na ujumbe uka kamilika pasipo kuchukua toka kwenye injili ya Paulo.

5. Kufanikiwa katika utumishi mdogo hukupa kufanikiwa katika utumishi mkubwa.
Hata leo unapowaona watumishi wakubwa, walianza kufanikiwa katika utumishi mdogo.

Kuna mifano ya watu waliyotumika na hawakuwa na vyeo kwenye kanisa la kwanza, maana kuna watu huamini kuwa kutumika mpaka uwe na cheo.

1. Epafra (mtu niliyempenda sana)
Huyu anapatikana kwenye kutabu cha Kolosai 4:12
Nimemuweka namba moja, kwasababu aliwabebea wenzake, na hakuna aliyemuona wakati huo, ila Paulo akaitambua huduma yake, na kuona wengine walistahimili na kuimarika kwa sababu yake.

2. Prisca na Akila.
Luka aliwandika kama Priscila na Akila kwenye kitabu cha matendo. Hawa walikuwa wakitumia pesa zao kusaidia huduma ya Paulo, walitumia nyumba zao kufundisha watu  Kristo, pale Paulo alipoenda kuhubiri injili. Na ndiyo wakiyotumiwa na na Paulo kuuza mahema aliyokuwa akiyatengeneza.

3. Luka tabibu. Huyu alitembea na Paulo popote alipoenda akiandika nini kinatukia na nini Paulo anasema.

4. Sira: aliyetembea na Paulo sehemu nyingi hata kukubali kufunga na Paulo.

5. Timotheo: kijana aliyekutwa Listra, Paulo na Sira walipo ona utumishi wake japo kuwa alikuwa ni kijana mdogo sana na baba yake hakuwa Myahudi, alikuwa na Myunani, Paulo akampenda, wazee wakamwekea mikono, akamtahiri kuogopa Wayahudi, na kuanza kutembea naye katika huduma.

6. Kreske, Tito, Tikiko, Karpo, Erasto, Trofimo, Eubulo, Pude, Lino, Klaudia: wengi kati ya hawa Paulo aliwa anzishia makanisa baaye.

7. Marko: paulo alisema kuwa anamfa sana.

NB: BADO WEWE... Chukua hatua, Inuka, Tumika, weka alama, Jenga jina jema.

MWISHO: Moja ya vitu ambavyo wapendwa wengi waliyofanikiwa kuwepo miaka ya 70 na 80, huwa vinawasikitisha ni mabadiriko ya kanisa.
Kanisa limebadirika
• tupo katika zama ambazo mabadiriko hatari yametokea kanisani
• utumishi umekuwa mtaji wa maisha
• karama za roho mtakatifu nyingi hazionekani
• huduma zimekuwa ni biashara
• sasa makanisani kuna utumishi wa matajiri na masikini. Mtu akishafanikiwa kuna baadhi ya kazi kanisani hafanyi tena.
• watu wanajenga majumba yao zaidi ya moja, na kuacha nyumba ya Bwana katika aibu.
• maombi yamekuwa ni ya watu fulani kanisani hasa wazee na wenye shida.
• mrundikano wa vijana kulima shamba la kanisa haupo tena, sasa  wachungaji ndiyo watumishi wa kazi zote.
• sadaka imekuwa ni ibada ya ziada.
• watu wanataka kuonekana na si kutumika.

Kama bahari inaweza kuhamisha vitu vyote ila si jiwe. Ni vyema wakati kanisa linabadirika, wewe usimame imara, kuweka alama na kujenga jina jema katika ufalme wa Mungu.

Kwa msaada wa Roho mtakatifu somo limeandaliwa na
ULENJE (Emanuel) MWAIPUNGU.

Monday, December 21, 2015



SEMINA DEC 2015 -DAY 1

FUMBO LA MAISHA NA KUFIKIA HATIMA NJEMA

Yer 29:11
Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho"

Bwana anakuwazia mema, mawazo ya amani, kukupa tumaini siku yako ya mwisho: swali wewe je?

Maisha yana mwanzo, kati na mwisho. Wote hapa bado hatujafika mwisho, kuna wengine wapo katikati, na wengine wanakaribia mwisho.

