Wednesday, January 11, 2023

 DHANA HALISI ZA MAFANIKIO

(PRECEPTS TO SUCCEED)

The Original Concepts for Personal Success


Dhana ni wa wazo kuhusu jambo fulani.

Natamani tuone wazo halisi kuhusu Mafanikio. 

Na wazo halisi kuhusu mafanikio tunalipata kwa Mungu. Wazo halisi ni la muhimu sana sababu ndilo linakupa mafanikio halisi.

Mafanikio unaweza kuyapata kwa namna yoyote, na watu wakahisi umefanikiwa na kumbe ni mafanikio feki, tutakuja kuona ufupi wa furaha ya maisha yako na mwisho wako.

Mwaka huu mpya natamani twende kwenye mafanikio halisi, mafanikio ambayo yanatokana na baraka ya Bwana, ambayo haichanganyikani na majuto ndani yake. Binafsi leo naweka agano la kuzifata.

Kwanza naomba ijurikane sisi wana wa Mungu, ni watoto wa Mungu ni mawakili wa ufalme wa Mungu, hivyo tupo duniani kumuwakilisha Mungu, tupo duniani kuwavuta watu wa duniani waje kwenye ufalme wetu. 

Na njia kuu ya kufanya hivyo, ni kutumia kanuni zetu za mafanikio kw usahihi na bidii ili watu wa ulimwengu huu wakiona, watamani kufata kanuni zetu na kuingia kwenye ufalme wetu. Lakini kama tutafanikiwa kwa njia zao, basi hatutakuwa na sababu yoyote ya kuwavuta wao kwetu.


Tunapomaliza mwaka 2022 kuingia mwaka 2023 dalili zimeonekana wazi kwa Tanzania na dunia kuwa uchumi unazidi kushuka, hata Oxford Economics yenye jopo la wachumi 300 wamefanyia utafiti nchi zaidi ya 200 na kuona uchumi unashuka toka pato la 3% mpaka 1.3%. kwa namna hii tunahitaji kanuni za Mungu ili kuwa salama


Jiandae kutembea na kanuni za Mungu ambazo hazitashindwa.


1.   MFANO WA MUNGU 

   ðŸ‘‰ ILI KUTAWARA

Biblia inasema katika 

Mwa 1:26 na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyaa, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho chini ya nchi 

na Sura ya 27 inaweka wazi kuwa Mungu akaumba mtu kwa mfano wake. 

Mungu alimpa mwanadamu cha kwanza ni mfano wake na sura yake, ndipo akasema wakatawale. 

Kutawala ndiyo siraha ya kwanza mwanadamu kufanikiwa, kama ukitawala katika huduma umefanikiwa, ukitawala katika biashara umefanikiwa, ukitawala kazini umefanikiwa. Kwa sababu ili ufanikiwe lazima watu wakujie, na ukitawala maana yake watu wanakujia kupokea bidhaa yako au huduma yako, hapo umefanikiwa


Lakini ili upate utawala wa kweli, sifa ya kwanza ni lazima ufanane na Mungu. Kufanana na Mungu ni katika nia ya ndani, katika nia ya matendo yake, na namna ya kuishi binafsi na watu wengine. Na hasa aliongelea utu wa ndani.

Paulo anasema katika 

Efeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Tuliumbwa katika Kristo, sababu kule kuumbwa kwa kwanza kwa lile kosa la adui kulitufanya kuharibika. Siyo muonekano wa nje, bali ndani. Na anaonyesha kuna matendo Mungu aliyaweka tangu awali, ambayo sababu ya anguko mwanadamu akawa hawezi tena kuyafanya.

Yesu anasema zamani haikuwa hivi, ila sababu ya ugumu wa mioyo yenu.

Ukisoma 

Efeso 4:24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. 

Ukisoma tena Kolosai 3:10 Paulo anasema mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

Kama tunataka kufanikiwa katika uchumi, dhana ya kwanza kabisa ni kuwa watawara, kutawala katika mauzo ya biashara zetu, kutawala kazini, kutawala katika huduma. 

Mwa 17:1-5 Mungu anamwambia Ibrahimu, Mimi ni Mungu mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. Abramu akanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi.  

Mungu alipomwambia awe mkamilifu alimaanisha awe afanane na yeye, awe tofauti na wanadamu. Na Ibrahim alipoanguka kifudifudi ishara kukubali, Mungu akwambia sasa nitafanya agano la kukupa kutawara.

Na Yesu anatuamuru tuwe tofauti na watu wengine katika Math 5:48 ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu


2.   PUMZI YA UHAI.

  👉 HAPO UTAWEZA FANYA CHOCHOTE.


Biblia inasema 

Mwa 2:7 Bwana akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Neno la msingi hapo ni mwanadamu akawa nafsi hai. Maana yake ile pumzi ya uhai ndiyo ikamfanya kuwa nafsi hai. Mtu asiye hai hawezi kufanya chochote. Adamu alipokufa kiroho ndipo mahangaiko ya mwanadamu yalianza. 

Lakini inaonyesha uhai wa mwanadamu unatoka kwa Mungu, mwanadamu hawezi chochote pasipo Mungu, mwanadamu pasipo Mungu kinachofata ni mahangaiko tu. 

Utaona mwanadamu alipopewa pumzi ya uhai akawa nafsi hai ndipo Bwana anampa kazi sasa ya kufanya. Kazi ni jukumu la kukuletea pesa, kukuletea mafanikio lakini huwezi fanya kazi pasipo ile pumzi ya uhai, mwisho wake ni mahangaiko,  

Kinachofanya wengi wasipate mafanikio ni kwa sababu wanahangaika na kazi, wanaacha walichopewa ili kufanikisha kazi. Na wengine wanapata mafanikio feki ambayo mwisho wake ni mauti.

Ibrahimu baada ya kutembea sana kuendea nchi ambayo Bwana atamuaonyesha. Mwanzo 12:7 Bwana anamwambia uzao wako nitawapa nchi hii. Kabla hata ya kuanza kuilima wala kujenga hema, akamjengea Madhabahu BWANA aliyemtokea, mstari wa 8 unasema ...akaliitia jina la BWANA.

Hii ilimaanisha Ibrahimu alijua, sawa Mungu amenipa sehemu ila lazima nimtake Yeye kwanza ambaye ndiye pumzi ya uhai ili nifanikiwe katika hii nchi...

Yesu amekaa miaka 30 bila kuanza kazi aliyoijia mpaka aliposhukiwa na Roho mtakatifu Luka 3:22-23. Neno la Bwana linamjia Zakaria kwa Zerubabeli Zekaria 4:6 kusema Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali kwa roho yangu, asema BWANA wa majeshi.

Wakati kanuni za dunia zimeshindwa, na umezijaribu sana, 2023 kaa chini na Roho Mtakatifu kwanza muulize nini nifanye, pili mshirikishe katika kila unalofanya. Ufanye 2023 siyo mwaka wa kujaribu bali wa kufanya. Baada ya Israel kuzunguka miaka 40 mlima Seiri, sauti ya Bwana ikamjia Musa peteni njia hii (Kumb 2:1-3). 

Weka mkazo sana katika kumtaka Bwana 2023 zaidi ya miaka yote, taka sana ufalme wake na haki yake, yale ambayo wengine wanayasumbukia hawayapati au wanatumia njia ya udhalimu kuyapata, wewe Mungu atakupa kibali na kukuweka katika nafasi ya kuyapata.