Lakini lipo tumaini: hata kama unakaribia mwisho au upo katikati unaweza kuyafanya maisha yako yaanze mwanzo.

Yesu alikuja ili mwanadamu apate fulsa ya kuanza tena mwanzo maisha. Hata kama alichezea kete anaweza kuanza tena mchezo na akashinda.

Ibrahimu alikuwa mwisho, Mungu anakamuita na miaka 70 na kuanza na mwanzo. Musa anaitwa akiwa anafikiri yupo katikati ya maisha, Mungu anamuita kuanza mwanzo mpya wa maisha yake. Petro vivyo hivyo na Paulo anaitwa akiwa katikati ya maisha, anaitwa na kuanza tena mwanzo.

Somo hili ni la muhimu sana kwenye maisha yako, muhimu sana. Maana Roho anakwenda kutufundisha namna ya kuutumia mwanzo wa maisha yetu kutengeneza katikati na namna ya kutumia katikati ya maisha yetu ili kujenga mwisho mzuri ambao Bwana Mungu ametuandalia.

Mungu alipokupa nguvu ya maamuzi; basi alikupa nguvu ya kuamua hatima ya maisha yako. Mungu anapanga mwisho wako, ila kuufikia au kutoufikia hayo ni maamuzi yako. Mfano Sauli Mfalme na Sulemani na Joashi.

Mungu kukuwazia mwisho mzuri haina maana kwamba Mungu anashuka na kuja kuishi kwa niaba yako. Yeye anakupa marighafi na vitendea kazi na kuwa na wewe na kukusaidia.

Na utakapojitoa na kusimama ndani ya mstari wa kufikia mwisho aliokuandalia basi atahakikisha unaufikia, lakini utakapotoka nje ya mstari basi anakuacha na kumfikiria mtoto wako au mtu mwingine kuufikia mwisho huo. Na atajitahidi kukurudisha siku zote hatochoka, mpaka siku zako za kuishi zitakapoisha. Sababu yeye ni wa rehema huwarudi wale wamrudiao, hupenda watu wamrudie.

MWANZO.
Tuanze sasa...
• Maisha yamejawa na matukio tusiyo yatarajia. Kila siku yanatokea yale ambayo hatukuyapanga wala kutarajia yatokee.
• Maisha yamejawa na hasa huendeshwa na matokeo tusiyoyatarajia. Tunapofanya vitu na kupanga mipango huwa tunataajia mema na kujikuta tunapata tofauti.

• Maisha yamejawa na matukio ya kushangaza sana.
   Watu wanakuwa tofauti na walivyotajia au kutarajiwa kuwa:
   Waliopanga kuwa madaktari wanaishia kuwa wachungaji, waliopanga kuwa maaskofu wanaishia kuwa wachungaji au mashemasi, waliopanga kuwa wanasiasa au wafanyabiashara wanaishia kuwa wafanyakazi wa kawaida, bodaboda, wakulima au walimu, na wengine kuwa walevi wa pombe, sigara au bangi na madawa ya kulevya.
   Mwanafunzi anapanga kufika chuo kikuu na mzazi anajitahidi ili kutimiza ndoto za mwanae, matokeo yake anaishia kukuletea mtoto nyumbani au kushindwa mtihani na kuishia kidato cha nne au cha tano.
   Wazazi wanashangaa wale watoto waliowapenda sana na kutarajia kuwa ndiyo watawasaidia na kuwaona kuwa ndiyo watoto wema ndiyo wanakuja kuwa hawafai na wale waliokuwa hawafai ndiyo baadae wanakuja kuwa wamaana.
     Pastors and bishop become prisoners, politician come from high ranks to prison, beautiful girls become prostitute, those we call bad girl, poor, ignorant, they become our boss, ministers, chief secretary and C. E. O.
     Those we love in public, we hate after we see them in private.

MYSTERY OF LIFE
• Life become mystery when we wonder Why we still doing what we hate (we do, what we don't wanna to do), and what we desire to do, we don't do.
"What you desire to do you're not doing and many-times you're even not able to carry them out, and what you hate you don't have the ability to stop yourself from doing.

"In fact every one has its fault that neither fear nor law can stop from doing"

• Life become mystery when we try harder and more harder to stop ourself from doing some action, and we fail. We try to stop some attitude and behavior and we fail.
Sometime we cry, explain to people, pray and asking God mercy and grace and we wonder why we still do what we pray and ask to stop.

• We know something is evil, and we try to stop our mind and our body to execute them, A force come from our heart, a force that we don't know  even its name that our body and our mind succumb to do what we truly hate to do.
  And what we know is right and is what God want us to do, we force our mind and body to do, we wonder we are not.
  Eg. I desire to wake up early in the morning to pray I don't, I plan to pray in mid night I fail, I desire to fast and pray but I don't, I desire to be more powerful and spiritual in the kingdom of God, but I'm not. We desire to have good relationship with God and doing what he want, but we wonder we don't, everyday instead of saying yes I win, we ask for mercy.

• And the mystery of all, Many of us we are not what we desire and wish to become when we're youth.

• This is mystery to more than 90% of the world population: Many folks they don't even know themselves.
  We pretend to, but we don't.

* We try to know God but not ourselves,
   Whilst is difficult to know God if you don't know yourself      what Make me wonder is that, Even God, has a desire to see all of us, to know ourselves. That why, He never call somebody without tell him who he is. Before telling Abraham Go! He first tell him, I call you be father of the nations, Before telling Moses Go! He first tell him, Saviour of His people, Before tell Jeremiah, he first tell him why he make his birth.
# In fact, Your purpose is what carry your real identity"

"You wander and wander doing everything because you don't know yourself"

* when you know yourself, will make you to know that you cant live without God, and God Joy is your Joy and strength.
* Many folks die, only they know they're names but not themselves.
* And some they don't even bothering, that they do not know they are. Only they care, is to make living.
* Some people they try harder and harder to know who they are, finding they're purpose. But they become old and die, without achieving they're desire, Why? They finding from wrong source. God is only source, because is one who created you. (Recommend Book : Purpose Driven Life By Rick Warren and The Power of Purpose By Dr Myles Munroe)
* Many Elites, They only know they're positions and they're bosses and not them self. That why most of them they die with stress and Blood Pressure.

• Life has no experts: We're all facing challenges, problem, thing we cant handle, unexpected and unplanned events, and unexpected results. But Those Who have Faith in God are always safe.

• Everyone need better life, better world, better marriage and better family. And this make human an Utopia

• we all want more and plenty money, while some they lie, pretending that they don't need money, they lie, they need more, and they want more than you.

"Money is not everything, but is important to everything" Robert Kiyosaki

But seek ye first the Kingdom of God and His Righteousness and Other Thing (including money) shall be added to you"

• We live life but we don't know the meaning of it
This is what I know "we can have many definitions about life, but experience will tell you the truth" #Ev.Ulenje

Kesho tunaendelea
Umbali si shida waweza kuwa karibu nasi.
Ubarikiwe Sana kwa kusoma.
Naamini kuna kitu umepata, pita soma tena na tena.

+255 718 721 848
imaf2b@gmail.com

Wednesday, December 9, 2015

SEHEMU YA SITA: BARAKA TANO ZA PETRO NA KUJENGA KESHO KWA HEKIMA

Asante kwa kusoma sehemu ya tano, kama bado nakuomba katika Jina la Bwana Yesu tenga mda na usome sehemu ya tano, sasa tuendelee... ulenje.blogspot.com

B. KESHO

Baada ya kujifunza kuhusu jana sasa ni vema tukajua zaidi kuhusu kesho na kuona namna Petro alivyoweza kutumia leo yake kutengeneza kesho yake.

Petro siku zote alifanya jambo pasipo kutazama jana, hakutazama makosa, kati ya wanafuzi 12 Petro alikuwa ndiye mwanafunzi aliyekaripiwa na Yesu mara nyingi na kukosolewa mara nyingi lakini ndiye aliyetumiwa na kuwekwa karibu sana na Yesu, si hivyo tu, baada ya Yesu kuondoka Petro ndiye maanafunzi aliyeachwa kuwa kiongozi kati ya watume, ndiye aliyeambiwa waimarishe wenzio, ndiye aliyeambiwa kisha kondoo wangu, unaona pamoja na makosa yake yote lakini Mungu aliyakusanya yote na kuyafanya mema kwa kutimiza kusudi lake duniani.