3.   BARAKA ZA BWANA.

 ðŸ‘‰ ILI UONGEZEKE


Baada tu ya mwanadamu kuwa nafsi hai, Mungu akambariki. 

Mwanzo 1:28 Biblia inasema Mungu akawabarikiwa, Mungu akawaambia Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini,na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Nikwambie tu wazi unahitaji baraka za Bwana kuliko unavyoweza ukafikiri. 

Watu wengi wanapenda kuongezeka, wanapenda kuzaa vitu, kuanzisha biashara, kampuni na wanataka waende dunia nzima pasipo baraka za Bwana. 

Baraka ni uwezesho wa Mungu ndani ya mtu wa kufanikiwa. Baraka ni kibali cha Mungu, ni neema.

Mtu aliyebarikiwa, ile baraka inampa kufanikiwa katika kila analogusa. Haina maana hatokutana na changamoto, ila ile baraka inampa ulinzi na kushinda.

Biblia inaweka wazi mtu aliyebarikiwa atakuwa tajiri, Mith 10:22 inasema Baraka ya Bwana hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo. 

Katika agano jipya 

Efeso 1:3, 4, Paulo anasema Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo. Kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo

Hilo neno kama na neno ili tuwe linaunganisha kuonyesha Kumbe kuwa mtakatifu, kuwa mtu usie na hatia mbele zake inaambatana kabisa na baraka zetu kutenda kazi, ndiyo maana hata Adamu utakatifu ndiyo ulilinda baraka yake.  

Ndiyo maana utaona baada ya Bwana kumaliza kumuumba mtu, na kumpatia baraka zote akampa Discipline. Adabu, akamwambia utaishi ndani ya bustani lakini kwa mipaka, kula miti yote lakini miti fulani usile. 

2023 jiandae kuishi kwa mipaka, ishi maisha ukifanya unayopaswa kufanya, achana na yale ambayo yanakuondoa kwenye reli, kwa maana yaliyofanya mpaka sasa una struggle ni kutoishi kwa mipaka.

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477 827 

FOLLOW ME KWA; 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram 

Kama Pastor Ulenje.


 



MAANA YA KUJITIA NGUVU KATIKA BWANA, INUKA

JITIE NGUVU KATIKA BWANA, INUKA.


1 SAMWELI 30:1-8

Kujitia nguvu katika Bwana ni kukumbuka ya kwamba yupo Mungu ambaye naweza nikamtegemea, yupo Mungu ambaye nikimtafuta atanipigania na kunipa ushindi.


KWANINI NIJITIE NGUVU KATIKA BWANA.


1.     KWASABABU BWANA AMETUHIFADHI HAI

Wakati wa changamoto zote, unachokihitaji hasa ni kuwa hai, kwa sababu ukiwa hai unaweza kugeuza yote uliyokutana nayo kuwa ushuhuda. Kwa sababu majaribu hayawezi kukuharibu kama bado una uhai wa kuendelea kujaribu. Pamoja na yote tuliyokutana nayo, ila Bwana alihakikisha yanatuliza, yanatuumiza, yanatuvunja moyo ila hayatuuwi. Siyo kwamba hayakuwa na nguvu ya kutuuwa, ila kwa sababu Bwana alikuwa upande wetu kuhakikisha tunaishi, ili siku moja tuje kusema Farasi na mpanda Farasi aliwatupa baharini. 1 Sam 27:8,9.

Pamoja na yote Daudi aliyokutana nayo, Bwana alihakikisha Suali hamuuwi, alihakikisha Wafilisti hamuuwi, alihakikisha Waamaleki hamuuwi_ kwanini kwa sababu Bwana alitaka kuyageuza yote aliyopitia kuwa kitabu cha SIFA CHENYE SURA nyingi kuliko zote kwenye Biblia 150. 

Biblia inasema Mhubiri 9:4 Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);


Maadamu Una Uhai, Bado Lipo Tumaini, Inuka Jitie Nguvu Katika Bwana.


2.     KWA SABABU MACHOZI TULIYOLIA HAYAJATUTOA TULIPO TEKWA.

Daudi na wenzie minne wakainua sauti zao na kulia, siyo tu walilia, bali waliinua sauti zao na kulia mpaka walipokuwa hawana nguvu za kulia tena; lakini majibu hayakutokea. Wakaanza kumlaumu Daudi lakini lawama hazikuwasaidia.

Mungu ameweka machozi ili kutujulisha kwamba kuna jambo la uchungu, ila siyo njia ya kututoa kwenye uchungu. Mungu ameweka machozi ili watu wajue kuwa upo matekani, ila siyo ya kukutoa kwenye mateka. Kama umeamua kulia ni bora ulie kuinuka kwa mkono wa Bwana ili siyo ulie kuonyesha namna unapitia. Adui amekuteka ili ulie, unapolia unampa sifa kuona amekuweza. Daudi akainuka, akajitia nguvu katika Bwana, ndipo ukombozi wao ukapatikana. 

Kama machozi hayajakupa matokeo, Leo inuka Jitie Nguvu katika Bwana, Mungu wako Anakusubiri umalize kulia na kulalamika ili Akusaidie. Wakati Daudi na wenzie wanalia, Mungu alikuwa akiwatazama, ila Daudi alipojitia nguvu, Mungu akainua mkono wake na kuwainua na hapo ukawa mwanzo wa Daudi kuwa Mfalme na wenzie kuwa majemedari wa jeshi na wakuu wa Israel ambao hapo kwanza walimfata Daudi sababu walikuwa na njaa na madeni.


3.     KWA SABABU BWANA AMEHAKIKISHA TUNABAKIWA NA NAIVERA.

Wakati adui anateka vyote kuhani tulibakiwa naye, na naivera nayo ikabaki. Naivera lilikuwa ni vazi la kikuhani, ambalo kuhani alivaa anapojihudhurisha kwa Bwana, na ni vazi lilibeba majina ya makabila ya wana wa Israel. 

Adui ameiba vyote, ila damu ya Yesu bado tunayo, ambayo haishindwi kwa dhambi zetu, haishindwi kwa nguvu za adui, haishindwi kwa nguvu ya pesa, adui ataiba vyote ili naivera bado tunayo, vazi la damu ya Yesu bado tunalo ambalo kwa hilo tunasogea mbele za Mungu wetu na kupokea nguvu mpya ya kumshinda adui aliyetushinda.

Ebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.


Maadamu bado una vazi la damu ya Yesu, Acha kubaki chini, Jitie nguvu katika BWANA 2023, inuka.


4.     UKIFUATA UTAYAPATA. 

Daudi alipoacha kulia na kujitia nguvu katika Bwana, ndipo Bwana anamwambia, Inuka_ Ukiwafuata utawapata na utawapokonya yote waliyoiba, yote waliyochukua. Kumbe tunayofikiri hayawezi kuisha, yanaweza kuisha, yale tunasema hatuwezi kupita, tunaweza kupita, yale tunawaza hayawezi kutuachia, yanaweza kutuachia; Lakini kama tutainua imani, na kujitia nguvu katika Bwana, basi tutavipata. Kwa nini, kwa sababu Bwana ameshaondoa nguvu zilizo juu yao.

Yoshua na Kalebu wakawaambia makutano; Hesabu 14:9. Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope. 