"Unataka kumjua mtu asiyekosea, mtafute mtu asiyetumia fulsa"

Unataka kumjua mtu anayekosea na kuibuka mshindi, mtafute Petro, anayeona fulsa na kuitumia, wakamuita kiherehere, wakamuita mnafki, wakamuita charismatic, wakamuita msariti, lakini ndiye huwezi taja maendereo ya kanisa la kwanza na kuacha jina lake, hata Paulo anajua hilo, hata wewe unayesoma unajua hilo.

Uanataka kuwa mtu wa mafanikio, jaribu sana, ukikosea umia tena umia sana ili usirudie kosa hilo, jisamehe jisamehe tena jisamehe sana, kisha jaribu tena, ukikosea jaribu tena usiache kujaribu, hata ukifika mbinguni, jaribu kuimba kila wimbo jaribu kila wimbo mpaka uwekwe kiongozi wa kuimba kama cheo hiko kipo, lakini kubwa usiache kujaribu.

Najua ungetamani leo iwe ya pili kuelezwa, lakini hapana, siku zote ni za muhimu lakini kwa mafanikio ya mwanadamu LEO ni kuu na muhimu kuliko zote.

Kesho ni mda wa mbere ambao bado haujafikiwa na kuanza kutumika"
Katika mda uliyopewa na Mungu, kesho ni mda ambao bado hujaufikia.
Yesu akasema "Basi msiyasumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe" Math 6:34. Yesu hapa alikuwa akizungumzia siku ya kesho, ambayo ipo mikononi mwako, ambayo katika mda uliyopewa kuishi, kesho ya kwako.
Mtu aliyekufa hana kesho, mtu aliye bado mzima ndiye pekee mwenye kesho. Hivyo kesho ni yako, ukiwa hujaamka kesho, ujue siku zako ziliisha.
Siku ya mkesha wa mwaka mpya wa mwaka 2014 mchungaji wa kanisa la CLC alitoa hadithi ya ajari ya mtu aliyegongwa na gari aina ya Toyota iliyotokea mda wa mchana wa tarehe 31/12/2013, siku moja kabla ya mwaka mpya wa mwaka huo, kisha akasema "fikiri kama tukirudisha dakika moja nyuma, wewe unadhani yule mtu atakuwa anawaza nini kichwani mwake?" Akajibu mwenyewe akasema "lazima atakuwa anawaza mipango ya kufanya baadae". Sijatoa hii hadithi kukwambia usipange ya kesho, nimetoa hii hadithi kukuonesha kuwa, kesho ni yako kama ukiifikia, usipoifikia si yako,

Hivyo kati ya siku tatu: jana, kesho na leo. Tunayoimiliki ni leo tu pekee, si jana wala si kesho. Na usiumize kichwa kwa habari ya kesho, panga tu kwa habari ya kesho, umiza kichwa kwa habari ya leo. Tukizungumzia leo, utanielewa.

"Weka mipango ya kesho na kuwa na dhamira dhabiti ya kuitimiza ila Usiumize kichwa kwa habari ya kesho, Wala usiwaze kwa habari ya jana, umiza kichwa nini unapaswa kufanya na usichopaswa kufanya Leo, maana leo ndiyo siku pekee tunayoimiliki"

Ndugu mpendwa leo ndiyo yenye nguvu kubwa ya kubadiri maisha yako, si jana, wala si kesho.