Unayoyaogopa yameondolewa nguvu zake, unayosema yanakutesa, yanakuliza, ni magumu, huwezi kutoka; yameondolewa nguvu zake_ tatizo siyo yenyewe tena, tatizo ni wewe hutaki kuinuka na kuyafuatia. Ukiyafuatia utayapata_ Ukiinuka na kupigana utashinda.

Kumbe tunavyohofu hatuwezi kuvipata, hatuvipati kwa sababu tunahofu ya kutokuvipata, kumbe kesho tunayohofu itakuwa mbaya, siyo kwamba ilitakiwa kuwa mbaya, inakuwa mbaya ni kwa sababu hatujaifuta tumeacha siku zote itufate sisi, YESU anasema 

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake. Math 6:34.

Kesho imewekwa ijisumbukie yenyewe, wewe ifuate kwa imani, maovu ya leo yasikukatishe tamaa maana siku inatosha kwa maovu yake.


Bado Lipo Tumaini, Kama utajitia nguvu katika Bwana, Utawapata Hakika.


Mimi ni Pastor Ulenje 

 +255 683 477827 

FOLLOW ME 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama 

PASTOR ULENJE


Tuesday, January 10, 2023

UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU

 UHUSIANO WA ROHO MTAKATIFU NA NENO LA MUNGU


1.    Roho ndiye analishuhudia neno ndani yetu.


Yoh 15:26 Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia

1 Yoh 5:7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli

Tena kuhusu kuokoka Yoh 3:5 Yesu anasema Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, maana yake siyo neno peke yake, Roho lazima awepo ili neno kumuokoa mtu.


2.    Roho ndiye analisema neno la Mungu midomoni mwetu.


Yesu anasema Marko 13;11 msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni; kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu

Kwenye Mathayo 10:20 anasema kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu

Siri ya kufikia hapa ni kujaa Roho Mtakatifu, Biblia inasema kwenye Mdo 4:8 Petro akijaa Roho Mtakatifu, alipoongea wazee wakashangaa mbona hawa watu hawajasoma wametoa wapi ujasiri huu.


3.    Roho ndiye anayekupa uwezo wa kuisikia sauti ya Mungu.


Ufu 1:10 Yohana anasema Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu

Ukisoma Eze 2:2 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami. 

Kumbe muda wote alikuwa hamsikii Yeye aliyesema naye.

Ukisoma Efeso 3:1-6

1 Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;

2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.

5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo 


4.    Roho ndiye anayetupa kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.


Ukisoma 1 Kor 2:9-12 

9 lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.

11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.

Kumbe yapo ambayo Mungu amekuandalia lakini kuyapata ni lazima Roho apate kukufunulia, la sivyo utaendelea kuteseka ikiwa uliyokirimiwa yapo.

Na siri kubwa ili Roho akufunulie ni kuwa mtu wa Rohoni, anasema katika mstari wa mwanadamu wa tabia ya asili yaani tabia ya mwilini hayapokei mambo ya Roho wa Mungu, kwake ataona ni upuuzi, kwanini kwa sababu yanatambulikana kwa jinsi ya Rohoni.


5.    Roho ndiye anatusaidia kulishika Neno


Eze 36:27 anasema Nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu,nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. 

Ni baada ya Mungu kuona mwanadamu ameshindwa kuenenda katika sheria zake wala kushika hukumu zake wala kuzitenda, ndipo akaweka roho yake ndani yako.

Ukisoma Warumi 7:23-25 Paulo anaonyesha wazi akipambana kuushinda mwili, lakini jibu anasema ni Roho mtakatifu ndiye anaweza kumuweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.


6.    Roho ndiye analithibitisha neno linapofika wakati wake.


Kila ahadi ya Mungu inapofika wakati wa kutimia unaona Roho anatokea kwenye tukio. Kuzaliwa kwa Yesu unaona mariamu anashika ujauzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu Luka 1:35.

Ukisoma Mdo 13:2 Paulo anaitwa kuwa mtume wa mataifa, lakini anakaa miaka 11 Antiokia bila kufanya wito mpaka Roho anashuka na kusema sasa ndiyo wakati Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi niliyowaitia.

Siri kubwa waliingia kufunga na kumsifu Mungu, waliingia rohoni, kama wasingeingia rohoni wakati ungewapita. Acha kujichelewesha kwa kupenda sana kuwa ubize, tenga muda wa kuwa rohoni huu ndiyo wakati wa kupiga hatua uliyoisubiri.


7.    Roho ndiye anathibitisha Neno kwa Ishara na Nguvu.


Watu walipoona Yesu anafanya ishara nyingi wakasema akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote... Math 8:16, 

Lakini Yeye anakuja anasema kwenye Sura ya 12 hiyo Math 12:28 Lakini nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu. Kumbe wao waliona neno lake pekee, kumbe neno lake lilichanganyika na Roho Mtakatifu.

Mdo 13:9 Inasema Sauli, ambaye ndiye Paulo akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho yule mchawi akamwambia angalia mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu. Ikawa, kwanini kwa sababu neno lake lilichanganyika na nguvu za Roho.

Ndipo anasema kwenye 1 Thes 1:5 Injili haikuwafikia katika maneno tu, bali katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu.

Kama unataka neno lako liwe na nguvu unapotamka katika maombi, siri ni Roho Mtakatifu, Unataka Neno litokee kwenye maisha yako, Roho ndiye anafanya neno litokee kwako pale unapolitenda.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

Follow me 

Tiktok, Facebook, Youtube, Instagram kama Pastor Ulenje... hakika Utabarikiwa



Tuesday, November 22, 2022

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KWA MKRISTO

 KWANINI TUNAMHITAJI ROHO MTAKATIFU?

Somo la Kwanza


Luka 24:45, Mdo 1:4-5

Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasitoke mjini mpaka wapokee Roho mtakatifu, maana yake ni muhimu sana kwa Mkristo. Yesu alileta ufalme wa Mungu, na alitaka watu kuingia ndani ya ufalme huo. Wanafunzi walipotaka kujua lini atawaletea ufalme, Yesu anasema kuhusu Roho Mtakatifu.

Yesu anamaanisha ili mfanikiwa ndani ya huu ufalme muhimu sana ni Roho mtakatifu.

  • Utaona kabla Yesu hajafanya chochote kwanza alipata Roho mtakatifu

  • Pia utaona anaawaacha wanafunzi wake, pia anawaambia wasitoke mpaka wapokee Roho

  • Na wanafunzi wake, utaona katika mahubiri yao, cha kwanza kabisa mtu akiokoka ni Roho mtakatifu, na ishara yao kubwa kama mtu amepokelewa na Mungu basi ni kupokea Roho Mtakatifu. Mfano mzuri ni habari ya Kornelio


KWANINI TUNAMHITAJI ROHO MTAKATIFU/ UMUHIMU WA RMT

  • ROHO NI MUHIMU KATIKA WOKOVU WETU.

Tunaokoka kwa njia ya Roho mtakatifu.

  • Yoh 3:5-6 tunazaliwa mara ya pili kwa njia ya Roho mtakatifu.

Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

  • Tito 3:5 Roho ndiye anayetufanya upya.

si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;

Roho ndiye anashuhudia kuwa sisi tu watoto wa Mungu

  • Rum 8:16 ndiye anashuhudia pamoja na roho zetu

Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;

Roho ndiye arabuni ya wokovu wetu

  • 2 Kor 1:22 Naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu. Arabuni ni ishara ya kitu kijacho. Muhuri ni dhamana au uthibitisho.

naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.