UTAENDA JEHANAMU SI KWA ULIYOFANYA JANA SI KWA UNAYOPANGA KUFANYA KESHO, ni kwa unayofanya LEO"

Kesho ni siku ndani ya mda tuliyopewa na Mungu ambayo hatujaifikia bado, tukiifikia inaitwa leo, hakuna mtu anayeimiliki kesho. Kama hatujui kuwa tutakufa lini ndivyo hatujui kuwa tuna kesho. Hivyo kesho ni miliki yetu ila ni milki hewa. Inaweza tokea au isitokee.
Kifupi ni kwamba: Mungu amempa kila mtu kusudi yaani kazi ya kufanya na kumpa mda ambao anajua hiyo kazi itakuwa imeisha, kuna wakati anaweza kuongeza, pia mwandamu anaweza kwa kuounguza mwenyewe, hasa pale mwanadamu anapotumia nguvu yake ya maamuzi kufanya jambo ambalo linaweza changia kuondoa uhai wake, Daudi alilia (paraphrase) "Bwana nipe kuzijua siku za kuishi kwangu ili tujue namna ya kuenenda"

1. Kesho ni siku mbere ya leo
2. Kesho ni siku ambayo bado haijatumika
3. Kila mwanadamu ni mjinga kuhusu kesho
4. Na ujinga huleta woga na hofu kwa kila mwanadamu kuhusu kesho.
5. Woga na hofu huleta watu kuisumbukia sana kesho.
6. Kesho ni makisio tu si kitu halisi.
7. Masikini wanahofu na kuacha ije inavyotaka, matajiri wanapanga wanavyotaka ije
8. Masikini wanaamini kutofika kesho, matajiri wanatumai kufika kesho bila kujari umri wao
9. Masikini wanajadiri kesho, matajiri wanawekeza kupata faida kesho.
10. Mabepari wanawekeza kesho kwa hofu ya watoto wao, wenye hekima wanawekeza kwa kizazi kijacho
11. Maisha unayoishi leo, ndiyo yatakuwa kesho yako; maisha ya kesho, yatakupa unachompa wewe leo.
12. Hakuna unachofanya leo, usivune kesho, na kile unachopanda leo, ndicho utakachovuna kesho
13. Maamuzi yako ya leo, ndiyo matokeo ya kesho.
14. Kesho hujaifika, iache siku itoshe kwa maovu yake
15. Usiseme nitafanya kesho hata mara moja, fanya sasa. Toa mchango sasa, panga mipango sasa, tekeleza sasa, kuwa muaminifu sasa, tenda mema sasa, jenga ndoa nzuri sasa, saidia watu sasa. Kuna watu wanatamani waume na wake zao wafufuke ili waweze kusema "nimekusamehe mume wangu, au nimekusamehe mke" ila haiwezi kutokea. Samehe leo, mpende mume au mke leo, fanya malenzi ya Mungu leo.

FIKRA TOFAUTI KUHUSU KESHO.
Tengeneza picha kwenye kichwa chako, wewe ndiyo Yusuph upo gerezani kwa kosa la kusingiziwa. Unapelekwa kufanya kazi za gerezani, unateswa na mijeredi, unakula chakula cha gerezani, miaka mitano inafika na huoni hata wa kuja kukuona au ndugu yako kujua kuwa mzima. Futa wazo kuwa unajua nini kiliendelea kwa Yusuph, fikiria haupo kwenye hadithi  na si hadithi, fikiria ni tukio la kweri kwako; hivi nini mawazo yatakuja kichwani mwako mfano; "nitatoka kweri?, nitatokaje?, itakuwaje wakiniuwa?, au nimkane Mungu wangu?, au nijifanye Mmisri?" Maswari mengi najua yalikuwa ndani ya Yusuph mpaka kufikia hatua ya kuwaambia wale wafanyakazi wa Farao waliopata fursa ya kutoka "msinisahau..." Kwanini alikuwa akitafuta njia ya kutoka, alikuwa hajui kesho yake. Ukweli wa hadithi ni kwamba anayeifahami hadithi anafahamu nini kinaendereana nini kitatokea, tofauti na yule asiyejua hadithi au yule ambaye anaipitia hadithi hiyo.
Yusuph alikuwa hajui nini kitatokea, wewe unajua nini kilimtokea, sasa kuielewa zaidi hadithi hii inatakiwa uivae hadithi hii ya Yusuph na iwe kama wewe, ndipo utajua kuwa mtu anayepitia hajui kesho.
Masikini kwao kesho ni kitendawili kisichokuwa na majibu. Kwao kesho siyo siku yao, ni siku ya wengine, kwao kesho kufika ni 0/100. Na hivyo hakuna anayewaza kesho. Anapopata pesa ya kula siku hiyo, anafurahi na kuona siku hiyo ni ya bahati sana, anafunga kazi na kupumzika. Anafungua pochi mda wa kula ukifika, akimaliza kula analala, akingoja kesho apate tena wapi ya kula. Maisha yote ni mkono na mdomo. Kwanini hawazi kwa habari ya kesho.
Matajiri hawawazi kwa habari ya kesho sana japo hofu yao kubwa kwa habari ya kesho, ni kushuka kiuchumi na kurudi kuwa kama jana yaani wanaogopa kurudi kuwa masikini. Hivyo kundi hili ni kundi lisilojiamini na lenye hofu kubwa sana, kuhusu kesho, utofauti wao na masikini, wao hawawazi kutofika, bali wao wanawaza itakuwaje wakifika wakiwa wameshuka chini kiuchumi na kurudi kama jana. Na hii huwafanya kuwa watu waoga sana wanapokuwa katika siku ya leo. Uzuri wao ni watu wa kupanga sana kwa habari ya kesho. Mabepari wao kesho ni siku ya muhimu sana na hivyo hutumia pesa, nguvu na tekinolojia  kupanga kwa habari ya kesho, mabepari huwaza faida, huwaza masikini atabaki vipi kuwa masikini, siku zote anafikiri na kubashiri kinachowesa kutokea kesho.