Tunatunza yale mazuri Mungu aliyotupatia kwa Roho Mtakatifu

  • 2 Tim 1:14 Tunalinda ile amana nzuri kwa RMT. Amana ni akiba nzuri au ya thamani. Pasipo Roho utapoteza kila kitu.

Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu.

Tunamshinda adui kwa Roho Mtakatifu

  • Mdo 1:8 mtapokea nguvu akishawajilia juu yenu RMT. Mfano wa Skewa Mdo 19:14-16. Hawa watu hawakuwa wameokoka, wakatamka jina la Yesu wakijaribu lakini hawakuwa na nguvu.

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

  • Mdo 8:5-7, 5:3-5. Filipo kwa sababu alijaa Roho mtakatifu akashinda nguvu zote za giza, mpaka mganga akasalimu amri.

Tunashinda tamaa za dunia na za mwili kwa RMT

  • Rum 8:13 

kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.

Tunakuwa imara katika wokovu kwa sababu ya Roho Mtakatifu

  • Mdo 4:8, 13 walipotikiswa Roho akawapa hekima ya kujibu kwa ujasiri mpaka mafarisayo wenyewe wakashangaa.

Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli,

Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Pastor Ulenje

+255 683 477827

MOROGORO, TZ.

Saturday, November 19, 2022

MAANA HALISI YA MAOMBI 01.

Mpaka tumejua maombi ni ‘serious task’ kwetu tulio-amini, Hapo tutaanza kuomba. 


 Yesu anasema tukiomba tusipayuke-payuke.

Kupayuka si maneno mengi, kupayuka ni kurusha maneno pasipo shabaha. haikuwa na maana ya kukataa kuomba kwa sauti, ila usifanye hivyo kwa kuamini kuwa sauti huleta ufanisi wa maombi au ndiyo maombi yanakuwa na matokeo. 

Sauti haileti matokea, sauti ni sauti tu. Bali kuomba bila shabaha, bila imani, bali kutamka maneno mengi tu ukifikiri ndiyo kupata majibu, hiyo ndiyo kupayuka. Bali maombi lazima yawe na shabaha, yawe na matarajio. 

Pasipo matarajio hakuna uhakika, pasipo uhakika hakuna imani, pasipo imani hakuna majibu ya maombi, pasipo majibu ya maombi, maana yake bado hujaomba. 

 Swali kwanini Yesu alisema tusipayuke? 

Yesu alitamani tuombe kwa shabaha. Na hii ndiyo siri ya kuombea jambo la mda mrefu, ng’ang’anizi, lililokufata mda mrefu. Unapoingia kuomba ni muhimu kujua kuwa, hitaji lako Yesu alilijua kabla hata ya hitaji kukufikia (Math 6:8, Zab 139: 16), maana Yeye ndiye aliyeziamuru siku kabla hata hazijaja bado. Ndiyo maana akasema “...Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba”

 Mjumuisho wa maneno yote ya mwanzo ndipo tunapata maana ya maombi. Maombi yana nguvu sana kama yakiombwa kwa shabaha. Yaani kuomba ukiwa na matarajio ya kitu fulani kitokee, na ukaomba mpaka kitokee. 

Majibu ya Mungu ni kama bahari, cha kushangaza wengine wanaenda na vijiko, nenda kwa Mungu na matarajio makubwa, matarajio yasiyo na kizuizi cha kutazama uwezo wako bali uwezo wa Mungu usio na kipimo.

 MAANA YA MAOMBI

Kama Yesu anasema Baba Yetu anajua haja zetu kabla hata hatujaomba, kwanini hayashuki TU!?

 Yesu akasema “Basi ninyi salini hivi; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni” (Math 6:9-10). 

 Hivyo tunapoingia kwenye maombi tunaingia kwenye very serious business of God’s Kingdom, kushusha mapenzi ya Mungu ambayo yalishakuwa tayari mbinguni hata kabla siku hizi hazijafika, Mungu alikuwa anakusubiri wewe uyashushe duniani (Muhimu 1Kor 2:9). 

Yesu anawaambia wanafunzi wasalipo, wamwambie MUNGU mapenzi yake yatimizwe, kwanini wakati Mungu si mwanadamu hata a-amuriwe na mtu. 

Hapana “Mungu pasipo mtu hafanyi, na Mtu pasipo Mungu hawezi”. 

Usipotamka nini kitokee duniani Mungu hafanyi bali anasubiri mtu mmoja/wawili/zaidi “aliyeitwa kwa jina lake, ajinyenyekeshe na kuomba, na kumtafuta uso, na kuziacha njia mbaya; basi atasikia toka mbinguni na kuwaamehe dhambi yao, na kuponya nchi yao” (2 Nya 7:14) 

Hivyo; Maombi ni kumruhusu Mungu kuingilia jambo duniani 

Kifupi: Maombi ni kushusha mapenzi ya Mungu duniani.

Usikose Sehemu ya pili ya Somo hili kwenye Blog hii ya ulenje.blogspot.com. 

Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827

Morogoro, TZ.


Saturday, November 12, 2022

LAZIMA UWE NA SHAHUKU YA KUKUA NA KUONGEZEKA

Bila shahuku ya kukua hakuna mtu aliyewahi kukua.

Shika sana hili_ Wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo na unaweza kuwa zaidi ya ulivyo leo.

📌 Kwa Mungu inatakiwa tukue, na Mungu anategemea tukue. Eph 4:13,14

Mungu ametupa nguvu ndani yatu, ikiwa na kazi ya kutufanya tukue. Kuna vitu Mungu hawezi kukupa, ijapokuwa ni vyako, mpaka ukue. Galatia 4:1-7.

Hata chakula, mafanikio, karama, vipawa, nafasi, fulsa na cheo, ambacho Mungu anakupa, kinatokana na ukuaji wako.


MAENEO MUHIMU UNAHITAJI KUKUA NA KUONGEZEKA.


1. Kua kwenye Kuomba

Math 26:40_ Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja.

Yesu alitaka wanafunzi wake wakue katika muda na stamina yao ya kuvumilia usingizi na kuomba.


2. Kukua kwenye kufunga

Math 9:15

Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga.

Yesu alimaanisha, siku atakayopaa basi lazima tuanze kuutisha mwili kuacha chakula kwa ajili ya Bwana kwa muda fulani.


3. Kukua kwenye imani

Math 17:16, 19-21

Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu.

Yesu alitegemea kwa muda aliokaa na wanafunzi wake, unatosha kukua imani, wakamvunja moyo alipoona kumbe bado wana mashaka hata kutoa pepo. Yesu anategemea kwa muda huo ulio kaa kwenye wokovu, uwe tayari una imani ya kutoa pepo na zaidi.


4. Kukua kwenye Neno.

Ebr 5:12

Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 

Kolosai 1:10 anasema "mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu"

Muda huu inatakiwa uwe tayari unaweza kufundisha siyo tena hata maziwa hujui, weka bidii kusoma neno ili ukue katika maarifa ya Mungu. 


5. Kukua katika kumtumikia Mungu.

Luka 5:10

Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu. 

Mungu anataka ufike hatua ya kuanza kuvua watu.

Yoh 15:16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Mengine yote ni mema, ila kusudi moja la kuokolewa ni ili ukazae matunda, uokoe wengine. "Mungu ametutuma kila sekta ili kuokoa watu kila sekta" huu ndiyo msemo wangu naupenda.


6. Kukua kwenye kiasi.

1 Thes 5:6-8

Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 

Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. 

Chochote fanya kwa kiasi, fanya kwa ratiba, ili ufanye kingine pia.


Mimi ni Pastor Ulenje 

+255 683 477827 

MOROGORO. TZ.

Saturday, April 23, 2022

JUA UNDANI KUHUSU MAISHA YA MILELE

 *** MAISHA YA MILELE NA MWAMINI 


-( 1 Wathesalonike 4:13-18)

-Kwanini tunajifunza maisha ya milele? Ni muhimu sababu mtu ataweza ishi kwa kujizuia (mithali 29-18).

-Mtu anaejua Kuna maisha ya milele ataishi kwa umakini Sana

-MUNGU ametupa maisha ya sasa ili tujiandae na maisha ya milele


- MUNGU ametupa maisha ya sasa ni mchujo na kigezo kikubwa alichoweka ni utii Yani unae mtii ndie BWANA  wako

- Tamaa za shetani ni 

1)Tamaa ya mwili

2)Tamaa ya dunia

3)Kiburi Cha uzima


*Mwanadamu akifa anaenda wapi ??

- katika Agano la kale neno walilopata ni kuzimu (Zaburi 49-14) Yani walio haki na wasio haki wote wanaenda kuzimu ( Zaburi 88-3)

-YESU anakuja kutuonyesha kuwa kule kuzimu walitenganishwa walio haki na wasio haki ( Luka 16-19) YESU anatuletea neno peponi na jehanamu.


-Mtu asiyeokoka akifa anaelekea jehanamu ( Marko 9-45)

-Mwenye haki akifa anaelekea peponi( luka 23-43)

- peponi sio mbingu mpya peponi ni Mahali pa kufarijiwa

-Jehanamu sio Mahali pa mwisho kwa wasio haki Mahali pa mwisho ni kwenye ziwa la moto ( ufunuo 21-13)

- Walio haki wakifa wanaelekea peponi wakisubili pia hukumu kwa matendo ya mwili waliofanya baada ya kuokoka .

- peponi sio Mahali pa mwisho kwa waliokoka Bali ni mbingu mpya ama yerusalem mpya biblia inasema Mahali huko  ni pazuri hamn mfano Kuna Kuna dhahabu Safi Kama bilauri pia Kuna kuta nne ambazo marefu na mapana yake zimefanana kuta zimepambwa na madin Kama zumaridi  ,yakuti nk

- katika yerusalem mpya hutokumbuka maumivu 


* Nini maana ya kufa kwa mwamini ???

-Ni kuondoka toka mwili huu wa batili na kwenda kukaa na BWANA(2 Wakorinto5-6)

- Paulo alitamn kukaa na BWANA (wafilipi 1-21)

-Paulo anasema tuziweke kando zile dhambi zinazotuzuia( waebrania 12-1)


* Unaishi kwa ajili ya Nani???

- MUNGU anasema mbele yenu nimeweka uzima na mauti Ila chagueni uzima ( kumbukumbu la torati 30-19)

-(wafilipi 1-21)

-(warumi 6-21)


* Kiti Cha hukumu Cha KRISTO 

- Kwa walio haki

-wafu watafufuliwa kuungana na walio hai siku ile ya parapanda kuu ( 1wakorinto 15:50-53)

-(warumi 14-10)

-(2 wakorinto 5-10)

- sisi tuliokoka hatutahukumiwa pamoja na wasiokoka sisi tutahukumiwa maisha yetu baada ya kuokoka 

- Paulo anasema wengine kazi zao zitaungua Kama nyasi anasema wataokoka Ila kwa Moto 

 

* Vitu ambavyo tutatolea hesabu 

1)namna gani umeshiriki kuleta watu kwa KRISTO ( Daniel 12-3)

2) kwa habari ya ulimi 

3) kwa habari ya kushindwa dhambi( warumi 6:1-4)


-From pastor ulenje EM

Written by kayombo jr

Friday, July 16, 2021

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI BORA WA YESU

25/06/2021, PREACHED 27/06/2021 AT VICTORY EMPOWERMENT TEMPLE 

FANYIKA MWANAFUNZI

WEWE NI ZAIDI YA JINSI ULIVYO. UNAWEZA KUWA ZAIDI YA JINSI ULIVYO LEO.


Yesu aliwakuta wanafunzi wake wakiwa wavuvi, hata Galilaya walikuwa hawafahamiki, lakini walipofanyika wanafunzi, wakafika mpaka kwa Wayunani, mpaka Asia. 
Unaweza kufanyika zaidi ya jinsi ulivyo leo, kwa sababu unaweza kufanyika mwanafunzi. Kufanyika mwanafunzi wa Yesu ni daraja la kukuvusha daraja la maisha, ni ngazi ya kupanda ngazi nyingine ya maisha. Kama unawaza wapi pa kuanzia ili upae kimaisha, basi anzia na kufanyika mwanafunzi wa Kristo.

Kusudi la Kristo ni Kujipatia Watumishi.

Math 28:19, Yesu anasema, “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Yesu anaweka wazi, anataka wanafunzi. Na ukweli hajatutuma kukufundisha bali kukufanya mwanafunzi. Yesu amekuokoa ili uwe mwanafunzi.
Yesu anasema “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; MATH 11:29.

Ukisoma mstari wa juu yake ‘28’ anasema “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”. Kusumbuka iwe mwisho_ umekopa sana kufanikisha mipango, umeomba, umetafuta, umelia_ leo nenda kwa Yesu_ kanunue Biblia sema “nitajifunza kwa Mungu nami nipumzike, nipate raha”

Kwanini uwe mwanafunzi?

1. Sababu mwanafunzi pekee ndiye unaweza kumbadirisha. 
Anayekufundisha anakufanya uwe mtu fulani_ na hasa anakufanya yeye alivyo. 
Yesu hataki ujifunze kwa dunia, kwa sababu ukijifunza kwa dunia utakuwa kama dunia. Ila ukijifunza kwa Yesu utakuwa kama Yeye. Yesu anasema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake”. LUKA 6:40. 
Yesu anataka uwe kama yeye. Na dunia wanataka uwe kama wao_ lakini wote hao ni wageni hapa duniani, Yesu ni zamani kuliko wote_ wote wameikuta Biblia_ na ina shuhuda ya kufanikisha wengi_ ni bora leo ukachagua kuwa mwanafunzi wa Yesu. 
Unapofungua Biblia na kusoma, unafanyika neno, unafanyika kama Yesu.

     ✅ Yesu Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu” MATH 4:19. Yesu anataka akubadirishe kutoka mtu fulani uwe mtu mwingine, 
Kila aliyeamua kufanyika mwanafunzi_ baada ya mda fulani, watu wakasema “siyo yule tunayemjua” wengine kwa mshangao wanasema “ni wewe kweli, au mwingine”
  Paulo anasema “Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ROM 8:30. TENA Anasema “tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 KOR 3:18.
Usijipime leo, Hayo unayopitia ni milima na mabonde tu ya njiani_ fanyika mwanafunzi_ wewe ni zaidi ya jinsi ulivyo. Kuna mtu Yesu anamtengeneza mwenye utukufu zaidi ya ulio nao leo. 