Mabepari huwa ni watu wa kufikiri sana, nini kitatokea kesho: uchumi kushuka au kupanda, pesa kushuka au kupanda, biashara kushuka au kupanda. Siku zote wanawaza hayo ili wajue namna ya kushindana na soko.

Wajamaa, wao na serikari tu; mara zote hutumia mda kusoma magazeti na kutazama television kuona nini serikari imepanga kufanya kesho, huwa makini kujua mipango ya serikari ya mda mfupi na muda mrefu na hufatiria kama inatimia. Watu hawa hupatikana hata nchi za kibepari pia.
"Watu wajamaa huwa wanawaza sana serikari imefanya nini kuliko hata wao wamefanya nini"

Watu wa ufalme wa Mungu wao huwa hawakondi wala kukosa furaja kwasababu ya kesho. Wao hutafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, kisha haki yao waliyonayo katika ufalme wa Mungu humfanya mfalme wao ambaye ni Mungu Baba kuwatengenezea fulsa. Soma vizuri kuwatengenezea fulsa, huwaandalia mazingira, huwapa kibari, huwapa hekima na maarifa zitakazowasaidia kufanikiwa. Kama ndege wa angani alivyokuwa hana shamba, hana ghara la kuifadhi chakula, wala hana duka ila Baba wa mbinguni humlisha.
Ukifanya uchunguzi wa ndege utagundua kuwa, yeye hutoka kiotani akiwa na matumaini kuna sehemu nitakuta chakula, nitakula na kupata chakula cha watoto wangu. Tazama maua ya kondoni, hayalimi wala hayavuni ila hata Sulemani na fahari yake hajapata kuvikwa kama maua hayo. Mauwa ili yaoate chakula, huwa yanaamini yakishusha mizizi yake na kuchanua maua yake wakati wa mchana yatapata chakuka na mwanga.

Jambo la msingi kuhusu ndege, anatoka kiotani kwenda kuchukua chakula alipowekewa na Baba wa mbinguni.

Maua huwa yanatoa mzizi na kuchanua ili yapate chakula na mwanga.

Nini cha kujifunza Yesu hakusema watu wa Ufalme wa Mungu wasifanye kazi au wasitoke mlangoni mwao na kutazama fulsa na kuzitumia, Kama Ndege anavyotoka kiotani na kwenda sehemu ambapo anaamini Mungu wake wa Mbinguni amemuandalia chakula, ndivyo nawe pia utoke mlangoni ukatazame fulsa pale ambapo Baba yake wa mbinguni amekuandalia.
Kama vile mauwa yanavyotoa miziz yake na majani yake yakiamini kwamba Baba wa Mbinguni amewaandalia maji na mwanga wa jua kwa chakula. Tafuta mtandao tafuta mawazo tafuta marafiki tafuta watu ukiamini kuwa Baba yako wa mbinguni kuna fulsa amekuandalia.

Jifunze katika mfano wa Yesu, kama Baba wa mbinguni anayalisha maua na ndege wa angani, itakuwaje wewe ambaye alikubali mpaka hata kufa kwaajili yako. Kuna fulsa nyingi amekuandalia toka mlangoni si kwa hofu, toka nje kwa imani, ukiamini kuna fulsa amekuandalia leo kufikia mafanikio yako.
Tuma tema barua ya maombi ya kazi, nenda tena kuomba kazi, fanya juhudi mpya maana Baba wa Mbinguni amekuandalia fulsa za kutosha.

Acha hofu na kesho, tafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na mengine hayo Yesu amekuandalia, wewe tazama fulsa na usonge mbele.

Mfano; Mungu atatoa watu kutoka mashariki na magharibi ya mbali kukuletea fulsa. Mamajusi toka mashariki ya mbali ni uthibitisho tosha kuwa Bwana atafanya hilo.

Watu wa ufalme wa Mungu huwa hawana tatizo, kwasababu wao, wameamini Baba yao wa mbinguni anawajua wao, na anashughukika kuwa mema. Hivyo kwao kesho siyo kitendawili, bali Mungu wao ndiyo tumaini kuu na kati ya watu wanaowaza na kutumaini kesho njema ni watu wa kundi hili.

FIKRA HASI KUHUSU KESHO.
watu wengi wanaoishi maisha ya kushindwa huwa wanaangukia kwenye makundi haya mawili.
1. Wale wanaosema "nani anayajua ya kesho" hivyo wanaishi kama wanakufa usiku na wanaona kufika kesho ni asilimia 0, wanaona kesho ni kama makisio tu, ni kama siku isiyofikika. Cha ajabu wanajikuta wamefika, hawana hata pesa ya kuanzia, au hata sehemu ya kuanzia, wanatafuta pesa ya kula, wanakula wanalala huku wakiwa na asilimia 0 za kuamka, wanajikuta wanaamka. Maisha yao huwa ni ya kujaa taabu, utumwa, manung'uniko, kukosa tumaini, kuhangaika, hawana malengo, hawana akiba, wanakula wanalala na kuamka.

Nimewahi kuwa na rafiki yangu nikiwa O-Level: baba yake alikuwa ni mtu mwenye pesa, na kuwafanya kuishi sehemu za watu wenye pesa maarufu kama Kilakala kwa watu wanaotoka Morogoro. Baada ya baba yake kustaafu, maisha yao yalibadirika na kuwa maisha ya shida sana kipesa, siku moja alikosa fedha ya nauli ya kurudi nyumbani kwao kutokea na shule, akanifata na kuniomba nauli, kwa kicheko nikamjibu "tatizo baba zenu wanakumbuka kujenga kwa pesa za kustaafu, nyumba ikiisha na pesa zimekwisha mnakuwa masikini" siku ile hakunielewa lakini akisha kuwa mkubwa atanielewa.

Watu wengi wanatumia pesa zao za mshahara zote, na kuacha kupanga ya kesho, wakiona watakufa kesho, wanashangaa hawafi.
• Watu hawa hutafuta pesa za leo bila kupanga kuhusu kesho yao.
• Huwa hawafanyi majukumu yao, wakiamini kesho itawafanyia majukumu yao.
• hawana mipango
• hawana maono wala ndoto
 • hawana uwekezaji wowote
• hawasaidii watu wengine

2. Kundi la pili ni wale wanaoitafutia kesho maisha na siyo wao wenyewe".
Watu hawa huangaika na kuhangaika wakaiitafutia kesho chakula, mavazi, heshima na utukufu. Kumbuka nimesema "wakiitafautia kesho" siyo "wakijitafutia".