2. Sababu anataka akujulishe siri za ufalme.
Ukishasikia siri, maana yake kuna watu maalumu wanaostahili kujua. Yesu hakuja kumwambia kila mtu siri za ufalme wake, bali wanafunzi wake pekee. Yesu anawaambia wanafunzi wake “Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa” MATH 13:11. 


3. Sababu anataka akutumie.
Yesu hajawahi kutumia mtu ambaye hajafanyika mwanafunzi. “watu wengi walimwamini…lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; YOH 2:23, 24. Kumwamini haina maana yeye amekuamini, na sifa ya kumuamini siyo kuwa mkamilifu, bali kuwa mwanafunzi. Pamoja na udhaifu alio nao Petro, lakini Yesu alimvumilia na akamuachia kanisa, kwanini_ wakati wengine wamekimbia, yeye akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, YOH 6:68.
Mungu sasa anataka kutumia watu wa kila sekta, wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, waimbaji ili kujipatia mavuno na kutangaza jina lake_ ili kuipa aibu dunia… wewe fanyika mwanafunzi. Naye atakutumia. 

Siyo Kila Mtu ni Mwanafunzi.

Kwenye biblia kuna makutano na wanafunzi. Kuhudhuria kanisani na kuokoka haina maana wewe ni mwanafunzi.
Unaweza ukahudhuria kanisani miaka 40 lakini usiwe mwanafunzi, kwasababu uwanafunzi siyo miaka uliyookoka, wala uliyohudhuria kanisani, uanafunzi ni maamuzi, siyo kuhudhuria. Wote ni mashahidi hasa kwa walimu ambao wanachapa sana, tulikuwa tunahudhuria darasani lakini tunasikia lakini hatusikilizi. 
Yesu anasema “Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. MATH 13:14, 15.
15. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Tunajuaje kuwa wewe ni mwanafunzi?

NAMNA YA KUWA MWANAFUNZI WA YESU.

Tuone sasa namna, unaweza kuwa mwanafunzi. Ni vigezo gani mwanafunzi anavyo.

1. Mwanafunzi Analiamini na Kulikubali Neno Lote.
Siyo nusu, siyo moja_ yote. 
Yesu siku zote alitumia maneno magumu ili kuchambua wanafunzi na makutano. Biblia inasema “wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena” wakakimbia wote, wakabaki wanafunzi tu. YOH 6:64-69. 
 Nao akawauliza “Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Petro akajibu akasema “Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele, Nasi tumesadiki, tena tumejua wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu”. Mwanafunzi anaamini yote. Paulo anasema “…nikiyaamini yote…” MDO 24:14. 
Na huwezi sema umeamini mpaka umekubali ulichosikia, umekipokea na kukitendea kazi ulichosikia. 
Huwezi sema ni mwanafunzi mpaka umekubali, na kukishika kile mwalimu amesema. Na mwalimu wetu ni Yesu, na shule yake ni Biblia. Na anatumia watumishi wake kukueleza alichoandika. Paulo hajaandika Biblia, Mathayo hajaandika Biblia, mimi sijaandika Biblia_ wote waliandika yale Roho Mtakatifu amesema, nami nahubiri yale Biblia imesema. Nami natenda hayo hayo na naona matokeo, na Mungu amenituma nisema nawe, ili tuinuke pamoja.


2. Moyo wa unyenyekevu.
Pasipo moyo wa unyenyekevu huwezi kumfundisha mtu yeyote. 
Mtu mwenye kiburi anajua kila kitu, hata ambacho yeye mwenyewe anajua kuwa hajui. Lakini atalazimisha kwa maneno mengi kuwa anajua. 
Watu kama hao_ hawawezi kuwa wanafunzi. Sababu wanaenda kwa Mungu, huku wakiwa na ya kwao. 
Wanasema Mungu tufundishe, lakini kama ni kinyume na aliyosema mjomba, bwana vicoba, hatuwezi kukusikiliza.
Hakuna kazi ngumu kama kumfundisha mwanafunzi mwenye tution nyingi.
 
Yesu anasema “kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa” LUKA 14:11. Unafikiri kwanini Mungu anainua wanyenyekevu, kwa sababu mnyenyekevu ni kama mtoto anabebeka (Math) anafundishika,
Mungu anasema “…Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. ISAYA 48:17

Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko. MITH 16:18.

3. Mwanafunzi wa Yesu  Anakuwa.

Sifa ya mwanafunzi ni kukuwa. 
Kila mwalimu anapima mwanafunzi wake kwa kukuwa katika kile anamfundisha. 
Haijarishi umetokeo wapi kwenye wokovu, lakini kila siku inabidi ukue kila eneo_ kuomba, kusoma neno, kuhudhuria ibada, kufunga, kushuhudia.
Yesu anasema “Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini. MATH 13:23.

4. Mwanafunzi lazima awe ametubu.

Yesu anapoanza injili yake tu_ akasema nini ufanye ili uwe mwanafunzi wake.
Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. MATH 4:17

Kutubu siyo kuomba msamaha, ni zaidi ya hapo. Kutubu ni kubadiri unavyowaza, kubadiri mfumo wa maisha.

Yesu anaweka wazi, nimewakuta mna ufalme wa dunia hii, sasa geukeni acheni kuwaza na kufanya kama dunia, sasa muwaze na kufanya mambo kama ufalme wa mbinguni unavyotaka.

Others
5. Usiogope watu
Huwezi kuwa mwanafunzi kama unaogopa watu wanasema nini. Sababu siku zote Yesu anakwambia mambo ambayo watu hawataki, ni kinyume na wanavyojua, ni kinyume na wanavyotaka uishi. Kilichomponza Sauli ni kuogopa watu, akaacha kufanya Mungu alichomfundisha.
Yesu akasema 
6. Jikane mwenyewe_ luka 14:26
7. Beba msalaba wako_ luka 14:27

Hitimisho.
Omba unyenyekevu na maombi ya agano_ kuwa wanafunzi. Na weka agano kutenda nini neno linasema.

Ushauri au maombi.
0683 477 827 
0718 721848 

Thursday, January 21, 2021

NAMNA HII HUPONYA NDOA MARA 100 ZAIDI.


Jambo hili likikosekana, mwanamke atachanganyikiwa, Mwanaume atakuwa wa lawama siku zote.

Nimetazama ndoa nyingi za mwanaume mvivu asiyejua majukumu yake.

Mwanamke akitazama kila kitu alichovaa ndani na nje, simu na vocha, na kila kitu alichonacho, kimetoka kwa mwanaume, Si tu, Atajivuna kwa marafiki, Lakini ATAKUHESHIMU na UTAMTAWARA.

MUNGU hakumpa Hawa Bustani, alimpa Adamu, Mungu hajawahi kumwambia Hawa ailime bustani, bali alimwambia Adamu, hata neno la kusema "matunda ya kila mti wa bustani waweza kula" MWA 2:16 hakumwambia Hawa, alimwambia Adamu.

Ina maana jukumu la kula na huduma, ni la Adamu kwenye familia, siyo Hawa. Ndiyo maana siku moja, siku moja tu, haikuhitaji nyingi, Adamu alipopumzika na kumuacha Hawa akajitafutie chakula, ndipo shetani anajitokeza, na ndipo anguko la familia ya kwanza linatokea, na madhara hadi sasa duniani tunayaona.

Nionyeshe familia ambayo, mwanamke anahusika kutafuta chakula, nitakuonyesha familia ambayo shetani amejenga nyumba karibu nao. Na ipo siku atawadondosha, as matter of time. GOD FORBID.

Hata uchumba ambao mwanamke ndiye chanzo cha pesa unahitaji mabadiliko.

Mwanaume asiyefanya kazi na kuhudumia mke wake na watoto, asitegemee kupata heshima na asiwe na tarajio la kumtawara mke wake. Biblia inasema...

Mithali 12 24
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.

Ukiwa na bidii, bila hata kumwambia "niheshimu" bali akitazama wewe ndiyo chanzo cha kupendeza kwake, chanzo cha kula yake, chanzo cha kila kitu alichonacho. ATAKUHESHIMU automatic. Mwanamke anaheshimu sana chanzo cha heshima yake, shika sana hili neno.

Nikiwa nasoma chuo kikuu cha Dar es Salaam, nilikuwa nasoma huku nafanya biashara stendi ya Ubungo, asubuhi naamka naenda Kariakoo kufata bidhaa, ndipo naenda chuo. Jioni naenda kanisani kuonyesha sinema watu waokoke, nikirudi moja kwa moja maktaba kusoma, nilikuwa naomba mara nne hata zaidi kwa siku. Nilikuwa sina mkopo lakini kuna watu wenye mkopo niliwakopesha pesa.

Kwa neema ya Mungu sijawa pata Disco, Wala sijawa Carry, Wala sijawahi fanya SAP, Na bado msimu wa mvua nilirudi Morogoro kulima, maana nilikataa kula unga wa dukani kwenye maisha yangu, na mchumba wangu alitumia Smartphone ambayo mimi nilinunua na nilimuongezea pesa za kutosha katika biashara yake. Kwanini nilikataa kuwa mvivu.

Nakumbuka watu waliniita speed man, sababu nilikuwa natembea speed ni hatari.

Vijana wa kizazi hiki Mungu atusaidie tuache uvivu. Tuhudumie familia zetu. Bila kujali mke anafanya kazi gani, usihesabu pesa yake, hesabu majukumu yako.

Kama bado hujapata kazi inayoendana na elimu yako nikutie moyo, 2021 Inuka "Kabla hujapata unachotafuta kufanya, fanya kilicho mbele yako" (before you find what you finding to do, do what you find"

Suleman anasema Mhubiri 9 10
"Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.

Kabla hujafa kama masikini, angalau ionekane umejaribu kuushinda umaskini, maana hakuna aliyeandikiwa umasikini. Wewe ni mzao mteule, umeumbwa kwa mfano wake anaye miliki mbingu na nchi. You're Born A Winner, God can never birth a failure, even once.

Mwanaume ambaye mke wake ndiye anahudumia kila kitu, ni ngumu hata kumuuliza mke wako "unaenda wapi?" maana atakujibu "nisipotoka tutakula nini!, acha nitoke ile tule"

Ukiona ukiulizwa Ada ndiyo unaanza kuwa rohoni, jua kuna shida mahali.

Mwanume kuhudumia familia ni utukufu kwa Mungu, maana ndivyo alivyoumba, mmoja mfanyakazi mmoja msaidizi.

Nimalize kusema, Mithali 13 4
Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

Ukiwa mvivu utatamani amani ya familia, utatamani uheshimiwe, lakini hutopata.

Na kuna wanaume ambao ni wachapakazi, wana pesa ila si wahudumiaji wa wake zao. Ndugu haijarishi kiwango cha pesa ulichonacho. Mwanamke anaheshimu sehemu ya chanzo chake cha heshimu. Mwanamke anapoishi na mwanaume asiyehudumia, hujiona ni bora kuishi na masikini.

Aliyekwambia kumpa zawadi mchumba wako dhambi nani, hata asipokumbuka sms zako, atakumbuka fadhila na utu wako.

Na mwanamke unayesoma ujumbe huu kumbuka...

Mke mwema... "Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato" MITH 31:11.

Mwanamke aliyejiweka kuwa mchumba au mke mwema ni, Biblia inasema hatakosa mapato. Hata kama hatofanya, lakini kama wewe ni mke mwema hutokosa mapato. Juhudi yako, ya kuhudumia familia yako, mume akiwa mbali, itaamsha akili yake, na atakuamini na hutokosa mapato.

Nionyeshe mwanamke mchapakazi na ni mwema kwa mumewe, huyo ndiye ambaye Mumewe atamwamini, na hatakosa mapato.

Ubarikiwe Sana.
Kwa Msaada wa Roho Limeandikwa na.
Pastor Ulenje EM.
0683-477827
2021 INAWEZEKANA.


Sunday, January 17, 2021

USIOGOPE, AMINI TU. MARKO 5:36.

 Mathayo 19 26 

 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.



Mungu anataka tufanikiwe,


Kumbukumbu la Torati 30 15 

 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya;



Mafanikio siyo karama, mafanikio ni uchaguzi. Mungu amekupa kuchagua kufanikiwa au kushindwa. Ila amekupa ushauri, chagua mafanikio.


INAWEZEKANA


1. Ni Kumwambia Mtu, Kuna Njia ya Kufanya ili Hilo Jambo Lifanikiwe.


Inawezekana alijaribu akashindwa kama Musa. Au wenda amejaribu mara nyingi sasa ameona haiwezekani. Au mbele yake anaona giza, hakuna kitu anaona anaweza fanya tena.


Sasa unamwambia INAWEZEKANA.


Katika kila jambo ambalo Mungu anaruhusu litokee kwenye maisha yako, kila mpango una njia ya kufanya. Kuna kitu hujajua tu bado ndiyo maana hujafanikiwa mpaka sasa.


Kuna mambo siyo kwamba hatuwezi ila kuna sehemu, kuna kanuni bado hatuijui.


Katika kila jambo linaloonekana haliwezekani, ni kweli kwamba kuna njia ya kulifanya liwezekane. Hata unayoyaona leo yamefanyika, mwanzo yalionekana hayawezekani.  Mwaka 1904 wana sayansi walikutana Uingereza kuthibitisha kuwa hakuna kitu kinaweza tembea angani. Lakini Ndugu wawili watoto wa Wright maarufu kama Wright Brothers, waligomea maamuzi yale, wakasema inawezekana. Mwaka 1910 wakatembeza ndege kwa mara ya kwanza.


Siyo kwamba haiwezekani, Tatizo umekata tamaa, kutafuta nini unatakiwa ufanye. Bado ipo Njia.


Marko 5:

Mwanamke alitokwa na damu miaka mingi na kuteswa na madaktari wengi, lakini alipogundua njia ya uzima wake. Kuwa nikigusa pindo la Yesu nitapona, akapona. Usikate tamaa, bado kuna kitu unaweza fanya ukafanikiwa.


Si kwamba haiwezekani, ila hujapata mbinu ya Kufanya. Unajua kujua namna ya kufanya mambo kunaondoa miaka mingi ya mateso ba kutoa jasho.


Kumb 2:1-3 Israeli walizunguka miaka mingi ndani ya jangwa wasiione njia. Siku moja Mungu akasema mlivyozunguka mlima huu vyatosha, geukeni upande wa kaskazini.


Israel wakakata tamaa, kuzunguka mda mrefu, siyo kwamba njia ya kufika haikuwepo, ila hawakuijua.


2021 Mungu anakwenda kukupa njia ya kufanya katika Jina la Yesu. Pokea.


Israel walipata neno la Mungu, neno likawaonyesha cha kufanya. Petro alifanya kazi ya kuchosha neno liliposhuka likampa cha kufanya, Mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12 alisikia habari za Yesu.