Kundi hili ni watu wenye hofu, mashaka, kuhangaika, na wengi huwa wanatumia mpaka njia ambazo si harari, njia hatarishi, dhuruma, ufisadi na rushwa, ili kutengeneza kesho yao. Watu hawa huishia kuitafutia kesho yao, na kusahau kujitafutia wenyewe maisha. Kuitafutia kesho haki na kusahau kujitafutia wewe haki, si mafanikio ni utumwa.
Mr Msofe alijitahidi kutafuta pesa kwa hari nyingi, aliuza bangi, madawa ya kulevya, akajiunga na rushwa za kuizurumu serikari na dhuruma nyingi akiihofu kesho yake, pesa nyingi alizopata aliweka akiba akiogopa kuteseka kesho yake; akajenga majumba na makampuni, alipomaliza kufanya yote sasa aanze kula faida, akavamiwa na majambazi wenzie akapigwa risasi akafa" Kesho inafaidika yeye ameenda na maji.

Patric the great kijana maarufu, akaenda kwa mganga ili apate utajiri, baada ya kupata utajiri, akaowa na kupata mtoto, baada ya miaka mitano akaumwa akafa, mke akapokonywa mari na ndugu wakatapanya mari zikaisha.

Mzee James ili kupata utajiri akaradhimika kuhudhuria kanisani siku ya jumaapili pekee na siku zingine alikataa kufunga duka lake ili aende kanisani, alipopata utajiri wa kuanza kufanya biashara nje ya nchi, akapata ajari akafa, ndugu wakatapanya mari na mke wake akaishi maisha ya shida.
Mr Tomson alipopata pesa zake za ajira yake ya kusafisha ofisi za watu, kufagia na kuzoa taka taka. Pesa alizopata aliziifadhi chini ya kitanda chake, akisema kesho nitazitumia katika uzee wangu. Siku moja akapata ajari ya gari kabla ya uzee wake, akafa. Hakuwa na ndugu maeneo yale, wakatangaza kwenye vyombo vya habari ili wapate ndugu zake, hakuna aliyejitokeza. Serikari ikachukua jukumu la kumzika. Walipoifungua nyumba yake, wakakuta Dola zaidi ya milioni kumi na tano. Mr Tomson aliishi maisha ya kimasikini sana, kila mtu aliyesikia habari ya kukutwa kwa pesa zile na maisha ya Tomson kila mtu alihuzunika. Kwanini alitafuta maisha ya kesho akasahau kuyatafutia maisha yake.
• Watu wa kundi hili hutumia pesa nyingi kuweka akiba na si kuzalisha pesa zingine
• watu hawa hutumia mda mwingi kujenga ya kesho kuliko kujenga maisha yao, wakihofu kushuka kiuchumi zaidi kuliko kushuka kwa maisha yao, wakihofu vipi fulani akinipita
• watu kama hao ni waoga sana kwa habari ya kesho. Huwa hawana amani siku zote. Wanahofu sana kuwa wasipotafuta leo kesho watateseka sana.
• watu kama hawa, huishi kama masikini wakihifadhi na kutafuta ya kesho. Husema moyoni mwao heri nilale njaa leo, kesho nitashiba na kusaza.
Robert Kiyosaki amewahi sema "haina maana kuishi masikini na kufa tajiri"

Watu wengi wanaishi kama masikini wakisema wanahifadhi, wanajikuta wanaishi masikini nankufa tajiri wakiwaacha watoto na ndugu zao kama Fisi wakigombea mari zao. Unahitaji kujipanga.

"Jenga ufalme wa mbinguni ambapo mwivi wala kutu haviwezi kuharibu"

Kesho ni mda wa mbere ambao Mungu ameundaa kwaajili yako. Na ana mpango na wewe, anachotaka ni wewe kutafuta ufalme wake na haki yake, kisha mengine utazidishiwa. Kwa maana ndogo fanya nafasi yako na umuache Mungu afanye nafasi yake.

FIKRA SAHIHI KUHUSU KESHO

Usikose sehemu ya sita tukizungumzi fikra sahihi kuhusu kesho.
Asante kwa kusoma naamini Roho mtakatifu hajakuangusha, neno hili ni ya hai na linaponya soma vema hata mara mbili ili uelewa
Uliza swali aunacha comment na share ili unisaidie somo hili kufika na kwa wengine.
MUNGU AKUBARIKI
From Holy Spiri