Kuna neno unalihitaji likupe cha kufanya...


A. Soma neno, Yoshua 1:8

B. Omba, Yoshua aliomba. Yoshua 7:6

C. Tafakari, kaa chini fikiri... Mda unaotumia kulia, ungekaa na kufikiri Neno La Mungu linasema nini kuhusu jambo lako na mpango wako, ungekuwa umeshapata njia.

D. Omba ushauri. MITH 13:10.


2. Unamwambia mtu Ambaye Anaona Jambo Au Mpango Hauwezekani.


Wakwanza anaona hakuna njia, huyu wa sasa anaona haliwezekani kabisa. Anaona ni jambo kubwa sana. Anaona ni mpango mkubwa kumzidi. Anaona Ha! Ngoja niwaze mengine, hii ni ndoto tu ya utotoni. Au watu wengi ameona hawajaweza na wengine wamemwambia haiwezekani.


Lakini naomba sikia....


Hakuna jambo haliwezekani kwa mtu aliyeokoka isipokuwa jambo lile ameliona yey mwenyewe kuwa haliwezekani.


Yesu anasema anabisha yupo mlangoni anabisha hodi mtu akifungua nitaingia ndani yake UFUN 3:20.


Aliyeingia ndani yako, Yeye anaweza yote. MATH 19:26 hilo kwa wanadamu haliwezekani ila kwa Mungu yote yanawezekana.


Yoh 14:10 Yesu anasema "bali ni Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake"


Kol 1:29 Paulo anasema "nikijitahidi kwa kadiri ya kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu. 


Tangu ulipookoka Mungu anafanya kazi ndani yako.


Fil 2:13 Neno linasema "Ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, katika kulitimiza kusudi lake jema.


Mungu yupo ndani yako kufanya hilo jambo liwezekane, Mungu aliye ndani yako, kwake yote yanawezekana.


Math 17:20 anasema "

Mathayo 17 20 

 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.


Maana yake, Ukiona ugumu unaongezeka, badala ya kukata tamaa, wewe amini sana.


Kuona inawezekana ndiyo mwanzo wa kushinda mambo yanayoonekana hayawezekani.


__Yesu alimwambia Yairo (Marko 5:36) "Usiogope, Amini Tu"


Kumbe 2021 Mungu anaposema Yote Yanawezekana, anasema "Usiogope, wewe inua imani yako"


A. Kula chakuka cha imani_ Neno. RUM 10:17

B. Meng'enya hiko chakula_ Tafakari YOSH 1:8

C. Tendea kazi_ Tumia hilo neno. YAK 1:22

D. Usiyumbishwe_ EBR 10:34 usiyumbishwe kile umeamini unapoona ugumu unaongezeka au kwa maneno ya watu.... Yesu hana too late.



3. Unamwambia Mtu Anayeona Hana Uwezo Wa Kufanya.


Anajiona hana uwezo. Hana uwezo wa kifedha, elimu, ndugu, mtaji, upako.


Hakuna mlima mrefu kwa mwanadamu, mlima ni jinsi wewe unavyouona. Maana hata mlima mrefu kuliko yote duniani, watu wameupanda.


Mungu bado hajaumba mwanadamu ambaye hawezi kitu. Alipoumba akasema "ni chema sana" vingine vyote alipotazama akasema ni vema, lakini kwa mwanadamu akasema chema sana.


Mafanikio yana siri hii, Ukijiona huwezi hutoweza. Ila ukijiona unaweza utaweza. Simba siyo mnyama mwenye nguvu kuliko wanyama wote, siyo mnyama mrefu kuliko wanyama wote, wala siyo mnyama menene kuliko wote.... Ila yeye ndiye mfalme wa mwitu.


Kwanini anapokutana nao, wao wanaogopa, ila yeye haogopi yoyote. Hata wale wenye nguvu zana. Tembo anaangusha mti, ila anakutana na simba analiwa, kwanini simba anaona "pamoja ni mnene wewe ni chakula"


Ukiona huwezi hutoweza, kwanini "siku ukisema naweza, basi utatafuta njia kwa kila hari, na utaweza"


Mwanamke mjamzito miezi 8, ilipotokea hatari aliruka ukuta. Aliambiwa rudia alishindwa. Kwanini, mwanzo alipoona hatari, kuna kitu kilisema ndani yake. UNAWEZA.


HESABU 13 MUSA anatuma wapelelezi, Wanarudi wanasema nchi ni nzuri, ila wanajiona hawana uwezo wa kuitamalaki. Wote wanafia jangwani.


Lakini Yoshua na Karebu wakasema "twaweza kushinda bila shaka HES 13:30.


Wengi wanapishana na mafanikio yao, uponyaji wao, majibu ya maombi yao, na kushindwa changamoto sababu wanaona haiwezekani. Inuka sema INAWEZEKANA.


Wanasema "Hakuna cha kufanya" No "Kipo cha Kufanya"


Wanasema "Hakuna Njia" No "Njia ipo" 


Unajua kwanini wanaosema hatuwezi huwa hawawezi "Sababu huwa hawafanyi hiko kitu"


Wanajeshi wa Israel walipoona hawawezi kunshinda Goloathi hata kumfata hawakumfata... Lakini Daudi aliona anaweza, AKAMFATA.... Kwa Jiwe tu Down.


Unachokiogopa na kukiona ni kigumu.... Ni kidogo sana.


Tengeneza ufahamu kuwa Unaweza. Aliye ndani yako ni Mkuu Kuliko Chochote. 


Mungu anatembea na watu wanaosema "Haijalishi Ugumu, Itafanyika"


_________________________



LAKINI KUMBUKA....


Neno linasema "bali kwa Mungu yote yawezekana" 


Maana yake_ Lazima Mungu ahusike. Biblia ya Kingereza inasema "with God, All things are possible"


Mungu hawezi husika mpaka umeomba. Paulo alifanya mambo makubwa ambayo wengine walishindwa, siri yake anasema...


Filipi 4:13 "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu"


Mungu akikutia nguvu yote yatawezekana kwako.


Maombi, Maombi, Maombi.


Lazima 2021 Tuombe Zaidi ya Miaka Mingine, kama tunataka kufanya yaliyoshindikana yawezekane.


Unapoomba  Unapata Vitu Viwili.


1. Uso wa Mungu_ Unakutana na uso wa Mungu kukupa njia ya kufanya, na nguvu zake.

2. Mkono wake_ wa kukusaidia unapokwama. Israel walikwama Misri na kufanywa watumwa lakini kwa Mkono wake aliwatoa.

3. Roho Mtakatifu_ kusafisha njia na kukufanya iwe unstoppable, uwe na ujasiri, uwe na imani, kukufanya ufanye mambo ambayo wanadamu wa kawaida hawawezi.


Unabii unapotoka unatoka kwa wote, lakini ni maamuzi ya mtu binafsi kufanya unabii utokee kwenye maisha yake. Hauji kuomba kumridhisha mchungaji, ila ni kwa ajili yako, ili upige hatua.


Leo unaona unaenda, ila kuna hatua ili upige ni lazima uombe leo. Kila mtu anakutana na hatua zisizowezekana, na ni hatua zisizowezekana zinawafanya watu wakuzidi kiuchumi na kiroho.


0718 721848

0683 477827

Pastor Ulenje EM